Ni wakati wa kutoa ultimatum kwa watawala, bila Katiba Mpya ya wananchi hakuna uchaguzi

Ni wakati wa kutoa ultimatum kwa watawala, bila Katiba Mpya ya wananchi hakuna uchaguzi

Hii itaishia kwenye social media tu na kwenye vijiwe !! Kitu chochote kinachotaka kipate sapoti kubwa ya watu ni lazima wawepo viongozi wa hicho kitu !!
Viongozi wapi unataka mkuu wa Dini au Katiba ya nani kama ni yetu wananchi Viongozi watakuwepo kwasabu ni wanachi katiba inatuhusu watu wote wenye nianjema na Taifa letu.
 
Mama ameruhusu mchakato uendelee lakini naona kama hatutaki.

Lakini mwisho wa yote tukianzia ngazi ya familia ni nani mwenye sauti ya mwisho ndani kwako, je ni mtoto, beki tatu, Mama au Baba?
 
Viongozi wapi unataka mkuu wa Dini au Katiba ya nani kama ni yetu wananchi Viongozi watakuwepo kwasabu ni wanachi katiba inatuhusu watu wote wenye nianjema na Taifa letu.
Hata kwenye ibada huwa zipo kengele zinawakusanya waumini au adhana kwenye maspika na shuleni tulikuwa tunakusanywa kwa kengele mkuu 😅😅🙏🙏
 
Ifike wakati Watanzania tutoe amri kwa watawala kwamba kama hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Nchi hii ni ya Watanzania. Watanzania ndio wanaotakiwa kuwa na maamuzi ya namna gani wanataka nchi yao ifanye kila kitu.

Katiba hii ambayo Baba wa Taifa alisema inamfanya Rais kuwa dikteta sasa ifike mwisho. Rais anatakiwa kupewa mwongozo tuliokubaliana namna anavyotakiwa kutuongoza, na siyo yeye kutupangia namna anavyotaka kututawala kama ilivyo sasa.

Leo hii kila kitu ni Rais, kama vile nchi ni ya Rais. Kodi ni ya mwananchi, lakini Rais ndiye anakuletea mkurugenzi kuja kusimamia matumizi ya pesa yako. Hata ukiona huyo mkurugenzi anaiba, wewe unayetoa pesa huna uamuzi, mpaka aliyemteua apende, asipopenda, mteule wake anaendelea kutafuta pesa ya wananchi na hamna uwezo wa kumfanya chochote.

Fikiria, mpaka pesa ya wananchi, siku hizi inatajwa kuwa ni pesa ya Rais, eti Rais emetoa bilioni kadhaa kwaajiki ya ujenzi wa kisima, zahanati, shule, n.k.

Hata huko kwenye mataifa yenye katiba nzuri, sheria nzuri na mifumo mizuri ya utawala, siyo kwamba watawala walikuwa malaika, bali pressure ya wananchi iliwalazimisha watawala kukubali matakwa ya wananchi.

Kwa kuwa Serikali inalegalega, na kupiga danadana nyingi kuhusiana na suala la katiba nzuri mpya, katiba ya wananchi, lazima nguvu ya wananchi ishike hatamu, na Serikali ilazimishwe kufuata matakwa ya wananchi.

Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.

Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?

Mambo haya inawezekana yanafanywa ama kwa shinikizo ama kwa kujipendekeza kwa Rais kwa sababu ni mzanzibari. Hatupingi kusamehe deni, tena kwa sehemu mojawapo ya muungano au kutoa msaada inapolazimu, lakini ni utaratibu upi umefuatwa kwa shirika linaloendesha kwa pesa za walipa kodi kuweza kufuta deni? Mbona hatujawahi kusikia kuwa TANESCO imewafutia deni wadaiwa sugu wa huku bara?

Katiba mpya itayaweka haya mambo yote wazi, na kuweka taratibu zilizokubalika na ambazo kila mmoja, na hasa viongozi, watatakiwa kufuata.

Hii ya kila kitu Rais, haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile. Kwenye teuzi, Rais aishie kuwateua mawaziri tu ambao wataidhinishwa na wabunge. Wengine wote waajiriwe au wachaguliwe. Wakivurunda, mamlaka za uajiri ziwafukuze kiurahisi.

Katiba siyo ya akina Lisu na Mbowe, siyo ya Rais wala Mutungi, siyo ya Chongolo, bali ni ya Watanzania wote. Yeyote anayetaka kujimilikisha uandaaji wa katiba ni adui yetu sote. Yeyote anayetaka kutushirikisha sote kwenye kupata katiba tunayoitaka, ni mzalendo wa Taifa letu, ni mtu mwenye upendo kwa Watanzania wa leo na vizazi vijavyo, na huyo ndiye tuandamane naye.

Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
Umesema kila kitu ni wakati wa kuchukua hatua,leo hii Ethiopia umeme ni tsh elfu kwa mwezi na maji tsh 10k kwa mwaka hio haijalishi matumizi
 
Bajeti na katiba ni vitu viweli tofauti sana. Bajeti ni mpango wa muda mfupi: siku moja, wiki, mwezi, miezi 3, 6 au mwaka. Katiba na sheria mama inayoandikwa ile kiweze kutumika muda mrefu kama miaka 50 au hata 100. Misingi ya Rasimu ya Warioba kwa sehemu kubwa hayajabadilika. Sana sana leo hii hatuhitaji kubadilisha hiyo misingi yake; pengine kuna mambo machache madogo madogo yanayohitaji kubadilika kutokana zaidi na uzoefu tuliopata miaka ya awamu ya 5. Kuna mambo ya msingi sana tumejifunza kama nchi ambayo ni muhimu sana katiba ikayazingatia.
Umenena kweli !
 
ultimatum sio mjadala ni amri, sio busara kumuamrisha rais ambaye ni Mkuu wa nchi.

Kiukweli wanaotaka katiba mpya ni the elites ambao ni just 20% ya Watanzania wote!. Wananchi wa kawaida wao wanataka tuu mambo yaende.
P
Mamlaka yote ya utawala hutoka kwa umma wa wananchi.

Japo siyo wakati wote, lakini wananchi katika ujumla wao wana mamlaka na haki ya kuiamrisha Serikali na kiongozi mwingine yeyote inapoonekana matakwa yao yanapuuzwa, au kucheleweshwa bila sababu.

Kama tangu tuambiwe kuwa mchakato wa katiba mpya umefufuliwa, halafu mpaka leo hatujui kama tunaanza mchakato mpya au kuboresha ule uliokuwepo, hiyo katiba kuja kupatikana si itachukua miaka hata zaidi ya 50?

Hatujaumbwa na Mungu kuishi miaka 1,000 au zaidi. Muda mfupi wa maisha tuliopewa ni lazima tuutumie vizuri kuyakamilisha yanayotakiwa kuyafanywa.

Yaani miaka miwili, hatujui hata tunataka nini, kuanza upya au kuendeleza tulipoishia na kufanya maboresho. Labda ndiyo maana nchi yetu hatua zake kwenye maendeleo ni mwendo wa kinyonga.

Malaysia tuliokuwa nao sawa kwenye uchumi mwaka 1961, taarifa ya UNDP inasema kuwa tukiendelea na speed yetu iliyopo, Malaysia wakabakia pale pale, wasiendelee zaidi, kufika mahali walipo, kwa Tanzania itachukua miaka 250. Hiyo inasababishwa na haya tunayoyafanya na tunaona kuwa ni sahihi. Hatujui thamani ya wakati.
 
[emoji38][emoji38][emoji38] Kuongea hayo mambo ukiwa umejificha Kwenye keyboard ni very easy

Toka nje, simama pale kariakoo then sema hayo uliyoandika, hapo ndio tutajua kweli Una maanisha
Usitishe watu. Tutayasema haya usiku na mchana, kwenye vyombo vya habari na hata sehemu za wazi kama barabarani au majukwaani.

Kama umezoea kutisha watu, umepitwa na wakati. Ulimwengu wa leo siyo wa kumtisha yeyote.
 
Mimi huwa nashindwa kuwaelewa wale wanaodai eti ile Rasimu ya katiba ya Warioba imeshapitwa na wakati kwa sababu imepita miaka kumi na mambo mengi yamebadilika [emoji849][emoji849] !!


Je ina maana yale yanayowekwa katika katiba ni mambo ya miaka kumi tu. ???!

Kisha baada ya miaka kumi katiba inatakiwa iandikwe nyingine maana ile imeshapitwa na wakati ????!

Hii ni Akili ya wapi ???!
Ukweli hiyo hoja haina msingi. Hao wanaosema kuwa katiba pendekezwa imepitwa na wakati, ina maana wakati ule zoezi lingekuwa limekamilika, sahizi tungeanza kuandika nyingine upya au kuifanyia maboresho?

Katiba inaandikwa kukidhi matakwa ya nchi kwa muda hata zaidi ya maiaka 50.
 
Sioni ni vipi hao wananchi wanaweza kujimobilise bila kuwa mobilised na watu wenye sauti katika jamii !!
Ni kweli. Hakuna mapambano yasiyo na viongozi. CHADEMA wameonesha njia, na wengine waje. Wananchi tuungane na watu wote wanatoa uongozi katika kudai katiba.
 
Ifike wakati Watanzania tutoe amri kwa watawala kwamba kama hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Nchi hii ni ya Watanzania. Watanzania ndio wanaotakiwa kuwa na maamuzi ya namna gani wanataka nchi yao ifanye kila kitu.

Katiba hii ambayo Baba wa Taifa alisema inamfanya Rais kuwa dikteta sasa ifike mwisho. Rais anatakiwa kupewa mwongozo tuliokubaliana namna anavyotakiwa kutuongoza, na siyo yeye kutupangia namna anavyotaka kututawala kama ilivyo sasa.

Leo hii kila kitu ni Rais, kama vile nchi ni ya Rais. Kodi ni ya mwananchi, lakini Rais ndiye anakuletea mkurugenzi kuja kusimamia matumizi ya pesa yako. Hata ukiona huyo mkurugenzi anaiba, wewe unayetoa pesa huna uamuzi, mpaka aliyemteua apende, asipopenda, mteule wake anaendelea kutafuta pesa ya wananchi na hamna uwezo wa kumfanya chochote.

Fikiria, mpaka pesa ya wananchi, siku hizi inatajwa kuwa ni pesa ya Rais, eti Rais emetoa bilioni kadhaa kwaajiki ya ujenzi wa kisima, zahanati, shule, n.k.

Hata huko kwenye mataifa yenye katiba nzuri, sheria nzuri na mifumo mizuri ya utawala, siyo kwamba watawala walikuwa malaika, bali pressure ya wananchi iliwalazimisha watawala kukubali matakwa ya wananchi.

Kwa kuwa Serikali inalegalega, na kupiga danadana nyingi kuhusiana na suala la katiba nzuri mpya, katiba ya wananchi, lazima nguvu ya wananchi ishike hatamu, na Serikali ilazimishwe kufuata matakwa ya wananchi.

Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.

Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?

Mambo haya inawezekana yanafanywa ama kwa shinikizo ama kwa kujipendekeza kwa Rais kwa sababu ni mzanzibari. Hatupingi kusamehe deni, tena kwa sehemu mojawapo ya muungano au kutoa msaada inapolazimu, lakini ni utaratibu upi umefuatwa kwa shirika linaloendesha kwa pesa za walipa kodi kuweza kufuta deni? Mbona hatujawahi kusikia kuwa TANESCO imewafutia deni wadaiwa sugu wa huku bara?

Katiba mpya itayaweka haya mambo yote wazi, na kuweka taratibu zilizokubalika na ambazo kila mmoja, na hasa viongozi, watatakiwa kufuata.

Hii ya kila kitu Rais, haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile. Kwenye teuzi, Rais aishie kuwateua mawaziri tu ambao wataidhinishwa na wabunge. Wengine wote waajiriwe au wachaguliwe. Wakivurunda, mamlaka za uajiri ziwafukuze kiurahisi.

Katiba siyo ya akina Lisu na Mbowe, siyo ya Rais wala Mutungi, siyo ya Chongolo, bali ni ya Watanzania wote. Yeyote anayetaka kujimilikisha uandaaji wa katiba ni adui yetu sote. Yeyote anayetaka kutushirikisha sote kwenye kupata katiba tunayoitaka, ni mzalendo wa Taifa letu, ni mtu mwenye upendo kwa Watanzania wa leo na vizazi vijavyo, na huyo ndiye tuandamane naye.

Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
Kama wananchi wanataka katiba mpya mnazunguka na helikopta kutafuta nini?
 
Mamlaka yote ya utawala hutoka kwa umma wa wananchi.
Ni kweli na ndivyo katiba yetu inavyosema.
Japo siyo wakati wote, lakini wananchi katika ujumla wao wana mamlaka na haki ya kuiamrisha Serikali na kiongozi mwingine yeyote inapoonekana matakwa yao yanapuuzwa, au kucheleweshwa bila sababu.
Very unfortunately hatuna haki hii ya kuanzisha, ila serikali isipotimiza wajibu wake, ah kunitendea ndivyo hivyo, tuna haki ya kuishitaki mahakamani, na mahalama ndio, ikaiamrisha serikali na sio wananchi kuamrisha serikali.
Kama tangu tuambiwe kuwa mchakato wa katiba mpya umefufuliwa, halafu mpaka leo hatujui kama tunaanza mchakato mpya au kuboresha ule uliokuwepo, hiyo katiba kuja kupatikana si itachujua miaka hata zaidi ya 50?
Lazima tujifunze kusikiliza, hatujaambiwa popote na yeyote kuwa mchakato wa katiba mpya umefufuliwa!, bali Mama aliunda kikosi kazi, ndio wananchi wakataka katiba mpya.

Mama akatoa room tusemezane, tunataka mchakato uweje, tuendelee na ile ya Warioba ila tuiboreshe, tuanze upya, au tumalizie na ile katiba pendekezwa ilipoishia tuipigie jura, it's up to us sisi wananchi. Msajili wa vyama vya Siasa, Jaji Mutungi ameanza kusemezana na vyama vya siasa.
P
 
Ukweli hiyo hoja haina msingi. Hao wanaosema kuwa katiba pendekezwa imepitwa na wakati, ina maana wakati ule zoezi lingekuwa limekamilika, sahizi tungeanza kuandika nyingine upya au kuifanyia maboresho?

Katiba inaandikwa kukidhi matakwa ya nchi kwa muda hata zaidi ya maiaka 50.
Wapo watu wanadhani watu wote ni wajinga wajinga tu hawajui kitu ! Na ukizowea tabia za kudanganya danganya watu wakati mwingine unasahau unaanza kujidanganya mwenyewe !! 😂😅
 
...hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.
Mleta mada kama utajali ninaomba unipatie mnyororo wa thamani wa kupata Katiba mpya. Na kwa Kila fundo la mnyororo huo unitajie wanaufaika.

Yaani kuanzia uratibu wa maoni wa ukusanyaji wa maoni, uchakataji na uandaaji nyaraka za kumsaidia kukusanya maoni..... mlolongo wote ukiwahusisha watu wa ugavi, watoa huduma....mpaka kupata katiba mpya.

Hii itasaidia kujua hawa wanaopiga zumali la katiba mpya wanafanya hivyo kuburudisha wasikiliza zumali na wao pia ama wanapiga zumali kwa sababu Kuna mlundikano wa kandarasi na posho kibao unaviziwa??

Swali chonganishi ama?
 
Kuna mahali hapo juu Pascal Mayalla amauliza mbona mama ameruhusu mchakato wa katiba uanze?
Nio acho mimi kilichofanyika ni kama umemuozesha mwanao mke na kumwambia kazaeni muniletee wajukuu kisha una mpatia mabox ya condom kama zawadi atumie. Nimeeleweka!
 
Mama akatoa room tusemezane, tunataka mchakato uweje, tuendelee na ile ya Warioba ila tuiboreshe, tuanze upya, au tumalizie na ile katiba pendekezwa ilipoishia tuipigie jura, it's up to us sisi wananchi. Msajili wa vyama vya Siasa, Jaji Mutungi ameanza kusemezana na vyama vya siasa.
Ikiwezekana kwa Kila njia itakayotumika kupata Katiba hiyo, tupewe mnyororo wa thamani wa Kila njia na wanaufaika wake na namna watakavyonufaika katika viwango vya malipo ya fedha.

Hili ni muhimu katika kutusaidia kufanya maamuzi sahihi juu ya hili.
 
Mleta mada kama utajali ninaomba unipatie mnyororo wa thamani wa kupata Katiba mpya. Na kwa Kila fundo la mnyororo huo unitajie wanaufaika.

Yaani kuanzia uratibu wa maoni wa ukusanyaji wa maoni, uchakataji na uandaaji nyaraka za kumsaidia kukusanya maoni..... mlolongo wote ukiwahusisha watu wa ugavi, watoa huduma....mpaka kupata katiba mpya.

Hii itasaidia kujua hawa wanaopiga zumali la katiba mpya wanafanya hivyo kuburudisha wasikiliza zumali na wao pia ama wanapiga zumali kwa sababu Kuna mlundikano wa kandarasi na posho kibao unaviziwa??

Swali chonganishi ama?
Posho zitaendelea kuliwa kila siku hata bila Katiba ! Hujasikia juzi hapa watu wanepitisha kwa nguvu kubwa posho ya bilioni 47 !!

Katiba mpya bora itakuja kuzuwia vitu vya namna hiyo !!
 
Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.
uTaifa kwanza,
uchama baadae na pale tu utakapoendana na uTaifa.
Kama unaipenda Tanganyika, utalitetea Taifa hili bila kujali madhara yake kwenye chama chako.
Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?
Mgongano wa Nia wa wazi ( clear conflict of interest)

Swali pana ni - Mzanzibari anapata wapi uhalali wa kuifanyia maamuzi Tanganyika katika mambo yasiyo katika Muungano?

Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
Tanganyika ni Republic, nashauri kwenye Katiba mpya tuondoe kabisa dhana ya "utawala/kutawala/Mtawala" na tuwe na "Uongozi/Kuongoza/Kiongozi"
 
Ikiwezekana kwa Kila njia itakayotumika kupata Katiba hiyo, tupewe mnyororo wa thamani wa Kila njia na wanaufaika wake na namna watakavyonufaika katika viwango vya malipo ya fedha.

Hili ni muhimu katika kutusaidia kufanya maamuzi sahihi juu ya hili.
Tukianza kuangalia mnyororo wa thamani, tutarudi kule kule kwenye bora katiba, Mchakato huu wa Katiba ni umasikini wetu. Tujikubali, tuukubali, tuupigie kura ya ndio sasa let's do the right thing tupate katiba bora na sio bora katiba.
P
 
Back
Top Bottom