Nimeacha Kazi Bila Mkataba, Sasa Nadaiwa Kulipa au Kufanya Kazi Bila Malipo – Naomba Ushauri wa Kisheria

Nimeacha Kazi Bila Mkataba, Sasa Nadaiwa Kulipa au Kufanya Kazi Bila Malipo – Naomba Ushauri wa Kisheria

ranchoboy

Member
Joined
Feb 22, 2022
Posts
46
Reaction score
49
Habari wanajukwaa,

Nahitaji msaada wa kisheria kuhusu suala linalonihusu. Nilikuwa nafanya kazi sehemu fulani bila kuwa na mkataba wa maandishi. Hivi karibuni niliamua kuacha kazi, lakini meneja wa kampuni amenipa chaguo mbili:

Kulipa pesa ya mshahara wa mwezi mmoja.

Kufanya kazi kwa mwezi mmoja bila malipo yoyote.

Amesema kuwa haya ni “taratibu za kitumishi,” lakini hatujawahi kuwa na makubaliano ya maandishi yanayosema hivyo. Pia sijawahi kupewa taarifa yoyote ya taratibu hizo kabla.

Swali langu ni:

Je, nina wajibu wa kisheria wa kulipa pesa au kufanya kazi bila malipo, hata kama hatukuwa na mkataba wa maandishi?

Sheria za kazi zinawaruhusu waajiri kudai haya kutoka kwa mfanyakazi bila msingi wa maandishi?

Ninapaswa kuchukua hatua gani kuhakikisha haki zangu zinalindwa?

Nipo tayari kutoa maelezo zaidi ikiwa yatahitajika. Naomba msaada wenu kuhusu suala hili ili nipate mwongozo wa kisheria.

Asanteni sana!
 
Simple Mwambie akupeleke uko wanako taka huo utaratibu (CMA) 😅😅😂hawezi thubutu kufanya ivyo ,endelea na mambo yako
 
Kama hauna mkataba hakuna kinachokufunga hapo. Agana nao kistaraabu ila hakuna kinachokufunga.

Utaratibu wa kulipa mshahara au kufanya kazi bure haupo ila hili suala hua linakuja endapo mkataba unataka utoe notice kwa kupindi fulani kabla ya kuacha kazi na wewe hukufanya hvyo.

Swali la msingi la kujiuliza ingekua wao ndio wanakuachisha kazi wangekulipa bila kufanya kazi? Kama hapana why wewe ndio ulipe?
 
Kama hamkuwa na mkataba rasmi wa maandishi hakuna kitu hapo. Tena ikiwezekana mwambie utamchomesha kwa kufanyisha watu kazi bila mikataba uone atakavyolaza mshale.

Kuhusu kama unapaswa kulipa au kufanya kazi bila malipo ni ndio kama ungekuwa na mkataba.

Utaratibu wa kuvunja mkataba lazima umpe mwajiri wako notice siyo chini ya siku 28.
 
Habari wanajukwaa,

Nahitaji msaada wa kisheria kuhusu suala linalonihusu. Nilikuwa nafanya kazi sehemu fulani bila kuwa na mkataba wa maandishi. Hivi karibuni niliamua kuacha kazi, lakini meneja wa kampuni amenipa chaguo mbili:

Kulipa pesa ya mshahara wa mwezi mmoja.

Kufanya kazi kwa mwezi mmoja bila malipo yoyote.

Amesema kuwa haya ni “taratibu za kitumishi,” lakini hatujawahi kuwa na makubaliano ya maandishi yanayosema hivyo. Pia sijawahi kupewa taarifa yoyote ya taratibu hizo kabla.

Swali langu ni:

Je, nina wajibu wa kisheria wa kulipa pesa au kufanya kazi bila malipo, hata kama hatukuwa na mkataba wa maandishi?

Sheria za kazi zinawaruhusu waajiri kudai haya kutoka kwa mfanyakazi bila msingi wa maandishi?

Ninapaswa kuchukua hatua gani kuhakikisha haki zangu zinalindwa?

Nipo tayari kutoa maelezo zaidi ikiwa yatahitajika. Naomba msaada wenu kuhusu suala hili ili nipate mwongozo wa kisheria.

Asanteni sana!
Mwambie tu nifanye hayo kwa Mkataba gani? Akikuonyesha mkataba fanya asipokuonyesha Sepa na hana cha kukufanya.
 
Habari wanajukwaa,

Nahitaji msaada wa kisheria kuhusu suala linalonihusu. Nilikuwa nafanya kazi sehemu fulani bila kuwa na mkataba wa maandishi. Hivi karibuni niliamua kuacha kazi, lakini meneja wa kampuni amenipa chaguo mbili:

Kulipa pesa ya mshahara wa mwezi mmoja.

Kufanya kazi kwa mwezi mmoja bila malipo yoyote.

Amesema kuwa haya ni “taratibu za kitumishi,” lakini hatujawahi kuwa na makubaliano ya maandishi yanayosema hivyo. Pia sijawahi kupewa taarifa yoyote ya taratibu hizo kabla.

Swali langu ni:

Je, nina wajibu wa kisheria wa kulipa pesa au kufanya kazi bila malipo, hata kama hatukuwa na mkataba wa maandishi?

Sheria za kazi zinawaruhusu waajiri kudai haya kutoka kwa mfanyakazi bila msingi wa maandishi?

Ninapaswa kuchukua hatua gani kuhakikisha haki zangu zinalindwa?

Nipo tayari kutoa maelezo zaidi ikiwa yatahitajika. Naomba msaada wenu kuhusu suala hili ili nipate mwongozo wa kisheria.

Asanteni sana!
Hii dunia kuna watu mnaonewa sana aisee. Mpotezee huyo mpuuzi.
 
Kimsingi wewe ulikua mwajiriwa HALALI wa kampuni/ofisi hio pasipo MKATABA wa ajira.
Lakini kanuni za kiutumishi zinakutambua, kukulinda au kukuhukumu pia.
Usingali kua mwajiriwa wa ofisi hio usinge ruhusiwa kuingia kwenye majengo ya ofisi hio na nadhani pia kwenye hio ofisi kuna mahali mwandiko wako upo, chunga ikiwa watu hawajauiga na kukusainia kwenye Mkataba wa ajira.
 
Mikataba ipo ya aina nyingi ikiwamo wa maandishi na usio wa maandishi.Yote inatambulika kwa mujibu wa sheria.

Hilo litathibitika kwa Ushahidi wa namna mlivyokuwa mkipeana malipo yenu.

Walikuwa wanakutimizia haki zako za Msingi kama kukulipia kwenye Taasisi ya Mafao, Bima,na Mshahara wako ulikuwa unalipwa vipi?

Kikubwa kama kuna shida imejitokeza kaeni chini muwekane sawa kabla nyie wote hamjapeana hasara ya kupoteza muda na pesa
 
Kisheria kama hakuna mkataba , unaweza kuacha kazi muda wowote au kusimamishwa bila taarifa, bila mkataba hakuna chochote hapo .
Nenda zako bila hofu.

Kiuhalisia hamna kitu kama inferred contract , kama hujaiba chochote na hudaiwi kitu ofisini usiwe na shaka.

Akiforce nyote mnakula hasara.
 
Habari wanajukwaa,

Nahitaji msaada wa kisheria kuhusu suala linalonihusu. Nilikuwa nafanya kazi sehemu fulani bila kuwa na mkataba wa maandishi. Hivi karibuni niliamua kuacha kazi, lakini meneja wa kampuni amenipa chaguo mbili:

Kulipa pesa ya mshahara wa mwezi mmoja.

Kufanya kazi kwa mwezi mmoja bila malipo yoyote.

Amesema kuwa haya ni “taratibu za kitumishi,” lakini hatujawahi kuwa na makubaliano ya maandishi yanayosema hivyo. Pia sijawahi kupewa taarifa yoyote ya taratibu hizo kabla.

Swali langu ni:

Je, nina wajibu wa kisheria wa kulipa pesa au kufanya kazi bila malipo, hata kama hatukuwa na mkataba wa maandishi?

Sheria za kazi zinawaruhusu waajiri kudai haya kutoka kwa mfanyakazi bila msingi wa maandishi?

Ninapaswa kuchukua hatua gani kuhakikisha haki zangu zinalindwa?

Nipo tayari kutoa maelezo zaidi ikiwa yatahitajika. Naomba msaada wenu kuhusu suala hili ili nipate mwongozo wa kisheria.

Asanteni sana!
Wewe lala mbele uendelee na mitikasi yako mtaani ,huyo bwana mdogo anakuzingua hawezi kukupeleka popote .
 
Hawawezi kukufanya chochote, wanakutishia tu. Ila ni vizuri pia kuwa muungwana, kwa sababu walikustiri pale ambapo ulikuwa huna kitu, jitahidi kutumia busara zaidi.​
 
Kama hamkuwa na mkataba rasmi wa maandishi hakuna kitu hapo. Tena ikiwezekana mwambie utamchomesha kwa kufanyisha watu kazi bila mikataba uone atakavyolaza mshale.

Kuhusu kama unapaswa kulipa au kufanya kazi bila malipo ni ndio kama ungekuwa na mkataba.

Utaratibu wa kuvunja mkataba lazima umpe mwajiri wako notice siyo chini ya siku 28.
Sio lazima inategemea mkataba.
 
Mkuu kwani uliandika barua ya kuacha kazi?

Huyo boss anakutisha hawezi kukupeleka popote. Akizisha usumbufu nenda CMA
 
Kuna chochote ambacho unahitaji bado kutoka kwa mwajiri wako. Kama barua ya utumishi n.k?
Ulishawahi kusinya mkataba mwingine awali?( kwa maana ya mkataba umeisha na hujaongezewa?)
Kama hamna basi safari njema.
Infact, hata kama ungetoa notice bado usingefanya kazi bure, unhelipwa kama kawaida,
Waajiri wanachezaga sana na maslahi ya watu tusiojielewa.
 
Mkuu kwani uliandika barua ya kuacha kazi?

Huyo boss anakutisha hawezi kukupeleka popote. Akizisha usumbufu nenda CMA
Nilimwambia kwa maneno sasa nataka nimwandikie barua
 
Back
Top Bottom