Makonda ni very ambitious, ni ngumu sana kutosheka na cheo cha RC, ili kuwa na vyeo venye power kubwa zaidi kama Uwaziri njia ya uhakika ni kuwa mbunge.
2020 alikurupuka ila round hii itakuwa kajipanga vilivyo
swali, je atatumia jimbo gani?
Ni ubovu tu wa katiba au kijitabu tu.
Lakini tungekua na katiba bora Wakuu wa mikoa ni watu wenye power kubwa kuliko Wabunge.
Wakuu wote wa mikoa wangekua kama Makondo nadhani tungesogea sana mana huko Halmashauri ndiko mijihela ya umma inapoliwa na mchwa wa CCM.
Wabunge watenganishwe na uwaziri halafu wakuu wa mikoa wachaguliwe kwa uwiano sawa na nafasi zao ziwekwe wazi watu waombe kwa miaka mitano kwa mkataba maalumu kama wasimamizi wa serikali kwenye mikoa na wawe na nguvu kubwa baada ya kuchaguliwa ila wafuate sheria.
Makonda akiendelea kubaki CCM atapoteza heshima yake baada ya 2025 kutokana na mnyukano mkubwa uliopo ndani ya chama chake.
Tatizo ya siasa za Afrika na hasa Tanzania ni siasa za chuki na roho Mbaya.
Bila kujua kuwa hakuna mtu mwema ndani ya CCM kutokana na mfumo wa katiba na chama kuwa chama dola.Hali hiyo inawalazimisha CCM wote kuwa watu wenye Roho Mbaya na wenye uchu wa madara na kujilimbikizia mali kwa njia halali na haramu kwa sababu ya kujihakikishia usalama .
Lakini kiuhalisia Makonda ni mtu jasiri mwenye uzalendo na kuipenda nchi yake sana.
Sasa mtu kama yule angefaa sana kuungana na Wapinzani lakini Wapinzani wanauadui na visasi sana kwa mtu mmoja mmoja badala ya mfumo na chama cha CCM ambacho kwa hakika kinaandaa watu waovu tangu wakiwa watoto wadogo yaani Chipukizi.
Chipukizi hawana tofauti na magaidi kwa roho mbaya walizo nazo. Wanaandaliwa kijeshi kupigania na kutetea kila uovu unaofanywa na serikali ya CCM .
Wapinzani nao wameambukizwa roho ya visasi bila kuangalia kuwa bila kuisambaratisha CCM hakuna njia ya kuingia madarakani kamwe.
Yaani watu wanajua wazi kuwa JPM yupo kwenye mioyo ya Watanzania wengi sana kuanzia alina mama ,vijana na hata Watoto Afrika nzima lakini bado mtu anapanda Jukwaani na kuanza kuporomosha matusi na kumdhihaki Marehemu JPM. Huu ni ujinga mkubwa sana. Binafsi sikuwahi kumuunga mkono wakati wa uhai wake akiwa Rais kutokana na kuwa sikupenda CCM ishinde lakini nikimlinganisha na watawala wa Afrika leo nimemsamehe 100% na Mungu ampe pumziko la Amani.
Hata ukiangalia umati wa watu mpinzani akimponda JPM unaona wazi nyuso za watu zinabadilika .
Siasa ni Sayansi ya kuteka akili za watu kwenye jamii.
Utaishindaje CCM inayowatumia wale wale inaowachukia kujijenga.?
Fursa ya kuotoa CCM madarakani ni Mwaka Kesho tuu baada ya hapo CCM itajivua gambaa na kuja na mtu maarufu na anayekubalika kuliko Wapinzani.
Wanaweza hata wakammchukua Mpina alimradi wabaki madarakani kama ni kumstaafisha watamstaafisha baada ya ushindi ili tu walinde mali zao na sio chama kingine.
Wapinzani jifunzeni kusamehe na kuteka silaha za adui na kuzitumia kummaliza. Covid 19 wakiomba msamaha wajadiliwe na kurudishwa kundini kwa masharti ya kupigania chama kwa nguvu zote . Tunatamani kuona serikali ya umoja wa kitaifa kulinda amani na umoja wetu na sio kuhodhi madaraka yote kama CCM.
Lisu atapata jeshima kubwa kumsalehe JPM kisiasa kuliko kumshambulia marehemu .Muda wote wakati jamii haikubaliani na mtu anayemhukumu Marehemu.
Hali kadhalika Mbowe . Sameheni kwa sababu Mungu ndiye aliyewapa nyie uhai kwa sababu zake yeye na sio nyie . Alimleta JPM ili watanzania waamke wajue kuwa nchi yao inaiibiwa sana.
Mwamko wa Watanzania ni kwa sababu ya JPM ndio maana wanampenda Makonda na Mpina na hata Lisu kwa misimamo ya kupigania rasilimali nchi . Magufuli alikuja kwa muda mfupi kuwaamsha watu na ndiye kitanzi cha kuinyonga CCM.