Ni wakati sasa benki zitanue 'ukomo' wa kutoa pesa kwenye ATMs, milioni moja haitoshi

Ni wakati sasa benki zitanue 'ukomo' wa kutoa pesa kwenye ATMs, milioni moja haitoshi

Kuingia ndani ni kwa muda wa mchana tu, pesa hailali mkuu…. kuna dharula sio za kusubiri.

Fikiria hilo pia.
Benki sio pochi useme kila unapohitaji pesa utaifungua! Benki unahifadhi kwa ajili ya dharula. N

Nafikiri ni salama zaidi kwenda ndani kuchukua kiasi chochote cha pesa kuliko kwenda ATM kuchukua kiasi kikubwa cha pesa!
 
Mimi ningekua DC ningekua natafuta watu kama nyinyi mnaoyeyusha M kaunta ili tueleweshane inakuaje kuaje.

Role model Ole.
 
Uongo!

Sio kwamba wanaifunga, bali inabadilishwa ‘tariffs' na hivyo unaondolewa zile benefits za ChapChap.
si uongo imenitokea, niko mkoa mwingine kikazi nikafungua chapchap kwa vile benki niliyokuwa nikitumia hawakuwa na tawi pesa ilipoingia wakanitumia sms kuwa akaunti yangu imevuka tsz milioni tano niende na kitambulisho na barua ya mtendaji ndani ya siku kumi na nne ili niendelee kuitumia nikaenda na nimefuata walivyotaka sasa ni wiki bado hawajaifungua na kwa kuwa niko field mbali na eneo ilipo benki nimepiga namba 08002002 ambayo ni toll free sijapata msaada sasa kama wewe ni mfanyakazi wa hapo shughulikia hilo maana isije ziakapita hizo siku kumi na nne ili mnisumbue zaidi
 
Unaweza kuomba kuongeza ukomo wa kutoa pesa kwenye Atm ,
Crdb kwa mfano limit nadhani mil 2 by default , again bado unaweza kuomba kuongeza Atm withdrawal amount.
 
Simbanking by haikuwepo? Ukiwa na simbanking ukifika ukomo kwenye ATM unaendelea kuchakata miamala kuhamisha Mobile Mpesa etc
That's the most expensive destination you can be . Simbanking ni options kwa walio mbali na huduma za kawaida, vijijini huko !

Muamala wa kutoa laki nne Atm, unagharimu sh 1200 Ukitoa milion kwa wakala , utachajiwa sh 8000. Ilihali ukitumia Atm itakuwa sh 3600. Kuna baadhi ya Atm za crdb zinatoa hadi laki sita , milion unatoa mara mbili tu kwa sh 2400.
 
That's the most expensive destination you can be . Simbanking ni options kwa walio mbali na huduma za kawaida, vijijini huko !

Muamala wa kutoa laki nne Atm, unagharimu sh 1200 Ukitoa milion kwa wakala , utachajiwa sh 8000. Ilihali ukitumia Atm itakuwa sh 3600. Kuna baadhi ya Atm za crdb zinatoa hadi laki sita , milion unatoa mara mbili tu kwa sh 2400.
Hilo jibu nilimpatia kama jawabu la kufikia ukomo wa kutoa kwa ATM bado fursa ya kutumia njia ya simbanking ipo kunusuru dharura husika.
 
Kaka mkubwa unaweza kuwa na kundi la wadogo zako mmepata dharula, pesa ipo, lakini ATM limit ikasumbua.

Nakumbuka kuna siku miaka kama 10 imepita nilikuwa nakwenda Zenj na kundi la wadogo zangu. Sasa hapo mimi nimerudi likizo nimekuwa kama mgeni tena jijini kwangu Dar. Tukawa na safari ya utalii wa ndani Zanzibar.Nikawa nawahimiza tuwahi kwenda bandarini. Wao wanasema tuna muda, mbona unakuwa kama umesahau Dar ndogo hii.

Nikawaambia sitaki tuchelewe. Nikaambiwa haina noma.

Long story short, tumeondoka nyumbani, tukakutana na foleni barabarani. By the time tunafika bandarini tukawa tumechelewa meli. Na tunatakiwa kwenda Zanzibar usiku huo huo.

Tukaulizia options, tukaambiwa hapo ni kuwahi airport kupanda ndege tu.

Tukafika Dar airport kupiga mahesabu nauli kwa wote ikawa kama laki tano.

You can imagine watu wangekuwa wamezidi mara mbili nauli ingekuwa zaidi ya milioni, hela ipo, halafu unashindwa kuitumia.

Naelewa kuna rationale ya kuweka hii limit, mfano kama mtu anafanya wizi kwenye ATM asiibe zaidi ya milioni. Lakini, kama mtu ana hela nyingi na biashara nyingi, awe na uwezo wa ku evaluate risk, akiikubali risk awe na option yana kuongeza limit.

Nafikiri benki nyingi zina option hiyo.
Mkuu ni suala la kwenda benki na kuomba kadi yako wairuhusu iwe inatoa kiasi gani ndani ya masaa 24 ,mie yangu nilipoenda niliomba iwekwe unlimited ila vigezo na masharti yangu nilipewa kiwango cha 2.5 m
 
Ndugu zangu!

Sijui vigezo walivyozingatia kwenye kuweka ukomo huo, lakini itoshe tu kusema zama zimebadilika sana.

Enzi hizo milioni iliitwa 'shitabalwa' [uncountable], na ilitosha kwa mambo mengi kwa walio wengi.

Tofauti kabisa na leo ambapo milioni MOJA unaweza kukaa kaunta tu ikayeyuka, pesa imezoeleka kwa wengi na imekuwa na matumizi mengi kirahisi.

Napendekeza angalau tuweze kutoa milioni TATU kwa siku kupitia ATMs, na 'mshindo' mmoja uweze kuvuta hadi MILIONI MOJA [emoji39]

Nasema uongo ndugu zangu?
Ama kweli mama anaupiga mwingi, hizi nyuzi hazikuwepo miezi kadha wa kadha iliyopita na kama zingekuwepo zingehusu kupunguza mwamala.
 
Back
Top Bottom