Nilichelewa sana kujua kwamba Mungu Baba ni huyu Baba yangu mzazi aliyenizaa na kunilea. Mzee nisamehe kwa kuabudu miungu wengine

Naona we huelewi ata una uliza nini, pengine Ulitaka nikwambie Mungu ni jirani yangu ndio uamini
Hapo ndio umethibitisha uwepo wa Mungu ? Mungu muweza wa yote hajawahi kuwepo ni nadharia tu ,nabinadamu ndio kaunda nadharia hiyo.
 
Hapo ndio umethibitisha uwepo wa Mungu ? Mungu muweza wa yote hajawahi kuwepo ni nadharia tu ,nabinadamu ndio kaunda nadharia hiyo.
“Mtu asiye na uzoefu huamini kila neno, lakini mtu mwerevu huzifikiria hatua zake.” (Methali 14:15 ) Biblia huwatia moyo Wakristo watumie ‘nguvu zao za kufikiri’ ili wajithibitishie wenyewe mambo wanayofundishwa.— Waroma 12:1, 2 .
 
Hayo ni maneno ya kiimani , ambayo pia yametungwa , bado haujathibitisha uwepo wa Mungu muweza wa yote anaechoma wanaomkosea .
 
Halafu pia huyo mungu kwanini awe mungu baba au mungu mwana kwanini apewe sifa za watu😀
Hayo ni maneno ya kiimani , ambayo pia yametungwa , bado haujathibitisha uwepo wa Mungu muweza wa yote anaechoma wanaomkosea .
 
Hayo ni maneno ya kiimani , ambayo pia yametungwa , bado haujathibitisha uwepo wa Mungu muweza wa yote anaechoma wanaomkosea .
Mkuu wewe unafuata mkumbo.
soma Bible kwa makini Hakuna sehemu Mungu amesema anachoma moto watu
 
Mkuu wewe unafuata mkumbo.
soma Bible kwa makini Hakuna sehemu Mungu amesema anachoma moto watu
Haunijui ,sikujui , kitabu hicho hakina uthibitisho wa uwepo wa Mungu kwanza kina mikanganyiko ya kutosha .



1. Mathayo 25:41
Yesu anasema, "Ndipo atakapowaambia wale walio kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake." Mstari huu unazungumzia moto wa milele kama adhabu kwa wasiomtii Mungu.


2. Ufunuo 20:10, 14-15

"Na yule Ibilisi aliyewapotosha, akatupwa katika lile ziwa la moto na kiberiti..."
Na tena: "Kisha mauti na kuzimu vikatupwa katika lile ziwa la moto. Hili ndilo mauti ya pili, yaani, lile ziwa la moto."


3. Marko 9:43
Yesu anasema, "Kama mkono wako unakukosesha, ukate. Ni afadhali kuingia katika uzima umepungukiwa na mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili ukaenda katika Gehena, kwenye moto usiozimika."


4. 2 Petro 3:7
"Lakini mbingu za sasa na dunia zimewekwa akiba kwa moto, zikiwekwa kwa siku ya hukumu na uangamivu wa watu wasiomcha Mungu."
 
Halafu pia huyo mungu kwanini awe mungu baba au mungu mwana kwanini apewe sifa za watu😀
Huyu Mungu ni dhaifu mno akikosewa na viumbe alivyo umba mwenyewe anakasirika eti ,wakati ni yeye mwenyewe kaviumba na hayo mapungufu 🤔
 
Uzuri wa haya mambo hakuna wa kukushikia bunduki Ili uamini kama Mungu yupo ni ubongo wako tu utakapokueleza
 
Ziwa la moto linawakilisha kifo cha aina tofauti, au cha pili. Ingawa kifo hicho kinawakilisha hali ya kutotenda kabisa, ni tofauti na kifo cha kwanza kwa sababu Biblia haisemi lolote kuhusu ufufuo kutokana na kifo cha pili.

Kwa mfano, Biblia inasema kwamba Yesu ana “funguo za mauti na za kuzimu [au, moto wa mateso],” kuonyesha kwamba ana mamlaka ya kuwafungua watu kutokana na kifo kinacholetwa kutokana na dhambi ya Adamu. ( Ufunuo 1:18; 20:13 , Union Version ) Hata hivyo, Yesu hana funguo za ziwa la moto wala hakuna mtu aliye na funguo hizo. Ziwa hilo la mfano linawakilisha adhabu ya milele inayoletwa kupitia uharibifu wa milele.— 2 Wathesalonike 1:9 .

Ina maana sawa na Gehena, Bonde la Hinomu
Gehena (Kigiriki geʹen·na ) inatajwa mara 12 katika Biblia. Kama lile ziwa la moto, Gehena ni neno linalowakilisha uharibifu wa milele. Ingawa watafsiri fulani hutumia neno hilo kumaanisha “moto wa mateso,” Gehena inatofautiana na moto wa mateso ( Kiebrania sheʼohlʹ, Kigiriki
haiʹdes )
 
Mistari mitano ya Biblia inayotaja “ziwa la moto” inalionyesha kuwa ziwa la mfano, si ziwa halisi. ( Ufunuo 19:20; 20:10, 14, 15; 21:8 )

Wafuatao watatupwa ndani ya ziwa la moto:
Ibilisi. (Ufunuo 20:10 ) Kwa kuwa Ibilisi ni kiumbe wa roho, hawezi kuumizwa na moto halisi.—Kutoka 3:2; Waamuzi 13:20 .
Kifo.

(Ufunuo 20:14 ) Kifo si kitu halisi lakini ni hali ya kutotenda, kutokuwepo kwa uhai . (Mhubiri 9:10 ) Kifo hakiwezi kuteketezwa.

Mnyama-mwitu” na “yule nabii wa uwongo.” ( Ufunuo 19:20 ) Kwa kuwa vyote viwili ni vitu vya mfano, je, haipatani na akili kufikiri kwamba ziwa hilo pia ni la mfano?—
Ufunuo 13:11, 12; 16:13 .
 
Ndio maana nikakumbia hizi ni hadithi tu haimaanishi ni ukweli , ndio maana inatakiwa uamini na sio kujua , watakuja wa dini nyingne nao wana hadithi zao tofauti kabisa na yakwako , bado haithibitishi uwepo wa Mungu kwa namna yoyote ile.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…