Habari wakuu, leo nafikia ukomo wa kiu yangu ya kutaka kuueleza ukweli umma wa watanzania kupitia jukwaa la siasa la JF.
Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu na ikizingatiwa kuwa baadhi ya wagombea wamekuwa wakilitumia tukio la kupigwa risasi kwa aliyekuwa mbunge wa Singida mashariki, Rais wa TLS na sasa mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA, Tundu Antipas Lissu kama ajenda ya kuombea kura huku wengi wakiituhumu serikali ya Tanzania kuhusika na ' jaribio hilo la kumwua' Lissu.
Jambo kubwa la kujijliza ni kuwa kwanini Lissu alipigwa risasi? Kwanini mpaka sasa hakuna mtu anayetuhumiwa na tukio hilo? Kwanini Lissu hashughuliki na kufungua jalada/shauri katika vyombo vya dola vyenye dhamana ya kulinda usalama wa taifa letu?
Haya yote yana maelezo niliyoyapata kutoka vyanzo tofauti vya kuaminika.
Ikumbukwe kuwa wakati tukio hilo linatokea nchi ilikuwa katika kipindi cha sintofahamu juu ya ujio wa ndege iliyokuwa imezuiwa na wadeni wa taifa, pia mvutano kati ya kampuni ya ACACIA mining PLC na serikali juu ya sakata la makinikia. Ni dhahiri kuwa haya yote yalikuwa mzigo mzito kwa serikali ya CCM iliyotaka kujiimarisha kisiasa.
Mbali na kuwa haya yalikuwa yakitokea Lissu hakusita 'kupiga spana' kwa serikali aliyokuwa akiipinga. Kimsingi mwenendo wa matukio ya wakati huo yaliashiria kuhusika kwa serikali katika shambulizi la Lissu lakini ukweli ni huu hapa: Tundu Lissu alikuwa akikaririwa kuwatetea wadeni na ACACIA MINING PLC, huku akitumia taaluma yake ya sheria na weledi wake wa kuwasilisha hoja kuendelea kuikandia serikali.
Alienda mbali zaidi hata kuzitaka nchi wahisani kusitisha misaada nchini na kuomba Tanzania iwekewe vikwazo na nchi hizo. Kufuatia jitihada zake hizo kukwama ndipo tukio la kupigwa risasi 16 likatokea. Naufahamisha umma kuwa Lissu alijaribu kukutana na viongozi waandamizi wa jumuiya ya wawekezaji wa kigeni wa madini nchini na kuingia makubaliano ya kutoa msaada kuhakikisha kuwa mkakati wa udhibiti wa biashara za madini nchini uliokuwa ukitekelezwa na serikali unakwama kupitia upinzani.
Kwa bahati mbaya au nzuri mkakati huo ulishindikana kuzuilika kwa mujibu wa makubaliano aliyoyafanya Lissu na wabia wake hao. Alilipwa kiasi cha fedha kutokana na makubaliano ya awali na wabia wake hao walitakiwa kumlipa 10% ya faida ya madini itakayokuwa inapatikana kwa miaka kumi kama mpango huo ungekamilika.
Ziko taarifa pia watu wanaomwezesha kiuchumi katika uchaguzi huu wamesaini makubaliano kama hayo ikiwa atashinda Urais mwaka huu. Baada ya mpango huo kukwama ndipo bodi ya wakurugenzi wa baadhi ya makampuni ya kigeni ya madini nchini walipojitoa katika makubaliano hayo na kuandaa shambulizi dhidi ya Lissu. Na hapo ndipo serikali iliposhindwa kutoa ushirikiano baada ya kuanza kusakamwa na kutuhumiwa katika shambulizi hilo.
Ili kupata kuelewa mwenendo wa matukio hayo, mambo yafuatayo yanafaa kuzingatiwa:
1. Kwanini Serikali haikumshambulia Dr. Wilbroad Slaa wakati wa vuguvugu la Richmond?
2. Kwanini Serikali haikumshambulia Freeman Mbowe wakati ikitekeleza malipo kwa DOWANS?
3. Kwanini Serikali haijazuia passport ya kusafiria ya Lissu alipokuwa akizunguka nchi kadhaa duniani huku akiipinga Serikali ya Magufuli?
Kwakweli haya yote yangewezekana kutekelezeka kwa namna yoyote lakini hayakufanyika.