Ni sahihi fundi kupiga picha kazi aliyopewa aifanye, na kuitumia kujitangaza bila makubaliano na mwenye kazi?

 
Je,isipokuwa ni tu niione kesho,unadhani pesa unayotoa ni sawa na kazi alokufanyia?
Maisha ya kiafrika ni kubangaiza,acha wajitafutie! Unadhani wanakuja kwako kwa sababu wanajiweza? We mbona unawatumia hao,kilikushinda nini kuleta kampuni kubwa isiyo na haja na hizo picha!?
 
So sahihi kwani mkataba wenu ulikuwa yeye afanye kazi na wewe umlipe alichofanya ni kinyume cha Sheria. Mkataba sio lazima uwe wa maandishi.
 
Mpeleke mahakamani ,mahakamani ndio inatoa ufafanuzi wa makosa cc raia hatuna umahiri wa maswala ya kijeshi
 
Ni sahihi ila unatakiwa uwe unawaambia mapema kwamba naomba Kaz zangu zisiende online, kwa mfano wewe mwenyewe ulivyokuq unatafuta photographer nadhan uliingia mitandaoni kuangalia ubora wa wapiga picha
 
Hapo haifai yaani ni km mm nimenunua malaya nikamzagamua then nikamlipa.... Halafu baadae aje aweke mtandaon kujibrand mizagamuo anayotoa... Sio vzr coz yeye anapata faida wakati jamii itaniona mm km mcheza x
Huu mfano umenichekesha sana🤣
 
Ni sahihi ila unatakiwa uwe unawaambia mapema kwamba naomba Kaz zangu zisiende online, kwa mfano wewe mwenyewe ulivyokuq unatafuta photographer nadhan uliingia mitandaoni kuangalia ubora wa wapiga picha
Sahihi kabisa. Niliangalia ubora wake lakini ilibidi anishirikishe kwamba naweza kutumia picha yako kwa matangazo?? mimi nimpe greenlight na sio mimi ndio nianze kumwambia asitumie picha zangu.

Pia angetaka kutumia picha zangu ilibidi nilipe kidogo. Ukiona picha za watu maarufu zinatumika ujue hao wapiga picha wanawapiga picha bure kwa lengo la kujitangaza. Hawalipwi hata shilingi.

Ukiona watu wa hotels wanasema mtu fulani kalala hotel kwetu ujue huyo mtu alipewa malazi bure kwa malipo ya kutangaza hiyo hoteli.

sasa nikulipe pesa yangu na bado unianike mitandaoni na hapo mimi mwejyewe hata kuziweka mitandaoni bado?
 
Apo kwenye kutumia picha yako bila idhini yako aliyumba pakubwq mno , ila kama picha ya nyumba au furniture anything ambayo haita reveal location yako au faragha io ukikataza utakua mkoloni mkuu
 
Huo mchoro / muundo umeusajili au na wewe umeuona mahali ukaupiga picha?

Mafundi wengi wanapiga picha kazi zao kwa sababu ni ubunifu wao wenyewe.
Hii ndio ile unakuta mtaa mzima mna vitu vimefanana hadi unajiuliza hizi ni nyumba za shirika au?
 
Mwaka jana Diamond aliingia kwenye mgogoro na muuza nguo chidi.

kisa diamond alinunua nguo kwq chid na akalipa hela kama inavyotakiwa ila kila diamond akivaa hizo nguo akipiga picha , jamaa muuza nguo anazichukua anapost kwake anaandika "amevalishwa na mimi".

Diamond akamwambia kama ulitaka kunitumia kupata wateja nisingelipia hizo nguo ilibidi unipe bure ila kwakuwa nimenunua hauna haki ya kutangazia watu nimenunua kwako.

mimi niliona ana point pia. Privancy ni muhimu
 
Kwangu mimi ni sahihi maana hapa nipo naangalia viti vya dining kwenye mtandao bila hata kulipia waliotengeneza...
sawa mkuu lakini kumbuka wengi wanaoweka mitandaoni ni design zao. Wamedesign wao. wao ni madiaigner.
na lengo ni kutengeneza hela.

sasa ngoja siku wewe upate design yako kwa lengo la kuwa unique umpe fundi kazi kisha akiipatia aanze kuwajengea hiyo design mtaa mzima ndio utajua haujui🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…