Ni taarifa gani Hayati Ally Kibao alikuwa nazo kiasi cha kuepelekea kifo chake?

Watu wengi walisema mabaya kwa JPM ila n miaka zaidi ya miwili sasa JPM hayupo ila matendo maovu yanaendelea, ndio tujue JPM hakuwa tatizo bali n mfumo mzima wa serikali.

Haya mambo hata kwa Nyerere yalikuwepo.
Sasa kwa nini hawabadili mfumo??
 
Ndio alisingiziwa.
Kama hajasingiziwa, mbona hayo mambo bado yanaendelea?
Taratibu. Alifanya na hayo mambo yanaendekea. Neno “alisingiziwa” halihusiki hapo. Au unataka kusema serikali haihusiki hata sasa?
 
Taratibu. Alifanya na hayo mambo yanaendekea. Neno “alisingiziwa” halihusiki hapo. Au unataka kusema serikali haihusiki hata sasa?
Kwahy nani anayaendeleza hayo mambo wakat JPM amekufa zaidi ya miaka miwili sasa?
 
Kwahy nani anayaendeleza hayo mambo wakat JPM amekufa zaidi ya miaka miwili sasa?
Correct. Na sio hayo tu, anaendeleza mengi ya JPM kujiimarisha madarakani.

Nyerere mwenyewe alilalamika warithi wake kuendeleza “mabaya” yake na kuacha “mazuri” yake. Ndiyo jadi yetu.
 
Kwa hiyo Chadema wako vizuri zaidi kuliko serikali na vyombo vyake vyote vya ulinzi na usalama!!! Mbona ni kama unaidharirisha serikali aisii!! Kwamba intelenjensia yote imezidiwa na Chadema!!! Acha kuizodoa serikali yenu bwana!!
 
Watu wengi walisema mabaya kwa JPM ila n miaka zaidi ya miwili sasa JPM hayupo ila matendo maovu yanaendelea, ndio tujue JPM hakuwa tatizo bali n mfumo mzima wa serikali.

Haya mambo hata kwa Nyerere yalikuwepo.
JPM kama angekuwa na nia njema na Tanzania, angeubadili huo mfumo mzima wa serikali.
 
Daah!!!
Wewe kweli ni kilaza wa kwanza.
 

Unachowaza na kufikiri ni kweli na ni sahihi...

Lakini unafikiri serikali (Rais Samia), Bunge na mahakama itakwepaje lawama iwapo hawachukui hatua stahiki kukomesha mauaji haya...?

Si ndiye Rais Samia huyu huyu alibeza malalamiko ya wananchi waathirika wa matukio haya kwa kusema "hizo ni drama tu.......??"

Kwa kauli hii ya Rais kwanini tusiseme kuwa kumbe serikali na vyombo vyake (polisi & TISS) ndiyo wahusika wa matukio haya kisha wanaenda kwa Rais na kumpa taarifa za uongo na kumfanya Rais aonekane kituko kwa raia...?

SIKILIZA BWANA: Rais anayo njia nzuri na salama kuitumia kuwang'amua hawa unaowaita wahuni iwe wapo ndani ya vyombo vya serikali kama polisi, TISS, jeshini, Baraza la mawaziri au wakiwa nje ya vyombo vya serikali....

Njia yenyewe ni Rais kutumia mamlaka yake ya U - RAIS, AMIRI JESHI WA MAJESHI YA ULINZI NA USALAMA, MKUU WA SERIKALI na zaidi MAMLAKA YA KIKATIBA kuunda kamati huru maalumu ya uchunguzi ya kijaji ili ichunguze mambo haya na kumpa ripoti....

Kamati haipaswi kuwa na polisi wala TISS maana hawa ndiyo wanatuhumiwa. Kwa kuwa wanatuhumiwa, hawataweza kujichunguza wenyewe badala yake wachunguzwe ili wasafishwe au watiwe hatiani kama wanahusika na Rais mwenye atajua cha kuwafanya kwa mujibu wa katiba....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…