Niliamua kumuacha huyu 'wife material' sababu ya umasikini wa kwao

Niliamua kumuacha huyu 'wife material' sababu ya umasikini wa kwao

Ipo shida

Ipo shida kubwa sana kuoa kwenye familia maskini sana kweli.Sababu ziko nyingi,ila tatu kubwa outstanding ni uelewa mdogo,kutojiamini na kuwa na maono madogo ambayo huwa nayaita ya Kuku.Kila kitu yeye sijui,it is so boring,Haya matatizo matatu yanawafanya Wanawake wanaotoka kwenye familia maskini kushindwa kabisa kuwa na msaada kimaisha kwenye familia zao.Mara nyingi wanabaki kuwa tegemezi na mzigo mkubwa kwenye familia.Ila wakiwa wamesoma inapunguza tatizo kwa kiwango kikubwa sana.

Mkuu mbona kama unafananisha elimu na umaskini, inawezekana mwanamke akawa na elimu ya juu na ufahamu mkubwa ila alipotokea hasa huko vijijini ni masikini.
 
Mwanamke akishakuwa Wife material (MKE Bora/Mwema) hicho ndio kigezo kikubwa cha kumfanya Aolewe.

Umaskini wa kwao haumhusu na hauhusu ndoa yenu ikiwa hauathiri U-wife material wake.

Sidhani kama Mtoa mada anazungumzia tukio halisi. Ila anachojaribu kukifanya ni kuwaambia Wanawake waache Tabia ya kuangalia wanaume Kwa kigezo cha Mali na utajiri wa nyumbani kwao.
Bali waangalie kama Mwanaume anavigezo vya kuwa Mume Bora(husband material) basi waolewe naye.

Mtoa mada anajaribu kueleza kuwa hata Sisi wanaume tunaouwezo wa Kutumia kigezo cha umaskini na kukosa Pesa Kwa Wanawake kuwabagua na kutokuwafanya kuwa Wake zetu. Kama vile baadhi ya Wanawake wanavyobagua wanaume Maskini.

Na hili likifanyika na tayari siku hizi linafanyika, basi Wanawake wengi watajikuta kwenye Wakati Mgumu kwani kiasili Wanawake hawakuumbwa kuwa watafutaji.

Msimamo wangu;
Sisi wote ni binadamu, tuna makundi yetu yanayotutofautisha, kimaumbile, kifikra, kiuchumi, kivipaombele, kiutamaduni n.k
Kila MTU atafute wakufanana naye linapokuja suala la Ndoa. Hiyo ndio huitwa Familia.

Maskini Kwa Maskini
Matajiri Kwa matajiri
Wazuri Kwa wazuri
Wabaya Kwa wabaya
Watawala Kwa Watawala
Watawaliwa Kwa watawaliwa.
Waovu Kwa waovu
Wema Kwa Wema.
Werevu Kwa Werevu
Wajinga Kwa wajinga

Kama MTU anataka kuvunja boundaries basi awe na chaku-offer
Mfano, MTU ni masikini anataka kuolewa na Tajiri. Basi itampasa awe Mzuri au mwenye Akili Sana.
Lakini tofauti na hapo ni kutafuta machafuko, kunyanyasana, na kubaguliwa.

Mwanaume anaoa Mwanamke anayefanana naye. Ukiona mwanaume anafanya uchaguzi katika kuoa, akapata Mwanamke vile umuonavyo Mwanamke huyo ndivyo alivyo Mumewe bila kujali yupoje.
Sasa hapo ndipo kipengele kilipo

Mwanzo 2:24
18 BWANA Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye. . 20Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye.


Mambo ya Walawi 19:19 SRUV
Mtazishika amri zangu. Usiwaache wanyama wako wa mfugo wakazaana kwa namna mbalimbali; usipande shamba lako mbegu za namna mbili pamoja; wala usivae mwilini mwako nguo ya namna mbili zilizochanganywa pamoja
Umeiweka vizuri sana
 
Mwanamke akijua kwenu hamna kitu lazma akutose.Watoto wa kimaskini wengi walengaji
Ndo ivyo mr unapokuwa upo vizur kiuchumi unatakiwa demu umfanyie interview akwambie anafanya kazi gani na ujue kiuchumi yukoje kama vile wanavyo tufanyia sisi interview kujua tunafanya kazi gani tuna pesa au huna akijua huna anakupiga chini mr hawa viumbe ukiwa na pesa utakiwi kuwa na uluma nao hawa ww kwa maskini uwone kama utapata demu mkali uwone mr
 
Halafu familia nyingi za kichawi hupenda kumuua mume wa mtoto wao, ni swala la muda tu !

Usije ukasema Mbona wana kupenda, Mbona wana kutegemea?

Aaah wapi?!

Wakishatega rada zao wakati ukifika wanamtungua mtu!

Akishakufa mume wa mtoto wao wanalia Kwa unafiki huku wakisema “watu wema hawaishi miaka mingi, hawafiki umri mkubwa “

Utasikia “kauli ya Mungu hakuna wakuipinga”kumbe ni wao wenyewe wachawi wameamua kumtanguliza!

The world is not fair sometimes,

Utawatendea mema watu wa kwenu na wakwezo, utakuwa tegemeo la wengi sawa, lakini sio guarantee kwamba wataacha kukupiga vita kubwa na uadui pamoja na mema unayowatendea!

Uchawi roho mbaya sana!

Hasidi hakosi sababu!
 
Ndo ivyo mr unapokuwa upo vizur kiuchumi unatakiwa demu umfanyie interview akwambie anafanya kazi gani na ujue kiuchumi yukoje kama vile wanavyo tufanyia sisi interview kujua tunafanya kazi gani tuna pesa au huna akijua huna anakupiga chini mr hawa viumbe ukiwa na pesa utakiwi kuwa na uluma nao hawa ww kwa maskini uwone kama utapata demu mkali uwone mr
Demu anakupimia kama ofisi sio bank au serikalini TRA huko anakuona mwehu tu
 
I’m impressed much with that last sentence!

Kwamba “ ng’ombe wa maskini hazai”

Maana yake hakuna mazidisho na maongezeko (additions and multiplications).
Mungu hakutuumba tuwe masikini, pia hakutupa utajiri

Diamond
Harmonize
Rayvany
Samata

Hawa wasingejikaza wangekuwa masikini pia.
Hawakutaka lalamika, waliamua jikaza.

Mi naamini utajiri ni matokeo ya kufikiria tofauti na wengine
 
Ndo ivyo mr unapokuwa upo vizur kiuchumi unatakiwa demu umfanyie interview akwambie anafanya kazi gani na ujue kiuchumi yukoje kama vile wanavyo tufanyia sisi interview kujua tunafanya kazi gani tuna pesa au huna akijua huna anakupiga chini mr hawa viumbe ukiwa na pesa utakiwi kuwa na uluma nao hawa ww kwa maskini uwone kama utapata demu mkali uwone mr
Kabisaa
 
Kuoa au kuolewa kwenye familia masikini ni mzigo ikiwa uko commited kujaribu kuwasaidia na wakawa hawaoni msaada wako....lakini kikubwa ni amani yenu na kustiliana kwenye hali zote... uwazi na upendo, hutajutia na Mungu wa Kweli hakutupi ukiwa na moyo wa utoaji. Utakuwa umefanya kosa sana kumwacha mtu anaekuheshimu ( ndio kupenda kwa wanaume) ukamkimbilia uliemtamani kisa familia yao inakauwezo.
Kadri utakavyoendelea kukua utaelewa ujinga ulioufanya na gharama zake kwenye furaha na amani ya moyo wako.
 
Wengine huona umasikini ndo gia ya kwenda mbinguni



Na kweli [emoji3]
Eti wanafikiri kuwa maskini ni mapenzi ya Mungu [emoji28]

Umaskini unaongelewa kwenye Biblia ni umaskini wa roho na sio wa mwilini.

Imeandikwa: “Kheri maskini wa roho maana hao watamuona Mungu”

Hilo neno roho linamaana kubwa sana.

Maskini wa roho sio maskini wa mwilini.

Kuna majitu huko Japan , China, Korea kaskazn hawamjui Mwenyezi Mungu wala hawaamini katika ufunuo wa wafu na kuwa na maisha mengine badala ya haya wanafanikiwa sana si sababu ya imani zao bali sababu ya kanuni moja ya kufanya kazi Kwa bidii na maarifa.

Hata chuo kikuu utakuta majitu kama mapagani vile , hayasali wala kuswali lakini ndio yanaongoza kupita kwenye red carpets [emoji108][emoji108]

Majamaa yanasoma Kwa bidii kubwa sana!

Walokole na wale swala wanadema!

Kanuni ya msingi ya maisha ni kufanya kazi matokeo utayaona halisi.

Ijapokuwa binafsi huwa naona iwapo mtu anasoma kwa kukesha ndipo ashinde mtihani basi mtu huyo asijione mashine wala kipanga.

Mashine inapaswa kurahisisha kazi, sasa wewe unakesha kusoma ukifaulu ujione mashine?! Hapana !
 
Back
Top Bottom