Ni taarifa gani Hayati Ally Kibao alikuwa nazo kiasi cha kuepelekea kifo chake?

Ni taarifa gani Hayati Ally Kibao alikuwa nazo kiasi cha kuepelekea kifo chake?

Watu wengi walisema mabaya kwa JPM ila n miaka zaidi ya miwili sasa JPM hayupo ila matendo maovu yanaendelea, ndio tujue JPM hakuwa tatizo bali n mfumo mzima wa serikali.

Haya mambo hata kwa Nyerere yalikuwepo.
Sasa kwa nini hawabadili mfumo??
 
Ndio alisingiziwa.
Kama hajasingiziwa, mbona hayo mambo bado yanaendelea?
Taratibu. Alifanya na hayo mambo yanaendekea. Neno “alisingiziwa” halihusiki hapo. Au unataka kusema serikali haihusiki hata sasa?
 
Taratibu. Alifanya na hayo mambo yanaendekea. Neno “alisingiziwa” halihusiki hapo. Au unataka kusema serikali haihusiki hata sasa?
Kwahy nani anayaendeleza hayo mambo wakat JPM amekufa zaidi ya miaka miwili sasa?
 
Kwahy nani anayaendeleza hayo mambo wakat JPM amekufa zaidi ya miaka miwili sasa?
Correct. Na sio hayo tu, anaendeleza mengi ya JPM kujiimarisha madarakani.

Nyerere mwenyewe alilalamika warithi wake kuendeleza “mabaya” yake na kuacha “mazuri” yake. Ndiyo jadi yetu.
 
Hapa kuna jambo la kukumbuka, mauwaji ya namna hii yanayohusisha tindikali, kuharibiwa uso vibaya sana sio mauwaji yanayofanya na polisi au serikali,

Kumbukumbu zinaonesha Mauwaji ya namna hii yamefanywa na Chadema dhidi ya wafuasi wake waliowatoa kafara ushahidi ni matamshi ya aliekuwa Katibu Mkuu wa Chadema Dr. Silaha.


Ni wakati umefika wa Watanzania Kuyatazama mambo kwa mapana zaidi ya hisia zetu ni mihemko ya wanasiasa.


Sina shaka kwamba Polisi hawawezi teka mtu mkubwa kisiasa kama alivykuwa Alli Kibao halafu wakafanye ujinga wa kitoto kiasi kile eti wateke hadharani wauwe na kutelekeza maiti hadharani hii sio polisi ya Tanzania..
Kwa hiyo Chadema wako vizuri zaidi kuliko serikali na vyombo vyake vyote vya ulinzi na usalama!!! Mbona ni kama unaidharirisha serikali aisii!! Kwamba intelenjensia yote imezidiwa na Chadema!!! Acha kuizodoa serikali yenu bwana!!
 
Watu wengi walisema mabaya kwa JPM ila n miaka zaidi ya miwili sasa JPM hayupo ila matendo maovu yanaendelea, ndio tujue JPM hakuwa tatizo bali n mfumo mzima wa serikali.

Haya mambo hata kwa Nyerere yalikuwepo.
JPM kama angekuwa na nia njema na Tanzania, angeubadili huo mfumo mzima wa serikali.
 
Hapa kuna jambo la kukumbuka, mauwaji ya namna hii yanayohusisha tindikali, kuharibiwa uso vibaya sana sio mauwaji yanayofanya na polisi au serikali,

Kumbukumbu zinaonesha Mauwaji ya namna hii yamefanywa na Chadema dhidi ya wafuasi wake waliowatoa kafara ushahidi ni matamshi ya aliekuwa Katibu Mkuu wa Chadema Dr. Silaha.


Ni wakati umefika wa Watanzania Kuyatazama mambo kwa mapana zaidi ya hisia zetu ni mihemko ya wanasiasa.


Sina shaka kwamba Polisi hawawezi teka mtu mkubwa kisiasa kama alivykuwa Alli Kibao halafu wakafanye ujinga wa kitoto kiasi kile eti wateke hadharani wauwe na kutelekeza maiti hadharani hii sio polisi ya Tanzania..
Daah!!!
Wewe kweli ni kilaza wa kwanza.
 
Nitakua mtu wa mwisho kuamini kua mauaji ya huyu ndugu yetu ni serikali yetu ya mama imeshiriki. Wahuni ni watu wabaya sana wanatumia mbinu zote kumchafua mama lakini mwisho wa yote watashindwa tu. Huu utekaji umeshamiri sasa hivi baada ya wahuni kutimuliwa kwenye baraza la mawaziri. Ila kwa vile wabongo wengi ni wapumbavu wataamini ni serkali ndio imefanya upuuzi huu.

Unachowaza na kufikiri ni kweli na ni sahihi...

Lakini unafikiri serikali (Rais Samia), Bunge na mahakama itakwepaje lawama iwapo hawachukui hatua stahiki kukomesha mauaji haya...?

Si ndiye Rais Samia huyu huyu alibeza malalamiko ya wananchi waathirika wa matukio haya kwa kusema "hizo ni drama tu.......??"

Kwa kauli hii ya Rais kwanini tusiseme kuwa kumbe serikali na vyombo vyake (polisi & TISS) ndiyo wahusika wa matukio haya kisha wanaenda kwa Rais na kumpa taarifa za uongo na kumfanya Rais aonekane kituko kwa raia...?

SIKILIZA BWANA: Rais anayo njia nzuri na salama kuitumia kuwang'amua hawa unaowaita wahuni iwe wapo ndani ya vyombo vya serikali kama polisi, TISS, jeshini, Baraza la mawaziri au wakiwa nje ya vyombo vya serikali....

Njia yenyewe ni Rais kutumia mamlaka yake ya U - RAIS, AMIRI JESHI WA MAJESHI YA ULINZI NA USALAMA, MKUU WA SERIKALI na zaidi MAMLAKA YA KIKATIBA kuunda kamati huru maalumu ya uchunguzi ya kijaji ili ichunguze mambo haya na kumpa ripoti....

Kamati haipaswi kuwa na polisi wala TISS maana hawa ndiyo wanatuhumiwa. Kwa kuwa wanatuhumiwa, hawataweza kujichunguza wenyewe badala yake wachunguzwe ili wasafishwe au watiwe hatiani kama wanahusika na Rais mwenye atajua cha kuwafanya kwa mujibu wa katiba....
 
Back
Top Bottom