Ni wimbo gani unaoutafuta sana bila mafanikio?
Natafuta wimbo ulioimbwa na Mbaraka Mwinshehe wa Super Volcano unaoitwa "Tabia Njema ni Silaha" Kuna clone iliyoimbwa na binti yakr haina ladha nzuri, halafu kuna mtu alipost kipande kifupi pale Youtube ambacho hakitioshi. Nautafuta wimbo wote
Tayari nimeuweka YouTube wimbo wote
 
Mimi natafuta wimbo wa Emmanuel Nkulila ambao jina lake silijui ila ulikuwa unapigwa sana na Radio one stereo miaka ya 1999. Atakayenipatia huu wimbo nitashukuru sana. Nime search sana nyimbo za huyu jamaa utube lakini huu wimbo sijaupata.
 
Kuna wimbo ulipigwa sana miaka ya katikati mwa 1980 .na bendi ya Kenya. Jina lake silijui ila una kipande kinasema " Usikubali kudanganywa na senene..................mabwana wa siku hizi ni waongo"
 
Tupo pamoja boss
Asante sana mzee wangu; umeniondolea kiu ya siku nyingi sana. Halafu huu unasikika safi kabisa kama vile ulivyotoka mara ya kwanza wakati huo miaka ya hiyo ya sabini, nadhani ilikuwa 1977 au 1978 hivi.
 
Mimi natafuta wimbo wa Emmanuel Nkulila ambao jina lake silijui ila ulikuwa unapigwa sana na Radio one stereo miaka ya 1999. Atakayenipatia huu wimbo nitashukuru sana. Nime search sana nyimbo za huyu jamaa utube lakini huu wimbo sijaupata.

 
Kuna wimbo wa injili wa wale mabinti wanaitwa J Sisters unaitwa "achilia roho wako" nautafuta bila mafanikio, maana hata kwenye YouTube yao haupo.
 
Back
Top Bottom