Ni wimbo gani unaoutafuta sana bila mafanikio?
Kuna nyimbo mbili nazitafuta bila mafanikio.
1. Wimbo Salamu Baba na Mama, wa National Servence.
Mashairi yaliyomo:
Salamu Baba na Mama, nazituma kwa furaha
Bila shaka zitafika,
Tufurahi nyote bila manung'uniko wapenzi yeee

Kwa mimi ninafuraha sana, kuwakumbuni nyie
Wala msiwe na shaka juu yangu mie
Mimi ninawaombe heri, na baraka nyote
Nisalimieni wakiyanga wote.


2. Wimbo wa pili Unaitwa Uzazi wa Majira, baadhi ya mashairi yaliyomo kwenye wimbo ni kama ifuatavyo :-

Shamba letu ee bwana limesimama,
Kilimo cha peke yako mpaka lini,
Usiku nimesikia saa, majira yanagongana mpaka sasa.

Band iliyoimba siikumbuki, Nadhani kati ya Western Jazz, Jamhuri Jazz, Dar Jazz ama Nuta Jazz.
Sina uhakika hasa, ila wahenga wenzangu, watanikumbusha.
 
msaada kuna nyimbo flani ilikuwa ikitumiwa na star tv saa tatu asubuhi na mtangazi Jacob, ilikuwa slow jamz flan matata , mtangazi alikuwa akitembelea watu na wakawa wanatauma salam, alafu wanachagua nyimbo,,

sasa mtangazaji alikuwa akitumia hiyo nyimbo kama background
 
msaada kuna nyimbo flani ilikuwa ikitumiwa na star tv saa tatu asubuhi na mtangazi Jacob, ilikuwa slow jamz flan matata , mtangazi alikuwa akitembelea watu na wakawa wanatauma salam, alafu wanachagua nyimbo,,

sasa mtangazaji alikuwa akitumia hiyo nyimbo kama background
Dont leave Me....umeimbwa na Blackstreet. Utafute upo youtube.
 
Mkuu me natafuta wimbo fulani hivi ambana nakumbuka baadhi ya mashairi ila aliyeuimba nimfahamu jina . Mashairi:Sio siri nilisota tangu uondokee, hakuna dili nikuchoka tangu uondoke
Mchana kweupe nili kusodoaa ukasema yaishe japo uliumia X2
Maadui walinizunguka ulikuwa kando yangu ukinilinda na kuniepusha namabayaa.

Nikama jamaa anatokea Mwanza. Aliyenao wimbo huo naomba anipe jamani
 
Sorry guys naomba mnisaidie wimbo wa awilo WA mbeya unapigwa sana misibani na kwenye sherehe hasa ila siufahamu jina
 
Wakuu kwema? Aise kuna wimbo mmoja wameimba nadhani ni msondo ngoma ila sina uhakika kuna kipande kaimba marehemu TX Moshi anasema "tumezaliwa wengi lakini hatusaidiani......." naikumbuka hiyo sehemu tuu, anaejua jina la wimbo anitajie au kama anao atuwekee hapa.
 
Naomba mnisaodie wimbo sikumbuki umeimbwa na nani hata jina siujui ila una kionjo kimoja kinasema hivi ...kama mapenzi yalikuwa zama zamani
 
Naomba mnisaodie wimbo sikumbuki umeimbwa na nani hata jina siujui ila una kionjo kimoja kinasema hivi ...kama mapenzi yalikuwa zama zamani
Banana Zorro huyo wimbo unaitwa Mapenzi gani!!
 
aise uzi mzuri haya sasa twende kazi mwenye anaweza kuweka nyimbo za Emanuel Nkulila itapendeza zaidi
 
Nyimbo aa zamani ya Ndala Kasheba Salim Ahmed Salim na mpenzi Rose
 
Back
Top Bottom