Nilionja machungu ya kuwa HIV+, unyanyapaa ni unyama

Nilionja machungu ya kuwa HIV+, unyanyapaa ni unyama

D
Doa la ukimwi likishakuangukia uwa HALITAKATI kamwe.

Bro wangu(sina udugu nae). Hadi leo kakubali yaishe na kapata single mama mmoja alieziba maskio na leo wanaishi.

Back then akapata kadada chap akakaslimisha mipango ya mahari ikafanyika chap. Siku 3 nyuma ya kupeleka mahari baba mkwe akamuita akamwambia:, mkwe 1/2/3.

Nasikia unatumia Dozi. jamaa akakanusha,akasema story isiwe ndefu twenden hospital kupima.
Baba bint akakubali, jamaa akarudi nyumbani kesho yake arudi kwa ajili ya vipimo.

Jion yake akapokea ujumbe, baba bint anasema vipimo vifanyikie mbali na mji(wilaya) waliyopo. Madaktar wengi waliopo ndani ya huo mji wanafahamiana na jamaa so uenda wakatoa majibu ya uongo ili kumlinda.

Jamaaa akasema si shida ni jambo dogo tu ilo,twenden wilayani. Asubuhi ilipofika akawapigia simu hawapokei. Makubaliano ilikuwa ni kukutana saa 3 asubuhi kwa ajili ya kwenda hospital lakin sasa simu hawapokei.

Wakati akiwa anatafakari ujumbe ukaingia unasema:, WATU WAMETUAMBIA MTU MWENYE VIRUSI VYA UKIMWI AKINYWA COKE VIRUSI UPOTEA KWA MUDA.

MKWE TUNAOMBA SAMAHANI KWA USUMBUFU ULIOUPATA SISI TUMEGHAILI.
Duuuh!
 
Hao wote wanatakiwa waje waishi Mbeya, Iringa, Njombe wakati nipo Dar nilikuwa naona ukimw kitu cha ajabu ila nilipofika Mbeya nilipoenda Chunya, Mbarali (ubaruku, kapunga) aisee ukimw ni kitu cha kawaida sana yaan watu hawana ata hofu nayo wanakwambia kabisa "ngoja nikachukue dawa niende porini nikafuate mzigo".
Kweli mkuu
 
Huu uvumi simple sana kuusolve
Kama wa vyeti feki

Mtu akikusema unamtumia cheti chako cha HIV Negative
Na msg ya 'Mnikome'..simple
Hata wawili au wa3
Watasambaziana wenyewe chaap sana
 
Hivyo vipimo hata mwaka 2005 vilikuwa havijagunduliwa..😂😂
Marekani kwenyewe hivyo vipimo vimeanza kutumika 2010

Halafu umesema kipindi hicho kulikuwa hakuna vocha za buku bali zinaanzia 5000 tu, 2005 kulikuwa hakuna vocha za buku?😂😂
Zilikuwa zinaitwa dollar moja
 
Hawa nawakumbuka sana kupitia kituo chao walinifungulia dunia ya internet na kujua computer kiujumla. Nakumbuka ulikuwa unalipa 500 unakaa 1hr. Wakanizoea hadi wakawa wananiachia ofsi weekend nilikuwa kidato cha pili naona raha tu nafanya kuwawekea muda wanaokuja via time watcher.
Haha mkuu ulishawahi kuwa pale maeneo ya manyanya/kinondoni enzi hizo unadesign webiste zile zakutumia subdomain???
 
Huu uvumi simple sana kuusolve
Kama wa vyeti feki

Mtu akikusema unamtumia cheti chako cha HIV Negative
Na msg ya 'Mnikome'..simple
Hata wawili au wa3
Watasambaziana wenyewe chaap sana
Wakikwambia umefoji karatasi za majibu?
 
Haha mkuu ulishawahi kuwa pale maeneo ya manyanya/kinondoni enzi hizo unadesign webiste zile zakutumia subdomain???
Via freeservers.com na freeweb.com 🤣 naiba na script za java naweka saa, na vieffect kwenye web pages zangu. Aliyekuwa ananiinspire na jamaa flani alikuwa mdogo enzi hizo ana website inaitwa georgebuliki.freeservers.com.
 
NNadhani hapo hakuna ajabu ,TB huambukiza kwa njia ya hewa hivyo itakuwa yeye ndiye kawaambukiza
Kubaguliwa sio kwenye Ukimwi tu hata TB naona watu wengi hawana uelewa,kuna jamaa alikua anabaguliwa na ndugu zake kisa tu anaTB inasikitisha sana,jamaa alitengwa huyo chumba chake walikua hawaingii msosi anapewa kama mfungwa vyombo vyake vilitenganishwa tena vinaoshwa kwa gloves eti vitawaambukiza Noma sana,jamaa alipona ikabid ahame akatafute maisha sehemu nyingine!Chakushangaza baada miaka 3kupita kwenye ile familia watu wawili wakapata TB malipo hapa hapa!
 
Doa la ukimwi likishakuangukia uwa HALITAKATI kamwe.

Bro wangu(sina udugu nae). Hadi leo kakubali yaishe na kapata single mama mmoja alieziba maskio na leo wanaishi.

Back then akapata kadada chap akakaslimisha mipango ya mahari ikafanyika chap. Siku 3 nyuma ya kupeleka mahari baba mkwe akamuita akamwambia:, mkwe 1/2/3.

Nasikia unatumia Dozi. jamaa akakanusha,akasema story isiwe ndefu twenden hospital kupima.
Baba bint akakubali, jamaa akarudi nyumbani kesho yake arudi kwa ajili ya vipimo.

Jion yake akapokea ujumbe, baba bint anasema vipimo vifanyikie mbali na mji(wilaya) waliyopo. Madaktar wengi waliopo ndani ya huo mji wanafahamiana na jamaa so uenda wakatoa majibu ya uongo ili kumlinda.

Jamaaa akasema si shida ni jambo dogo tu ilo,twenden wilayani. Asubuhi ilipofika akawapigia simu hawapokei. Makubaliano ilikuwa ni kukutana saa 3 asubuhi kwa ajili ya kwenda hospital lakin sasa simu hawapokei.

Wakati akiwa anatafakari ujumbe ukaingia unasema:, WATU WAMETUAMBIA MTU MWENYE VIRUSI VYA UKIMWI AKINYWA COKE VIRUSI UPOTEA KWA MUDA.

MKWE TUNAOMBA SAMAHANI KWA USUMBUFU ULIOUPATA SISI TUMEGHAILI.
kubababake...
 
Naelewa sana unachokisema maana mimi nimenyanyapaliwa hivyohivyo. Mwaka 2013 Niliugua TB lakini hadi leo watu wanajua nina ukimwi. Tena aliyenichafua zaidi ni babamdogo'angu na hadi sasa 95% wanandugu wanaamini nina ukimwi. Nimeoa na watoto wawili na sina ukimwi ila inasemekana ninao.
 
So huyo mpenzi wako alifarariki mwaka 2007 na ndio mkaanza na huyo spicy, so mwaka 2007 kulikuwa hakuna vocha za buku?
watu huwa wana distort story kuepuka kutambuliwa.

stori yako imejaa matobo mengi, tukiachana na huo uwongo huo, hebu tuaambie mwaka 2007 kulikuwa hakuna vocha za buku? najua hili hutaweza kujibu, utalipotezea kama hujaona

Kwamara ya kwanza nilipoona comment za kuniponda nilijaa sana sumu, fikiria mtu umejipinda kuonyesha hisia zako na machungu uliyopitia alafu mtu kirahisi tu anakwambia "Chai hii" 😀. Jana hadi nichelewa kwenda lunch sababu ya kujitahidi kujibu madongo ya wadau ving'ang'anizi. Lakini kwa sasa nimejifunza kitu na niwashukuru kwa kuzidi kuniongezea elimu.

Aina yangu ya uandishi ni kufikiria kilichotokea na kuanza kuandika wakati huo huo na kufanya masahihisho ya maneno tu, huwa naongeza vinyama kidogo kuongeza uhalisia na kumfanya msomaji akumbuke nyakati hizo. Lakini kumbe kuna mambo natakiwa kuzingatia ikiwezekana kuwa na kumbukumbu nzuri kabla ya kuandika.

Mfano kwenye uzi huu ni kweli kabisa hayo yalinitokea sasa kwenye kuleta uhalisia wa nyakati hizo na vitu vingine vilivyokuwa kwa wakati huo imeleta changamoto. Lakini kuna mambo nauhakika nayo ambayo nayakumbuka viziri; kama hili la kufikiria kumpima nyumbani na kuwa nampigia simu akiwa shuleni.

Uandishi ni taaluma na kipaji pia, mimi si muandishi kwa taaluma japokuwa napenda sana kuandika. Nimejifunza machache kuhusu uandishi kwa kusoma vitabu. Maoni yenu yamenijenga zaidi sikutakiwa kuchukia na kujibu kwa mihemko, niliowakwaza naomba mnisamehe.
 
Naelewa sana unachokisema maana mimi nimenyanyapaliwa hivyohivyo. Mwaka 2013 Niliugua TB lakini hadi leo watu wanajua nina ukimwi. Tena aliyenichafua zaidi ni babamdogo'angu na hadi sasa 95% wanandugu wanaamini nina ukimwi. Nimeoa na watoto wawili na sina ukimwi ila inasemekana ninao.
Pole sana mkuu, haya machungu nayajua aisee
 
stori yako imejaa matobo mengi, tukiachana na huo uwongo huo, hebu tuaambie mwaka 2007 kulikuwa hakuna vocha za buku? najua hili hutaweza kujibu, utalipotezea kama hujaona
Baada ya mdau kuleta evidence za uwepo wa vipimo vya fasta vya HIV, mnarukia lingine sasa. Sometime soma tu ukiona haikufai puuzia ondoka.

Na ngozi nyeusi tulivyo wanafiki kama nyama ya mk.... waliokuwa wamekomalia vipimo non of them will come back kusema sorry.
Unang'ang'ania vocha za buku 2007, itakusaidia nini?. Mwaka 2006 nilikuwa naenda mtaa wa miti mirefu, pamba road Mwanza napiga simu kwenye vibanda unajua nilikuwa natozwa sh ngapi kwa dakika?

Ni miaka mingi Sana imepita inawezekana kashasahau, yeye ni binadamu. Lakini pia inawezekana mahali alipokuwa hazikuwepo, just read the story.
 
Kwamara ya kwanza nilipoona comment za kuniponda nilijaa sana sumu, fikiria mtu umejipinda kuonyesha hisia zako na machungu uliyopitia alafu mtu kirahisi tu anakwambia "Chai hii" 😀. Jana hadi nichelewa kwenda lunch sababu ya kujitahidi kujibu madongo ya wadau ving'ang'anizi. Lakini kwa sasa nimejifunza kitu na niwashukuru kwa kuzidi kuniongezea elimu.

Aina yangu ya uandishi ni kufikiria kilichotokea na kuanza kuandika wakati huo huo na kufanya masahihisho ya maneno tu, huwa naongeza vinyama kidogo kuongeza uhalisia na kumfanya msomaji akumbuke nyakati hizo. Lakini kumbe kuna mambo natakiwa kuzingatia ikiwezekana kuwa na kumbukumbu nzuri kabla ya kuandika.

Mfano kwenye uzi huu ni kweli kabisa hayo yalinitokea sasa kwenye kuleta uhalisia wa nyakati hizo na vitu vingine vilivyokuwa kwa wakati huo imeleta changamoto. Lakini kuna mambo nauhakika nayo ambayo nayakumbuka viziri; kama hili la kufikiria kumpima nyumbani na kuwa nampigia simu akiwa shuleni.

Uandishi ni taaluma na kipaji pia, mimi si muandishi kwa taaluma japokuwa napenda sana kuandika. Nimejifunza machache kuhusu uandishi kwa kusoma vitabu. Maoni yenu yamenijenga zaidi sikutakiwa kuchukia na kujibu kwa mihemko, niliowakwaza naomba mnisamehe.
Usijisumbe kumridhisha kila mtu humu. Elimu na funzo tumepata kwenye bandiko lako
 
Back
Top Bottom