Nilichokiona mara ya kwanza baada ya kuagiza kitu ebay

Nilichokiona mara ya kwanza baada ya kuagiza kitu ebay

Nilikuwa sijawahi kufanya manunuzi ya kitu mtandaoni, kwa mara ya kwanza tarehe 5/08/2024 nilifanya manunuzi ya miwani ya macho katika mtandao wa eBay, hii ni baada ya miwani yangu kupasuka.
Niliingia katika mtandao wa eBay, nikasearch aina ya miwani ninayoitaka, nilishangaa sana bei nilizoziona, kuna miwani ya macho inauzwa mpaka dollar 3 😂😂😂.
Nilichagua aina ya miwani inayonifaa, bei yake ilikuwa ni dollar 5, free international shipping.
Tarehe 18/09/2024 nilitumiwa sms kuwa mzigo wangu umefika posta ya wilaya niliyopo, hivyo natakiwa niende kuuchukua, jana tarehe 19/09/2024 nimeenda Posta kuchukua mzigo wangu, miwani nimeikuta iko vizuri, na prescription zangu zimefuatwa vyema kabisa.

Sasa kuna mama nilimkuta pale ofisini posta, ni mtoa huduma wa pale. Nilimuuliza maswali kadhaa kuhusu kuagiza vitu nje na gharama ambazo ninatakiwa kulipia pale Posta. Yule mama alinielekeza kuwa hii mizigo tunayoagiza nje huwa tunapewa tracking number, kama tracking number yako inaanza na herufi R, ina maana mzigo wako umetumwa kwa kutumia Registered tracking code, inamaana mzigo wako ukifika Posta utapigiwa simu ukauchukue na hautolipia kodi yoyote, utachukua mzigo wako bila malipo yoyote. Lakini akaniambia kuwa kama tracking number yako inaanza na herufi tofauti na R, mzigo wako ukifika Posta utalipia kiasi cha shilingi 3000. Hii 3000 unapewa control number kisha unafanya malipo, baada ya kukamilisha malipo unapewa mzigo wako.
Lakini nilimuuliza swali, vipi kama mzigo wangu ni mkubwa unavuka kilo 5, yule mama aliniambia package za aina hiyo huwa zinakuja na maelekezo kutoka makao makuu, ila kodi yake haizidi shilingi 10000, hivyo aliniambia niache uoga kama kuna kitu nataka kuagiza niagize tu.

Okay, sasa mimi nina swali wataalamu wa hizi mbanga. Ninawezaje kuagiza mzigo kwa dealer ambayo nina uhakika atanimba tracking number ambayo ni registered, yaani tracking number inayooanzia na herufi R?
Ebay!

Mzigo kama umeagiza USA, ama Ulaya kuna mingine utalipia pesa ya Posta na baada ya kulipia watakwambia subiria mtu wa TRA aje akufanyie makadirio ya kodi😀😀😀
 
Na mzigo wako ulifanya kazi vizuri mpaka leo? Mana mm niliwahi kuagiza SSD kupitia kikuu ila haikufanya kazi.
Nimeagiza vitu kupitia kikuu mda sasa, nimegundua kuwa hizo SSD, flash na memory cards nyingi ni magumashi sana kutoka kikuu. So far ni flash moja tu ilifanya kazi, memory cards, baadhi ya flash na ssd hadi leo zipo hazifanyi kazi.
 
Ninachoona mimi mzigo ni afadhali upitie Posta ambayo iko nje ya mji wa Dar Es Salaam, nilipokuwa naagiza na mizigo ikipitia Dar Es Salaam ilikuwa ni lazima nilipie lakini tangu nimeanza kupitishia Posta ya huu mkoa ninaoishi sijawahi kulipia.
Mkuu unatuchomesha sasa
 
siku nyingine ni MARUFUKU kuagiza kwa kutumia soko mjinga la kuitwa Kikuu. we huoni jina lenyewe limekaa kidwanzi.
Sijawahi kukutana na changamoto yoyote kupitia kwao, labda kuchelewesha mzigo, nayo sio mara zote. Hawajawahi kunitapeli
 
Nimeagiza vitu kupitia kikuu mda sasa, nimegundua kuwa hizo SSD, flash na memory cards nyingi ni magumashi sana kutoka kikuu. So far ni flash moja tu ilifanya kazi, memory cards, baadhi ya flash na ssd hadi leo zipo hazifanyi kazi.
Kila nikichomeka SSD kwenye pc inanitaka nii-format nikaona ujinga huu nikampa dogo afanye kama rula shulen
 
Cha kwanza Kabisa wawe na account huko ebay na muhimu wewe na PayPal ndio tamu maana hizi kadi za tigo na voda mda mwingine zinaleta usumbufu sana

Duh Bora uagize za AliExpress au ebay mkuu
si mtumie MasterCard za bank tu mbona ni rahisi zaidi mpk mtapetape..😅
 
Mzee wa Series naomba mwongozo jinsi ya kuanza kufanya manunuzi ebay
Cha kwanza kuwa na kadi za kulipia mtandaoni kama MasterCard za bank PayPal afu hapo fungua account hapo ebay

Cha pili
Nunua kwa muuzaji anayekubaliwa na weteja wengi.

Utajuaje kama muuzaji anakubalika sokoni na anauzoefu wa kuuza vitu kwenye mtandao? Rahisi! Kwa mfanounataka kununua saa Ebay au kitabu cha electrniki (PDF) kwenye Amazon, chini ya hiyo bidhaa iliyoichagua utaona maoni ya watu walionunua kabla yako

Cha tatu
Chagua namna ya kutumiwa mzigo wako.

Unatakiwa kuchagua namna kutumiwa mzigo wako ambayo itakuwa rahisi kwako kuupata. Gharama za kutuma mzigo zitaoneshwa pale kwenye mtandao na muda wa kufika kwa kila gharama.

Cha nne
Hakikisha muuzaji anahudumia eneo ulilopo.

Baadi ya wauzaji huchagua nchi au miji wanayoweza kutuma mizigo na wengine huuza dunia nzima. Taarifa hizi huwekwa chini ya bidhaa unayotaka kununua , hii itakusaidia kuokoa muda kuondoa usumbufu usio wa lazima.
 
Mimi nimewahi kuagiza simu zaidi ya mara nne, saa za mkononi mara tatu saa niliyovaa sasa hivi niliagiza online, niliwahi kuagiza smart watch, earpods nk.

Muongozo ni wewe kujisajili kwenye app husika kwa kuweka taarifa zako sahihi, mfano wa taarifa ni jina lako, address yako ya posta, namba ya simu nk.

Kuhusu namna ya kufanya malipo napo ni rahisi tu, mfano mimi nimewahi kufanya malipo kupitia MasterCard kwa maana ya kadi yangu ya NMB, sasa hii ya NMB inabidi uende kwenye branch ili waiwezeshe kufanya malipo online. Visa card ya CRDB yenyewe imeshawezwesha kufanya miamala online , uchaguzi ni wako.

Nimeona mdau amegusia swala mitandao kama tigo au voda,, huko sina utaalamu nako nazungumzia kile nimekiishi. Mtandao ambao nimeagiza bidhaa ni AliExpress huko eBay sijawahi kuagiza. Mwanzoni kutokana na uoga nilikuwa naagiza tuvitu tudogo tudogo na tunafika fresh tu, baadae nikaanza kuagiza items mpaka za 700K.

Ukizoea kuagiza online raha sana utajikuta hata soksi unaagiza online.. karibuni kwa swali au nyongeza ya maelezo ambapo hujaelewa. Kuagiza bidhaa inawezekana wala usihofu.


NB: Sio lazima uwe na sanduku la posta hata ukiandika la mtu mwingine au taasisi unayofanyia wewe andika physical address ya mahali ulipo mfano Bagamoyo, kumbuka mahali ulipo pawe na posta, kwisha habari
Uoga ni pale ambapo unashindwa kuelewa hii ni og au feki kwa maana pale ni mwendo wa picha tu afu kuna bidhaa unakuta bei iko chinii mno mpk unahisi kama ni feki
 
Yaani sasa tupe elimu jinsi ya kuagiza bidhaa bila usumbufu. Mkuu sisi wengine bado tupo kwenye mfumo wa 'Pager' yaani kama vile VW Beetle, Ford Cortina, Morris Marina, n.k.
Okay, mimi nafahamu kuagiza bidhaa kwa kutumia mtandao wa ebay.

Hatua ya kwanza kabla haujaanza kuagiza bidhaa ebay, unatatakiwa ujiunge na mtandao wa ebay, yaani ufungue akaunti ili uweze kufanya manunuzi.
Utajisajili hapa kwenye hii link.
Security Measure

Hatua ya pili, baada ya kuwa umejisajili. Utatakiwa kuweka taarifa za mahali ambapo unahitaji mzigo utumwe endapo utafanya manunuzi.

IMG_20240920_153804.jpg

Ukishakamilisha usajili utaingia kwenye akaunti yako, kisha utabonyeza hako kamshkaji nilikokazungushia duara.

Itakuletea hivi.
IMG_20240920_154303.jpg

Ikikuletea hivi utabonyesha hapo palipoandikwa Account, nimezungushia duara nyekundu.
Ukibonyeza hapo, itakuleta hapa
👇👇👇
IMG_20240920_154858.jpg

Hapa utajaza taarifa zako binafsi kama vile email na namba za simu, pia sehemu unapoishi na Zip Code, Zip Code utagoogle tu, kwa mfano kama unaishi Mtama, utaenda google utaandika "Mtama Zip Code" zitakuja zip code za Mtama, utachagua iliyosahihi kulingana na eneo unaloishi.
Ukishamaliza hiki kipengere, utarudi tena hapo kwenye kimtu, utabonyeza tena kwenye neno Account, kisha utabonyeza kwenye payments (duara nyekundu).
Yaani hapa 👇👇👇
IMG_20240920_160040.jpg

Hapo utapewa njia za malipo, utaweka namba zako za kadi ya benki, kama unatumia Paypal unaweza pia kuweka taarifa zako za PayPal(email).
Ukikamilisha hivi vipengere vyote unakuwa upo tayari kununua bidhaa yoyote katika mtandao wa ebay.

Hatua ya pili, kutafuta vitu unavyotaka kununua.
Ebay homepage utakutana na hii sehemu iliyozungushiwa duara nyekundu.
IMG_20240920_160936.jpg

Hapo andika kitu unachokitaka. Kwamfano tunaandika "laptop", kisha tunasearch.

Watatuletea matokeo ya "laptop" kama hivi. 👇👇👇
IMG_20240920_161714.jpg

Ukiangalia hapo juu unaona kuna duara nyekundu nimezungusha, ina maneno All, Auction, Buy It Now. Yeah, uzuri wa ebay ni kuwa kuna vitu huwa vinauzwa kwa mnada, kwa hiyo kama unataka kuona laptops ambazo zinauzwa kwa njia ya mnada utabonyeza hapo palipoandikwa Auction, kama unataka vitu vinavyouzwa kawaida utabonyeza hapo palipoandikwa Buy It Now, kama unataka kuona vitu mchanganyiko utaacha hapo kwenye All.

Tufanye umechagua bidhaa ambayo inauzwa kawaida, sio mnada yaani Buy It Now.
Itakuleta hapa 👇👇👇
IMG_20240920_163633.jpg

Utabonyeza hapo palipoandikwa Buy It Now.
Itakuleta kwenye sehemu inayoitwa Checkout, hapa utathibitisha mahali unapotaka mzigo utumwe, na njia unayotaka kutumia kufanya malipo utaithibitisha ama kuibadilisha hapa.
Itakuwa kama hivi 👇👇👇
IMG_20240920_164248.jpg

Ukishakubaliana na hizo taarifa hapo juu, utabonyeza hapo palipoandikwa "confirm and pay"

Tufanye umechagua bidhaa ambayo inauzwa kwa njia ya Auction.
Itakuletea hivi 👇👇👇

IMG_20240920_162636.jpg

Kama bidhaa umeipenda na unataka kuipigania, utabonyeza hapo palipoandikwa place bid. Ukishabonyeza hapo utaingiza kiasi ambacho upo tayari kutoa, lakini kumbuka kiasi utakachoingiza ni lazima kiwe kikubwa kuliko mtu wa mwisho. Nadhani unaelewa namna mnada unavyofanya kazi. Ukishinda mnada utatakiwa kuilipia bidhaa.

🤔🤔🤔Pia bila kusahau, ebay wana kitu inaitwa eBay money back guarantee, yaani hapa mzee ikitokea umepokea mzigo na ukakuta upo tofauti na maelezo na picha za muuzaji, una uwezo wa kufungua madai na kurudishiwa pesa zako.

eBay Money Back Guarantee

Aisee, mkongwe nimejitahidi sana kukuelekeza japo kuna mambo mengi sana pia nimeyaacha, kuna mengine utajifunza kwa njia ya AAANHA KUMBE CONCEPT 😂😂😂
Kama kuna sehemu haujaelewa utauliza swali, tutasaidiana na wadau wengine kukujibu.
 
Okay, mimi nafahamu kuagiza bidhaa kwa kutumia mtandao wa ebay.

Hatua ya kwanza kabla haujaanza kuagiza bidhaa ebay, unatatakiwa ujiunge na mtandao wa ebay, yaani ufungue akaunti ili uweze kufanya manunuzi.
Utajisajili hapa kwenye hii link.
Security Measure

Hatua ya pili, baada ya kuwa umejisajili. Utatakiwa kuweka taarifa za mahali ambapo unahitaji mzigo utumwe endapo utafanya manunuzi.

View attachment 3101114
Ukishakamilisha usajili utaingia kwenye akaunti yako, kisha utabonyeza hako kamshkaji nilikokazungushia duara.

Itakuletea hivi.
View attachment 3101115
Ikikuletea hivi utabonyesha hapo palipoandikwa Account, nimezungushia duara nyekundu.
Ukibonyeza hapo, itakuleta hapa
👇👇👇
View attachment 3101118
Hapa utajaza taarifa zako binafsi kama vile email na namba za simu, pia sehemu unapoishi na Zip Code, Zip Code utagoogle tu, kwa mfano kama unaishi Mtama, utaenda google utaandika "Mtama Zip Code" zitakuja zip code za Mtama, utachagua iliyosahihi kulingana na eneo unaloishi.
Ukishamaliza hiki kipengere, utarudi tena hapo kwenye kimtu, utabonyeza tena kwenye neno Account, kisha utabonyeza kwenye payments (duara nyekundu).
Yaani hapa 👇👇👇
View attachment 3101121
Hapo utapewa njia za malipo, utaweka namba zako za kadi ya benki, kama unatumia Paypal unaweza pia kuweka taarifa zako za PayPal(email).
Ukikamilisha hivi vipengere vyote unakuwa upo tayari kununua bidhaa yoyote katika mtandao wa ebay.

Hatua ya pili, kutafuta vitu unavyotaka kununua.
Ebay homepage utakutana na hii sehemu iliyozungushiwa duara nyekundu.
View attachment 3101142
Hapo andika kitu unachokitaka. Kwamfano tunaandika "laptop", kisha tunasearch.

Watatuletea matokeo ya "laptop" kama hivi. 👇👇👇
View attachment 3101152
Ukiangalia hapo juu unaona kuna duara nyekundu nimezungusha, ina maneno All, Auction, Buy It Now. Yeah, uzuri wa ebay ni kuwa kuna vitu huwa vinauzwa kwa mnada, kwa hiyo kama unataka kuona laptops ambazo zinauzwa kwa njia ya mnada utabonyeza hapo palipoandikwa Auction, kama unataka vitu vinavyouzwa kawaida utabonyeza hapo palipoandikwa Buy It Now, kama unataka kuona vitu mchanganyiko utaacha hapo kwenye All.

Tufanye umechagua bidhaa ambayo inauzwa kawaida, sio mnada yaani Buy It Now.
Itakuleta hapa 👇👇👇
View attachment 3101173
Utabonyeza hapo palipoandikwa Buy It Now.
Itakuleta kwenye sehemu inayoitwa Checkout, hapa utathibitisha mahali unapotaka mzigo utumwe, na njia unayotaka kutumia kufanya malipo utaithibitisha ama kuibadilisha hapa.
Itakuwa kama hivi 👇👇👇
View attachment 3101174
Ukishakubaliana na hizo taarifa hapo juu, utabonyeza hapo palipoandikwa "confirm and pay"

Tufanye umechagua bidhaa ambayo inauzwa kwa njia ya Auction.
Itakuletea hivi 👇👇👇

View attachment 3101156
Kama bidhaa umeipenda na unataka kuipigania, utabonyeza hapo palipoandikwa place bid. Ukishabonyeza hapo utaingiza kiasi ambacho upo tayari kutoa, lakini kumbuka kiasi utakachoingiza ni lazima kiwe kikubwa kuliko mtu wa mwisho. Nadhani unaelewa namna mnada unavyofanya kazi. Ukishinda mnada utatakiwa kuilipia bidhaa.

Aisee, mkongwe nimejitahidi sana kukuelekeza japo kuna mambo mengi sana pia nimeyaacha, kuna mengine utajifunza kwa njia ya AAANHA KUMBE CONCEPT 😂😂😂
Kama kuna sehemu haujaelewa utauliza swali, tutasaidiana na wadau wengine kukujibu.
Kamanda bila kupepesa macho nakupa 5🌟 umejitahidi saana na kupitia hii comment yako kuna watu wataanza kufanya manunuzi
 
Kamanda bila kupepesa macho nakupa 5🌟 umejitahidi saana na kupitia hii comment yako kuna watu wataanza kufanya manunuzi
😂😂😂
Hapo tumeacha masuala ya tracking number, na vitu vingine vidogo vidogo ambavyo ni rahisi kuvijua akishapita hizo hatua zote.
 
Back
Top Bottom