Ni nani alitaka kumuua Tundu Lissu?
Ma
Nasema "alietaka kumuua" kwa sababu ukiangalia yale matundu ya risasi upande wake wa gari utajua kuwa hawa watu hawakutaka kumtishia tu. Walidhamiria kumuua.

Niungane na Watanzania wenzangu kumuombea Tundu Lissu dua/sala ili apone kikamilifu, Amin.

Nimejiuliza maswali mengi kuhusu shambulio hili la kipekee kwa mbunge (sijui kama kulikwishatokea shambulio jingine kama hili), hapa Tanzania.

Yafuatayo ni malumbano ya kifikra ndani ya nafsi yangu kuwa ni nani hawa waliotaka Tundu Lissu afe. Maoni yako yanahusika, tafadhal.

Nimefikiria wahusika katika dhana 4. Nitazichambua hizi dhana moja moja.

Dhana zenyewe ni hizi. Washambuliaji ni:

1. Vichaa fulani tu. (Random act)

2. Raia wenye chuki na Lissu kwa kuikalia kooni serikali.

3. Serikali yenyewe

4. Watu wenye chuki na serikali (false-flag attack) ili waisingizie serikali uovu huu.


1. Vichaa fulani tu. (Random act)
Hii inawezekana lakini inakinzana na taarifa za kuwa Lissu alikuwa anafuatiliwa na magari kwa kipindi kirefu. Huu mpango ulisukwa na pia walijua wanaemtaka hadi kumfuata mpaka nyumbani kwake. Sidhani hii ilikuwa ni Random Act. Dhana hii ni potofu.

2. Raia wenye chuki na Lissu kwa kuikalia kooni serikali.
Hii inawezekana kabisa. Wengi walimshutumu Lissu kwa kupinga sera zote za serikali (mimi nikiwa mmojawao). Kuna watu walikwenda mbali zaidi na kusema wanataka serikali iwaruhusu wamuue. Ndio maana kuna umuhimu wa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watu hawa.

Katika demokrasia watu tunashambuliana vikali kwa hoja na sio kwa kuumizana au kuuana. Kama hii itathibitika, basi kuna umuhimu wa kuwapatia ulinzi wanasiasa machachari wanaoibua hisia kali.

Kuna uwezekano mkubwa dhana hii ni sahihi.

3. Serikali yenyewe
Kuna watu mitandaoni wanadhani ni serikali yenyewe ndio imeunda hii mbinu ya kumuua Lissu ili awaondolee kelele. Wengi wanasema Lissu amefichua siri nyingi za serikali kufikia kuwa tishio kwa hii serikali.

Kwa maoni yangu huu ni upuuzi. Serikali hii inakubaliwa na watanzania wengi. Hoja karibuni zote alizotoa Lissu dhidi ya serikali zinaweza kujibiwa kirahisi sana. In fact, baadhi ya shutuma za Lissu zinaipaisha serikali kwa Watanzania. Kelele za Lissu zinaweza kuwa baraka (blessing) kwa CCM ifikapo 2020. Kumuua Lissu kutajenga hisia za uonevu na kuwaonea huruma CDM ifikapo uchaguzi mkuu. Serikali haiwezi kufanya kosa hilo.

Kwa hiyo dhana hii ni potofu

4. Watu wenye chuki na serikali (false-flag attack) ili waisingizie serikali uovu huu.
Hii dhana inahusisha watu wanaoichukia serikali (sio lazima wapinzani, inaweza kuwa watu wa nje) wanaotaka kumuondoa Rais Magufuli madarakani ifikapo 2020 kwa kuihusisha serikali yake na mauaji ya Lissu.

Serikali ya Magufuli imeathiri maslahi ya watu wengi sana wa ndani na wa nje. Akiendelea hivi hivi ana uhakika kabisa wa kupita ifikapo 2020. Sasa utaitoaje hii serikali madarakani ifikapo 2020. Jenga chuki kwayo.

Kama nilivyoeleza kwenye dhana namba 3, watu wakiamini kuwa serikali imemuua Lissu kinyama basi watawaonea huruma CDM na kuichukia CCM. CDM watachukua dola ifikapo 2020.

Je ni nani hawa wanaotaka kufanya unyama kama huu na kuisingizia serikali ya CCM (false-flag attack)?

Nina dhana nyingine 2 au 3 hivi (mfano, internal politics within CDM) lakini ni za pembeni sana na uwezekano wake ni karibu na sifuri. Kwa sasa hayo ndio malumbano yanayoendelea kichwani mwangu.

Please tell me I am not crazy.

==============================
Baada ya michango mingi iliyowekwa hapa kuna dhana niliyoigusia tu (Internal politics within CHADEMA) na wengi kuuliza kwa nini sikuifafanua. Hapa chini naiongeza ingawaje mwanzoni sikuipa kipaumbele.

Dhana ya 5.
Maadui wa ndani wa CHADEMA walitaka kumuua Lissu ili watimize malengo 3 yafuatayo.

1. Lissu aondoe ushindani katika uchaguzi ujao wa Uenyekiti.

2. Lissu aondoe ushindani katika uteuzi ujao wa mgombea urais ifikapo 2020.

3. Lissu atumiwe kama kafara ili kuipa CHADEMA mvuto na kuonewa huruma na kuichukia serikali katika uchaguzi wa 2020.
Mahaba yamekuharibia FOCUS, ulianza vizuri sana but umeshindwa kuficha unachokipenda.
 
Kwanza I declare interest sipo katika mlengo wowote wa chama chochote cha siasa hivyo bandiko langu halina uhusiano na political interests zozote.

Naomba kujuzwa inawezekanaje mtu risasi ikapiga upande wa kushoto wa gari ila muhanga akajeruhiwa mguu wa kulia kama inavyoonekana kwenye picha na dereva akasalimika.

Nimeweka picha apo chini kusindikiza uzi wangu.
FB_IMG_15927259733342944.jpeg
FB_IMG_15927259626837196.jpeg
 
Jitahidi japo Mara chache utazame movie za kihidi,jibu utalipata 99% ni uongo
 
Turudi kwenye hoja yangu unamanisha haiwezekani
Huamini? hata Mimi hivyo hivyo siamini
Kwa hivyo hata kwa lissu hata ni movie ilichezwa na washamburiaji walikuwa mahiri sana kama walivyoelekezwa
 
Risasi zilipopigwa dereva wake alishusha kiti chake lisu then akalala wakati wa Hilo shambulio lisu pia alifanikiwa kugeuka akalalia tumbo hivyo mguu uliokuwa kushoto automatically unakuwa upande wa kulia na dereva wake alifanikiwa kushuka bila kudhurika na yeye hakuwa Target hivyo hawakudili nae.
 
Hiyo haiwezekani kwa maisha ya kawaida labda kwenye movie tu. Naomba tukutane kesho
 
Kwanza I declare interest sipo katika mlengo wowote wa chama chochote cha siasa hivyo bandiko langu halina uhusiano na political interests zozote.

Naomba kujuzwa inawezekanaje mtu risasi ikapiga upande wa kushoto wa gari ila muhanga akajeruhiwa mguu wa kulia kama inavyoonekana kwenye picha na dereva akasalimika.

Nimeweka picha apo chini kusindikiza uzi wangu.View attachment 1485493View attachment 1485494View attachment 1485495

Namkubali sana Tundu Lissu na nilisikitika mno kwa Kilichomtokea ila hadi Leo hii najiuliza kwanini Risasi zote zimpate tu Yeye na si Dereva wake? Kwa kutaka Kujiridhisha zaidi juu ya hili nililazimika kuwatafuta baadhi ya Marafiki zangu ambao ni wana Medani ( Wanajeshi ) na Mmoja wao ni wa Kikosi Maalum kabisa Wazee wa Sanga Sanga wanielimishe zaidi juu ya Masuala haya.

Elimu ya awali niliyoipata kutoka Kwao ni kwamba kwa aina ya Bunduki iliyotumika katika Tukio ikitoa Risasi yake basi ina uwezo wa Kusafiri kwa Kasi ya kuanzia mita 50 hadi 75 na ikiwezekana hata 100. Pia wakasema hata iweje Risasi za aina ya Bunduki iliyotumika kwa jinsi ilivyo mkiwa mmekaa Watu Wawili pamoja inaweza ikapenya kutoka kwa Mmoja hadi kwa mwingine kulingana na Mazingira waliopo hao Wawili.

Gari inayoonekana hapa Pichani tunaona jinsi ilivyokoga Risasi nyingi tu na wakati zinapigwa nakumbuka Dereva alisema alikuwemo ndani yake na alikuwa amelala ila baadae kidogo akafungua Mlango na Kushuka kisha akajificha chini. Kinachonichanganya na Kuniumiza Kichwa imekuwaje Yeye hakuna hata Moja iliyomgusa na zote zikamiminika tu Kwake Tundu Lissu wakati walikuwemo wote ndani ya Gari hiyo?

Na hapa ndipo Mzukulu Mimi nakumbuka mno maneno ya Mzee wa Busara Mmoja aliponiambia kuwa kuna ninayoyajua na pia nisiyoyajua kabisa.
 
Kwa kuongezea ni kwamba Lisu pamoja na dreva wake walikuwa wameshashtuka kuhusu gari inayowafuatilia na ndo maana walipoingia parking hawakushuka wakawa wanaangalia ni nini kitafuatia

Na ndo maana hawakufanikisha hadhima yao kwa Lisu

Mungu ni mkubwa....[emoji120][emoji120][emoji120]
 
Na ku
Kwa kuongezea ni kwamba Lisu pamoja na dreva wake walikuwa wameshashtuka kuhusu gari inayowafuatilia na ndo maana walipoingia parking hawakushuka wakawa wanaangalia ni nini kitafuatia

Na ndo maana hawakufanikisha hadhima yao kwa Lisu

Mungu ni mkubwa....[emoji120][emoji120][emoji120]
Na kutokushuka kulisaidia Sana maana wangeshuka wangepigwa za kichwa au kifua na biashara ikaishia hapo. Gari ilisaidia Sana kuweka shield.
 
Back
Top Bottom