Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wanarithi kwa baba na mama
Kama nyie ni vilaza msahau watoto wenu kua na akili nyingi![]()
Maneno ya busara sana haya. Hasa hili la kuwachapa watoto na kuwatukana ''jinga hili, shuleni halijui kitu''. Halafu unakuta mzazi anajaribu kushindanisha mtoto wake na wengine, eti ni lazima ushike namba moja. Busara ni kumpenda mtoto, kutokum-overwork na kumsaidia kuelewa na siyo kushindana kimasomo.Albert Einstein alipokuwa mvulana mdogo akiwa shuleni, uwezo wake ulikuwa mbovu kiasi kwamba mwalimu alifikia hatua ya kumuambia aache shule kwani hawezi kuja kufanikisha chochote. Lakini ndiye alikuja kuwa winner wa nobel prize 1921, tuzo za heshima kubwa sana duniani.
Thomas Edison mwanasayansi aliyegundua bulb, kipindi ni mvulana mdogo akiwa shuleni uwezo wake darasani ulikuwa mbovu kiasi kwamba mwalimu wake akamuambia ''wewe ni mjinga sana na huwezi ukaelewa chochote'', Siku moja dogo kipindi anatoka shuleni, akamuambia mama yake "mama mwalimu kanipatia karatasi hii, lakini kaniambia usome ni wewe pekee unapaswa kusoma, kwani barua hio inasemaje mama?"
Mama alibubujikwa na machozi na akasoma ile karatasi kwa sauti "mtoto wako ni genius sana, hii shule ni ndogo sana kwake na hakuna walimu wanaoweza kumfundisha, tafadhali mfundishe mwanao mwenyewe."
Miaka mingi baadae baada ya mama yake na Thomas Edison kufariki na Edison amekwisha kuwa mwanasayansi mkubwa wa karne aliweza kukuta ile barua kwenye kabati la nguo la mama yake, kumbe kile kikaratasi kiliandikwa "mtoto wako ana upungufu wa akili, hatuwezi kumuacha aendelee na shule yetu, tumemuachisha shule", kwa lugha ya kiingereza mentally deficiency tukitafsiri ni mtu mwenye upungufu wa akili, wengine huku wanasema dishi limecheza, sasa you can imagine Edison uwezo wake ulivyokuwa mdogo darasani.
Baadae Edison aliandika kwenye diary yake “Thomas A. Edison was a mentally deficient child whose mother turned him into the genius of the century.” --
Akiwa na maana kwamba "Thomas A. Edison alikuwa mtoto mwenye upungufu wa kiakili ambaye mama yake alimgeuza kuwa genius wa karne hii."
Hio tunaita ni nguvu ya maneno, maneno ya mama yalimfanya mtoto awe mgunduzi wa bulb ambayo tunaitumia leo, mkuu jaribu kukaa karibu na watoto wako, wapende, wajali, wape moyo, usiwachape hovyo na kuwaita wajinga ukifikiri unawajenga wakati unawaua ndani kwa ndani, ndio watoto wako Mungu kakupa hakuna wengine, mbeleni wanaweza kuja kufanya maajabu kama Edison 🙂
Sio elimu tu iyo ipo kwenye kila nyanja tunaamini kila mtu anatakiwa kutaabika kwanza kabla ya kufanikiwa. Waafrika tuna uraibu wa kupenda maisha ya shida.Kuna watu wanaamini ugumu wa elimu ndio ubora wa elimu.
Sioo kweliii mkuuu nakupinga hiloo ndoaa pekee ndio inafwata ukoo wenh watototo akili zaoo na jinsi ta kuwatengeneza wawe vichwa ngoja nkakojoe narudiAkili hufuata mkondo,kama wazazi bichwa maji,likewise kwa watoto,hakuna dawa hapo ulikosea kuchagua mke kilaza kwa kuangalia shape badala ya kichwa
Kuishia darasa la saba hakumaanishi mama yao hana akili. Aidha, wewe kuwa na digrii hakumainishi kuwa una akili kuliko mke wako. Kuwachapa wakishindwa kupata maksi unazotaka wewe hakusaidii isipokuwa kunawatia uoga kiasi cha kutofanya vizuri. Waonyeshe upendo na uwatie moyo kila wakifanya vibaya. Angalia wanapenda vitu gani ( hata upishi ni fani nzuri) na uwape moyo wajiendeleze huko. Wewe ni mtu wa IT, washirikishe katika mambo unayofanya. Badala ya kufanya mambo ya darasani kuwa ni kigezo pekee wekeza nguvu zaidi kuwa wanakuwa na tabia njema na upendo kwa binadamu wengine. Mwisho, ujue kuwa kuna wanaoitwa late bloomers. Unaweza kushangaa watakavyokuwa vipanga wakipata fani wanayoipenda na kuimudu.Mama ni wa la saba tu, baba ana diploma ya IT, na anadigrii ya uongozi na maendeleo ya jamii, pia anacheti ya veta ya udereva. Huyo bado sio, hata kwao baba ndugu zake ni wasomi waziristan tu hata mzazi wa baba naye msomi mzuri tu.
Hii kitu bila supplement ya heavy protine ya maziwa na samaki kwisha habari ya watoto kuwa na akili. tegemea kuwa na makuli na wasukuma mikokoteni wenye manguvu.Mtoto anatengenezwa siku 1000 za mwanzo ukikosea hapo tegemea muujiza mtoto kuwa kipanga, sijasema hawez ila ni nadra sana.
Swali la msingi, unawalisha wanao ugali?
Ni kweli mkuu, mtoto akishakuwa kwenye hofu, hawezi kujiamini tena, hivyo itampelekea kutojiamini kwenye kila jambo.Maneno ya busara sana haya. Hasa hili la kuwachapa watoto na kuwatukana ''jinga hili, shuleni halijui kitu''. Halafu unakuta mzazi anajaribu kushindanisha mtoto wake na wengine, eti ni lazima ushike namba moja. Busara ni kumpenda mtoto, kutokum-overwork na kumsaidia kuelewa na siyo kushindana kimasomo.
Alikimbilia matakoAkili hufuata mkondo,kama wazazi bichwa maji,likewise kwa watoto,hakuna dawa hapo ulikosea kuchagua mke kilaza kwa kuangalia shape badala ya kichwa
Mkuu watakuwaje na akili nyingi wakati wazazi wenyewe akili zenu za kuungaunga kwa gundi!Miongoni mwa mambo ya maana katika hii dunia mbaya ya siku za mwisho ni Elimu. Kila mzazi anatamani kama mimi ninavyotamani wanangu wawe vichwa darasani katika masomo yao, lakini wengi, kama mimi pia tunaishia kutamani tu hasa tunapoona watoto wa wengine wakifanya maajabu katika masomo yao.
Kwangu mimi wanangu hawaendi nitakavyo, mimi pamoja na wanangu kusoma shule za binafsi, English mid. Anayejua siri ya watoto kufanya vizuri anipe wandugu.
Nimejitahodi kuwakazania kusoma na kuwasaidia mimi mwenyewe. Tuition za kufa mtu, vitabu nanunua. Wakifeli na fimbo wanapata, wakifaulu zawadi wanapata. Lakini sioni kufanya vizuri kule mimi ninakotaka, inaniuma sana.
NIFANYEJE
Kwenye ugali mkuu umedanganya! Kwenye mahindi kuna co-enzyme ya muhimu sana katika kuimarisha akili kama ulikuwa hujui! Sisi tuliokuwa tunakamata nguna kwa samaki na maziwa pembeni darasani tulikuwa njema sana!Ukitaka kuwa na watoto vipanga darasani hakikisha unaoa mke kipanga haswa.Yaani mkeo awe mwerevu Kweli Kweli.
Then hakikisha watoto wako hawali ugali kbsa coz Ni chakula kinachodumaza akili.
Siyo Kwa damu ya kibongo....bila fimbo Maji hayapandi ni wachache mno eatapandaKwanza wanajitambua yaani wana uelewa mzuri ukitoa mambo ya shule?
Ikiwa jibu ni ndio waelekeze katika vipawa vyao zaidi .
Mfano ikiwa hawapati A Ila pia hawapiati D basi hao wako vizuri.
Mimi Kama Mwalimu natoa ushauri kuwa tumia mbinu za kuwajengea mentality ya ushindi kuanzia ndani yao. Hii waweza tumia subconscious mind.
Usitumie nguvu kubwa mfano viboko nk hizo mbinu hazisaidii chochote.
Mtoto mjenge taratibu kwa kumtia moyo na hata akipata marks ndogo wewe mtie moyo
Acha kujidanganya wewe. Kupata A ni kipimo kizuri na cha kuaminika kwa mtoto. Sifuri ni dalili ya ujinga.Wabongo tunadanganyw sana na zile A na Division 1 kwamba ndio akili zenyewe. Akili sio kupata A mtoto anaweza pata zero darasana lakini akawa na akili nyingi sana za kufanya mambo makubwa sana.Akili ni pale mind ya mtoto inapo weza kutafasiri au kuchakata yale masomo na kufanya vitu vikibwa sana.
Bahati mbaya tulienda kusomea A na kushindana kutafuta Division ndio maana tuko hapa tulipo.
Shida ni pale tunapo ingizwa chaka na kulipa mamilion ya pesa ili watoto wapate A na Waongee Kingereza.
Ndio maana tuna import kila kitu make tumewekeza sana tena mno kutafuta A na Division One.
Kama una mtoto ambaye ana think beyond darasani hio ndio akili yenyewe, kama anasoma na unaona anafanyia kazi anayo yasoma hio ndio akili. Ila kama ni bingwa wa kupata A hizo ni kukariri tu, sana wanakaririshwa wajibu papper wapate A