Nilijikuta naishi maisha ambayo sikuyategemea ila sina jinsi

Nilijikuta naishi maisha ambayo sikuyategemea ila sina jinsi

Mpe nafasi ya kumsikiliza, kama anataka kulea watoto nakushauri ukubali tu....

Maana nakuhakikishia, hao watoto watakuja kumtafuta baba yao.. na hapo itakuuma zaidi
 
Mimi nilikimbia mwanamke nilimuacha na watoto wawili mmoja wa kwake umri miaka mitano na mwingine miaka miwili ndio Morgan wangu huyo.

Sababu zilizofanya nimkimbie.

1. Toka mwanzo naanza naye mahusiano nilishamuweka wazi kuwa nipo mkoa ule sina furaha na kazi nayofanya na at anytime naweza kurudi nyumbani kwetu Namtumbo hapo tupo Kagera so akaamua kubeba mimba kama kunishawishi niendelee kubaki ile mimba iliharibika ilipofikisha umri wa miezi 7 tukaendelea na mahusiano kumbe kabeba mimba nyingine ndio Morgan huyo.

2. Morgan akazaliwa tukawa tunaishi lakini mimi roho yangu ilikuwa inaniuma kuona kama amenilaghai kwa gia ya mtoto ili nisiweze kurudi kwetu Namtumbo mnaweza kuhoji kwa nini nisirudi naye Namtumbo jibu ni kuwa sikuwa tayari kuwa na mwanamke pia financial sikuwa vizuri kwenda kuanza maisha Namtumbo nikiwa na familia.

3. Nilikuwa na madeni ambayo nilikataa kuyalipa nilimripoti mdeni wangu Takukuru akanambia nitakuonesha mimi na wewe nani mjanja alikuwa mtu wa Mara Chacha nikaona kabisa hapa mapanga yananihusu usalama wangu mdogo.

4. Kuongeza viugomvi vya ndani ya nyumba na stress za kuingia kwenye maisha ya ndoa bila ya kutarajia na ugumu wa maisha nikaona wakati sahihi wa kutoroka familia umewadia.

Kwa kipindi cha miaka miwili wazo nililokuwa nalo kichwani ni kurudi nyumbani nikimuangalia Morgan zile stage zake za ukuaji kama kutambaa, kutembea naona nikomae tu na huyu mwanamke lakini bado wazo la kurudi nyumbani liliponizidi nguvu.

Ilikuwa hivi siku nimerudi jioni nikamwambia nimeomba likizo naenda nyumbani jioni hii akafikiri utani akaleta chakula nikala nikachukua bag dogo nikaweka vyeti vyangu suruali kadhaa na tisheti nikamuachia hela ya matumizi nikachukua bodaboda huyo nikaanza safari ya kuitafuta Namtumbo.

Nipeni Maua yangu nimalizie hii true story.
 
Mpe nafasi ya kumsikiliza, kama anataka kulea watoto nakushauri ukubali tu....

Maana nakuhakikishia, hao watoto watakuja kumtafuta baba yao.. na hapo itakuuma zaidi
Sio baba yake tu, kuna member alifungua uzi humu majuzi ana zaidi ya miaka 50 anawatafuta ndugu zake upande wa mama na upande wa baba, scenario yake inafanana kidogo na ya huyu mama tofauti yake ni kidogo, walipofiwa na mama yao hawakuwajua ndugu zao mpaka leo, yaan mtu mpaka anafika 50 yrs old hajui ndugu upande wa mama Wala upande wa baba
 
Mwenye watoto ameshakuambia anataka ahudumie watoto wake wewe unaweka kiburi halafu unaanza kulia lia, pambana
 
Mimi nilikimbia mwanamke nilimuacha na watoto wawili mmoja wa kwake umri miaka mitano na mwingine miaka miwili ndio Morgan wangu huyo.

Sababu zilizofanya nimkimbie.

1. Toka mwanzo naanza naye mahusiano nilishamuweka wazi kuwa nipo mkoa ule sina furaha na kazi nayofanya na at anytime naweza kurudi nyumbani kwetu Namtumbo hapo tupo Kagera so akaamua kubeba mimba kama kunishawishi niendelee kubaki ile mimba iliharibika ilipofikisha umri wa miezi 7 tukaendelea na mahusiano kumbe kabeba mimba nyingine ndio Morgan huyo.

2. Morgan akazaliwa tukawa tunaishi lakini mimi roho yangu ilikuwa inaniuma kuona kama amenilaghai kwa gia ya mtoto ili nisiweze kurudi kwetu Namtumbo mnaweza kuhoji kwa nini nisirudi naye Namtumbo jibu ni kuwa sikuwa tayari kuwa na mwanamke pia financial sikuwa vizuri kwenda kuanza maisha Namtumbo nikiwa na familia.

3. Nilikuwa na madeni ambayo nilikataa kuyalipa nilimripoti mdeni wangu Takukuru akanambia nitakuonesha mimi na wewe nani mjanja alikuwa mtu wa Mara Chacha nikaona kabisa hapa mapanga yananihusu usalama wangu mdogo.

4. Kuongeza viugomvi vya ndani ya nyumba na stress za kuingia kwenye maisha ya ndoa bila ya kutarajia na ugumu wa maisha nikaona wakati sahihi wa kutoroka familia umewadia.

Kwa kipindi cha miaka miwili wazo nililokuwa nalo kichwani ni kurudi nyumbani nikimuangalia Morgan zile stage zake za ukuaji kama kutambaa, kutembea naona nikomae tu na huyu mwanamke lakini bado wazo la kurudi nyumbani liliponizidi nguvu.

Ilikuwa hivi siku nimerudi jioni nikamwambia nimeomba likizo naenda nyumbani jioni hii akafikiri utani akaleta chakula nikala nikachukua bag dogo nikaweka vyeti vyangu suruali kadhaa na tisheti nikamuachia hela ya matumizi nikachukua bodaboda huyo nikaanza safari ya kuitafuta Namtumbo.

Nipeni Maua yangu nimalizie hii true story.
We malizia tu maua yatakuja muda sio mrefu,
 
Swali la kizushi kwahiyo miaka yote iyo ujawahi toa mbususu kwa mtu yoyote hadi kesho?
 
Utakua ni mmoja ya wazazi mnakimbia majukumu ya kifamilia, huyo dada alivyoteseka unaona kirahisi tu amsamehe?
Hakuna kisicho sameheka. Na msamaha hukaribisha Mungu rohoni.
Ukisamehe hata huwezi kuja kujieleza mtandaoni huku kwa sababu yalisha isha moyoni
 
Niliachana na aliyekuwa mume wangu miaka 5 imepita, kuachana kwetu kulikuwa kubaya sana kwa mambo mabaya yaliyopita katikati yetu. Sipendi kuyaeleza maana ni mabaya ila nilishayasahau na kuyaacha yapite.

Baada ya kuachana (aliondoka bila kuniaga na kodi ikiwa tunadaiwa miezi 5 bila kulipa) nilibaki na watoto huku nikiwa sina pa kuishi kwani mwezi 1 baadaye mwenye nyumba alinitaka kumuachia vyumba vyake, sina kazi, sina hata kitu kimoja kwa kuwa aliondoka na kila kitu hadi nguo zangu na za watoto na kwenda kusikojulikana alihama nikiwa sipo.

Kabla ya yeye kuondoka nilikuwa sijui kama tunadaiwa kodi, kwa kuwa kodi ya mwanzo ilipoisha alinambia kuwa kodi imeisha na yeye hana pesa kwa kuwa kazini kwake wamepata hasara analipwa nusu ya mshahara ambao ndio tunatumia kujikimu nyumbani.

Tukashauriana nikope pesa kwa ndugu yangu ambaye amekuwa akitusaidia kutukopesha pale tunapokwama na tunamlipa kidogokidogo, nikamtafuta na akatukopesha, nikamkabidhi 1,200,000 ambayo ndio ilikuwa kodi ya miezi 6 nikajua kalipa kumbe kampa mwenye nyumba kodi ya mwezi 1 tu na nyingine sijui alikopeleka hadi leo.

Sasa alipoondoka ndio mwenye nyumba kunitafuta kuwa nadaiwa miezi 5 hadi siku ile na nimeshaanza mwezi wa 6 ivyo ananipa wiki 1 nimuachie nyumba yake, kumbuka hapo nalala chini mimi na watoto kwa kuwa kila kitu kilishaondoka na yeye. Na nafanya kazi ndogondogo kupata chakula cha watoto.

Nikawaza kurudi nyumbani, Kilichonishangaza ni kuona ndugu zangu wote hawapokei simu zangu na wakipokea wananilaumu tu kuwa nimeyatafuta mwenyewe na nisiwasumbue na wanakata simu. Nikawaza nimeyataka yapi? Nimekosea nini? Mbona changamoto zangu pande zote wanazijua kulikoni nalaumiwa leo, nikajaribu upande wa aliyekuwa mume wangu ndio balaa zito.

Mtu 1 akaniambia unajua kuwa Unatuhumiwa kuzaa nje ya ndoa? Nikahamaki, akaendelea kusema baba fulani amewaambia ndugu zako na zake kuwa mtoto huyo mdogo sio wa kwake na ndio maana kaondoka. Nikamwambia hapana haiwezi kuwa kweli kwa kuwa sijawahi kutoka nje ya ndoa hata siku moja. Na kama kasema hayo basi ana lake jambo huenda kaamua kuficha mambo yake kwa kunitwisha mzigo maana tayari alikuwa hana pa kukwepea kutokana na mambo yake.

Basi nikatuma ujumbe mfupi kwa ndugu zangu kuwa, nashukuru kwa kuwa nimejua sababu ya nyie kunichukia ila nawaambia siyo kweli na sijawahi kufanya uchafu huo ila nipo tayari wakapime DNA nchi yoyote na ikibainika ni kweli basi wanihukumu nikazima simu ili nipate muda wa kuwa peke yangu kuwaza nini cha kufanya, nikaanza kuwaza cha kufanya nalia peke yangu.

Nikaanza safari ya kutafuta chumba japo sijui nalipa nini, nikapata mama mmoja nikamweleza hali yangu akanambia nakupa chumba ila utakuwa unanilipa mwezi mmoja mmoja sh. 60000 na mwezi huu nakupa ukae bure utaanza kunilipa mwezi ujao, nikaona chumba ni gharama ila kwangu ilikuwa ahueni maana nina mwezi mmoja wa kuanza maisha kutafuta kodi ya watu.

Nikahamia hapo, na wanangu tukaanza maisha, mwezi mmoja baadae nikapata kazi japo haina mshahara mzuri ila inaniwezesha kupata chakula na kulipa kodi ya 60000 kila mwezi, nikaanza kujibana na kununua vyombo, godoro, kitanda, nguo za watoto nk.

Miezi 7 baadaye nikaja kujua alikokwenda yule mwanaume, na kwamba alipohama alihama na mwanamke mmoja ambaye alikuwa mchepuko wake wa siku nyingi wakaanza maisha yao, nilikutana na ndugu wa huyo mwanamke ndiye aliyenipa taarifa hizo.

Baada ya miaka 2, mwanaume huyo alinipigia simu, akidai anataka kuniona kanikumbuka, nikamwambia huwezi kuniona na wala hutakaa ujue naishi wapi, kwa kuwa sikutaka hata waliokuwa wanatufahamu wajue naishi wapi pia, baada ya kumjibu ivyo akasema kwa kuwa hutaki nikuone basi nilichotaka kusema sitasema, japo nilikuwa na lengo la kuonana na wewe ili nianze kukupa hela ya matumizi ya watoto kwa kuwa umekataa na mimi sihudumii hao watoto, nikamwambia kama wameishi miaka 2 bila huduma yako, basi wataishi tu.

Akawa anaendelea kunitafuta kwa namba mbalimbali huku akifoka na kuniita nina kiburi, jeuri, sina adabu kwake, nitakuwa nimepata mwanaume ananipa kiburi nk, mara aseme nitakuwa nimewalisha watoto sumu kuwa yeye mbaya ila yeye sio mbaya anataka kuwatunza ila mimi ndio nazuia. Mwisho alikata tamaa na sasa imepita miaka 5 nikiwa naishi na wanangu.

Inaniuma sana kuishi na wanangu wakubwa sasa ndani ya chumba 1 kikiwa ndio chumba na ndio sebule kwa kuwa sina uwezo wa kulipia zaidi ya chumba 1 ukizingatia ni wa kiume ila sina jinsi najipa moyo kuna siku nitapata nafasi ya kupata walau vyumba 2 wanangu wakalala tofauti na mimi mama yao.

Nimejitahidi kuandika matukio machache kwa kuyakata sana ili nisiwacoshe
Mkuu

Kama ulichosimulia ni kweli!

Bas ni ile mwendelezo wa wanaume wenzetu kufeli na kuumiza watoto!

Mimi nakuelewa sana ulichopitia kama ni kweli ulivoeleza!

Kumlea kijana HADI akajitamgua mwenyewe ni kazi ngumu SANA!!

Nakushauri UKIPATA nauli jaribu kwenda kwenye wilaya zilizo chamgamka na maisha ni nafuue hasa chakula na malazi!!

Using'ang'anie Miji mikubwa kama Dar na n.k!

Wilaya kama Tunduma, malinyi njombe hata makambako kuna shughuli za kilimo na vibarua ambavyo vitakuinua na ukatunza fedha ukajenga na kuishi na wanao!!!


Mungu hajawahi muacha mama mwenye WATOTO bila msaada hugeuka na kuwa baba halisi wa watoto hao na mume wa mama aliyetelekezwa!!

Mungu wabariki kina mama kama nyie!!!
 
Siwezi ruhusu kupasha kiporo ili watoto wapate matunzo, kama wa kuwatunza anewatunza bila kuhitaji kukutana na mimi. Mbona mnaona mwanamke mnaweza kumchezea tu mkitaka loh
Siamini kama kuna mwanaume ataweka condition ya kupasha kiporo ili ahudumie wanae.

Nachojua akitaka kupasha kiporo ataanza kuhudumia na kulipa bili zote plus zako binafsi e.g kununua nguo na zawadi za mara kwa mara bila kuombwa, na mwisho kiporo unakipeleja mwenyewe.

Maelezo yako umejiweka wewe ni safi sana jambo ambalo inaonesha wewe ndio mchafu zaidi.
Pole dada, uzuri maisha hayawezi kusimama iwe kwako au kwa huyo adui yako. Kwahiyo Take it easy.
 
Nimesoma uzi wako kwa umakini,
Ila nitakua mbaya kusikiliza upande mmoja,
Ila kuna namna pia wewe una tatizo sehem...

Hakuna mkamilifu, mwanaume alikukosea na hauwezi badilisha huo ndio ukweli...
Ameomba nafasi ya kulea wanae na una mkatalia..je unadhani umefanya hekima?
Angalau ungepata unafuu wa maisha,je unamkomoa nani?
Baba,watoto ama wewe mwenyewe?

Utajitesa kuwalea mwenyewe ila mwisho wa siku watoto wakikua watamtafuta baba yao, kama kuna todauti watazimaliza.
Lengo la kuandika huu uzi hapa ni nini ikiwa unakataa msaada wa mzazi mwenzio...je lengo tukuchangie watu baki angali baba wa watoto yupo?

Mpe mzazi mwenzio haki yake,
Hao ni watoto wake pia.
 
Hakuna kisicho sameheka. Na msamaha hukaribisha Mungu rohoni.
Ukisamehe hata huwezi kuja kujieleza mtandaoni huku kwa sababu yalisha isha moyoni
Ukiendelea na hio mitazamo una safari ndefu. Akishamsamehe atapata faida gani? Ndio wale wachungaji anapitisha donation church anunue gari ya kutembelea we ukitaka gari anakuombea.

Bro achana na hio mindset utatumika sana, kwani asipomsamehe ni dhambi? Binadamu kuna mambo usipomuonyesha hato kuheshimu.
 
Miaka mitano bado una kinyongo? Achilia na samehe, kutanisha watoto na baba yao, move on penda mtu mwingine, sahau yaliyokukuta
 
Back
Top Bottom