Nifanyeje wanangu wawe na akili nyingi darasani

Nifanyeje wanangu wawe na akili nyingi darasani

Uongoo huo kufanya vizuri sio elimu ya wazazi ni uelewa wa mtu binafsi kuna wale wazito kuelewa na wepesi kuelewajua hilo so usiseme huo ujinga elimu mtu aliyonayo sio vigezo vya watoto kupata ufaulu darasani.
Jamaa fix ingekuwa hvyo kule vijiji kusingekuwa na sekondani

wazee wa zaman walikuwa na elimu gani wengi wameishia darasa la 7 na wana watoto vipanga
 
Miongoni mwa mambo ya maana katika hii dunia mbaya ya siku za mwisho ni Elimu. Kila mzazi anatamani kama mimi ninavyotamani wanangu wawe vichwa darasani katika masomo yao, lakini wengi, kama mimi pia tunaishia kutamani tu hasa tunapoona watoto wa wengine wakifanya maajabu katika masomo yao.

Kwangu mimi wanangu hawaendi nitakavyo, mimi pamoja na wanangu kusoma shule za binafsi, English mid. Anayejua siri ya watoto kufanya vizuri anipe wandugu.

Nimejitahodi kuwakazania kusoma na kuwasaidia mimi mwenyewe. Tuition za kufa mtu, vitabu nanunua. Wakifeli na fimbo wanapata, wakifaulu zawadi wanapata. Lakini sioni kufanya vizuri kule mimi ninakotaka, inaniuma sana.

NIFANYEJE
Siku ukigundua kipaji cha watoto wako kilo kwenye Nyanja zingine za maisha utaacha kuumba gego na kuamini kwenye elimu Walee vizuri wawe wema kama unaamini ktk dini yoyote Ile wakazanie,wafundishe upendo,wawe watu wema Kwa wenzao na wengine pia,wafundishe kuwa na bidii ktk kazi zingine kuosha vyombo NK,usiwaaminishe Tu kwamba elimu ya darasani ndio pekee ktk maisha kuna mengine nje ya uwanja na pia punguza fimbo ndio maana hujagundua bado shida iko wapi unaweza ukawa unawapa zawadi Tu ili wasome vizuri Ila hawako huru kukwambia feelings zao zingine
 
Mwanangu anajua Sana mahesabu yupo kayumba standard 4 akili nyingi sanaa amekua wa 5 Kati ya 278

NB.
Usitegemee kuoa au kujaza mimba mwanamke asiye na akili IQ ukategemea utazaa watoto wenye akili..my friend never.

Nyumbani kwetu tumboni mwa mama angu watoto wake wote wa 5 wote wanaelimu ya chuo kikuu wakati mwingine hizi akili zinaendana na ukoo..
Mbona wazee wetu wa darasa la saba wana watoto vipanga darasan?
 
Jamaa fix ingekuwa hvyo kule vijiji kusingekuwa na sekondani

wazee wa zaman walikuwa na elimu gani wengi wameishia darasa la 7 na wana watoto vipanga
Kuna akili za Maisha na za darasani 👤
Sijuwi unanielewa mfano Mimi Babu yangu watoto wake wote watano walibahatika kufaulu kwenda secondary school vipaji maalum mpaka waliitwa wachawi 😊
 
1.usiwape pressure ya kufaulu
2.safiri nao sehemu mbalimbali yenye mafunzo,mf.moshi mt.kilimanjaro,vijitovya maji,ndege aina mbalimbali,na vitu vingine vingi.
3. Kucheza ni sdhemu ya kurelax kiakili kimwili, .
4. Tafuta mwalimu anayejua kufundisha,yule ambaye ni rafiki kwao.
5.mpende kuomba kila siku ,asubuhi,mchana,jioni.
Wasome biblia sana,...
5.muda wakulala uwepo.
Family meeting,ongeeni nao .

Jingine kuwa mkali sio solution nikuwa mwelewa ndio maisha,kumwonya ni mtu naukali upo tofauti. Good day kingine usiwastress
 
Usiwafananishe na familia nyingine, kuwa karibu nao , shiriki nao katika kazi zao za shule , usikasirike anapokosea mtie moyo.

Binadamu hatujaumbwa sawa katika uelewa wa masomo , hakikisha ule uelewa wa kati anaupata watakushangaza sana huko mbele.
 
Uongoo huo kufanya vizuri sio elimu ya wazazi ni uelewa wa mtu binafsi kuna wale wazito kuelewa na wepesi kuelewajua hilo so usiseme huo ujinga elimu mtu aliyonayo sio vigezo vya watoto kupata ufaulu darasani.
Sasa tuambie kwanini unadhani watoto wengine wanakuwa wazito kuelewa na wengine wepesi kuelewa?

Tuanzie hapo na ukijibu hilo swali vizuri ndio nitajua kiwango cha uelewa wako kuwa ni wale wenye elimu ya tia maji tia maji / elimu ya hapa na pale au upo smart vertically
 
Akili ya darasani ina faida gani? Waombee wawe na akili ya maisha ya kitaa
 
Watoto huwa 70% ya akili hurithi kutoka kwa Mama.

Sasa kama ww ulipenda Matako ndo malipo yake hayo
 
Sasa tuambie kwanini unadhani watoto wengine wanakuwa wazito kuelewa na wengine wepesi kuelewa?

Tuanzie hapo na ukijibu hilo swali vizuri ndio nitajua kiwango cha uelewa wako kuwa ni wale wenye elimu ya tia maji tia maji / elimu ya hapa na pale au upo smart vertically
Mmh! Ni akili ya mtu tu kunamwingine ni mshap katika vitu sio darasani tu. Na mwingine ni mzito kuelewa.
Huyu mzito ni kwa sababu ni mvivu kujishughulisha katika utambuzi wa vitu ,kujishughulisha katika mambo ya kumfanya ubongo uwe active ,yeye hukaa tu kufanya vitu ambavyo havimpi mwongozo wa kufanya vizuri .

Kuogelea humfanya mtoto ajisikie vizuri,kulala na pia kusafiri . Kusoma vitabu na mengineyo
 
Miongoni mwa mambo ya maana katika hii dunia mbaya ya siku za mwisho ni Elimu. Kila mzazi anatamani kama mimi ninavyotamani wanangu wawe vichwa darasani katika masomo yao, lakini wengi, kama mimi pia tunaishia kutamani tu hasa tunapoona watoto wa wengine wakifanya maajabu katika masomo yao.

Kwangu mimi wanangu hawaendi nitakavyo, mimi pamoja na wanangu kusoma shule za binafsi, English mid. Anayejua siri ya watoto kufanya vizuri anipe wandugu.

Nimejitahodi kuwakazania kusoma na kuwasaidia mimi mwenyewe. Tuition za kufa mtu, vitabu nanunua. Wakifeli na fimbo wanapata, wakifaulu zawadi wanapata. Lakini sioni kufanya vizuri kule mimi ninakotaka, inaniuma sana.

NIFANYEJE
Pole sana mkuu,

Kwanza nikupe moyo kitu kiitwacho akili nyingi ni illusion ,Akili nyingi kwenye upande upi?

Mtoto wako(watoto) wanaweza wakawa hawana hizo akili nyingi darasani lakini Kuna sehemu Wana akili nyingi sana lakini hujuhi

Magenius wapo wa kuzaliwa na kutengeneza(Ref Polgar sisters) kila mtu ni genius ni basi TU hatukuandaliwa ama tulikatiwa tamaa na wazazi wetu au walimu wetu mapema.

Naungana na wengine pia waliosema wakati mwengine akili/uelewa kwa wepesi urithiwa kutoka kwa wazazi(hili pia Lina nafasi yake) ,japo ni mjadala wa Nature Vs Nurture .Meaning zinaweza kurithiwa au mazingira yakamshape mtoto kua na ufaham mkubwa.

Nashauri ,acha watoto wasome wapate wanachopata ,Don't over expect much from them , Kazi Yako ni kuwapa vitabu na mahitaji Yao mengine muachie Mungu,Kuwashinikiza sana kwa mikwaju au maneno hakutawasaidia zaidi ya kuwabomoa.
 
Back
Top Bottom