Nilichokiona mara ya kwanza baada ya kuagiza kitu ebay

Nilichokiona mara ya kwanza baada ya kuagiza kitu ebay

Okay, mimi nafahamu kuagiza bidhaa kwa kutumia mtandao wa ebay.

Hatua ya kwanza kabla haujaanza kuagiza bidhaa ebay, unatatakiwa ujiunge na mtandao wa ebay, yaani ufungue akaunti ili uweze kufanya manunuzi.
Utajisajili hapa kwenye hii link.
Security Measure

Hatua ya pili, baada ya kuwa umejisajili. Utatakiwa kuweka taarifa za mahali ambapo unahitaji mzigo utumwe endapo utafanya manunuzi.

View attachment 3101114
Ukishakamilisha usajili utaingia kwenye akaunti yako, kisha utabonyeza hako kamshkaji nilikokazungushia duara.

Itakuletea hivi.
View attachment 3101115
Ikikuletea hivi utabonyesha hapo palipoandikwa Account, nimezungushia duara nyekundu.
Ukibonyeza hapo, itakuleta hapa
👇👇👇
View attachment 3101118
Hapa utajaza taarifa zako binafsi kama vile email na namba za simu, pia sehemu unapoishi na Zip Code, Zip Code utagoogle tu, kwa mfano kama unaishi Mtama, utaenda google utaandika "Mtama Zip Code" zitakuja zip code za Mtama, utachagua iliyosahihi kulingana na eneo unaloishi.
Ukishamaliza hiki kipengere, utarudi tena hapo kwenye kimtu, utabonyeza tena kwenye neno Account, kisha utabonyeza kwenye payments (duara nyekundu).
Yaani hapa 👇👇👇
View attachment 3101121
Hapo utapewa njia za malipo, utaweka namba zako za kadi ya benki, kama unatumia Paypal unaweza pia kuweka taarifa zako za PayPal(email).
Ukikamilisha hivi vipengere vyote unakuwa upo tayari kununua bidhaa yoyote katika mtandao wa ebay.

Hatua ya pili, kutafuta vitu unavyotaka kununua.
Ebay homepage utakutana na hii sehemu iliyozungushiwa duara nyekundu.
View attachment 3101142
Hapo andika kitu unachokitaka. Kwamfano tunaandika "laptop", kisha tunasearch.

Watatuletea matokeo ya "laptop" kama hivi. 👇👇👇
View attachment 3101152
Ukiangalia hapo juu unaona kuna duara nyekundu nimezungusha, ina maneno All, Auction, Buy It Now. Yeah, uzuri wa ebay ni kuwa kuna vitu huwa vinauzwa kwa mnada, kwa hiyo kama unataka kuona laptops ambazo zinauzwa kwa njia ya mnada utabonyeza hapo palipoandikwa Auction, kama unataka vitu vinavyouzwa kawaida utabonyeza hapo palipoandikwa Buy It Now, kama unataka kuona vitu mchanganyiko utaacha hapo kwenye All.

Tufanye umechagua bidhaa ambayo inauzwa kawaida, sio mnada yaani Buy It Now.
Itakuleta hapa 👇👇👇
View attachment 3101173
Utabonyeza hapo palipoandikwa Buy It Now.
Itakuleta kwenye sehemu inayoitwa Checkout, hapa utathibitisha mahali unapotaka mzigo utumwe, na njia unayotaka kutumia kufanya malipo utaithibitisha ama kuibadilisha hapa.
Itakuwa kama hivi 👇👇👇
View attachment 3101174
Ukishakubaliana na hizo taarifa hapo juu, utabonyeza hapo palipoandikwa "confirm and pay"

Tufanye umechagua bidhaa ambayo inauzwa kwa njia ya Auction.
Itakuletea hivi 👇👇👇

View attachment 3101156
Kama bidhaa umeipenda na unataka kuipigania, utabonyeza hapo palipoandikwa place bid. Ukishabonyeza hapo utaingiza kiasi ambacho upo tayari kutoa, lakini kumbuka kiasi utakachoingiza ni lazima kiwe kikubwa kuliko mtu wa mwisho. Nadhani unaelewa namna mnada unavyofanya kazi. Ukishinda mnada utatakiwa kuilipia bidhaa.

Aisee, mkongwe nimejitahidi sana kukuelekeza japo kuna mambo mengi sana pia nimeyaacha, kuna mengine utajifunza kwa njia ya AAANHA KUMBE CONCEPT 😂😂😂
Kama kuna sehemu haujaelewa utauliza swali, tutasaidiana na wadau wengine kukujibu.
Natumia NMB hiyo huduma ya Paypal unajiunga au?
 
Natumia NMB hiyo huduma ya Paypal unajiunga au?
Hao PayPal ni kama mtu wa kati kwenye kufanya malipo, wanasaidia kulinda taarifa zako za kibenki kupitia kadi yako.

Unachokifanya unajiunga na PayPal, halafu unawaruhusu wawe wanatoa pesa kwenye akaunti yako pale unapofanya malipo mtandaoni, kwahiyo badala ya kuandika taarifa za kadi yako unapofanya manunuzi unaandika email uliyotumia kujiandikisha Paypal.

Pia faida nyingine ya PayPal ni kuwa ikitokea umepokea mzigo wa ovyo, PayPal watabeba jukumu la kurudisha pesa yako kutoka kwa muuzaji aliyekufanyia uhuni.

Jisajili PayPal hapa👇👇
PayPal
 
Hao PayPal ni kama mtu wa kati kwenye kufanya malipo, wanasaidia kulinda taarifa zako za kibenki kupitia kadi yako.

Unachokifanya unajiunga na PayPal, halafu unawaruhusu wawe wanatoa pesa kwenye akaunti yako pale unapofanya malipo mtandaoni, kwahiyo badala ya kuandika taarifa za kadi yako unapofanya manunuzi unaandika email uliyotumia kujiandikisha Paypal.

Pia faida nyingine ya PayPal ni kuwa ikitokea umepokea mzigo wa ovyo, PayPal watabeba jukumu la kurudisha pesa yako kutoka kwa muuzaji aliyekufanyia uhuni.
Prices zimewekwa in US DOLLARS kama nini fedha in TSH inakuwaje hapo
 
Screenshot_3.png
 
Tafuta bidhaa ukiiipenda angalia reviews za watu walionunua hiyo bidhaa kujiridhisha la sivyo baadhi ya bifhaa ambazo hakuna reviews ikikufikia unaweza ukajicheka mwenyewe.
Hakika, hili ni jambo la msingi sana, unakuta muuzaji hana review hata moja, halafu unaenda tu kichwakichwa unanunua bidhaa yake. Lazima ule za kichwa.

Pia kuna uhuni mwingine nimeuona eBay, unaweza kukuta iphone 14 Pro inauzwa. Kwenye picha limewekwa boksi la simu jipya kabisa. Ukiangalia bei ni kitonga mpaka macho yanakutoka.
Kichwa kimeshapagawa na Iphone ya bei chee, na uvivu wa kusoma maelezo unakurupuka unafanya malipo kumbe wahuni wamekuwekea boksi tupu, na kwenye maelezo ya bidhaa katikati au mwisho unakuta wamekuchomekea neno EMPTY BOX.
 
Cha kwanza kuwa na kadi za kulipia mtandaoni kama MasterCard za bank PayPal afu hapo fungua account hapo ebay

Cha pili
Nunua kwa muuzaji anayekubaliwa na weteja wengi.

Utajuaje kama muuzaji anakubalika sokoni na anauzoefu wa kuuza vitu kwenye mtandao? Rahisi! Kwa mfanounataka kununua saa Ebay au kitabu cha electrniki (PDF) kwenye Amazon, chini ya hiyo bidhaa iliyoichagua utaona maoni ya watu walionunua kabla yako

Cha tatu
Chagua namna ya kutumiwa mzigo wako.

Unatakiwa kuchagua namna kutumiwa mzigo wako ambayo itakuwa rahisi kwako kuupata. Gharama za kutuma mzigo zitaoneshwa pale kwenye mtandao na muda wa kufika kwa kila gharama.

Cha nne
Hakikisha muuzaji anahudumia eneo ulilopo.

Baadi ya wauzaji huchagua nchi au miji wanayoweza kutuma mizigo na wengine huuza dunia nzima. Taarifa hizi huwekwa chini ya bidhaa unayotaka kununua , hii itakusaidia kuokoa muda kuondoa usumbufu usio wa lazima.
Very useful.
 
Okay, mimi nafahamu kuagiza bidhaa kwa kutumia mtandao wa ebay.

Hatua ya kwanza kabla haujaanza kuagiza bidhaa ebay, unatatakiwa ujiunge na mtandao wa ebay, yaani ufungue akaunti ili uweze kufanya manunuzi.
Utajisajili hapa kwenye hii link.
Security Measure

Hatua ya pili, baada ya kuwa umejisajili. Utatakiwa kuweka taarifa za mahali ambapo unahitaji mzigo utumwe endapo utafanya manunuzi.

View attachment 3101114
Ukishakamilisha usajili utaingia kwenye akaunti yako, kisha utabonyeza hako kamshkaji nilikokazungushia duara.

Itakuletea hivi.
View attachment 3101115
Ikikuletea hivi utabonyesha hapo palipoandikwa Account, nimezungushia duara nyekundu.
Ukibonyeza hapo, itakuleta hapa
👇👇👇
View attachment 3101118
Hapa utajaza taarifa zako binafsi kama vile email na namba za simu, pia sehemu unapoishi na Zip Code, Zip Code utagoogle tu, kwa mfano kama unaishi Mtama, utaenda google utaandika "Mtama Zip Code" zitakuja zip code za Mtama, utachagua iliyosahihi kulingana na eneo unaloishi.
Ukishamaliza hiki kipengere, utarudi tena hapo kwenye kimtu, utabonyeza tena kwenye neno Account, kisha utabonyeza kwenye payments (duara nyekundu).
Yaani hapa 👇👇👇
View attachment 3101121
Hapo utapewa njia za malipo, utaweka namba zako za kadi ya benki, kama unatumia Paypal unaweza pia kuweka taarifa zako za PayPal(email).
Ukikamilisha hivi vipengere vyote unakuwa upo tayari kununua bidhaa yoyote katika mtandao wa ebay.

Hatua ya pili, kutafuta vitu unavyotaka kununua.
Ebay homepage utakutana na hii sehemu iliyozungushiwa duara nyekundu.
View attachment 3101142
Hapo andika kitu unachokitaka. Kwamfano tunaandika "laptop", kisha tunasearch.

Watatuletea matokeo ya "laptop" kama hivi. 👇👇👇
View attachment 3101152
Ukiangalia hapo juu unaona kuna duara nyekundu nimezungusha, ina maneno All, Auction, Buy It Now. Yeah, uzuri wa ebay ni kuwa kuna vitu huwa vinauzwa kwa mnada, kwa hiyo kama unataka kuona laptops ambazo zinauzwa kwa njia ya mnada utabonyeza hapo palipoandikwa Auction, kama unataka vitu vinavyouzwa kawaida utabonyeza hapo palipoandikwa Buy It Now, kama unataka kuona vitu mchanganyiko utaacha hapo kwenye All.

Tufanye umechagua bidhaa ambayo inauzwa kawaida, sio mnada yaani Buy It Now.
Itakuleta hapa 👇👇👇
View attachment 3101173
Utabonyeza hapo palipoandikwa Buy It Now.
Itakuleta kwenye sehemu inayoitwa Checkout, hapa utathibitisha mahali unapotaka mzigo utumwe, na njia unayotaka kutumia kufanya malipo utaithibitisha ama kuibadilisha hapa.
Itakuwa kama hivi 👇👇👇
View attachment 3101174
Ukishakubaliana na hizo taarifa hapo juu, utabonyeza hapo palipoandikwa "confirm and pay"

Tufanye umechagua bidhaa ambayo inauzwa kwa njia ya Auction.
Itakuletea hivi 👇👇👇

View attachment 3101156
Kama bidhaa umeipenda na unataka kuipigania, utabonyeza hapo palipoandikwa place bid. Ukishabonyeza hapo utaingiza kiasi ambacho upo tayari kutoa, lakini kumbuka kiasi utakachoingiza ni lazima kiwe kikubwa kuliko mtu wa mwisho. Nadhani unaelewa namna mnada unavyofanya kazi. Ukishinda mnada utatakiwa kuilipia bidhaa.

🤔🤔🤔Pia bila kusahau, ebay wana kitu inaitwa eBay money back guarantee, yaani hapa mzee ikitokea umepokea mzigo na ukakuta upo tofauti na maelezo na picha za muuzaji, una uwezo wa kufungua madai na kurudishiwa pesa zako.

eBay Money Back Guarantee

Aisee, mkongwe nimejitahidi sana kukuelekeza japo kuna mambo mengi sana pia nimeyaacha, kuna mengine utajifunza kwa njia ya AAANHA KUMBE CONCEPT 😂😂😂
Kama kuna sehemu haujaelewa utauliza swali, tutasaidiana na wadau wengine kukujibu.
Asante mkuu!
 
Sio mbaya, ni kama Bi Mkubwa alivyosema, haizidi 10000.
Hii sio kodi ila ni gharama za usafirishaji za posta. Inawezekana wanapima uzito wa kitu ili kujua unatakiwa ulipie shilingi ngapi. Shirika la posta halisafirishi bidhaa bure. Ukiona hujalipa chochote posta basi ujue ni bahati tu unaipata.
Kuhusu kulipa kodi ya kitu ulichoagiza inategemea kama TRA wamehusishwa au la. Ikiwa wamehusishwa na posta ujue lazima ulipe kodi na usishangae au kuhuzunika maana ni kawaida. Tena unaweza walipa posta pesa yao na TRA pesa yao.
Kwa kuhitimisha tu ni kuwa kuna tofauti kubwa kati ya gharama za posta kukusafurishia mzigo wako toka posta makao makuu hadi posta yako wewe uliopo na kodi(TRA). Hivi ni vitu viwili na taasisi mbili tofauti.
 
Hao PayPal ni kama mtu wa kati kwenye kufanya malipo, wanasaidia kulinda taarifa zako za kibenki kupitia kadi yako.

Unachokifanya unajiunga na PayPal, halafu unawaruhusu wawe wanatoa pesa kwenye akaunti yako pale unapofanya malipo mtandaoni, kwahiyo badala ya kuandika taarifa za kadi yako unapofanya manunuzi unaandika email uliyotumia kujiandikisha Paypal.

Pia faida nyingine ya PayPal ni kuwa ikitokea umepokea mzigo wa ovyo, PayPal watabeba jukumu la kurudisha pesa yako kutoka kwa muuzaji aliyekufanyia uhuni.

Jisajili PayPal hapa👇👇
PayPal
Mkuu naona aliexpress vitu vingi ni kama fake tofauti na ebay
 
Ebay & Amazon via DHL huduma yao safi kabisa....nimeanza kutrade nao 2014.
 
Nilikuwa sijawahi kufanya manunuzi ya kitu mtandaoni, kwa mara ya kwanza tarehe 5/08/2024 nilifanya manunuzi ya miwani ya macho katika mtandao wa eBay, hii ni baada ya miwani yangu kupasuka.
Niliingia katika mtandao wa eBay, nikasearch aina ya miwani ninayoitaka, nilishangaa sana bei nilizoziona, kuna miwani ya macho inauzwa mpaka dollar 3 😂😂😂.
Nilichagua aina ya miwani inayonifaa, bei yake ilikuwa ni dollar 5, free international shipping.
Tarehe 18/09/2024 nilitumiwa sms kuwa mzigo wangu umefika posta ya wilaya niliyopo, hivyo natakiwa niende kuuchukua, jana tarehe 19/09/2024 nimeenda Posta kuchukua mzigo wangu, miwani nimeikuta iko vizuri, na prescription zangu zimefuatwa vyema kabisa.

Sasa kuna mama nilimkuta pale ofisini posta, ni mtoa huduma wa pale. Nilimuuliza maswali kadhaa kuhusu kuagiza vitu nje na gharama ambazo ninatakiwa kulipia pale Posta. Yule mama alinielekeza kuwa hii mizigo tunayoagiza nje huwa tunapewa tracking number, kama tracking number yako inaanza na herufi R, ina maana mzigo wako umetumwa kwa kutumia Registered tracking code, inamaana mzigo wako ukifika Posta utapigiwa simu ukauchukue na hautolipia kodi yoyote, utachukua mzigo wako bila malipo yoyote. Lakini akaniambia kuwa kama tracking number yako inaanza na herufi tofauti na R, mzigo wako ukifika Posta utalipia kiasi cha shilingi 3000. Hii 3000 unapewa control number kisha unafanya malipo, baada ya kukamilisha malipo unapewa mzigo wako.
Lakini nilimuuliza swali, vipi kama mzigo wangu ni mkubwa unavuka kilo 5, yule mama aliniambia package za aina hiyo huwa zinakuja na maelekezo kutoka makao makuu, ila kodi yake haizidi shilingi 10000, hivyo aliniambia niache uoga kama kuna kitu nataka kuagiza niagize tu.

Okay, sasa mimi nina swali wataalamu wa hizi mbanga. Ninawezaje kuagiza mzigo kwa dealer ambayo nina uhakika atanimba tracking number ambayo ni registered, yaani tracking number inayooanzia na herufi R?
Tafuta mtu pale awe anakutolea

Ila mingi kama sim ina makadirio ya kodi hadi laki 3 kitegemea na sim
 
Mkuu naona aliexpress vitu vingi ni kama fake tofauti na ebay
AliExpress ni Wachina!
Products za Wachina zinafahamika zilivyo. Ila ukiwa makini ninaamini unaweza kupata kitu kizuri.
Uzuri wa soko la China gharama za shipping ziko chini sana, nahisi serikali ya China inawasaidia wafanyabiashara wa China kwenye upande wa usafirishaji.
 
Back
Top Bottom