Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Dah yani toka nimeanza kusoma huu uzi, naona kabisa maswali yangu mengi yanajibiwa humu ndani...... Kwanza huu uzi umefanya sahv nipate amani ya moyo!!!

Maana nilikuwaga najiona kama mtu wa hovyo sana kuwa na connection na majin
(Sahv nimegundua Kumbe sio mtu wa hovyo ila n mtu wa maana😄😄😄😄😋😋)
Kunaviumbe aina kadhaa tupo navyo ambavyo havionekani na vinaweza kua na koneksheni na sisi.

Arsis anafafanua mbele huko.
 
Hapo kwenye kijerumani hapo...... Wajeruman kwenye maficho yao ya mali huwa wameweka majini ambao n very powerful 😄😄😄

Mzee wangu alitafuta mali za wajeruman sana bila mafanikio... Alikutana na visa vingi maana wale jamaa n wachawi balaah

Pia ili utoe mali zao lazima utumie code zao, ukienda na uchawi wa kiafrica utaona cha moto
Kimeshaanza kisa cha Arsis na mali za Wajerumani. Kimeanza juu hapo ndicho kinaendelea kwa sasa.
 
Kwa mtazamo wangu ibada ndio nyepesi kuliko zote. kwani ibada sio kitu cha kukitfuta au kulazimishwa, ni maisha yetu. Waislam tunaamini tunaishi ili tuabudu.

Arsis alinipa maana sana ya neno :kuabudu", itakuja mbele huko katika "vionjo vya Arsis".
Kaka ibada ni ngumu kaka..... Mimi nilipewa uradi wa kumtaja Mwenyezi Mungu mara 24000 kwa siku.
Hapo bado hatujaweka swala za sunna na faradh (mwaka mzima)

Ili nimalize uradi ilinibidi niwe nashinda msikitini siku nzima
(Kuna muda nilikuwa napelekwa itikaf msiktin siku 3 bila kutoka nje)
Na Kuna wakati nakaa mwezi mzima ndani
Kuna wakati nafunga miez 2 mfululizo

(Unahisi ni simple kaka?
 
Inawezekana kwa kua nimekua nao na ndio chanzo kikuu cha uchumi ytulichoachiwa na babu yetu. Kamba ni mali sana kwa sassa, haunipiti msimu wa kamba, hata nikiwa wapi, naacha kilu nawahi kamba.

Hapo kwetu, soko letu kubwa sana ni Kenya, zinakuja boti za ftreezer kununua kila msimu. tunauza kamba kwa hesabu ya dollar kwa siku hizi, hakuna TRA wla fordha wala sijui mwenyekiti wa serikali ya mtaa, manispaa au upuuzi wowote wa kutozana kodi pale kwetu, wao wapo bize kukamata magendo ya kutokea Kenya hapo Duga maforoni,. Shambani kwa mzee Mabruki wanapaogopa kama ukoma, wanachezea fimbo na wanaowachapa hawawaoni. Hapo hata waiba nazi na embe wanapaogopa, Nyani wanapatazama kwa pembeni itakua binadam?
Aisee ntakuja na kikapu changu huko nivune kamba wa kutosha, au arsis anasemaje?
 
Kaka ibada ni ngumu kaka..... Mimi nilipewa uradi wa kumtaja Mwenyezi Mungu mara 24000 kwa siku.
Hapo bado hatujaweka swala za sunna na faradh (mwaka mzima)

Ili nimalize uradi ilinibidi niwe nashinda msikitini siku nzima
(Kuna muda nilikuwa napelekwa itikaf msiktin siku 3 bila kutoka nje)
Na Kuna wakati nakaa mwezi mzima ndani
Kuna wakati nafunga miez 2 mfululizo

(Unahisi ni simple kaka?
Simba; Hio ngumu, pole sana. Itakua huo uradi alikupa katika watu wa Kadiria, wanaoitwa muridi. Wale masufi, sio ibada tu hizo, ni elimu ya kipekee. Arsis anawaelezea hao, natumai itafika wakati tutawasoma hapa.

Arsis ana mengi sana, ulivyonielezea nimeelewa ndugu yangu ulichokumbana nacho. Elimu hio Arsis anaileta kiwepesi sana mpaka utashangaa. Ukipenda kuelewa uliza tu, itakufanyia wepesi.
Simba.
 
😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭

Nasubiri kwa unyenyekevu kabisa mwalim...... Mimi kweli nimepita kwenye twariqa hiyo

Dah kweli kabisa,,,, Kumbe na hao kawaelezea😳😳😳😳😳😳

Nasubiri Sana hii
 
😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭

Nasubiri kwa unyenyekevu kabisa mwalim...... Mimi kweli nimepita kwenye twariqa hiyo

Dah kweli kabisa,,,, Kumbe na hao kawaelezea😳😳😳😳😳😳

Nasubiri Sana hii
Arsis ni kiumbe wa ajabu sana, kuliko tunavyofikiria. Ndio maana ananishikilia sana nimuelezee mafundisho yake.

Hivi nimeanza tu, intro ya nilipoanzia mimi , sasa nimeingia intro ya Arsis alivyokutana na babu yangu. Tukitoka hapo ndio tutaingia "vionjo vya Arsis". hapo kuna mengi na matamu sana.
Simba.
 
B
Inatokea post namba 223.


Nimeona tuwekane wazi kidogo. Kisa kilichowisha post namba 223 kimeelezea nilipokabidhiwa majini na babu yangu, yeye alikuita kufunguliwa macho. Kwa kiwango fulani kweli nilifunguliwa macho. Kisa kilochofatia nikaonesha safari yangu ya kwanza baada ya kuoa, ilionipeleka Shinyanga na majini wakafanikiwa kumfanyia mwanamke aliekua anasumbuliwa na majini. Ieleweke kua sijatibu mimi na wala sijui walitibu vipi zaidi ya mimi kumshika kichwa tu yule mwanamke na walichonielezea hao majini siku ile na baadae.



Kisa hicho ni cha miaka mingi sana nyuma, sasa hivi ni mtu mzima. Babu yangu alishatangulkia mbele ya haki. Shamba letu la ufukweni Duga, lipo mpaka leo, wanaokaa pale kwa sasa ni watoto na wajukuu wa babu walioamua kuishi pale. Watoto waliopo pale ni mmoja mkubwa kwa baba yangu wa kike. Na wakiume na mkewe na wanawe ni kwa mama mwingine na baba yangu, wanachangia baba tu.

Binafsi huwa nakwenda sana Duga shamba la babu, kwa sana namaanisha kila msiumu wa kamba huwa tunaenda mimi na mzee kuvuna kamba. Licha ya kamba, kwa babu kuna minzi mingi sana, kuna miembe mingi. Babu yangu alikua anapenda sana miti ya kudumu, kuna miembe ya aina )ofautoi isiopungua 500 na minazi zaidi ya 1000 aliyoiacha marehemu babu.

Bhati watoto zake wote wanajiweza, wanashughuli zao na mali zao, na wawili, mkubwa wa kike na miumewe na watoto zao na mkubwa wa kiume watumbo lingine ndio wanaoishi huko full time. Waliamua wenyewe waishi huko ili shamba lisikose mtu na lina utajiri wa kutosha. Mbali ya minazi na miembe alioicha babu, kuna miti mingi ya hapa na pale ya matunda, ambayo haipo kwa kiwangi cha biashara. Babu alipanda kila aina ya matunda kidogpo kidogo, shamba la babu ni kubwa sana, sio la kitotpo na nazi karibia kila siku zinangushwa, na pesa wanagawa kwa kila ndugu, Hakuna tatizo, wasimamizi ni wazuri sana na wacha Mungu.

mambo ya tiba na pango kuna wanafunzi wa babu lakini hawako kwa kiwango cha babu lakini mradi wapo tu. Umaar8fi wa kwenda kutibiwa watu kwa mzee Mabruyki uliisha alipoondoka mwenyewe. Mimi binafsi sijairithi kazi ya uganga ya babu, kabisa tena. Wapo majini alioniwachia babu, ikitokea, wao ndio wanatibu watu bila mimi kujua wanachokifanya zidi ya kunijulisha tu.

Arsis yupo, pete yake naivaa kila siku. Jini wa bakora yupo na bakora ya babu aliirithi binti yake ambae anakaa shamba kwa sasa, yeye ndio anaitumia kwa tiba watu wakienda. Anaelewa mwenye anatibu vipi, mimi simuingilii wala simuulizi. Ni shangazi yangu, yeye ananipenda sana na anawaambia kila mtu., mimi ndio mroithi wa babu kwenye uganga.

Visa vinavyofatia sana sana vitakua vya mahojiano kat yangu na Arsis, nitajitahidi kuvifanya vyepesi vieeweke ingawa mimi sio mwandishi.

Arsis mpaka leo ni rafiki yangu na anakuja kila nikimuita xile sehemu zake za kumuita. Mwenyewe anapenda sana kila nikija kwenye msimu wa kamba nimuite kila siku tuongee. Mpaka leo kwa Dar nikita kumuita nakwenda pale oshen road, [pia alinionesha na sehemu nyingine mtajijua wakati kisa kinaende;lea. Hii ipo nje ya mji kidogo.

Visa vijavyo vina elimu kubwa ssna ya Arsis, sio yangu. Mimi najifunza kwake.

Kuna watu wengi wanaongelea kuhusu majini waongo, wazuri, wabaya. Kwenye mahojiano na Arsis tutapata mwanga mkubwa sana kwa mujibu wa Arsis. Napend ieleweke, Arsis anasisitiza sananijifundishe kusoma uandishi ili niandike vizuri, ananambia yeye atanisaidi kumbukumbu kwa niliyoyasahau na atanisaidia kunielezea yale amabyo nitahisi yanahitaji aeleee zaidi.

Nawaahidi nitapitia post moja moja za nyuma na kurekebisha maandishi, kupunguza au kuzidisha na kurekebisha nilipokosea na kuyakusanya kwenye post moja ikiwezekana, yaani kufanyia editing. Ardis kanambia kuna makosa mengi sana, afahamu kua anusoma huu uzi, sifahamu kama ni member JF au hapana, nimemuuliza hilo akanambia " mimi nimekwambia nasoma tu, usiniulize zidi kuhusu hilo". Hiyo ni kawaida yake Arsis, mtajionea mbele huko namuuliza mpaka anakasirika.lakini ni mtummwema sana. Mwenyewe anashikilia nimwite mtu. Ingawa kiukweli sijui ni kiumbe wa aina gani. Mimi nachukulia ni mtu kama mimi lakini hataki aonekane. Isipokua anasema umeshaniona mara nyingi lakini hujui kama ni mimi. Anasisitiza anakuja kwa sura na muonekano tofauti bila mimi kufahamu.


Itaendelea.
Bora tu arsis akufundishe kuandika maana ni unachapia balaa mpaka mwanzo nikajua ni arsis ndio anayeandika
 
N
Inaendelea kutokea post namba 1.

Babu akatupokea pale, tukakumbatiana kwa futraha, mara na bibi nae akaja aliposikia nimefika, akanambia "aah, sasa mume wangu ndio kaingia, sio hiki kizee, sina habari nacho tena". na yeye bibi akanikumbatia akanipiga mabusu ya ngubu ya shavuni, akanambia twende ndni mume wangu, nimekutayarishia chumba chako.

Nyumba ya babu yangu ilikua ni kubwa sana kwa maisha ya kijijini, inavyumba self contain vitatu, umeme utafikiri upo mjini. maana umeme umepita hapo hapo kijijini kwao, wenyewe wanasema huu unakwenda Kenya, unagtikea Hale. Kwa ufupi hauhisi kabisa kama upo kijijini mpaka utoke nje ya bma lake. babu alikua na nyumba hiyo yake kubwa na nyingine ndogo ndogo z vyumba viwili auj kimoja zimetapakaa pote kumzunguka. Nyingi zilikua za kufikia wageni wanaokuja kwa matatizo yao kwa babu yangu, babu alikua mganga wa jadi, tena anaesifika kweli. Kwake hapakosi wageni, mpaka mawaziri utawakuta huko. Kila mmoja na shida yake.

Babu toka nimefika alikua haniwachi peke yangu, ana nyumba moja ipo karibu na kwake hiyo mwenyewe ndio ofisi yake, ina chumba kizuri tu, cha kufanyia shughuli za ke na wageni wake, na kama ina baraza kubwa ndipo wanapoisubiri wageni wanaokuja kumuona, na ina vumba viwili vidogo ndani, mwenyewe anavoiita "operation rooms". Babu alikua anaongea na kuandika Kingereza na Kijerumani kwa ufasaha kabisa. Kabla ya kaumua kurudi kuishi kijijini alikua ni fundi mekanika, tena fireman, wa idara ya vifaa na magari ya serikali hapo tanga. Alikua ni mtua anaejulikana sana Tanga na anaheshimika sana. Ni mcheshi sana, kutwa anatabasamu, akikasirika humjui kabisa, wewe kutwa kucha unamuona ni mtu wa furaha tu.

Itaendelea.
Ni hadithi hii mzee? Am real thing
 
Mimi ninachoweza kufanya ni kukuelekeza tiba ninazozifahamu tu. sina kilinge kama marehemu babu yangu.

Kwa ufupi, mimi sio mganga isipokua kuna tiba nazifahamu na mwenye kutibu ni Muumba wetu.
Natumaini unaweza kunisaidia kwenye jambo ila naomba sana kama unaamini kuwa roho unayotumia haipingani na Roho wa Mungu aliyeziumba mbingu na nchi.
 
Arsis ni kiumbe wa ajabu sana, kuliko tunavyofikiria. Ndio maana ananishikilia sana nimuelezee mafundishpo yake.

Hivi nimeanza tu, intro ya nilipoanzia mimi , sasa nimeingia intro ya Arsis alivyokutana na babu yangu. Tukitoka hapo ndio tutaingia "vionjo vya Arsis". hapo kuna mengi na matamu sana.
Kuna watu wanasoma kama story halafu kunawengine tupo darasani🤝

Kwahyo ukiwa unaeleza kwenye mafunzo elezea kwa kina, maana kuna watu tunajifunza na kuingiza kwenye utendaji


Mfano juzi.... Baada ya kusoma uzi hapa, na mm nikaenda kuwaita hawa marohani niliorith kwa mzee wangu (nikapanda juu kwenye uwazi sehem ilotulia kwa mbaramwezi, si nikawaita bhana........... Maana nishawazoea kila siku lazima waje karibu muda wote nikiwa pekeangu wanapenda kuja

Sasa juzi nikawaita huku nawapiga beat,,,,, leo staki mje kimyakimya nataka mje muongee hapa au niwaone live😁😁😁😁

Bwama weeeh si upepo ukaanza kuvuma pale,,,,,, nikaanza kuwaza kimoyomoyo "Leo yule jamaa wa Jf kaniponza😂😂😂😂"


Ila walikuja lakini sikuwaona wala hawakusema chochote.... Nikashuka zangu huyooooooo safari🚶🚶🚶
 
Back
Top Bottom