Ni mstari gani kwenye biblia unautumia sana upitiapo nyakati ngumu katika Maisha

Ni mstari gani kwenye biblia unautumia sana upitiapo nyakati ngumu katika Maisha

Screenshot_20231006-104256.jpg
 
1. Kipofu hawezi kumuongoza kipofu mwenzake.


2. Usihukumu nawe utahukumiwa.
Kuna watu wanapenda kukosoa sana wenzao kama vile wao ni watakatifu

3.Mimi ndimi njia ya kweli na uzima mtu hawezi kwenda kwa Baba bila kupitia kwangu
 
Bwana wetu Yesu kristo asifiwe wana Jf

Katika maisha yetu hapa duniani kuna wakati tunapitia nyakati zilizo na mambo magumu sana, kiasi kwamba kwa uwezo wetu unakosa majibu na kubaki kujiuliza maswali magumu yasiyo na majibu.

Nyakati kama za Kufukuzwa kazi, Ugumu wa maisha, kupoteza wapendwa wetu tuliowapenda sana. Usaliti katika maisha ya mahusiano na ndoa, kukosa kazi, kupakaziwa maneno yasiyo na ukweli pengine ugonjwa wa muda mrefu.

Tunapitia dhiki, mateso na maumivu katika maisha. Ukipata hiki unakosa kile ndivyo maisha yalivyo.

Natumaini letu linabakia kwa Muumba wetu.

Je ni mstari gani kutoka kwenye biblia unautumia sana kukupa faraja mpendwa.

Kwa upande wangu, Mstari unaoniongoza kila siku ni

Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Zaburi 23:6

Karibu.
Tusichoke kutenda wema.
Zaburi ya 23
 
Zaburi 23
BWANA ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Naam, nijapopita kati ya bonde la kivuli cha mauti,
Sitaogopa mabaya;
Kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
5Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika.
6 Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu;
Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Hiyo hapo
 
Bwana wetu Yesu kristo asifiwe wana Jf

Katika maisha yetu hapa duniani kuna wakati tunapitia nyakati zilizo na mambo magumu sana, kiasi kwamba kwa uwezo wetu unakosa majibu na kubaki kujiuliza maswali magumu yasiyo na majibu.

Nyakati kama za Kufukuzwa kazi, Ugumu wa maisha, kupoteza wapendwa wetu tuliowapenda sana. Usaliti katika maisha ya mahusiano na ndoa, kukosa kazi, kupakaziwa maneno yasiyo na ukweli pengine ugonjwa wa muda mrefu.

Tunapitia dhiki, mateso na maumivu katika maisha. Ukipata hiki unakosa kile ndivyo maisha yalivyo.

Natumaini letu linabakia kwa Muumba wetu.

Je ni mstari gani kutoka kwenye biblia unautumia sana kukupa faraja mpendwa.

Kwa upande wangu, Mstari unaoniongoza kila siku ni

Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Zaburi 23:6

Karibu.
Tusichoke kutenda wema.
Zaburi:23
 
Back
Top Bottom