Ni wakati sasa wa kubadili Falsafa za Mwalimu Nyerere na kuchunguza na kuhoji mienendo yake

Tuanze kuponda kichwa cha koboko CCM
 
Maoni ya mtoto wake haya.
 
kwa kumulinganisha na nani??
Lazima tutafute wa kumlinganisha kwanza?? otherwise mwandishi hana akili
 
Nyerere ni binaadamu kila mwana Adam ana makosa yake sasa imekuwa vibaya Nyerere kukosolewa makosa yake?.
Unahangaika na marehemu wakati wenzetu wanapambana na teknolojia kuhakikisha wanatafuta maisha kwenye sayari zingine,waafrika tulilogwa na malaika mchafu
 
Unahangaika na marehemu wakati wenzetu wanapambana na teknolojia kuhakikisha wanatafuta maisha kwenye sayari zingine,waafrika tulilogwa na malaika mchafu
Wewe umefanya lipi la maana kwenye kufatilia hayo ya kwenye sayari mpaka sasa?.
 
Tunamheshimu lakin alikuwa Tapeli mkubwa
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ana sura nyingi katika siasa za Tanzania, Africa na Duniani kote.
Nyerere mara baada ya kuwa Raisi wa Tanganyika alikuja gundua kuwa bila Nchi za kiafrika kuwa huru Tanganyika baadae Tanzania haijakuwa uhuru.Akaja tumia nguvu nyingi na muda mwingi kwenye vita vya ukombozi hasa kusini mwa Africa.
Akiwa anatawala nchi maskini iliojaa maradhi na wajinga pammoja na wanyonyaji akaanzisha Azimio la Arusha lakini utekelezaji wake ulileta shubiri badala yafaraja.
Kama haitoshi kupinduliwa kwa rafiki yake Dr Milton Obote raisi wa Uganda na General Iddi Amin kulileta changamoto nyingi ilisababisha kuvunjika Jumuiya ya Africa Mashariki na baade vita vya Kagera
Baada ya kushinda vita vya Kagera ,taasisi za Fedha World Bank na IMF walitaka Raisi Nyerere afanye reform za kiuchumi,ikashindikana wakamyima pesa za maendeleo na kuwekewa Tanzania vikwazo vya uchumi.
Uhaba wa vitu muhimu na hali ya maisha ikazidi kuwa ngumu,ulanguzi ukapaa,na ndipo matukio ya kuteka ndege ya ATC kumshindikiza achie madaraka na baadae wanajeshi wakala njama za kupindua serikali yake na huku Marekani akiongeza vikwazo vya uchumi,ilipofika 1985 Mzanaki akasalimu amri hakutaka kuendelea na uraisi.

Yawezekana Nyerere ilibidi wakati mwingine afanye maamuzi magumu yalioleta simanzi kwa kutetea ukombozi kusini mwa Africa, kutaifisha mali za makabaila,uanzishaji wa vijiji vya Ujamaa .Chimbuko la Vita vya Kagera.Msajili wa Nyumba,kunyanganywa watu magari yao ya mitumba,maduka ya kaya,Scopo,State House clearance kibali cha kusafiri nchi ya nje.Nchi ilikuwa na vibali vya sukari,mchele,unga wa yanga,kununua bati,soda,beer eee R.I.P Mwalimu Julius Nyerere.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…