#COVID19 Nilivyojisikia baada ya kuchanjwa chanjo ya COVID-19

#COVID19 Nilivyojisikia baada ya kuchanjwa chanjo ya COVID-19

Watu hawajaanza kukataa chanjo tu bali walishagomea hata kuchukua tahadhari za kujikinga na hiyo corona yenyewe, pamoja na yote yanayozungumzwa kuhusu corona kuanzia kifo cha rais na viongozi, uhitaji wa mitungi ya oksijeni n.k ila bado watu wamegoma kuvaa barakoa,wamegoma level seat,wamegoma kunawa mikono, wamegoma social distance yani kwa kifupi watu wanaendelea na maisha kama hawajawahi kusikia kuhusu corona hata serikali imefeli katika hili.

Sasa sijui hapo mkuu unafikiri ni kipi ambacho kinafanya ufikiri kuwa itafika muda watu hao hao ambao wamegoma kuchukua tahadhari za kujikinga na corona watahitaji kuchanjwa?
Kaka, nyumbani kwa shujaa kunaingia vilio na kwa muoga kunaingia vicheko. Burundi na Tanzania kulikuwa na mashujaa (Nkruzinza na mwenzake) ona vilio vilivyoingia kwenye nyumba zao. Tuache kushindanisha Sayansi na mtazamo.
 
Hakuna maswali yeyote, kinachosumbuwa watu kwa sasa ni utandawazi.

Hivi zile chanjo za surua, ndui, nk Nini walijadiliana na nani zikaletwa huku Africa? Au zikakubalika na wengine?

Si tumeletewa tu? Au kulikuwa na mjadala kama huu wa chanjo ya uviko?

Kuna yeyote aliyehoji usalama wa chanjo zile?
Kwanini watoto hawachanjwi hii uviko?
 
Kwanini watoto hawachanjwi hii uviko?
Watoto na vijana under 20 ni ngumu sana kuathirika na covid.
90% ya wanaokufa na covid wana magonjwa mengine ambayo yanatokana na umri.

Ndy maana wazee au watu over 50 ndy haswa walengwa namba moja wa kupata kinga..
Mtoto anaweza akapata covid na kupona yenyewe bila madhara.
Mzee ndy ana risk kubwa ya kupoteza maisha..
Tusiwe tunapinga kila jambo,hata kama lina manufaa.
 
Mkuu usitumie nguvu nyingi sana kuwaaminisha watu kuhusu usalama Wa chanjo.

Kumbuka hata mababu zetu walipoletewa ustaarabu wa kujenga vyoo na kujisaidia chooni, vita vya kupinga kujisaidia chooni ilikuwa kubwa kuliko hili la wapinga chanjo.

Maana walishazowea kujisaidia vichakani.

Mimi nimechoma faizer, tena muda tu sasa na nipo okay...

Na hakuna tatizo lolote.

Waache waendelee kupinga ,,huku wakiumwa wanakimbilia hospital kwenye dawa za kizungu

Badala ya kwenda kwa mganga wa kienyeji kutibiwa.
Wajinga ndio waliwao ,hii nchi ina watu wajinga sana munakataa kuchanjaa bure mutakuja kuchanja kwa pesa na musipate vile vile .Mimi nimechanja PFIZER safi sana kabisa maisha yanaendelea ,mwenye macho haambiwi tazama.
 
Watu ni wabaya sana aisei. Siku ya uzinduzi wa chanjo nilikuta misururu mirefu ya watu wanaotaka kuchanja. Nikasema kweli akili za kuambiwa changanya na zako. Watu wanasema hatuchanji kumbe wameshachanja. Askofu ameahachanja halafu anawaambia wenzake wasichanje
Mh! Kwa Magufuli ilisemwa hivyo kuwa alishachanjwa kisirisiri ila alipokufa tunasikia madai ya kwamba kafa kwa corona.
 
We hata ukisema mkunyenge wako tokea uchanjwe hadi leo umesimama sisi hutushawishi kihivyo,umechanja ni wewe bas!

Sent from my Infinix X656 using JamiiForums mobile app
Usitumie neno "sisi" badala ya "mimi" kwenye mijadala kama hii inayohitaji hiari ya mtu. Hata mimi na wenzangu tuliweka msimamo kuwa hakuna kuchanja, tutapata kinga mbele ya safari wakati tunapopata maambukizi madogomadogo kwenye jamii, lakini baadae mimi nikaenda kuchanja hata bila ya kuwaomba ushauri wala kuwataarifu, sikuomba ushauri kutoka kwa mke wangu wala watoto wangu.

Nilipata marafiki wapya kabisa wanaokwenda kuchanja na hata mke wangu nilimjulisha baada ya wiki moja kupita na kujiona niko fiti, hata hivyo alianza kuishitukia "speed na viwango" vilivyobadilika.
 
Mkuu usitumie nguvu nyingi sana kuwaaminisha watu kuhusu usalama Wa chanjo.

Kumbuka hata mababu zetu walipoletewa ustaarabu wa kujenga vyoo na kujisaidia chooni, vita vya kupinga kujisaidia chooni ilikuwa kubwa kuliko hili la wapinga chanjo.

Maana walishazowea kujisaidia vichakani.

Mimi nimechoma faizer, tena muda tu sasa na nipo okay...

Na hakuna tatizo lolote.

Waache waendelee kupinga ,,huku wakiumwa wanakimbilia hospital kwenye dawa za kizungu

Badala ya kwenda kwa mganga wa kienyeji kutibiwa.
njoo apa bada ya miaka 10 au mi 5 uje unipe mrejesho na kama umepata watoto wangapi ndo ntachanjaa hv hv hapana
 
Mh! kwa Magufuli ilisemwa hivyo kuwa alishachanjwa kisirisiri ila alipokufa tunasikia madai ya kwamba kafa kwa corona.
Marais wote wanachanja hadharani, hata Biden, Kagame, Godon, Museven, Samia, Kenyatta wote walichanja mbele ya camera, kwanini JPM achanjwe kisirisiri? unachosema hakina ukweli.
 
njoo apa bada ya miaka 10 au mi 5 uje unipe mrejesho na kama umepata watoto wangapi ndo ntachanjaa hv hv hapana
tumia sayansi kupinga sayansi, hata hiyo simu yako ina miyonzi tahari kwa afya yako lakini hatuna mbadala wa simu za aina nyingine. Usitumie maono kujibu sayansi. kufwa utakufwa tu.
 
Mimi ni miongoni watu waliochanjwa chanjo ya COVID-19 Johnson And Johnson siku ya pili tu baada ya zoezi la kuchanja kuzinduliwa na Rais

Nilijisikia yafuatayo:
1. Nili
Namba 6,7 na 8 pana leta faraja sana,kama namuona Gwajima anarudia rudia kusoma hapo......
 
Wajinga ndio waliwao ,hii nchi ina watu wajinga sana munakataa kuchanjaa bure mutakuja kuchanja kwa pesa na musipate vile vile .Mimi nimechanja PFIZER safi sana kabisa maisha yanaendelea ,mwenye macho haambiwi tazama.
Dawa yao ni kulazimishwa hiyari.
 
Kaka, nyumbani kwa shujaa kunaingia vilio na kwa muoga kunaingia vicheko. Burundi na Tanzania kulikuwa na mashujaa (Nkruzinza na mwenzake) ona vilio vilivyoingia kwenye nyumba zao. Tuache kushindanisha Sayansi na mtazamo.
Nimejenga hoja tu kutokana na huo mtazamo wa kwamba baadaye watu watakuja kukubali tu wenyewe kuchanjwa, ndio nimesema kwamba hadi sasa bado wanagomea tu kuchukua tahadhari hivyo sidhani watu hao watakuja kukimbilia chanjo hali ya kuwa hadi sasa hawajaona umuhimu wa kuchukua tahadhari za kujikinga na corona kitu ambacho hata baada ya kuchanjwa unatakiwa kuendelea kuzingatia.

Halafu mkuu sidhani kama ni sahihi kuhusisha kupinga chanjo kuwa na tafsiri ya kutoamini sayansi na kuamini sayansi hakuna maana ya kukubali tu lolote lenye kuhusishwa na sayansi, ni vizuri tukawekana sawa kwenye hilo na ndio maana kuna hadi wanasayansi wenye kupinga hizi chanjo kwa hoja za kisayansi sasa si sawa kuwafananisha watu wote wapinga chanjo kuwa sawa na watu waliyopinga ujenzi wa vyoo.
 
Marais wote wanachanja hadharani, hata Biden, Kagame, Godon, Museven, Samia, Kenyatta wote walichanja mbele ya camera, kwanini JPM achanjwe kisirisiri? unachosema hakina ukweli.
Sio mimi mkuu niliyesema hivyo bali kuna watu ndio walisema hivyo na sababu ni kwamba Magufuli alionekana waziwazi kupinga chanjo hivyo asingeweza kuchanja mbele ya camera kama ambavyo wewe unadhani kuwa Gwajima yawezakuwa ameshachanja nyuma ya camera, ndio maana nikakumbusha hiyo hoja ya kwamba Gwajima pengine kuwa ameshachanja inakuwa sawa na ile ya Magufuli.
 
Watoto na vijana under 20 ni ngumu sana kuathirika na covid.
90% ya wanaokufa na covid wana magonjwa mengine ambayo yanatokana na umri.

Ndy maana wazee au watu over 50 ndy haswa walengwa namba moja wa kupata kinga..
Mtoto anaweza akapata covid na kupona yenyewe bila madhara.
Mzee ndy ana risk kubwa ya kupoteza maisha..
Tusiwe tunapinga kila jambo,hata kama lina manufaa.
Kwahiyo hapo maana yake ni kwamba watoto wadogo kinga zao ni imara zaidi?
 
Mimi ni miongoni watu waliochanjwa chanjo ya COVID-19 Johnson And Johnson siku ya pili tu baada ya zoezi la kuchanja kuzinduliwa na Rais

Nili
Umesikika Kwa Sasa mkeo ni mwenye amani !! Hiyo ni reaction ya muda mfupi . Endelea kutuhabarisha kinachoendelea mwilini wako baada ya mwezi, miezi 5,mwaka, miaka 2 nk. Tunafuatilia kwa umakini. Sisi tutabaki kama sample Kwa ajili ya control experiment.
 
Mmmh wazidi kujitokeza kueleza. Huenda inaweza kufanya ngongingo zika vibrate. Maajabu kabisa haya. Na pengine wakaja watakao pata hamu ya kupakwa mafuta.
 
Wajinga ndio waliwao ,hii nchi ina watu wajinga sana munakataa kuchanjaa bure mutakuja kuchanja kwa pesa na musipate vile vile .Mimi nimechanja PFIZER safi sana kabisa maisha yanaendelea ,mwenye macho haambiwi tazama.
Mkuu ishu ya chanjo bado sio ya kutoa hitimisho kama hilo, ukiangalia kinachoendelea sasa hivi unaona tunaambiwa virusi vinazidi kubadilika kiasi cha kuhitaji waliyochanjwa kwenda kuboost na vitu kama hivyo. Kwa maana hiyo ndio maana wengine huona kuwa hili zoezi la chanjo bado lipo kwenye majaribio.
 
Back
Top Bottom