Jemima Jackson
JF-Expert Member
- Dec 15, 2019
- 748
- 934
Viongozi wapi unataka mkuu wa Dini au Katiba ya nani kama ni yetu wananchi Viongozi watakuwepo kwasabu ni wanachi katiba inatuhusu watu wote wenye nianjema na Taifa letu.Hii itaishia kwenye social media tu na kwenye vijiwe !! Kitu chochote kinachotaka kipate sapoti kubwa ya watu ni lazima wawepo viongozi wa hicho kitu !!
Hata kwenye ibada huwa zipo kengele zinawakusanya waumini au adhana kwenye maspika na shuleni tulikuwa tunakusanywa kwa kengele mkuu 😅😅🙏🙏Viongozi wapi unataka mkuu wa Dini au Katiba ya nani kama ni yetu wananchi Viongozi watakuwepo kwasabu ni wanachi katiba inatuhusu watu wote wenye nianjema na Taifa letu.
Umesema kila kitu ni wakati wa kuchukua hatua,leo hii Ethiopia umeme ni tsh elfu kwa mwezi na maji tsh 10k kwa mwaka hio haijalishi matumiziIfike wakati Watanzania tutoe amri kwa watawala kwamba kama hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.
Nchi hii ni ya Watanzania. Watanzania ndio wanaotakiwa kuwa na maamuzi ya namna gani wanataka nchi yao ifanye kila kitu.
Katiba hii ambayo Baba wa Taifa alisema inamfanya Rais kuwa dikteta sasa ifike mwisho. Rais anatakiwa kupewa mwongozo tuliokubaliana namna anavyotakiwa kutuongoza, na siyo yeye kutupangia namna anavyotaka kututawala kama ilivyo sasa.
Leo hii kila kitu ni Rais, kama vile nchi ni ya Rais. Kodi ni ya mwananchi, lakini Rais ndiye anakuletea mkurugenzi kuja kusimamia matumizi ya pesa yako. Hata ukiona huyo mkurugenzi anaiba, wewe unayetoa pesa huna uamuzi, mpaka aliyemteua apende, asipopenda, mteule wake anaendelea kutafuta pesa ya wananchi na hamna uwezo wa kumfanya chochote.
Fikiria, mpaka pesa ya wananchi, siku hizi inatajwa kuwa ni pesa ya Rais, eti Rais emetoa bilioni kadhaa kwaajiki ya ujenzi wa kisima, zahanati, shule, n.k.
Hata huko kwenye mataifa yenye katiba nzuri, sheria nzuri na mifumo mizuri ya utawala, siyo kwamba watawala walikuwa malaika, bali pressure ya wananchi iliwalazimisha watawala kukubali matakwa ya wananchi.
Kwa kuwa Serikali inalegalega, na kupiga danadana nyingi kuhusiana na suala la katiba nzuri mpya, katiba ya wananchi, lazima nguvu ya wananchi ishike hatamu, na Serikali ilazimishwe kufuata matakwa ya wananchi.
Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.
Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?
Mambo haya inawezekana yanafanywa ama kwa shinikizo ama kwa kujipendekeza kwa Rais kwa sababu ni mzanzibari. Hatupingi kusamehe deni, tena kwa sehemu mojawapo ya muungano au kutoa msaada inapolazimu, lakini ni utaratibu upi umefuatwa kwa shirika linaloendesha kwa pesa za walipa kodi kuweza kufuta deni? Mbona hatujawahi kusikia kuwa TANESCO imewafutia deni wadaiwa sugu wa huku bara?
Katiba mpya itayaweka haya mambo yote wazi, na kuweka taratibu zilizokubalika na ambazo kila mmoja, na hasa viongozi, watatakiwa kufuata.
Hii ya kila kitu Rais, haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile. Kwenye teuzi, Rais aishie kuwateua mawaziri tu ambao wataidhinishwa na wabunge. Wengine wote waajiriwe au wachaguliwe. Wakivurunda, mamlaka za uajiri ziwafukuze kiurahisi.
Katiba siyo ya akina Lisu na Mbowe, siyo ya Rais wala Mutungi, siyo ya Chongolo, bali ni ya Watanzania wote. Yeyote anayetaka kujimilikisha uandaaji wa katiba ni adui yetu sote. Yeyote anayetaka kutushirikisha sote kwenye kupata katiba tunayoitaka, ni mzalendo wa Taifa letu, ni mtu mwenye upendo kwa Watanzania wa leo na vizazi vijavyo, na huyo ndiye tuandamane naye.
Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
Umenena kweli !Bajeti na katiba ni vitu viweli tofauti sana. Bajeti ni mpango wa muda mfupi: siku moja, wiki, mwezi, miezi 3, 6 au mwaka. Katiba na sheria mama inayoandikwa ile kiweze kutumika muda mrefu kama miaka 50 au hata 100. Misingi ya Rasimu ya Warioba kwa sehemu kubwa hayajabadilika. Sana sana leo hii hatuhitaji kubadilisha hiyo misingi yake; pengine kuna mambo machache madogo madogo yanayohitaji kubadilika kutokana zaidi na uzoefu tuliopata miaka ya awamu ya 5. Kuna mambo ya msingi sana tumejifunza kama nchi ambayo ni muhimu sana katiba ikayazingatia.
Mamlaka yote ya utawala hutoka kwa umma wa wananchi.ultimatum sio mjadala ni amri, sio busara kumuamrisha rais ambaye ni Mkuu wa nchi.
Kiukweli wanaotaka katiba mpya ni the elites ambao ni just 20% ya Watanzania wote!. Wananchi wa kawaida wao wanataka tuu mambo yaende.
P
Usitishe watu. Tutayasema haya usiku na mchana, kwenye vyombo vya habari na hata sehemu za wazi kama barabarani au majukwaani.[emoji38][emoji38][emoji38] Kuongea hayo mambo ukiwa umejificha Kwenye keyboard ni very easy
Toka nje, simama pale kariakoo then sema hayo uliyoandika, hapo ndio tutajua kweli Una maanisha
Ukweli hiyo hoja haina msingi. Hao wanaosema kuwa katiba pendekezwa imepitwa na wakati, ina maana wakati ule zoezi lingekuwa limekamilika, sahizi tungeanza kuandika nyingine upya au kuifanyia maboresho?Mimi huwa nashindwa kuwaelewa wale wanaodai eti ile Rasimu ya katiba ya Warioba imeshapitwa na wakati kwa sababu imepita miaka kumi na mambo mengi yamebadilika [emoji849][emoji849] !!
Je ina maana yale yanayowekwa katika katiba ni mambo ya miaka kumi tu. ???!
Kisha baada ya miaka kumi katiba inatakiwa iandikwe nyingine maana ile imeshapitwa na wakati ????!
Hii ni Akili ya wapi ???!
Ni kweli. Hakuna mapambano yasiyo na viongozi. CHADEMA wameonesha njia, na wengine waje. Wananchi tuungane na watu wote wanatoa uongozi katika kudai katiba.Sioni ni vipi hao wananchi wanaweza kujimobilise bila kuwa mobilised na watu wenye sauti katika jamii !!
Kama wananchi wanataka katiba mpya mnazunguka na helikopta kutafuta nini?Ifike wakati Watanzania tutoe amri kwa watawala kwamba kama hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.
Nchi hii ni ya Watanzania. Watanzania ndio wanaotakiwa kuwa na maamuzi ya namna gani wanataka nchi yao ifanye kila kitu.
Katiba hii ambayo Baba wa Taifa alisema inamfanya Rais kuwa dikteta sasa ifike mwisho. Rais anatakiwa kupewa mwongozo tuliokubaliana namna anavyotakiwa kutuongoza, na siyo yeye kutupangia namna anavyotaka kututawala kama ilivyo sasa.
Leo hii kila kitu ni Rais, kama vile nchi ni ya Rais. Kodi ni ya mwananchi, lakini Rais ndiye anakuletea mkurugenzi kuja kusimamia matumizi ya pesa yako. Hata ukiona huyo mkurugenzi anaiba, wewe unayetoa pesa huna uamuzi, mpaka aliyemteua apende, asipopenda, mteule wake anaendelea kutafuta pesa ya wananchi na hamna uwezo wa kumfanya chochote.
Fikiria, mpaka pesa ya wananchi, siku hizi inatajwa kuwa ni pesa ya Rais, eti Rais emetoa bilioni kadhaa kwaajiki ya ujenzi wa kisima, zahanati, shule, n.k.
Hata huko kwenye mataifa yenye katiba nzuri, sheria nzuri na mifumo mizuri ya utawala, siyo kwamba watawala walikuwa malaika, bali pressure ya wananchi iliwalazimisha watawala kukubali matakwa ya wananchi.
Kwa kuwa Serikali inalegalega, na kupiga danadana nyingi kuhusiana na suala la katiba nzuri mpya, katiba ya wananchi, lazima nguvu ya wananchi ishike hatamu, na Serikali ilazimishwe kufuata matakwa ya wananchi.
Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.
Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?
Mambo haya inawezekana yanafanywa ama kwa shinikizo ama kwa kujipendekeza kwa Rais kwa sababu ni mzanzibari. Hatupingi kusamehe deni, tena kwa sehemu mojawapo ya muungano au kutoa msaada inapolazimu, lakini ni utaratibu upi umefuatwa kwa shirika linaloendesha kwa pesa za walipa kodi kuweza kufuta deni? Mbona hatujawahi kusikia kuwa TANESCO imewafutia deni wadaiwa sugu wa huku bara?
Katiba mpya itayaweka haya mambo yote wazi, na kuweka taratibu zilizokubalika na ambazo kila mmoja, na hasa viongozi, watatakiwa kufuata.
Hii ya kila kitu Rais, haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile. Kwenye teuzi, Rais aishie kuwateua mawaziri tu ambao wataidhinishwa na wabunge. Wengine wote waajiriwe au wachaguliwe. Wakivurunda, mamlaka za uajiri ziwafukuze kiurahisi.
Katiba siyo ya akina Lisu na Mbowe, siyo ya Rais wala Mutungi, siyo ya Chongolo, bali ni ya Watanzania wote. Yeyote anayetaka kujimilikisha uandaaji wa katiba ni adui yetu sote. Yeyote anayetaka kutushirikisha sote kwenye kupata katiba tunayoitaka, ni mzalendo wa Taifa letu, ni mtu mwenye upendo kwa Watanzania wa leo na vizazi vijavyo, na huyo ndiye tuandamane naye.
Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
Ni kweli na ndivyo katiba yetu inavyosema.Mamlaka yote ya utawala hutoka kwa umma wa wananchi.
Very unfortunately hatuna haki hii ya kuanzisha, ila serikali isipotimiza wajibu wake, ah kunitendea ndivyo hivyo, tuna haki ya kuishitaki mahakamani, na mahalama ndio, ikaiamrisha serikali na sio wananchi kuamrisha serikali.Japo siyo wakati wote, lakini wananchi katika ujumla wao wana mamlaka na haki ya kuiamrisha Serikali na kiongozi mwingine yeyote inapoonekana matakwa yao yanapuuzwa, au kucheleweshwa bila sababu.
Lazima tujifunze kusikiliza, hatujaambiwa popote na yeyote kuwa mchakato wa katiba mpya umefufuliwa!, bali Mama aliunda kikosi kazi, ndio wananchi wakataka katiba mpya.Kama tangu tuambiwe kuwa mchakato wa katiba mpya umefufuliwa, halafu mpaka leo hatujui kama tunaanza mchakato mpya au kuboresha ule uliokuwepo, hiyo katiba kuja kupatikana si itachujua miaka hata zaidi ya 50?
Wapo watu wanadhani watu wote ni wajinga wajinga tu hawajui kitu ! Na ukizowea tabia za kudanganya danganya watu wakati mwingine unasahau unaanza kujidanganya mwenyewe !! 😂😅Ukweli hiyo hoja haina msingi. Hao wanaosema kuwa katiba pendekezwa imepitwa na wakati, ina maana wakati ule zoezi lingekuwa limekamilika, sahizi tungeanza kuandika nyingine upya au kuifanyia maboresho?
Katiba inaandikwa kukidhi matakwa ya nchi kwa muda hata zaidi ya maiaka 50.
Kabisa !Ni kweli. Hakuna mapambano yasiyo na viongozi. CHADEMA wameonesha njia, na wengine waje. Wananchi tuungane na watu wote wanatoa uongozi katika kudai katiba.
Mleta mada kama utajali ninaomba unipatie mnyororo wa thamani wa kupata Katiba mpya. Na kwa Kila fundo la mnyororo huo unitajie wanaufaika....hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024, wala uchaguzi mkuu mwaka 2025.
Mama ana Nia njema anawapima kuona Nia yenu kama ni njema ama la!!!Mama ameruhusu mchakato uendelee lakini naona kama hatutaki.
Ikiwezekana kwa Kila njia itakayotumika kupata Katiba hiyo, tupewe mnyororo wa thamani wa Kila njia na wanaufaika wake na namna watakavyonufaika katika viwango vya malipo ya fedha.Mama akatoa room tusemezane, tunataka mchakato uweje, tuendelee na ile ya Warioba ila tuiboreshe, tuanze upya, au tumalizie na ile katiba pendekezwa ilipoishia tuipigie jura, it's up to us sisi wananchi. Msajili wa vyama vya Siasa, Jaji Mutungi ameanza kusemezana na vyama vya siasa.
Posho zitaendelea kuliwa kila siku hata bila Katiba ! Hujasikia juzi hapa watu wanepitisha kwa nguvu kubwa posho ya bilioni 47 !!Mleta mada kama utajali ninaomba unipatie mnyororo wa thamani wa kupata Katiba mpya. Na kwa Kila fundo la mnyororo huo unitajie wanaufaika.
Yaani kuanzia uratibu wa maoni wa ukusanyaji wa maoni, uchakataji na uandaaji nyaraka za kumsaidia kukusanya maoni..... mlolongo wote ukiwahusisha watu wa ugavi, watoa huduma....mpaka kupata katiba mpya.
Hii itasaidia kujua hawa wanaopiga zumali la katiba mpya wanafanya hivyo kuburudisha wasikiliza zumali na wao pia ama wanapiga zumali kwa sababu Kuna mlundikano wa kandarasi na posho kibao unaviziwa??
Swali chonganishi ama?
uTaifa kwanza,Na kwenye hili wananchi tushikamane, tuache mambo ya uCHADEMA, uCCM, uCUF, uACT, au tofauti zile nyingine za kijinga eti huyu ni sukuma gang, yule ni msoga gang, nasema huo ni upuuzi, sote tuunganishwe na utaifa wetu.
Mgongano wa Nia wa wazi ( clear conflict of interest)Leo mmesikia kuwa TANESCO, inayoendeshwa kwa ruzuku ya Serikali ya bara (nishati siyo suala la muungano) imesamehe deni la zaidi ya shilingi bilioni 60 iliyokuwa ikiidai Zanzibar. Hizi ni pesa za wananchi walipa kodi. Msamaha huo umetolewa kwa namna gani? Ni utaratibu upi uliofuatwa? Ni nani aliyetoa uamuzi wa kusamehe hilo deni? Ana mamlaka hayo?
Tanganyika ni Republic, nashauri kwenye Katiba mpya tuondoe kabisa dhana ya "utawala/kutawala/Mtawala" na tuwe na "Uongozi/Kuongoza/Kiongozi"Hatutaki katiba maslahi ya watawala au wanasiasa tu, bali katiba itakayompa mamlaka makubwa mwananchi.
Tukianza kuangalia mnyororo wa thamani, tutarudi kule kule kwenye bora katiba, Mchakato huu wa Katiba ni umasikini wetu. Tujikubali, tuukubali, tuupigie kura ya ndio sasa let's do the right thing tupate katiba bora na sio bora katiba.Ikiwezekana kwa Kila njia itakayotumika kupata Katiba hiyo, tupewe mnyororo wa thamani wa Kila njia na wanaufaika wake na namna watakavyonufaika katika viwango vya malipo ya fedha.
Hili ni muhimu katika kutusaidia kufanya maamuzi sahihi juu ya hili.