Ni nani waliongeza cha juu kwenye manunuzi ya ndege ya mizigo?

Ni nani waliongeza cha juu kwenye manunuzi ya ndege ya mizigo?

Tatizo mahaba yanakupofusha, angalia ripoti ya CAG Toka 2014 ATCL inapata hasara ya mabilioni ya pesa ila hapo katikati tuliambiwa ATCL imepata faida wakatoa na gawio? Halafu Kwa Nini ripoti ikionyesha ubadhilifu wa kuanzia 2016-2020 mnachukia na kusema sio kweli ila ukionyeshwa wa sasa mnafurahi sana
Kumbe na wewe mbumbumbu tu. Huwezi anzisha biashara ukapata faida mara moja. Unafahamu kitu inaitwa Business Plan au unanipotezea muda
 
Tatizo hamkumjua JPM au kwa kutojua au kwa makusudi. Nitaanzisha sredi kuhusu ukweli wake
Sredi utakayoanzisha itakua ni ya kumsifu tu huwezi kuongelea ubaya wake, tatizo mahaba yamezidi ila kiuhalisia CCM haikuwahi kuwa na msafi. JPM alikuwa ni mwizi asiyetaka kushirikisha wenzake, hili hata Kangi Lugola analijua vizuri
 
Ifike mahali mama aache kulalama badala yake achukue hatua sasa. Yeye ndiyo amiri jeshi mkuu, yeye ndiyo mwenye dola, kamata wote weka ndani huku uchunguzi ukiendelea. Atakayebainika filisi mali rudisha hela serikalini iwe fundisho kwa wengine
Hii nchi adui yetu mkubwa ni CCM!!na usitegemee hatua kali kuchukuliwa,yaani mwenye mamlaka naye anatulalamikia sisi sasa tufanyeje?!!nenda kwenye mikopo ya halimashauri huko ilikuwa ni kama mali ya wana ccm,kujigawia tu!!kwa hali hii uje utegemee kuna siku maisha yatakuja kuwa bora?!!Kwanza bora hata hiyo ripoti ya CAG isiwe inafanywa tu kwani ni kutia watu machungu tu!!
 
Si mliambiwa bunge lenu ni dhaifu mkaishia kum harass CAG Prof Assad na kumfurusha ofsini kibabe
Hili bunge hata halieleweki linafanya nini, mambo ya msingi kama haya, tungetamani kuona..kamati za bunge zinawahoji kwa dharula wahusika, tena live bila chenga...
 
Mama kalalamika kwamba invoice ya mwisho ilikuwa tulipe $37,000,000 lakini ikaja invoice ya $86,000,000 ongezeko la zaidi ya asilimia 100 nje ya mkataba wa awali na mama alipohoji akaambiwa spare zimepanda bei.. Je ni nani wanaruhusu malipo ya serikali yatoke? Hawa wafuatao sahihi zao ndio zinahusika
1. Mwanasheria Mkuu wa Serikali
2. Waziri wa fedha
3. Mlipaji Mkuu wa Serikali
4. Gavana wao BoT
5. Waziri wa Uinzi(?) Kwa vifaa vya usalama na jeshi
6. CDF (?) Kwa vifaa vya usalama na jeshi
7. Mkaguzi Mkuu wa Serikali?
8....
9....

Hiyo ndio timu na sidhani kama kuna wengine nje ya hao.. Je mama aliposema kwamba kama huko nyuma walikula hazikuwatosha.. Alimaanisha hawa ama?

Kwa nchi zinazojali utawala wa kisheria katika uhalisia wake nusu ya hao hapo juu kufikia muda huu hawakupaswa kuwepo ofisini
Katibu mkuu wizara ya fedha
 
Hawezi, mkono wa mstaafu uko hapo.

Narudia tena, hawezi.

Hakuna wa kufukuzwa hata mmoja.

Mama kama angekuwa na uwezo huo hakupaswa kutoka na kutuambia. Tulitakiwa tuone watu ni fired bila sisi kujua kinachoendelea. Ndo uongozi.

Mama aliona Magu hana huruma. Akasahau kuwa hii nchi ina wajanja fulani wanaendesha nchi kama choo binafsi.

Atamkumbuka Magu, na nchi ishamshinda. Watu wanapekenyua hadi kilemba chake.
Wamemshauri mheshimiwa Rais Dr Samia achukue uamumuzi wa ajabu kuendelea kutumia fedha ya walipa kodi aunde kamati ya kuchunguza. Ni uozo uleule, wachunguze iishie hewani wasitoe majibu. Nauliza kinachochunguzwa ni nini wakati wahusika wanaopitisha malipo wanajulikana? Nashauri kuwa 1. Mkataba wa kununua ndege uishie hapo na kwa kuwa wauzaji wameonyesha kutokuwa waadilifu, basi warudishe ile down payment.
2. Waliohusika wote wajiuzulu au wafukuzwe kazi.
3. Wapelekwe mahakamani na kulipa gharama yoyote iliyopotezwa na serikali.
4. Vyeti vyao vya masomo, degree, certificates vyote vifutwe.
 
Hii nchi adui yetu mkubwa ni CCM!!na usitegemee hatua kali kuchukuliwa,yaani mwenye mamlaka naye anatulalamikia sisi sasa tufanyeje?!!nenda kwenye mikopo ya halimashauri huko ilikuwa ni kama mali ya wana ccm,kujigawia tu!!kwa hali hii uje utegemee kuna siku maisha yatakuja kuwa bora?!!Kwanza bora hata hiyo ripoti ya CAG isiwe inafanywa tu kwani ni kutia watu machungu tu!!
Na ofisi ya CAG ifutwe tu,gharama ya kuiendesha waendelee kuipiga. Jinamizi linalomaliza nchi hii ni CCM. Siku tukilikwepa hili,tutatoboa. Na kwa ufupi hii nchi haina mwenyewe.
 
Wanamchukulia poa sana.

Ila kama kweli typo serious aanze na yule mkubwa wao amtie discipline wengine wote watarudi nyuma na kuona anamaanisha.
Kama mnadhani WAnasiasa watafungana mtasubiri Sana
 
Mama kalalamika kwamba invoice ya mwisho ilikuwa tulipe $37,000,000 lakini ikaja invoice ya $86,000,000 ongezeko la zaidi ya asilimia 100 nje ya mkataba wa awali na mama alipohoji akaambiwa spare zimepanda bei.. Je ni nani wanaruhusu malipo ya serikali yatoke? Hawa wafuatao sahihi zao ndio zinahusika.

1. Mwanasheria Mkuu wa Serikali
2. Waziri wa fedha
3. Mlipaji Mkuu wa Serikali
4. Gavana wao BoT
5. Waziri wa Uinzi(?) Kwa vifaa vya usalama na jeshi
6. CDF (?) Kwa vifaa vya usalama na jeshi
7. Mkaguzi Mkuu wa Serikali?
8....
9....

Hiyo ndio timu na sidhani kama kuna wengine nje ya hao. Je, mama aliposema kwamba kama huko nyuma walikula hazikuwatosha.. Alimaanisha hawa ama?

Kwa nchi zinazojali utawala wa kisheria katika uhalisia wake nusu ya hao hapo juu kufikia muda huu hawakupaswa kuwepo ofisini.
Rais na yeye anashangaa,wakati wezi kawateua yeye!!!speed aliyotumia kumtumbua Balozi Liberata Mulamula,angeitumia hapa ingekuwa poa sana,
Ccm wanatuchezea maigizo tu,unalalamika kuhusu ufisadi kwenye plea bargain,wakati waliokuwa wanasimqmia,umewapacvyeo na leo ni majaji!harsfu unakuja unalia Lia hapa,huu ni u.....nge kqbisa
 
Yaani watu wezi sana, $ 49 mil ni sawa na fedha zetu tshs 114 bil, watu hawa hawajali kabisa, mimi naona Mama angewafukuza pale pale aliposema waondoke wenyewe, yaani angesema barua zao za kufukuzwa kazi zipo tayari leo baada ya kikao hiki waondoke kabisa wezi hawa wakubwa sana, sbb itakuwa ni chain kubwa ya wapigaji ktk dili hilo
Si mmeambiwa vifaa vimepanda bei?
 
Si mmeambiwa vifaa vimepanda bei?
Tena hao wezi sana, ukifunga mkataba, hakuna tena bei kubadilika kubwa hivyo, toka $ 37 mil hadi $ 86 mil, yaani watu wezi jamani, hawaogopi chochote, Mh. Rais wangu, kamata haraka sana hao, sugu sana, piga ndani, watatajana kila mmoja dili lilikuwa la nani na nani, yaani watakwanbia kila kitu..

Vifaa kwenye ndege ya mizigo, hivi unajua hao wezi walimuona Mama Samia hajui kitu labda, watamuibia haraka walidhania, kumbe Mama kawanasa wazi kabisa.. Naamini leo hadi jioni, watajiuzulu wakurugenzi kadhaa..!!
 
Baada ya ulafi wa mali za umma kuanikwa na CAG, hakika rais wetu Samia anatakiwa asaidiwe pakubwa na kwa haraka, ikiwemo kumwombea Mungu ampe ujasiri, akili na hekima itokayo juu.

Kakwama kabisa na kuishia tu kulalamika na kutukana: "...stupid..., ...pumbavu..."!

Nani ataogopa kuendelea kuiba na kula fedha za umma kwa kulalamikiwa na kutukanwa tu bila kuchukuliwa hatua kali za kinidhamu na kisheria?!

Credit: Gwappo Mwakatobe
Rais Dkt Samia anahitaji kulindwa kwa nguvu zote na kumuombea sana Mungu amlinde maana lile kundi linalipiza kisasi cha kuiba kwa nafasi waliyokosa enzi za Dkt Magufuli.
 
Mama kalalamika kwamba invoice ya mwisho ilikuwa tulipe $37,000,000 lakini ikaja invoice ya $86,000,000 ongezeko la zaidi ya asilimia 100 nje ya mkataba wa awali na mama alipohoji akaambiwa spare zimepanda bei.. Je ni nani wanaruhusu malipo ya serikali yatoke? Hawa wafuatao sahihi zao ndio zinahusika.

1. Mwanasheria Mkuu wa Serikali
2. Waziri wa fedha
3. Mlipaji Mkuu wa Serikali
4. Gavana wao BoT
5. Waziri wa Uinzi(?) Kwa vifaa vya usalama na jeshi
6. CDF (?) Kwa vifaa vya usalama na jeshi
7. Mkaguzi Mkuu wa Serikali?
8....
9....

Hiyo ndio timu na sidhani kama kuna wengine nje ya hao. Je, mama aliposema kwamba kama huko nyuma walikula hazikuwatosha.. Alimaanisha hawa ama?

Kwa nchi zinazojali utawala wa kisheria katika uhalisia wake nusu ya hao hapo juu kufikia muda huu hawakupaswa kuwepo ofisini.
No 7.mkaguzi mkuu kwa maana ya CAG??
 
Back
Top Bottom