Niko njia panda yenye maumivu moyoni: Biashara yangu imelala sana je, niende kwa mganga?

Niko njia panda yenye maumivu moyoni: Biashara yangu imelala sana je, niende kwa mganga?

1. Nina watoto wawili wako Shule...
Mmoja darasa la 3 mwengine kaanza la kwanza.

Wote wapo Dar wanasoma Private, Kazi yangu ni kutuma ada na school bus fees.

2. Nisiende kwa waganga ila NIMUOMBE MUNGU [emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]
MGANGA huwa anamuomba nani?

Nakumbuka nilisoma mwaka wa 1 bachelor kwenye foundation of Faith (African religous Vs. western religoous facts).

Anyway MUNGU YUPO.

#YNWA


#YNWA
Kumbe wee Ni kiaz HV unasema mganga anaomba kwa Nani Mbna una majibu ya kipuuz HV kama wee na familia yenu Ni washirikina nenda huko Kama unaona watakuokoa kwenye biashara zako


Je lini umewahi kufanya tour kwenye maduka mengine au wale wateja wako wanauzaje kwa Sasa HV na Ni Wapi wanapata mzigo hujawi wee uko hapa kuomba uungwaji mkono juu ya uganga


Na Bado itadorora Hadi umtafute mwamposa alipo

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Huna haja ya kukata tamaa mwezi mmoja tu unawaza wataalam, huu mwezi ni mgumu wengine hapa unaenda kupambana unarudi kama ulivyoenda ndio biashara waulize wateja wako mnaoshibana kama wanauza kama zamani kabla haujaenda kuharibu,pesa za masharti hazina Raha muda zinaisha.
 
Kumbe wee Ni kiaz HV unasema mganga anaomba kwa Nani Mbna una majibu ya kipuuz HV kama wee na familia yenu Ni washirikina nenda huko Kama unaona watakuokoa kwenye biashara zako


Je lini umewahi kufanya tour kwenye maduka mengine au wale wateja wako wanauzaje kwa Sasa HV na Ni Wapi wanapata mzigo hujawi wee uko hapa kuomba uungwaji mkono juu ya uganga


Na Bado itadorora Hadi umtafute mwamposa alipo

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app

Cool down buddy..!!
"Kiazi" stop attacking people personally..!!

Halafu mwamposa hivi analipa kodi na ile biashara yake ya Mafuta ya upako?

#YNWA
 
Kwa kukufahamisha mwanadamu hapati janga lolote isipokuwa kutokana na chumo la mikono yake.

Sasa mbona watu wa dini mnatuchanganya..
Wachungaji husema, biblia inasema "Mapito hayapaswi kuja ......" Yaani Mungu karuhusu majanga kutupima.

Wewe Mzee wa Quran unasema "Tunayaleta"

Kwahiyo wa Ukraine wamefanya nini kustahili machumo Yale wapitiayo sasa?

#YNWA
 
Mimi ni mtumishi wa umma Ila pia nina ndoto za kuwa mfanyabiashara mkubwa sanaa...
Hivyo vitu mara nyingi haviendi Pamoja.

USHAURI

Watengenezee Ofa ya Valentine mwezi huu. Punguza kidogo faida yako wape Offer. Hii pia iwe mbinu ya kuzungumza na Wateja wako(Yaani upate cha kuanzia kuongea na Mteja wako kwenye Simu). Jaribu hili kwa Wiki hii then uone Mwitikio wa Wateja wako. Wajulishe hii Offfer wale wateja wako WAKUBWA wengi kuliko wadogo.

Hakuna mganga zaidi ya MUNGU. Usidanganywe na hao Washikaji zako.

Mwisho kabisa Mkuu Liverpool VPN , Magumu huyapitii peke yako kaka, na hakuna ambaye hajatoka mbali. Just Relax hizo ni changamoto za kawaida saaaaaana katika Biashara. Ulitakiwa uanze kuwa na Mashaka endapo hio hali itaendelea for 3 months consecutive.
 
Hivyo vitu mara nyingi haviendi Pamoja.

USHAURI

Watengenezee Ofa ya Valentine mwezi huu. Punguza kidogo faida yako wape Offer. Hii pia iwe mbinu ya kuzungumza na Wateja wako(Yaani upate cha kuanzia kuongea na Mteja wako kwenye Simu). Jaribu hili kwa Wiki hii then uone Mwitikio wa Wateja wako. Wajulishe hii Offfer wale wateja wako WAKUBWA wengi kuliko wadogo.

Hakuna mganga zaidi ya MUNGU. Usidanganywe na hao Washikaji zako.

Mwisho kabisa Mkuu Liverpool VPN , Magumu huyapitii peke yako kaka, na hakuna ambaye hajatoka mbali. Just Relax hizo ni changamoto za kawaida saaaaaana katika Biashara. Ulitakiwa uanze kuwa na Mashaka endapo hio hali itaendelea for 3 months consecutive.
Umempatia wazk zuri sema naona tayari Imani yake iko rigid akadai kuwa Ana masters amesoma vitabu vya robati kiyosaki as if ni guarantee ukivisoma unatoka
 
Unakosa Business psychology due to lack of experience. Business almost zote huwa na uptrend, down trend and sometimes huwa na consolidations za kutosha. Kuna biashara nyingine, miezi kadhaa huwa na faida ndogo sana lakini hapo unatakiwa uwe na subira maana unaweza kuwa na mauzo machache mwezi mmoja au miwili ila miezi mingine ukapiga pesa ambayo itafidia miezi yote uliyokuwa chini. Achana na mambo ya waganga.
 
Hivyo vitu mara nyingi haviendi Pamoja.

USHAURI

Watengenezee Ofa ya Valentine mwezi huu. Punguza kidogo faida yako wape Offer. Hii pia iwe mbinu ya kuzungumza na Wateja wako(Yaani upate cha kuanzia kuongea na Mteja wako kwenye Simu). Jaribu hili kwa Wiki hii then uone Mwitikio wa Wateja wako. Wajulishe hii Offfer wale wateja wako WAKUBWA wengi kuliko wadogo.

Hakuna mganga zaidi ya MUNGU. Usidanganywe na hao Washikaji zako.

Mwisho kabisa Mkuu Liverpool VPN , Magumu huyapitii peke yako kaka, na hakuna ambaye hajatoka mbali. Just Relax hizo ni changamoto za kawaida saaaaaana katika Biashara. Ulitakiwa uanze kuwa na Mashaka endapo hio hali itaendelea for 3 months consecutive.

Najua ajira na biashara haviendi pamoja ila sikua na njia ya kupata mtaji zaidi ya mshahara.

Na kwa hii biashara nathibitisha Asilimia 100 mtaji umetoka kazini.

Kwahiyo bila huu Utumishi wa umma NISINGEKUWA HAPA.

#YNWA
 
MGANGA ATANIRUDISHA KWELI KWENYE RELI.

INTRODUCTION:

Mimi ni mtumishi wa umma Ila pia nina ndoto za kuwa mfanyabiashara mkubwa sanaa...

Na nikiri NAPENDA HELA SAA.
Yaani ukitaka niwe na Amani basi laki kadhaa ziwe kwenye wallet yangu.

Katika kukimbiza ndoto zangu niliamua kufungua biashara ya vinywaji ya Jumla na rejareja (jina la mtaani tunaita Depo).

Nilikusanya mtaji nikiwa tayari nina idea na ilipofika mil 9 nikafungua depo.
Mil 6 bidhaa na mil 3 sunk cost kama kodi, Matengenezo frame na mengine yale ya maandalizi ya biashara.

Nauza vinywaji vyotee vikali na baridi, kwa jumla na reja reja, na kwasasa biashara yangu ina mtaji wa mil 25.

SCENARIO
Biashara ilianza vizurii mpaka nikawa nadata, yaani wateja walikuwa wengii.

Hawa wakani-force kukuza mtaji fasta mpaka kufika hizo mil 25.

Pia nikawa na vijana wa3 wa dukani, yaani ni fast delivery. Yaani mteja akikata tu simu basi bidhaa ipo mlangoni mwake.

Aisee nilipata jina fasta na kubwaa sanaa.

Mauzo yangu yalikuwa makubwa ya mil 3 Kwa siku na siku nisipouza yalikuwa hayashuki mil 1.

Kwasasa Nina Miaka kadhaa kwenye biashara (from July 2020).

Ila ndugu sasa biashara sielewi..

PROBLEM
Tokea January 2023 BIASHARA IMEKUWA NGUMU mnooo.

Mauzo mil 1 Tena jana ndio Majanga, nimefunga na laki 5..!!!

Pia hapa Nina miamala ya simu, na juzi (01/02) nililipwa commission ya 150k kwa mitandao yotee mi 4.

Wakati nilifika commison ya laki 5 kwa mitandao yote mi4.

Wateja simu sizioni, wakati Kuna kipindi walikua wanapiga simu mpaka saa 7 usiku kuniomba niwauzie bidhaa.

Hiyo saa 7 usiku watakukodia boda utakuja kufungua store utawauzia, wanakulipa na boda inakurudisha gheto kwa gharama zao.

Nina masters na bachelor ya mambo ya biashara, hivyo nimejaribu marketing skills kibao kama za kutuma sms kila asubuhi kuomba order kwa wateja, kupost status za WhatsApp ila 2023 bado ngumu kwenye biashara.

Sasa nimeshauriwa na raia NIENDE KWA MTAALAMU NIKAPIKWE.

Naambiwa, nilikua na nyota kalii hivyo competitor wameona waizime ili wao wauze.

DILEMA
Nimedata mwenzenu, ukicheki hii biashara ndio naitegemea kuwa ndio tobo la kunifanya nije kuachana na ajira za serikali ya CCM ila MBELE NAONA GIZA.

Nina mengi aisee siwezi kuandika yote, mfano: siku hizi nafungua saa 1 kamili asubuhi na kufunga saa 5 usiku.
Na hata kazini (halmashauri) nimepasusa naona pananichanganya tu (wiki yotee hii (Tokea 30/01)SIJAFIKA KAZINI.

KUHUSU VITABU-
Hivi vitabu sijui vya Robert koyasaki na wengine NIMESOMA SANAAA.
Tokea 2020 nishasoma vitabu kama 30 hivi vya mambo ya biashara na fedha na Robert Koyasaki pekee yake ni vitabu vi5 kuanzaia Rich Dad mpaka Money Quadrant.

Vingi vinazungumzia "Kwenye financial world Usikate tamaa, pambana"" ila nahisi Kuna kamba ipo nyuma ya mapambano yangu inanivuta nyuma.

NAPAMBANA NYIE...
1. Muda wote duka nalifanya safi
2. Rangi zinavutia (mashelf na ukuta)
3. Kama elimu, Nina degree mbili za biashara (bachelor + masters)
4. Kama ni experince, nishauza sanaa biashara za watu Tena bila mshahara (kipindi najifunza biashara)
5. Kama ni ukarimu, basi ni mkarimu sanaa. Humu Kuna watu wawili tulishaongea sanaa Japo kwa simu (kama wako comfortable wanaweza thibitisha hapa).

Kifupi nafanya mengii ila 2023 imekua ngumu.
Imefikia mpaka kupunguza wafanyakazi dukani kutoka 3 mpaka 1..!!!

Na kilichonifanya nipost ni baada ya commision kushuka kutoka 500k mpak 150k kwa Jauary/2023.

Huwezi amini:-
Jumapili ya wiki hii sikufungua, ili tu nione upepo wa wateja, ila chakusangaza mpaka unaingia usiku sijapokea simu hata ya mteja mmoja kulalamika "Mbona nimefunga"

Kwasasa sijui si-exist kwenye phone book zao..!! Niko kudata balaaa yaani waliokuwa wakinipigia simu usiku nao hawapigi hata mchana..!!!

Kazini sijaenda wiki maana kichwa ni cha moto balaaa.

Nipeni mawazo wajasiliamali wenzangu.
Nipeni mawazo wafanyabiashara wenzangu.

Nishapitia msoto mkubwa sanaa kwenye maisha ya uyatima, kazini, kwenye ujana wangu ila Jambo gumu linapogusa biashara NADATA KABISAAAA.

Nahitaji kuacha Kazi na hili ndio TOBO LANGU.

MGANGA ATANIRUDISHA KWELI KWENYE RELI?

#YNWA
yaani january ambayo kila mtu analia pesa zote zimeenda mashuleni hata wenye mabasi ya abiria wamepunguza mabasi barabarani kwa sababu abiria ni wachache, hilo umeshindwa kuliona, umeanza kulia na kutamani kwenda kwa wachawi. Pole sana.....watu kama wewe ndiyo mnaamini ushirikina kuliko uhalisia.
 
yaani january ambayo kila mtu analia pesa zote zimeenda mashuleni hata wenye mabasi ya abiria wamepunguza mabasi barabarani kwa sababu abiria ni wachache, hilo umeshindwa kuliona, umeanza kulia na kutamani kwenda kwa wachawi. Pole sana.....watu kama wewe ndiyo mnaamini ushirikina kuliko uhalisia.
Ni kweli kuna jamaa yangu ana biashara ya usafirishaji kwasasa kayasimamisha. Ni kipindi tu
 
MGANGA ATANIRUDISHA KWELI KWENYE RELI.

INTRODUCTION:

Mimi ni mtumishi wa umma Ila pia nina ndoto za kuwa mfanyabiashara mkubwa sanaa...

Na nikiri NAPENDA HELA SAA.
Yaani ukitaka niwe na Amani basi laki kadhaa ziwe kwenye wallet yangu.

Katika kukimbiza ndoto zangu niliamua kufungua biashara ya vinywaji ya Jumla na rejareja (jina la mtaani tunaita Depo).

Nilikusanya mtaji nikiwa tayari nina idea na ilipofika mil 9 nikafungua depo.
Mil 6 bidhaa na mil 3 sunk cost kama kodi, Matengenezo frame na mengine yale ya maandalizi ya biashara.

Nauza vinywaji vyotee vikali na baridi, kwa jumla na reja reja, na kwasasa biashara yangu ina mtaji wa mil 25.

SCENARIO
Biashara ilianza vizurii mpaka nikawa nadata, yaani wateja walikuwa wengii.

Hawa wakani-force kukuza mtaji fasta mpaka kufika hizo mil 25.

Pia nikawa na vijana wa3 wa dukani, yaani ni fast delivery. Yaani mteja akikata tu simu basi bidhaa ipo mlangoni mwake.

Aisee nilipata jina fasta na kubwaa sanaa.

Mauzo yangu yalikuwa makubwa ya mil 3 Kwa siku na siku nisipouza yalikuwa hayashuki mil 1.

Kwasasa Nina Miaka kadhaa kwenye biashara (from July 2020).

Ila ndugu sasa biashara sielewi..

PROBLEM
Tokea January 2023 BIASHARA IMEKUWA NGUMU mnooo.

Mauzo mil 1 Tena jana ndio Majanga, nimefunga na laki 5..!!!

Pia hapa Nina miamala ya simu, na juzi (01/02) nililipwa commission ya 150k kwa mitandao yotee mi 4.

Wakati nilifika commison ya laki 5 kwa mitandao yote mi4.

Wateja simu sizioni, wakati Kuna kipindi walikua wanapiga simu mpaka saa 7 usiku kuniomba niwauzie bidhaa.

Hiyo saa 7 usiku watakukodia boda utakuja kufungua store utawauzia, wanakulipa na boda inakurudisha gheto kwa gharama zao.

Nina masters na bachelor ya mambo ya biashara, hivyo nimejaribu marketing skills kibao kama za kutuma sms kila asubuhi kuomba order kwa wateja, kupost status za WhatsApp ila 2023 bado ngumu kwenye biashara.

Sasa nimeshauriwa na raia NIENDE KWA MTAALAMU NIKAPIKWE.

Naambiwa, nilikua na nyota kalii hivyo competitor wameona waizime ili wao wauze.

DILEMA
Nimedata mwenzenu, ukicheki hii biashara ndio naitegemea kuwa ndio tobo la kunifanya nije kuachana na ajira za serikali ya CCM ila MBELE NAONA GIZA.

Nina mengi aisee siwezi kuandika yote, mfano: siku hizi nafungua saa 1 kamili asubuhi na kufunga saa 5 usiku.
Na hata kazini (halmashauri) nimepasusa naona pananichanganya tu (wiki yotee hii (Tokea 30/01)SIJAFIKA KAZINI.

KUHUSU VITABU-
Hivi vitabu sijui vya Robert koyasaki na wengine NIMESOMA SANAAA.
Tokea 2020 nishasoma vitabu kama 30 hivi vya mambo ya biashara na fedha na Robert Koyasaki pekee yake ni vitabu vi5 kuanzaia Rich Dad mpaka Money Quadrant.

Vingi vinazungumzia "Kwenye financial world Usikate tamaa, pambana"" ila nahisi Kuna kamba ipo nyuma ya mapambano yangu inanivuta nyuma.

NAPAMBANA NYIE...
1. Muda wote duka nalifanya safi
2. Rangi zinavutia (mashelf na ukuta)
3. Kama elimu, Nina degree mbili za biashara (bachelor + masters)
4. Kama ni experince, nishauza sanaa biashara za watu Tena bila mshahara (kipindi najifunza biashara)
5. Kama ni ukarimu, basi ni mkarimu sanaa. Humu Kuna watu wawili tulishaongea sanaa Japo kwa simu (kama wako comfortable wanaweza thibitisha hapa).

Kifupi nafanya mengii ila 2023 imekua ngumu.
Imefikia mpaka kupunguza wafanyakazi dukani kutoka 3 mpaka 1..!!!

Na kilichonifanya nipost ni baada ya commision kushuka kutoka 500k mpak 150k kwa Jauary/2023.

Huwezi amini:-
Jumapili ya wiki hii sikufungua, ili tu nione upepo wa wateja, ila chakusangaza mpaka unaingia usiku sijapokea simu hata ya mteja mmoja kulalamika "Mbona nimefunga"

Kwasasa sijui si-exist kwenye phone book zao..!! Niko kudata balaaa yaani waliokuwa wakinipigia simu usiku nao hawapigi hata mchana..!!!

Kazini sijaenda wiki maana kichwa ni cha moto balaaa.

Nipeni mawazo wajasiliamali wenzangu.
Nipeni mawazo wafanyabiashara wenzangu.

Nishapitia msoto mkubwa sanaa kwenye maisha ya uyatima, kazini, kwenye ujana wangu ila Jambo gumu linapogusa biashara NADATA KABISAAAA.

Nahitaji kuacha Kazi na hili ndio TOBO LANGU.

MGANGA ATANIRUDISHA KWELI KWENYE RELI?

#YNWA
Acha imani potofu wewe! Hata mimi pia ni mdundulizaji, natokea Tanga! Lakini sijatanguliza hizo imani za kishirikina. Huko ukienda utaishia tu kupigwa, na kupotea mazima.

Biashara kuna wakati inapooza kidogo! Halafu kuna wakati inachangamka. Hivyo jitahidi kuwa mpole. Na usisahau hii miezi ya mwanzoni mwa mwaka, watu wako busy na ada. Hivyo baadhi wanapunguza matumizi yasiyo ya lazima, yakiwemo hayo ya vinywaji.

Mambo yakitengemaa utaendelea kulaza hizo milioni zako 2-3 kwa siku.


Ila binadamu tunatofautiana! Mimi kwenye kijiwe changu nikilaza laki, basi ujue siku hiyo mambo yameenda vizuri. Sasa wewe laki 5 unataka kwenda mpaka kwa mganga wa kienyeji! 🤔
 
MKuu pole kwa kipindi unachopitia kibiashara.
Kwa ufupi tambua biashara ina kupanda na kushuka kwahiyo ukiona imeshuka unapaswa kuangalia je wakati huo biashara huwa zinakuwa chini?
Kuna nyakati ambazo biashara inakuwa mbaya tuu si kuwa unakosea mahali ila ni kipindi ambacho watu hawali na hawanywi.

Ukiona kuwa ni kipindi ambacho biashara inatakiwa kuwa juu na unafanya vibaya basi inafaa ujitathimini wapi unakosea.
Kunakipindi kwenye biashara hata ufanye matangazo huwezi ongeza kitu maana ni kipindi za mzoroto wa biashara mkuu

Ushauri wangu kwako. Tuliza kichwa na anza kupitia jambo moja moja katka nlokwandikia.

Mganga achana naeee atakuondoa kwenye mstari wako milele
 
Back
Top Bottom