Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Hio ngumu, pole sana. Itakua huo uradi alikupa katika watu wa Kadiria, wanaoitwa muridi. Wale masufi, sio ibada tu hizo, ni elimu ya kipekee. Arsis anawaelezea hao, natumai itafika wakati tutawasoma hapa.

Arsis ana mengi sana, ulivyonielezea nimeelewa ndugu yangu ulichokumbana nacho. Elimu hio Arsis anaileta kiwepesi sana mpaka utashangaa. Ukipenda kuelewa uliza tu, itakufanyia wepesi.
masufi toka enz na enz wao ni watu wa kushinda miskitin na kufanya uradi. sasa ukipewa fadhailul amal na kadiria lazima uchemke mana yeye atakwambia utaje kitu fulan mara laki 1
 
1. Mahojiano na Arsis

Yafuatayo ni mahojianao yangu (nitajiita simba kuanzia sasa) ambayo sio ya kwanza kati yangu na Arsis, lakini nimwyaweka namba 1 kwa kua nahisi yataleta mpangilio mzuri wa mahojiano yatakayofatia.

Mimi; Arsis, Arsis, Arsis, upooo?

Baada ya kumwita ikapita kama nusu dakika hivi.

Arsis; Nipo Simba, vipi hali yako?
Mimi; Mimi mzima kabisa na wewe?
Arsis; Mimi nipo salama namshukuru Muumba wetu.
Mimi; Arsis, leo nina swali moja tu, nataka nikuulize utakaponijibu ndio naweza kua na maswali mengine.
Arsis; Uliza Simba.

Mimi; Arsis kuna siku nilikuuliza wewe umejuana vipi na Babu yangu, nikahisi kama kuna vitu umenificha hukunieleza vyote. Ulinielezq umefahamu kupitia Jini wa bakora, nikahisi umenip9ga [piga chenga. Leo nieleze bila chenga, tumeshakua marafiki muda sasa.

Kabla ya kujibu Arsis akacheka kma mtu aliyefurahi. Naomba kusisitiza hapa, Arsis ni kiumbe mmoja ambae ukiongea nae utaona raha sana, hacheki kwa majivuno au kwa kebehi, unamhisi anacheka kwa kua anacheka kweli.

Arsis; Sikiliza, leo umenifutrahisha sana, nilikua nanhgoja siku uwe serious kama leo ili unielewe vizuri. Nilikiua nakuhisi kama ninayokwambia yanakuingia na kutoka. Nisikilize kwa makini.

Simba, mimi nilikua kifungoni kwa miaka zaidi ya 900, mndio ni 925 alaiejitahidi mpaka nikafunguliwa kifungojni ni babu yako kupitia jini wa bakora. Simba nataka uelewe, jini wa bakora ni jini mwenye heshima sana katika majini. Nafahamu kua ukoo wake walikua na uhusiano na ukoo wa babu yako, yaani ukoo wako kwa baba yako kwa muda mrefu sana., karne nyingi sana, vizazi na vizazi, lakini ni wachache sana katika ukoo wenu siku za nyuma wakaweza kukabidhiwa bakora kama uliopewa wewe. Wote wengine waliopewa bakora au wanapewa bakora za ukoo tu, lakini babu yako alipewa bakora kutoka kwa mwenyewe jini bakora, lakini liitengeza, sio ya kurithi. Bakora ya jini bakora ya kurithi kwa wazeewake ni ile uliopewa wewe tu. Ile bakora kuwepo tu kwako ni kinga kubwa na heshima kubwa sana kutoka kwa majini wote watakao kuona nayo. Nakushangaa wewe umeifungia chumbani.

Miimi; Nimeiweka Arsis, siwezi kutoka na kutembea nayo kila mahali.
Arsis; Nafahamu hilo na Jini bakora anafahamu hilo, dunia ya siku hizi hambebi bakora kama zamani, ni watu na makabila machache sana yenye kujua thamni ya mwanamme kubeba bakora. Mimi nakwambia jizoeshe kua nayo katribu zaidi ile bakora. Usiwe na wasi wasi, Jini bakora hasikii haya maongezi yetu wala hawezi kusogea hapa kusikiliza tunachoongea, tunaheshimiana sana.

Mimi; Arsis; Unaanza kunipiga chenga tena? Hujajibu swali langu.
Arsis; Tafadhali tumia lugha nzuri ukiongea na mimi, kqnza mimi ni mtu mazima sana kwako kwa kiwango chochote kile, halafu mimi ni Mwalimu wako. Acha lugha hizo mitaani. Sikupigi chenga, nipo katika kukujibu swali lako lakini nataka uelewe kwa undani zaisi, fanya dsubira.
Mimi; Samahani, unajua lugha zetu za siku hizi, Nitakua mwangalifu.
Arsis; Usijali Simba. Nisikilize kwa makini. Babu yako alikutana na watu kutoka Pemba wakati anaishi Tanga, hao watu walikuja kutafuta mali za Mjetrumani, miaka mingi sana nyuma.
Mimi: Hujui mwaka gani?
Arsis; Najua ilikuwa mwaka gani, ni mwaka wa 1072 kwa miaka ya dunia ya kwanza, hii dunia tuliopo. Hawa watu, alikua ni kijana mmoja ambae alihadithiwa na babu yake kabla hajafa, kua Tanga, nje kidogo ya mji kuna mali ya Wajerumani imefukiwa. Babu yake alimwabia na yeye kahadithiwa na rafiki yake ambae ameshfariki, lakini ameandika jina ya hio sehemu na alama zilizowekwa. Aliambiwa kua asijaribu kwenda boila kutafuta mwenye nguvu za majini na mwenyeji wa Tanga. Bila hivyo itakua ni hatari sana. Ataekwenda tu bila ulinzi wa nguvu za majini anaweza kufa.

Huyo kijana ndio akaanza kutafuta mtu mwenye nguvu hizo kwao Pemba, wapemba kila akiwaambia au wengine wanadhatrau hio habari au wengine wanaogopa. Ukapata mtu mmoja akamwabia kuna mama wa Kipenda yupo Darisalam, anajua kua huyo mama ana majini wakubwa anawatumia kwa kuondoa matatizo ya watu. Ndio kafunga safari akaja Mjini Dar. Akafanikiwa kumuona huyo mama, huyo mama kweli alikua na majini wakubwa sana na anapandisha kichwanikwake. Walipokuja wale majini wakasema sisi hatujui kuhusu hizo mali lakini kuna mganga mmoja yupo Tanga, huyo mganga ni mtu wa Lamu, Mgunya lakini anaishi Tanga, yeye ana majini wakubwa wa kutokea Tanga wanaweza kujua Yule jini wa mama akawapa anuani mpaka mtaa watakapompata huyo mganga wa kigunya, alikua barabara ya tisa, karibusana na sokoni pale Tanga.

Yule mama wa Kipemba hafanyi ile kazi yake peke yake, yeye anapandisha jini lakini mtu anaetafsiri na lazima anakua karibu yake ni mume wake. Yule mume akasikia kisa chote kile akawa na yeye kapata tamaa ya mali.

Mimi; Arsis kumbe ni mtu wa mikasa mingi wewe.
Arsis; Leo umesikia mali ndio unasikiliza kwa makini? Subiri nimalize, usije kusema nakupiga chenga, nyamaza usikilize mpaka nimalize, usitie neno lako.
Mimi; sawa Arsis, mbona leo unakua mkali hivi?
Arsis; Umeuliza kitu ambacho inabidi nikueleze kwa yundani, vipi nimejuana na babu yako, au hutaki tena kujua?Nyamaza. usijibu.

Nikanyamaza kimya.

Arsis; Leo huondoki hapa mpaka nimalize kukufahamisha.

Basi yule mume na ytule kijana wakahangaika kufanya safari ya kuja Tanga kwa mganaga wa Kigunya, alikua hodari sana wa kusoma vitabu huyo mganga, mtu mzima sana, lakini alikua anajulikana sana kwa kutibu watu na alikua anaweza kuita majini wakubw wakubwa sana. Alikua na maarifa mingi sana.

Baada ya muda, wakafanikiwa kuja Tanga, wakakutana na yule Mzee wa Kigunya wakamueleza ile habari. Yule mzee akawasikiliza kawaambia basi nyinyi kaeni hapa kwangu wakati mimi nafanya uchunguzi wa hiyo habari. Watu wengi wanakuja kuuliza habari za mali za Wajerumani, na wanakwenda kuhangaika san, hakuna alierudi kwangu akanambia kama kafanikiwa au hajafanikiwa, lakini inasemekana zipo, wapi mimi sijui, Kwa sababu mmenipa jina ya hio sehemu, wacheni mimi ntauliza nipeni siku mbili tatu, nikipata jibu lolote nitawajulisha.

Basi wale mabwana wakakaa pale siku ya tatu akwaita. Akawaambia nisikilieni kwa umakini sana.

Hapa Tanga Wajerumani wamekaa sana na njia hio mlionambia kuna mtu hapa anfanya kazi serikalini, ni fundi mkubwa sana, huyu amerithi majini wakubwa sana wa ukoo wake, bipi nimejua hii habari msiniulize. Lakini mimi simjui huyo mtu. Nyie tafdoiteni wenyeji wakepelekeni ile sehemu ya serikali wanapotengeza mashine na magari yao, Muulize fundi mkubwa wa pale, mkimpata njooni nae hapa tuongee nae.

Wale wageni hawakupata tabu kuna baraza ya kahwa na hakua pale jirani waklikua wameshizoea na watu wanacheza bao. Wakauliza pale. Kuna mtu akawaambia kuna fundi pale nyumba ile wa hukohuko karakana, ngija tumtume mtoto akamuite kama yupo.

Basi akatumwa mtoto akaenda, kuuliza akaambiwa hajarudi lakini akirudi watampa salaa kua kuna wageni wao kwenye kahawa atakuja, basi akija kama hampo hapa tutawafata hapo kwa Sheikh.


Basi kufika jioni wanarudi kusali alasiri hawjakaa sana wakaja kuitwa wakedna kibaraza cha kahawa, wakampata yule mtu wakamuita pembeni wakamwabia wao wageni kuna mtu wanamtafuta lakinihamwajui jina isipokua ndio fundi mkubwa wa serikali. Yule mtu akawauliza mzungu huyo au mtu wa hapa tanga? maana pale mimi ndipo ninapofanya kazi, kuna Mzungu ndio Worksjop manager. Na kuna funid wetu mkubwa, mtu wa hapa hapa Tanga maarufu sana anaitwa Mabruki. Wakasema itakua huyo wa Tanga. Maana ingekua mzungu wangetuambiwa mzungu. Akawaambia kama ni huyto basi mmeshampata turudi tukanywe kahawa niwape mtoto awapeleke nyumnai kwake, hayupo mali yupo hapo usagrfam barabara ya saba mwisho kule.

Wakarudi kwenye kahawa, akwaambia wale waliokwenda kumwita , hawa wanamtafuta Mabruk sio mimi jamani. Watu wakasheka, walikua hawamjui jina wanaemtafuta, mbona wangeshafika zamani kwa Mabruki.

Wakapewa mtoto akawapeleka kwa babu yako. Wal wakamwabia unaitwa na Sheikh Mgunya katutuma tuje kukita. Huyu Sheikh Mgunya wa barabara ya tisa? Wakamwabia ndio yeye anakuhitaji kwa ajili yetu. Akawaabia haya, tangulieni nikisha sali magharibi nakiuja huko. Mwambieni ikisha magaharib tu mguu wake huu.

Wakaondoka, kweli baada ya kusali magharibi babu yako akaenda, w)alipofika Mzee wa Kigunya kawaambia haya muhadithieni na mwenyeji wa hapa. Mbruki akmwambia mzee Mgunya, wewe ushaoa wake wanne Tanga mimi nakuona wewe kuaniz mdogo hata huko ugunyani kwenu sijui kama unapajua tena, unasema mi mi mwenyeji. Wewre mwenyeji zaidi yangu bwana.

Mzee wa kigunya kawaambia wale wageni wampoishe kidogo aongee faragha na babu yako wakanywe kahawa akiwa tauayari wataenda kuitwa. Mzee Mgunya akamwabia kwanini alimwita yeye, alimwabia mimi nimeongea na majini wakubwa sana, wao wakanmbia wewe una jini mkubwa mwenye hiyo bakora ulioibeba, yeye mwenyeji wa mitaa hiyo walioitaja, si umeisikia bwana wametaja Amboni lkini sio mapangomi upande unaotazama mapango kwa bharini. Nikaambiwa wewe una wenyeji wa huko watatoa mwangza ndio kisa cha kukuita bwana Mabruki.

Babu yako aksema usemayo kweli lakini hio mali sijawahi kusikia, ningeisikia si ningeshakwenda kuichukua? Mzee mgunya akmwabia akmwabia kweli huijui, hata mimi siijui lakini uradi uliopo hapa, ni uwaulize hao wakubwa huko, tutapata fununiu. Babu yako akasema swa atawaita kwa muda wao wampe siku mbili tatu ataleta majibu.

Wakakubalina hivyo. Wakaitwa wlae mbawna waendelee kusubiri, ikwa yule bwana Mihamed hawei kusuniri tena, akrudimDar, yule kijana akasema miminitasubiri. Mzee Mgunya kamwabia wewe subiri na usiwe na shka ni mgeniwa y. Tuombe iwe heri tu. Tumsubiri Mabruki atupe jibi lake na yeye.


Itaendelea.
Safi saana
 
Inatokea post namba 294.


usiku kama nilivyoahidi kama saa 4 hivi nikaenda viwanja vya kukutana na Arsis, nilipomwita hajachelew akaja.

Arsis; Vipi hali yako Simba?
Mimi; salama, Arsis.
Arsis; Tuendelee. Simab ndio baba yakao akaenda pale mapoangoni akamwita Jini Balra, wakatoka wakaenda kuweka alama ya shamba, wamemaliza siku nzima ya kwanza hawakumaliza, wakafanya ile kazi wiki mzima. Ilikua pori kubwa sana, wanyama wengi, nyoka wengi, tena wewe unapenda pale kwenye mto ule mdogo, pale kuna chatu wakubwa sana, bahati mzuri Jini Bakora ameweka jini inakimbiza ile kila akija. Majani yale ya nyasi ya kule kwenu, manyoezekea yalikua mengi sana, Bahati mzuri walichukua wale wenyeji wanakaa pale karibu karibu wakawasaidia sana, na kundi kubwa ya majini ya Jini Bakora yamesaidia sana kusafisha njia.

Alipomaliza baba yako akaenda kumueleza Mzee Mgunya, wakapanga siku wakaja baba yako na mzee Mgunya mpaka kwenye mapango yale uliolala wewe, wakafanya mkutano wao iakapangwa siku waje pale ndani kugfanya kazi.

Siku ilipofika Mzee Mgunya akasoma vitabu vyake, babu yako amesshapewa njia zote za kufanya, amepewa na kisu cha kukatia lakiri ya ile chupa akaelekezwa akiiona imefika mbele yake, asiogope kitu chochote atachokiona, achukue chupoa akate lakiri, kitu chochote kitakachotoka kwenye chupa asiogope wala asikisemeshe, kikitoka tu ye avunje chupa aikate lakiri na kisu, aifungue akisha ifungua, kuna mawe ya kuvunjia chupa alipewa, alipewa na miti minne aigongelee chini kama mita kila mti kwa pembe nne, kabla ya kuwasha moto. Pale ndani ya miti ndio awashe moto, akiipata chupa akisha ifungua aivunjie chupa pale ndani na atupie pale kwenye moto. Zikaletwa kwanza nyasi nyingi sanaz ikawekwa pembeni zikaletwa kuni nyingi zikawashwa kwanza kuni, ukikolea moto, ndio Mgunya aanze kazi ya kuivuta ardhi kwa elimu yake.

Basi walipowasha moto wa kuni, haikuchukua muda Mgunya akaanza kazi yake, chupa ikaonekana, babu yako akaiona, ilikua imezungukwa na vitu vitu vya kutisha lakini shjaaa yule hakuogopa kabisa na Qur'an aliokua anasoma vile vitu havikuweza kumsogelea, hakupoteza muda akafanya kama alivyoelekezwa huku anaendelea kusoma, akifungua chupa, akaivunjia mule ndani ya moto akaongeza nyasi na juu ya nyasi akaweka magogo ya kuni akjaza nyasi juu yake, Mgunya akamwabia sasa mimi nakwenda zangu, kazi imekwisha. Wewe ondoka hapa, moshi mwingi, kaa nje pale mchangani usiwe na wasi wasi endelea kusoma Qur'an baadae atakuja jini Bakora atakupa maelkezo. Babu akauliza mbona sikuona kitu kilichotoka? Mgunya akacheka akatoka nje. babu yako kutoka nje hamuoni Mgunya, kisha ondoka haonekani hata njia aliopitia. Basi babu yako akakaa pale nje akawa ansoma Qur'an, akasoma pale kama masaa mawili au zaidi kidogo ndio Jini Bakora akaja.

Kuna watu wanasoma kama story halafu kunawengine tupo darasani🤝

Kwahyo ukiwa unaeleza kwenye mafunzo elezea kwa kina, maana kuna watu tunajifunza na kuingiza kwenye utendaji


Mfano juzi.... Baada ya kusoma uzi hapa, na mm nikaenda kuwaita hawa marohani niliorith kwa mzee wangu (nikapanda juu kwenye uwazi sehem ilotulia kwa mbaramwezi, si nikawaita bhana........... Maana nishawazoea kila siku lazima waje karibu muda wote nikiwa pekeangu wanapenda kuja

Sasa juzi nikawaita huku nawapiga beat,,,,, leo staki mje kimyakimya nataka mje muongee hapa au niwaone live😁😁😁😁

Bwama weeeh si upepo ukaanza kuvuma pale,,,,,, nikaanza kuwaza kimoyomoyo "Leo yule jamaa wa Jf kaniponza😂😂😂😂"


Ila walikuja lakini sikuwaona wala hawakusema chochote.... Nikashuka zangu huyooooooo safari🚶🚶🚶
Hata mimi nipo darasani..yaan najifunza mengi
 
Nimefuatilia story yako toka mwanzo kuna elimu kubwa hapa hasa kuhusu viumbe wengine ambao binadamu tunawachukulia poa lakini maisha yetu mengi yanaathiriwa na viumbe hivyo either in positive way or negative way.
Kwa ufupi nikuwa:-
1. Majini wapo wazuri na wabaya kama walivyo binadamu ila ulimwengu wao hauonekani kwa macho ya kawaida.
2. Majini wema wanaweza kutoa misaada kwa mtu hasa aliyekumbwa na majini wachafu hii kwa wasomaji wa ruqya wanalijua sana
3. Qur an ina nguvu kubwa sana isiyomithilika ila wengi katika waislamu wanaichukulia poa.
Mwisho nina maswali ndugu la kwanza embu muulize Arsis anayajua majina ya BARHATIYAH na je ni katika shirki ?
Swali la pili, Muulize Je ni kweli mafuta ya miski yanawaumiza majini wabaya?
 
Kwa mujibu wa imam shafii masufi ni watu wapumbavu
Wasomi wengi wa dini hasa Sunni wanawachukulia sufi kama watu wasio katika usahihi hii ni kutokana na mambo yao hasa wengi kujihusisha na mambo ya uganga ijapokuwa wapo masufi wanaelimu kubwa tuu na ni wachamungu kwelikweli.
Moja katika masufi wakubwa ni huyu Ahmad Al Buni yeye aliandika kitabu maarufu kiitwacho Shams al maarifa inadaiwa ni kitabu cha uganga na mambo ya talasimu.
 
masufi toka enz na enz wao ni watu wa kushinda miskitin na kufanya uradi. sasa ukipewa fadhailul amal na kadiria lazima uchemke mana yeye atakwambia utaje kitu fulan mara laki 1
Hahahaha. nawafahamu sana masufi, Kuna shangazi yangu, Mungu amrehem, alikua na tasbi yake ina shanga za kuhesabia 1000, zina kaa ndani ya kikapu, akianza uradi wake anavuta kikapu chake anakaa nacho pembeni anaanza vitu. Tulikua tunamtania sana utotoni na tasbih yake.

Kunapia rubani mmoja atc ni sufi, huyu tulikua tunakutana kwenye nyumba moja ya uradi hapo Ilala. masufi watu wa karibu sana kwangu, napenda sana nyiradi zao, Hao wa Ilala, wapo na mtaa wa Muhesa pia wapo na Sinza. Tariqa hio hio, kwa wiki wanahama hama tu. tena hao ndio napenda sana kikundi chao, mana wanapiga uradi huku wanapiga mirungi. hawana tatizo kabisa na gomba.

Sema hawa Dheikh wao, amefariki siku nyingi, nilikua napenda sana darsa zake na niliuliz habari kwa Arsis siku moja.

Arsis akanambia anamfahamu huyo Sheikh kupitia makhadim wake, alikua ana makhadim, Ndio jibu la Arsis. Huyo marehem alikua kazi yake ni kutoa elimu ya Kiislam tu na alikua hana makuu kama masufi wengine. Alikua very simple.
 
Wasomi wengi wa dini hasa Sunni wanawachukulia sufi kama watu wasio katika usahihi hii ni kutokana na mambo yao hasa wengi kujihusisha na mambo ya uganga ijapokuwa wapo masufi wanaelimu kubwa tuu na ni wachamungu kwelikweli.
Moja katika masufi wakubwa ni huyu Ahmad Al Buni yeye aliandika kitabu maarufu kiitwacho Shams al maarifa inadaiwa ni kitabu cha uganga na mambo ya talasimu
Masufi watakupotezea muda tu
 
Back
Top Bottom