Nilivyonusurika kuuawa na wananchi wenye hasira kali miaka 15 iliyopita. Tanzania kufariki ni dakika 0 tu!

Nilivyonusurika kuuawa na wananchi wenye hasira kali miaka 15 iliyopita. Tanzania kufariki ni dakika 0 tu!

Mwalimu wetu moja alifariki alipokuwa masomoni South Afrika kwa kuitiwa mwizi.kuna jamaa yetu naye aliuwawa Dar es salaam kwa kuitiwa mwizi kumbe alifananishwa.

Miafrika na ujinga ni kama kopo na mkojo,viongozi wao wanaiba mabilioni na mabilioni hawawachukulii sheria lakini kusingizia ndio wanajua.
 
Mtu mzima na akili zako timamu unawezaje kuishi tabora?
Nilipomaliza chuo nilizunguka sana kutafuta AJIRA hasa kwenye majiji makubwa kama mwanza, Dodoma na na Daressalam huko kote niliambulia holaaaa, nilikaa nikafikiria sana nikaona sehemu pekee ya kwenda kutafuta maisha ni mikoa ambayo haijaendelea kwa sababu ushindani katika sekta ya ajira unakuwa ni mdogo na uhitaji unakuwa ni mkubwa pia, nikaona Bora niende tabora huko nilifanikiwa kupata ajira japo nilikuwa nalipwa mshahara mdogo sana..Mimi ni mtaalamu wa Afya ya binadamu japo kwa sasa najishughulisha na biashara niliisha Toka huko....soko la ajira aliliharibu zaidi magufuri likawa gumu balaa......
 
istockphoto-1323328073-612x612.jpg
 
Umeharibu ulipoelezea kuwa polic walikuambia wewe ni mrembo,,,,, ni sawa pengine uliambiwa hivo, haka ka -segment ungekaruka ili kulinda uanaume wako ,,, !! Hongera Shombe
Hii sentensi iliniumiza kiasi ndio maana sikuweza kuipotezea
 
Huyu mwanamke ilitakiwa umchape ngumi mbili tatu, na mtama mmoja matata sana in the act of self defense...

Haiwezekani mtu anakushambulia then unajitetea kizembe...
Usichokijua ni sawa na usiku wa Giza....pale nilikuwa kwenye himaya ya watu ningejifanya ngarambe wangeniuwa.....
 
Ni miaka 15 sasa imepita tangu ninusurike kuuawa na walimwengu. Nilikuwa nikiishi Tabora, na jioni moja, nilikuwa natembea mjini Tabora. Wakati natembea, nikajihisi kubanwa haja ndogo, nikawa nakatiza mtaa wa Salimini. Kwa wale wenyeji wa Tabora, mnafahamu ule mtaa ulivyo wa Kiswahili. Nikawaona niingie kwenye nyumba moja mtaani hapo ili niombe sehemu ya kujisaidia haja ndogo (chooni).

Nje ya nyumba ile alikuwa amesimama kijana mwenye umri wa miaka 18 au 19, nilimuomba na akaniielekeza nipite kwenye korido niende mpaka uwani. Wakati napita kwenye korido, nilikutana na mwanamke na mwanaume wakiwa wanazungumza. Niliwasalimia, na mimi nikaendelea na safari yangu kuelekea uwani. Nilipofika uwani, kabla ya kuingia chooni, nikawa ninakunja suruali yangu mpaka ukaribu na magotini (kawaida yetu Waislamu huwa tunafanya hivi ili utakapokuwa unajisaidia haja ndogo, zile cheche za mikojo zisirukie nguo). Ghafla nilisikia sauti ya mwanamke ikitokea nyuma ikiita "mwiziiiiii, mwiziiiiii."

Ile kugeuka, namuona yule mwanamke niliemuona kwenye korido anakuja mbio huku akakamata kuni. Akaanza kunipigia na ule ukuni sehemu za mabegani huku mimi nikihangaika kupangua kile kipigo na kujitetea kuwa mimi sio mwizi. Yule mwanamke alipoona ananipiga na ukuni na mimi sianguki, akabeba sufuria iliyokuwa na maji ya moto ili animwagie usoni. Dah, lahaula! Akatokea yule mwanaume aliyekuwa nae akamuambia "achaaaaa!" Kujinusuru, nilibidi nirukie kwenye korido nitokee mlango wa mbele ili nikimbie (hapa nilifanya kosa kubwa). Nilianza kukimbia barabarani huku yule mwanamke akiendelea kuita "mwiziiii, mwiziiiiii."

Watu wakaanza kunikimbiza. Kadiri nilivyokuwa nakimbia, watu walizidi kuongezeka, huku wengine wakiwa wamebeba mapanga. Niliingiwa na fikra za haraka za kuingia kwenye nyumba ya mtu ili ninusuru maisha yangu. Bahati nzuri, nyumba ile niliyoingia ilikuwa ya mjumbe wa serikali ya mtaa. Alichokifanya yule mjumbe (mwanamke wa makamo) aliniambia niingie nijifiche chumbani na yeye akafunga mlango. Lile kundi la watu wenye mapanga walifika kwenye nyumba ile niliyokuwa nimejificha na wakaanza kumlazimisha yule mjumbe anitoe nje huku wakiimba "tunamtaka mwizi weeetúu."

Yule mjumbe alisimama mlangoni na kuwaambia wale watu, "Simtoi nje huyu kijana, ila nitakachofanya, napiga simu polisi waje wamchukue, mtamkuta kituoni." Hii ndiyo ilikuwa salama yangu. Haikupita masaa mawili, walikuja polisi na kunichukua kwenye gari lao. Polisi mmoja alinipiga vibao huku akisema, "Kumbe jamaa mwenyewe mrembo!" (Mimi nina asili ya ushombe shombe kwa mbali).

Nilipofikishwa kituoni, nilijieleza kwa ufasaha na pia nikatoa vitambulisho vyangu ili viwe ni uthibitisho wa kile nilichokizungumza. Bahati nzuri, mfukoni nilikuwa na shilingi laki moja, nikatoa 30,000/- nikawapa wale askari, wakawa wameniachia niende nyumbani usiku ule na kesho yake niende kuripoti. Kesho yake niliripoti polisi, na askari walinikabidhi vitambulisho na kuniambia hakuna kesi. Nikaendelea na majukumu yangu.
Huyo mama aliyekuita mwizi hukumtafuta?
 
Usichokijua ni sawa na usiku wa Giza....pale nilikuwa kwenye himaya ya watu ningejifanya ngarambe wangeniuwa.....

Kulikuwa na watu wawili tu walioleta ukuda, ujasiri wako ungewatia uoga...

Pia umetaja kwamba uliingia ndani ya nyumba hiyo kwa kuomba, hivyo kungekuwa na watu wa kukutetwa...

Unamkata huyo mwanamke ngumi ya shingo, na pua, mtama ukimsindikiza na maneno "***** mimi sio mwizi nimeomba kuja kutumia choo"...

Kamata huo ukuni mtishie kumchoma mdomo wake kama akiendelea kuleta zogo...
 
Kulikuwa na watu wawili tu walioleta ukuda, ujasiri wako ungewatia uoga...

Pia umetaja kwamba uliingia ndani ya nyumba hiyo kwa kuomba, hivyo kungekuwa na watu wa kukutetwa...

Unamkata huyo mwanamke ngumi ya shingo, na pua, mtama ukimsindikiza na maneno "***** mimi sio mwizi nimeomba kuja kutumia choo"...

Kamata huo ukuni mtishie kumchoma mdomo wake kama akiendelea kuleta zogo...
Ukiwa nje ya uwanja ni rahisi sana kuyaona makosa ya mchezaji.....ingia wewe uwanjani ndio inakuwa kimbembe😁
 
Ni miaka 15 sasa imepita tangu ninusurike kuuawa na walimwengu. Nilikuwa nikiishi Tabora, na jioni moja, nilikuwa natembea mjini Tabora. Wakati natembea, nikajihisi kubanwa haja ndogo, nikawa nakatiza mtaa wa Salimini. Kwa wale wenyeji wa Tabora, mnafahamu ule mtaa ulivyo wa Kiswahili. Nikawaona niingie kwenye nyumba moja mtaani hapo ili niombe sehemu ya kujisaidia haja ndogo (chooni).

Nje ya nyumba ile alikuwa amesimama kijana mwenye umri wa miaka 18 au 19, nilimuomba na akaniielekeza nipite kwenye korido niende mpaka uwani. Wakati napita kwenye korido, nilikutana na mwanamke na mwanaume wakiwa wanazungumza. Niliwasalimia, na mimi nikaendelea na safari yangu kuelekea uwani. Nilipofika uwani, kabla ya kuingia chooni, nikawa ninakunja suruali yangu mpaka ukaribu na magotini (kawaida yetu Waislamu huwa tunafanya hivi ili utakapokuwa unajisaidia haja ndogo, zile cheche za mikojo zisirukie nguo). Ghafla nilisikia sauti ya mwanamke ikitokea nyuma ikiita "mwiziiiiii, mwiziiiiii."

Ile kugeuka, namuona yule mwanamke niliemuona kwenye korido anakuja mbio huku akakamata kuni. Akaanza kunipigia na ule ukuni sehemu za mabegani huku mimi nikihangaika kupangua kile kipigo na kujitetea kuwa mimi sio mwizi. Yule mwanamke alipoona ananipiga na ukuni na mimi sianguki, akabeba sufuria iliyokuwa na maji ya moto ili animwagie usoni. Dah, lahaula! Akatokea yule mwanaume aliyekuwa nae akamuambia "achaaaaa!" Kujinusuru, nilibidi nirukie kwenye korido nitokee mlango wa mbele ili nikimbie (hapa nilifanya kosa kubwa). Nilianza kukimbia barabarani huku yule mwanamke akiendelea kuita "mwiziiii, mwiziiiiii."

Watu wakaanza kunikimbiza. Kadiri nilivyokuwa nakimbia, watu walizidi kuongezeka, huku wengine wakiwa wamebeba mapanga. Niliingiwa na fikra za haraka za kuingia kwenye nyumba ya mtu ili ninusuru maisha yangu. Bahati nzuri, nyumba ile niliyoingia ilikuwa ya mjumbe wa serikali ya mtaa. Alichokifanya yule mjumbe (mwanamke wa makamo) aliniambia niingie nijifiche chumbani na yeye akafunga mlango. Lile kundi la watu wenye mapanga walifika kwenye nyumba ile niliyokuwa nimejificha na wakaanza kumlazimisha yule mjumbe anitoe nje huku wakiimba "tunamtaka mwizi weeetúu."

Yule mjumbe alisimama mlangoni na kuwaambia wale watu, "Simtoi nje huyu kijana, ila nitakachofanya, napiga simu polisi waje wamchukue, mtamkuta kituoni." Hii ndiyo ilikuwa salama yangu. Haikupita masaa mawili, walikuja polisi na kunichukua kwenye gari lao. Polisi mmoja alinipiga vibao huku akisema, "Kumbe jamaa mwenyewe mrembo!" (Mimi nina asili ya ushombe shombe kwa mbali).

Nilipofikishwa kituoni, nilijieleza kwa ufasaha na pia nikatoa vitambulisho vyangu ili viwe ni uthibitisho wa kile nilichokizungumza. Bahati nzuri, mfukoni nilikuwa na shilingi laki moja, nikatoa 30,000/- nikawapa wale askari, wakawa wameniachia niende nyumbani usiku ule na kesho yake niende kuripoti. Kesho yake niliripoti polisi, na askari walinikabidhi vitambulisho na kuniambia hakuna kesi. Nikaendelea na majukumu yangu.
Mtaa wa Salmin ambao Rc Mwanri aliuita Toronto na weekend ukawa unafungwa kuruhusu wachuuzi kufanya biashara.

Juzi juzi nimepita Tbr nimekuta mtaa huo umebadilika sana, Soko kuu limevunjwa wanataka kulijenga jipya, mtaa huo wa Salmini uliopo pembezoni mwa Soko, walanguzi hawapo tena!

Pole mkuu, watu wengi wanaoitiwa 'mwizii' huwa siyo wezi, huwa ni wadhaniwa ama huwa ni fitina za ugoni ama makosa mengine.

Huyo mama aliyekushambulia na kukusakizia, kuna kitu kilimchanganya!

Mwizi hawezi kuingia kufanya uhalifu mchana kisha akawasalimia.
 
Kwanini haukurudi kwa mjumbe kumpa chochote kitu na ukawapa polisi pekee?
 
Mkuu story yako imetaka kufanana na yangu.
Nikiwa nimemaliza zangu chuo nikaona kukaa mtaani ni shuguli ikabidi nijichange niingie kwenye usafirishaji watu kwa kutumia bajaji katika mji wa ifakara.

Nakumbuka mchana moja napata abiria wa kumpeleka sehemu moja wanapaitwa mtaa wa maendeleo.

Huyu mteja wangu alikuwa ni mama mtu mzima lakini kidgo kama bado anawaka kidgo. Safari inaanzia ifakara mjini kutafta maendeleo. Kama kawaida angu sio muongeaji ni mkimya sana abiria akishanambia anaposhukia.

Mimi huyo ni kupangua tu gia kufika mtaa wa silent inn mteja wangu anavunja ukimya ananiuliza kama akinipa dili naweza? Namuuliza dili gani?

Ananiambia yeye ni mfanya biashara hvyo kwa kuwa kaniona kama mtulivu atakuwa anatuna oda kwa wateja wake anafungiwa mzigo mm nampelekea bila yeye kuja mjini nkasema sio kesi anipe dili.

Kweli bwana kazi ikaanza kama wiki moja hiv nakuwa nampelekea mzigo kumbe mzigo wenyew n ndizi za kukaanga. Tulipiga kaz kama mwezi hivi sikuwahi kufika kwake kwan huwa anapokelea mzigo wake njian kwa maana kutoka sokoni kwenda kibaoni lazima utaokota vichwa hata viwili hvyo huwezi kuacha barabara kuu uchepuke na abiria.

Baada ya kumzoea na yeye kunizoea akawa ananiambia nipitie pesa ya nauli akimaliza kuuza na mimi nkaona so kesi.

Ukisikia shetani yupo kazini ndio hii. Siku hiyo nimempitishia mzigo kama saa mbil asbh akanambia kufika saa tano nimcheki anipe changu na hii siku ndio nilipata abiria wengi sana mpaka saa kumi na mbili jioni sijapoa nmekuja kupoa saa moja na nusu na nimepoa nikiwa sehemu moja wanapaita kibaoni nikatega vichwa kama nusu saa hola.

Nkasema isiwe kesi ngoja nkalale nampigia simu ananiambia nitamkuta njian ninakoshusha mizigo nafika pale hola kisha ananiambia nishuke na njia ambayo huwa namuona anatokea tukutane njian asee ningejua bora nsingethubutu.

Kumbe muda ananielekeza tutakutana njian ndo muda mumewe katoka kwenye mihangaiko hivyo mumewe akawa anamfuata nyuma nyuma. Kufika tu kwangu na kunikabidhi pesa angu mumewe huyu hapa na kuanza kumshushia kipigo cha haja sasa hapa kosa moja nililofanya ni kutaka kuleta umwamba kumtetea asee yule mmewe akaanza kuita mwizi mwizi mwizi nikaona watu wanaanza kujaa kumbuka yule mwanamke alipewa kipigo heavy mpka kazima.

Asee nilichomoka kama mshale ili nkafate jambia huwa natembea nayo kwenye bajaji ila kila nkikimbia ndo kelele za mwizi zinaongezeka ikabidi nibadili mawazo nkabadili na uelekeo wa kuelekea nkapita kuna sehemu wanakunywa gonga nkasema hawa walev ndo wataleta na petrol kabsa niunguzwe.
Nikazama kwenye mji moja hivi wamekaa nje nikawaelezea pale chap chap kilichotokea wakanielewa na kuniwekea ulinzi. Na mtaa ule kulikuwa na askari wa kike anakaa simjui jina ila chap akawa amefika pale akanihoji hoji na kunielewa.

Toka hapo kwenye kazi yangu ya kusafirisha abiria sikutaka tena mazoea na mwanamke yyte yule. Panda lipa nauli shuka.

Ila pale nipotoka ndio nikaona kwa tanzania hii kufa ni dk 0 kwa maana ningekaa pale watu wangefika na kuanza kunishushi kipigo bila kuhoji.

TANZANIA HII ndio sehemu mtu atatekwa mchana kweupe na wasitoe msaada ila wakisikia mwizi tu wanamshambulia kama hawana akili timamu.
 
Back
Top Bottom