Ni wakati sasa kwa Serikali kumuomba radhi Tundu Lissu aliyeshauri mapema kuachana na madai ya Barrick

Ni wakati sasa kwa Serikali kumuomba radhi Tundu Lissu aliyeshauri mapema kuachana na madai ya Barrick

Kuwa kiongozi Jamhuri ya wadaganyika hata kichaa inawezekana tu ,Leo hii wote waimba mapambio sijui wataficha wapi sura zao au na wao watacheza kulingana na mdundo unavyopigwa ?

Cha kutuokoa kama nchi ni katiba mpya tu vinginevyo tutakuwa tunaendelea hatua tatu mbele halafu tunakuja rudi nyuma hatua hamsin
 
Kwa hiyo mtu akiwa na PhD akiongea/kuandika ujinga uitwe werevu kisa yeye amesoma ana PhD?
Mm nasema hapana ujinga ni ujinga hata kama mtu ni mzee,ana digrii milioni tuwe wakweli kuna wasomi nchi hii ni mizigo na useless kabisa.
Ni afadhali useme ukweli. Hivi hawa maprofesa wanajisikia je?
 
Kwani msamaha tafsiri yake ni nini?

Ukisema kusomeshwa nje ni kigezo cha kutokosoa aliyekusomesha ni ujinga mpevu.
Imagine hapo pichani kuna msomi aliyesomeshwa kwa kodi za watanzania urusi miaka 7 ila wewe unasema ni "bure" alisema hakunq umuhimu wa chanjo dhidi ya UVIKO bali watanzania wanywe michanyato ya tangawizi na mananasi je watu watanzania wangapi walipoteza wapendwa wao lini wataombwa msamaha kwa upotoshaji mkubwa kama huu.?
View attachment 2366367
Kwani kuna ubaya upi kutumia vitu hivyo! mbona sisi huku mtaani nilivitumia na akuna Mtu aliyeguswa na coronavirus,na mpaka Sasahivi akuna aliyepigwa chanjo na tunadunda kama kawa.Sio kila kitu anachofanya mzungu kinafaa asilimia zote,ndio Maana kwenye fom zao za chanjo walijiondoa pamoja na serikali ili likitokea jambo wasilaumiwe.
 
Kila mwenye akili timamu alijua kuwa madai yale ulikuwa uwongo mkubwa. Ni sawa uambiwe kuwa mwenye duka la mtaji wa 2m anadaiwa kodi ya sh 2 bilioni. Lazima uwe punguani kiasi kuweza kuliamini hilo.

Total gold resource ya migodi yote ya Barrick kwa Tanzania ni 0.75MOz Tulawaka + 4MOz Buzwagi + 7MOZ North Mara + 12MOZ Bulyanhulu = 23.75MOz. Mineable resource haiwezi kuzidi 60% = 14.25MOz. Dhahabu iliyokwishachimbwa, japo sina uhakika, haiwezi kuzidi 50%.= 7.1MOz. Thamani ya hii dhahabu iloyochimbwa, kwa bei ya juu kabisa, ya U$2,000 kwa oz = $14 billion (14 billion ×2,300 = TZS 32 trillion)

Hata ungesema hiyo hela yote iwe kodi, halafu wasiwe wametoa kodi hata shilingi moja, bado haifikii hata 10% ya trilioni 360 ambayo waliotuona wajinga walikuwa wakituaminisha.

Hata kama walitaka kuwadanganya wananchi, wangeweka huo uwongo wao uwe unakaribia na ukweli. Lakini wahusika kwa vile walijua wanaongoza nchi ya wasio na kitu vichwani, walijua wapo wenye vichwa vitupu kabisa, ambao ni wengi, watashangilia na kuwaona ni mashujaa. Uwongo ule ni miongoni mwa mambo yaliyotufanya waafrika tuendelee kuonekana kuwa siyo binadamu timilifu.

Kwa namna ambavyo baadhi ya watu wakati ule walivyokuwa wameshibishwa ujinga, hata wangeambiwa kuna mpango wa Serikali wa kumnunulia kila mwananchi ndege aina ya Boeing 737-800, wangeshangilia na kusema tumepata mkombozi. Ujinga ni laana kubwa, hasa ujinga ule unaoelekea kwenye upumbavu.
Kwenye negotiation yeyote demand zako lazima ziwe juu.Mjinga ni wewe.
 
Japo ni kweli lakini sio busara kufanya ukosoaji kwa kutumia maneno makali yenye lugha ya maudhi, wewe huna Ph.D, ripoti ya Ph.D holder, huwezi kuita "a professional rubish". Hata akina sisi tuliikosoa ripoti hiyo lakini tulitumia lugha ya kistaarabu! Sensationalism kwenye Professional Presentations inakubalika? Ni swali tu...


Serikali, mabenki na taasisi za fedha ziko huru kusamehe sehemu ya deni au deni lote, kitu muhimu ni wenye fedha zao kujulishwa. Licha ya umasikini wote uliotopea wa nchi yetu, hakuna ubaya wowote kusamehe deni lolote kwa yeyote, lakini lazima utoe sababu why unasamehe, ila pia unaposamehe majizi ndio muhimu zaidi kuwa transparent, ili isije kuonekana viongozi wetu wamekuwa compromised !.

Kwenye hili aombwe radhi kwa lipi?.
P
Mkuu !!! kwann sikuhizi unapotea sana
 
Kwani kimantiki professorial rubbish ni kitu kisichowezekana? Ile report ilikuja na viwango vya ajabu vya madini na ikapelekea wataalamu wetu kuja na makisio ya ajabu kabisa ni nini tunawadai acacia.

Na toka waliporejea kupeleka hayo makinikia hawaja thubutu kutueleza ni kiwango kipi kimekutwa. JPM asingechelea kuonyesha kuwa lissu hakusema ukweli.

Hivyo report ile ilijaa hadaa. Sasa tunajua ni mengi tu baba yule alituhadaa. Na report zile hazikuwa sahihi. Zilikuwa Professorial rubbish.
Ndugu P anatakiwa kujua kuwa, kamwe waungwana wa kweli hawatakiwi kuogopa ukweli.
Ni aibu na dhambi kubwa kuogopa kuwaambia ukweli wasomi na wote waliyoshiriki kutoa uongo; uchafu kitaalamu. Tukifanya hivyo tunaliua taratibu taifa letu wenyewe sijui kwa faida ya nani.
Mungu alituachia tupitie haya ili tujifunze. AMEN
 
Japo ni kweli lakini sio busara kufanya ukosoaji kwa kutumia maneno makali yenye lugha ya maudhi, wewe huna Ph.D, ripoti ya Ph.D holder, huwezi kuita "a professional rubish". Hata akina sisi tuliikosoa ripoti hiyo lakini tulitumia lugha ya kistaarabu! Sensationalism kwenye Professional Presentations inakubalika? Ni swali tu...


Serikali, mabenki na taasisi za fedha ziko huru kusamehe sehemu ya deni au deni lote, kitu muhimu ni wenye fedha zao kujulishwa. Licha ya umasikini wote uliotopea wa nchi yetu, hakuna ubaya wowote kusamehe deni lolote kwa yeyote, lakini lazima utoe sababu why unasamehe, ila pia unaposamehe majizi ndio muhimu zaidi kuwa transparent, ili isije kuonekana viongozi wetu wamekuwa compromised !.

Kwenye hili aombwe radhi kwa lipi?.
P

Sio professional rubish bali "professorial rubbish".
 
U
Kwani kuna ubaya upi kutumia vitu hivyo! mbona sisi huku mtaani nilivitumia na akuna Mtu aliyeguswa na coronavirus,na mpaka Sasahivi akuna aliyepigwa chanjo na tunadunda kama kawa.Sio kila kitu anachofanya mzungu kinafaa asilimia zote,ndio Maana kwenye fom zao za chanjo walijiondoa pamoja na serikali ili likitokea jambo wasilaumiwe.
Ndio maana umesema ni wewe , kaa ukifahamu kuna watu walihitaji chanjo pia kwanini wanyimwe haki hiyo na kushurutishwa kunywa michanyato.
 
Yes tulisoma naye Ilboru ilikuwa ni bure hadi nauli iliyokuleta unawasilisha risiti kwa School Basa unarudishiwa fedha zako. Siku ya kufunga shule unapewa warrant una safiri bure.

Chuo Kikuu, pia kasomeshwa bure LL.B , UDSM
P
Kwa hiyo ukisomeshwa bure hutakiwi kuhoji chochote kile ambacho ni Cha hovyo kutoka serikalini?
 
Naona kama kawaida Chadema wamevamia hii issue, hawajui purpose ya kuibuka kwake! Hawajachunguza facts za hili jambo, tayari wamebeba mwenge! Haya mambo yamejaa sarakasi ambazo ukikurupuka utatumika kama daraja huku ukibakia pale pale [emoji17]

Tutakumbushana ...
Chadema tena? unakosea.

Ila naungana nawe unaposema hili jambo ni fumbo, wote wanaolipigia kelele hawana data za kutosha, haijulikani kama serikali ililipwa au haikulipwa, naona ni "hesabu zao za kawaida" na mapenzi kwa Lissu, ndio yametawala mjadala.
 
Naona kama kawaida Chadema wamevamia hii issue, hawajui purpose ya kuibuka kwake! Hawajachunguza facts za hili jambo, tayari wamebeba mwenge! Haya mambo yamejaa sarakasi ambazo ukikurupuka utatumika kama daraja huku ukibakia pale pale [emoji17]

Tutakumbushana ...

Hakuna anayejali yaliyoko nyuma ya kuibuka hilo suala sasa, lakini toka wakati lilipoibuka huko nyuma tulisema kuna uongo mwingi kwenye ripoti ile. Wafuasi wa CDM wako active, hivyo ni lazima wajadili jambo lolote kwa namna wanavyoona wao. Hao wafuasi wa vyama vingine wao wako wapi kujadili, au wao ni maiti hai hivyo hawajigusi kwa lolote?
 
Back
Top Bottom