Ni smart TV gani 4K kwa sasa ipo vizuri sana?

Ni smart TV gani 4K kwa sasa ipo vizuri sana?

Pia watu wafanyabiashara hawakupeleki Samsung sababu ya Margin ni ndogo hasa maneno yenye competition.

Mfano tv ya kichina ni 250,000 wanaweza wakauza 450,000 margin kubwa, ila Samsung wanapata 550,000 wanauza 600,000.

Samsung wapo official kabisa Tanzania, sidhani kama kutoa mstari ni issue, ukiwa na warranty na unajielewa wataitengeneza bure.

Nakubaliana nawewe chief, ila kumbuka pia me naongelea muuzaji ambae mnajuana au ambae umeunganishwa nae, kama unafanya biashara utaelewa kuwa kuna baadhi ya biadhaa huwezi kabisa kumpa mtu wako wa karibu bali unasubiri mtu baki umpe

Lakini pia kariakoo ndio iko hivo ata siku moja huwezi kuuziwa kitu chenye shida endapo unafahamika sehemu husika au umeagizwa na mtu ambae anajulikana hapo

Ni kweli kabisa kuwa bidhaa nyingi za ubora mdogo zinakuwa na faida nzuri na watu tunapenda ziwe na mazunguko mzuri ili faida iwe maradufu, ila kamwe huwezi kumuuzia hiyo biadhaa mtu unaemjua unless otherwise offer yake ndio iliishia hapo na pamoja na kumuelewesha atauziwa bei ndogo zaidi ya anayouziwa mwingine

Na issue ya kununua Samsung kutoka official store ni watu wachache sana mkuu, wengi wananunua kariakoo na wanapewa warranty pia Ila issue inakuja ni huo mstari, ni ngumu kuamini kuwa TV imejichora tu mstari bila physical approach

Ata ukisoma warranty wanasema kuwa wataripea endapo tu kifaa chako kimezingua "malfunctions under normal operation" sasa wengi ambao wananunua TV kariakoo hawatengenezewi Kwa sababu hiyo

Huwezi kumwambia muuzaji eti nimekuta tu TV yangu imeweka mstari, hapo kivyovyote vile hiyo utarudishiwa wewe, utaambiwa uliigonga,uliweka kitu kizito, ulifunga ukutani ikacheza ghafra nk, in short ndo inakuwa imekula kwako na warranty yako
 
Hizi ndio shule nilikuwa nahitaji mpaka kufunguwa huu Uzi.

Mkuu kwa kunisaidia nimebaini LG wako vizuri ingawa hawakuwa mawazoni kwangu kabisa, Sasa nataka nijilipuwe na LG.

Kwa Sasa LG hiyo Qled ya inch 43 inakwenda kwa bei gani na authorized agent au dealer anapatikana wapi?
LG hawana Qled... Qled ni technology ya Samsung.

LG wana Nanocel na OLED.
 
We jamaa Xiaomi naye anazo simu expensive. Watu wengi wanaojaribu kuelezea hii mada kupitia reference ya simu naona wanaboronga. Hata Samsung ana A series ambazo ni simu za chini na kati ndio kama hizo TV zao za laki sita. Kama bajeti ni laki sita na nusu nunua Hisense

Mkuu nimejibu kulingana na ubora wa bidhaa tunazozipata zaidi Tz

Najua kama zipo Xiaomi kali
Hizo TLC na Hisense zinazo kuja bongo ni za kichovu kama Xiaomi zinazopatikana kwa wingi huku
Jamaa wana product zinacompete na wakina LG, Sony Philips nk

Haya Samsung tv nyingi zinazokuja huku sio zile zenyewe ni za quality ya chini
 
Wadau nilikuwa na smart TV 4 K nchi 50 wale wajaa laana wakasepa nayo.

Nina Samsung Hd nchi 32 ilikuwa chumbani ndio nimeileta sebuleni yani tofauti ni kubwa sana.

Sasa nimeokota pochi la mzungu nataka ninunue TV ya kweli nirudi kwenye modern life.

Karibuni kwa ushauri.
Hama kwanza unapokaa kama ni Nyumba ya kupanga la sivyo utaibiwa Tena. Kama ni Nyumba Yako boresha ondoa mazingira yote yanayotoa gepu Kwa wezi na pia ongeza ulinzi. Ukishindwa kufanya hayo hiyo mpya utayonunua au hata hiyo 32 itaibwa tena
 
Ni bajeti yako tu mkuu

Wale wachovu wenzangu wanakwenda na Boss, StarX
Hizi ni sawa na watumiaji wa simu wa Tecno, Itel, infinix

Wale wa uchumi wa kati wanakwenda na Hisense, TLC
Hizi ni sawa na watumiaji wa simu za Oppo Xiaomi nk

Wale wanaojiweza wanakwenda na Sony LG Samsung Apple Tv
Hizi ni sawa na watumiaji wa simu za Samsung iPhone nk
Apple tv ndo tv gani hiyo?..

Apple walichonacho sio tv box tu?
 
Humu naona watu wana bwabwaja tu wala hawatoi jibu la kueleweka. Hawa TV manufacturers wote wana TV za level mbali mbali kwa budget mbali mbali. Mfano LG zipo za kawaida, nanocell, QNED,OLED etc! sasa wewe unapomwambia mtu nunua LG/samsung/Sony/Hisense ndio bora! Ni LG ipi? na ni bora kuliko hisense ipi? Maana hisense wana za kawaida, ULED (QLED/ Mini LED) etc! Mshauri mtu kwa specific model kutokana na budget yake lakini si kulinganisha the whole brand
Watu wanajiropokea tu.."Sony kali,sony kali..bila hata kusema ni type ya sony.
 
Watu wanajiropokea tu.."Sony kali,sony kali..bila hata kusema ni type ya sony.

Kuna watu wa ajabu sana aisee, kazi yao huwa kukosoa tu na hawatoi huo ushauri wanao ona upo sahihi

Brand ndio kitu cha kwanza bana haswa kwa mtu anayesema ameokota pochi na anataka Tv kali

Sasa wewe unataka tuanze kumwambia habari za Boss na StarX tulizo nazo ambazo zinajibadilisha chaneli bila kuguswa [emoji23][emoji23]
Wengine hizo tv wala hatuna tunasoma reviews

Hizo alizotajiwa ndio brand nzuri kwa mwenye hela zake
Mambo ya nchi ngapi atajiongeza mwenye
 
IMG_0475.jpg



Nano cell price from authorized dealer+warranty
 
Nilipoanza kununua flat TV nilianza na LG ya LED 43" ila aliporudi mbabe wa kioo bwana Hitachi kwa jina la TCL sikujishauri kuvuta smart TV ya 55" kwao, kutokana na durability ya product zao. Nna imani hiki kioo kitapiga kazi kwa hadi miaka 15 mbele bila tatizo (kuna tv ya Hitachi ya 21" ilinunuliwa na dingi 1998 na mpaka sasa inapiga kazi, imekuwa inahama vyumba tu pale home na kwa sasa iko ghetto la msaidizi wa kazi wa home ikiwa haijachora hata mstari mmoja)
 
Nilipoanza kununua flat TV nilianza na LG ya LED 43" ila aliporudi mbabe wa kioo bwana Hitachi kwa jina la TCL sikujishauri kuvuta smart TV ya 55" kwao, kutokana na durability ya product zao. Nna imani hiki kioo kitapiga kazi kwa hadi miaka 15 mbele bila tatizo (kuna tv ya Hitachi ya 21" ilinunuliwa na dingi 1998 na mpaka sasa inapiga kazi, imekuwa inahama vyumba tu pale home na kwa sasa iko ghetto la msaidizi wa kazi wa home ikiwa haijachora hata mstari mmoja)
Hitachi na TCL Mbona hamna uhusiano wowote?
 
Mimi natumia sundar inatumia umeme mdogo kioo ni 4k harafu inakuja na screen protector wenyewe wanaita double screen. Tatizokubwa sio multpurpose yani huwezi kuchart whatsap huku unasikiliza mziki wa kwenye tv hiyo iyo. Harafu mda mwingine ni kama inazidiwa uwezo kama nikiitumia kuchat na kubrowse mtandaoni ila kwa kutizama movie tu ama kusikiliza music hii tv ni nzuri sana. Kwenye application za smart tu ndio ina kera sana
 
Mkuu nimejibu kulingana na ubora wa bidhaa tunazozipata zaidi Tz

Najua kama zipo Xiaomi kali
Hizo TLC na Hisense zinazo kuja bongo ni za kichovu kama Xiaomi zinazopatikana kwa wingi huku
Jamaa wana product zinacompete na wakina LG, Sony Philips nk

Haya Samsung tv nyingi zinazokuja huku sio zile zenyewe ni za quality ya chini
Nikweli Samsungu zinazo kuja Tanzania siyo zinazo kwenda Ulaya, we jaribu kutafuta Samsung ya Ulaya na Ya Tanzania utaona utofauti kwenye Menu, Samsung zaki bongo hazina mambo mengi yani ata mshamba anaweza kuichezea na akiifahamu kwa haraka
 
Ukianzia Mwanzo wa thread mpaka hapa tayari jibu unalo na tofauti ya hizi tech sijui HD, Qled, 4K Dolby sijui nini nini kwenye upande wa TV tayari una muongozo nzuri ujilipuwe wapi.

Binafsi naona nilijilipuwe na LG ila kuna mdau kanitisha hapo anadai remoti ya LG ikiharibika inauzwa laki mbili, huu nao ni mtihani kwa sisi wenye Watoto ambao bado watundu.
Nilinunua remote ya LG Home Theater (watoto waliharibu) kwa bei ya kawaida kabisa pale Kariakoo, labda hizo za Tvs zinaweza kuwa juu. Ukipata latest tech ya LG nadhani utafurahia hata kuangalia TV yako.
OLED/QLED/NANO tech.
A7/A9 Al processor.
 
Ukianzia Mwanzo wa thread mpaka hapa tayari jibu unalo na tofauti ya hizi tech sijui HD, Qled, 4K Dolby sijui nini nini kwenye upande wa TV tayari una muongozo nzuri ujilipuwe wapi.

Binafsi naona nilijilipuwe na LG ila kuna mdau kanitisha hapo anadai remoti ya LG ikiharibika inauzwa laki mbili, huu nao ni mtihani kwa sisi wenye Watoto ambao bado watundu.

mkuu kuna remote pia ya elfu 30 inafanya kazi zote isipokuwa sio magic. so nyumba kama ina watoto hakikisha magic remote inafichwa
 
Nunua Original Samsung TV ya Series yoyote , amini hautajutia kwa ubora wake.Nina Samsung 32 inch niliinunua 2013 kwa authorized Samsung dealer naitumia hadi leo haijawai kuwa na tatizo lolote.
 
Mimi TV yangu ya kwanza nilinunua Sharp from Hong Kong tv nzuri sana ila ilikuwa na changamoto joto likiwa kali inachemka na baada ya dakika inajizima, nikaja kuisoma vizuri nyuma imeandikwa kwa matumizi ya Hong Kong tu kwa joto la bongo ikawa inachemka inaandika High temperature ikawa inajizama.Tv ya pili nikanunua Blackstone lakini sikuipenda ilikuwa haina mambo mengi ni ya kawaida ikabidi niipigee bei , kwa sasa nina Sony bravia hii ipo vizuri kisasa zaidi naweza muiwasha masaa 24 na isiwe ya moto ata ukiishika nyuma aiwi ya moto
 
Back
Top Bottom