Ni wakati sasa wa kubadili Falsafa za Mwalimu Nyerere na kuchunguza na kuhoji mienendo yake

Hakuna mtawala yoyote hapa duniani asie na dark side, kama yupo mtaje.
Kila mtawala ni binadamu sio malaika, kukosea kupo.
 
Kwamba tunamchukia Muasisi au Tunachukia Wazenji?
Hatujielewi sisi wa huku bara. Na wengi wetu ni wakristo hivyo msingi wa mada hii ni udini unaojificha katika kuhoji masuala ya muungano.

Msingi wa hizi hisia ni chuki dhidi ya Samia na uislamu wake walianza chokochoko wakati wa kupitisha mkataba wa DP World huu ni muendelezo tu.
 
Porojo
 
Mbona unachanganya vitu, hoja ya Muungano imeanza leo?
 
Zahanat
Zahanati na Muungano wapi na wapi?

Falsafa za Mwalimu mambo ya Samia kuhusu Maji na Afya yametoka wapi?
Mbona unachanganya au unavamia uzi ichwakichwa.

Kwanza mambo ya afya si ya Muungano mbona Mzanzibari anahangaika na Afya za Tanganyika, wakat Mtanganyika haruhusiwi kuhusimamia Afya za Zanzibar?

Je ni Falsafa za Nani tunaziishi hapo kama si za hayati Kambarage?
 
... kama bado zinatukwamisha, kwa baadhi ya waumini wake kuturudisha miaka ya 1960s kila siku, kwanini tusihoji na kukosoa?
 
Hakuwa mwanademokrasia, alienda Zanzibar kubadilisha matokeo na huku bara kuhakikisha Mrema haingii ikulu. Hayo mambo yanamtia doa jeusi
 
Nikifatilia historia ndio nitapata maana ya keai za uhaina?
Sasa utazipata wapi kama hujafuatilia historia ya nchi yako. Kafuatilie kwanza ndo uje kubisha.

Unamjua Titi Mohammed Salum Mandangwa?

Unamjua Oscar Kambona.

Among others.

Kwa kifupi Babu alikuwa hataki kuwa challenged na aliwapa makosa ya uhalifu tofautitofauti wapingaji wake IKIWEMO UHAINI

“BY THE ORDER OF THE PEAKY FUCKING BLINDERS” 😎
 
Zanzibar ni nchi ndogo sana ni sawa na wilaya mojawapo ya mkoa wa Morogoro. Tumeungana nao kwa sababu za kijiografia tu, hawatupungizii chochote na ni ajabu sana kuona wanatuumiza vichwa vyetu.

Falsafa za Mwalimu zilikuwa na mashiko kwa wakati ule, sisi tunaziona zmepitwa na wakati kwa sababu tunaishi katika dunia ya 2024. Zina mashiko kwa Tanzania yetu.
 
... kama bado zinatukwamisha, kwa baadhi ya waumini wake kuturudisha miaka ya 1960s kila siku, kwanini tusihoji na kukosoa?
Mada nyingi huja na kuondoka kulingana na matukio yanayoendelea. Hakuna namna falsafa za Mwalimu zimewahi kuikwamisha Tanzania.

Zimekuza umoja huu huu unaoliweka taifa hili kwenye ramani na heshima kimataifa, zinaweza vipi kuwa zimepitwa na wakati?.

Kuvunja umoja huu ni rahisi sana lakini kuurudisha tena kuna gharama kubwa na nyingine zinahusiana na uhai wa baadhi yetu.
 
Hauko makini ndio maana hujagundua ninachokukosoa. Kasome quote yangu ya kwanza, angalia rangi ya njano.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…