Nimeamini masharti ya marehemu wakiyasema kabla ya kukata roho

Nimeamini masharti ya marehemu wakiyasema kabla ya kukata roho

Binafsi hatukuweka jiwe ila tuligehza jeneza mbele nyuma nyuma pakawa mbele ili marehemu asitusumbue napo cha moto tulikiona.Msiba ulifika kwa tabu sana na maiti ilikua inalia machozi kabisa ma shingo ilikua imeangalia pembeni.Kaburi lilichimbwa matatu maana mawe makubwa yalikua yanajitokeza kuzuia kuzikwa.ikafanyika mila ndio kaburi la nne likawa saaa akazikwa.Ila cha moto tulikiona
Dah, hii inakuaje
 
Mishuaa kila Rangi nmeandaa
Sindano tayari
Kitambaa kipo
Parachichi tayari (au tunda la kimasihara?)
Udi zipo Aina nne tofauti
Chumvi tayari
Aya Twende kazi au na nyanyo za pisi pia zinahitajika??
Kwa taarifa yako ushakuwa mwanga tayari kwa hayo matakataka unayomiliki ukipewa na ngozi ya fisi tu unapaa usiku
 
Binafsi hatukuweka jiwe ila tuligehza jeneza mbele nyuma nyuma pakawa mbele ili marehemu asitusumbue napo cha moto tulikiona.Msiba ulifika kwa tabu sana na maiti ilikua inalia machozi kabisa ma shingo ilikua imeangalia pembeni.Kaburi lilichimbwa matatu maana mawe makubwa yalikua yanajitokeza kuzuia kuzikwa.ikafanyika mila ndio kaburi la nne likawa saaa akazikwa.Ila cha moto tulikiona
Mara nyingi marehemu akiwa na mambo haya-Ni ishara mbaya sana ya huko anapokwenda au alipo (No peace at all).
 
Asikudanganye Mtu popote pale ulipo kuwa kauli za Watu waliokufa namaanisha Marehemu wakizisema huwa hazitimii. Ni kwamba huwa hawatanii kabisa na wayasemayo hutokea na hutimia.

Mwaka jana nilihudhuria Msiba Mmoja ambapo kumbe Marehemu wakati anakata Roho alisema akifa azikwe Dar es Salaam na Ndugu wakampuuza wakamsafirisha wanafika tu Segera wakapata Ajali na wale wale waliolazimisha asafirishwe Wakafa na Msafara ukageuka na kuja Kuzikwa Dar kama ambavyo Marehemu aliagiza.

Mwaka huu Mwezi February kuna Marehemu alisema akifa tu asizikwe Dar es Salaam na akazikwe Kijiini Kwao na Ndugu walipolazimisha Kumzikia Dar es Salaam kwa Kigezo cha Kuokoa Gharama Jeneza lake liligoma Kubebeka ila baada ya muda tu Ndugu walipokubaliana asafirishwe kama alivyoagiza Jeneza lilikuwa jepesi mno Kubebeka na akasafirishwa Kijiini Kwake kwa Maziko.

Leo hii kwa wale Wakazi wa Chang'ombe Temeke nadhani Ajali mbaya iliyotokea Mataa na kusababisha Vifo na Majeruhi mmeisikia.

Ni kwamba Marehemu ambaye ndiyo alikuwa anasafirishwa kwenda Kuzikwa kabla ya kufa kwa Hasira alisema kuna Watu Wawili katika Familia yake akifa hataki waende Kumzika kwani wakati anaumwa na Kalazwa Hospitali walishindwa kwenda Kumuona huku uwezo huo wakiwa nao isipokuwa Dharau na Kupuuza kuliwatawala.

Na katika Ajali hi ya leo ambayo ilikuwa na Msafara wa Gari kadhaa Gari ambayo imegongwa na Kuharibika vibaya ni ya Watu wale wale Walengwa Wawili ambapo wote Wamefariki huku Mmoja Viganja vyake vikikatika.

Hivyo basi baada ya Msiba huu kutokea Msafara wa kumsafirisha Marehemu umeendelea na wale Watu aliowakataa wasimzike nao Wamefariki hivyo Maiti zao zipo Mochwari kwa sasa ukisubiri Msafara ulio Safarini ukirejea ndiyo waanze Kuhangaika nao na Wawazike.

Hata hivyo kuna Mbinu moja nilipewa na Wabobezi wa Kusafirisha Maiti / Marehemu wenye Masharti magumu hasa ya Kusafirishwa kuwa mkianza tu Safari tafuta Jiwe Kubwa / Jiwe Dogo liweke juu ya Jeneza na Marehemu / Mwili hautowasumbueni hadi mnafika. Bado sijaiamini ila kama hapa JamiiForums kuna wenye kuijua zaidi watufafanulie tafadhali.

Jamani tujitahidi mno na sana Kuziheshimu Kauli za mwisho mwisho za Marehemu kwani nimeamini kuwa kwa 85% huwa zinatimia japo kwa 15% zinaweza zisitimie vile vile kama ilivyo kwa Chanjo ya UVIKO-19 ambapo kwa 15% inaweza isikusaidie na ikakuathiri ila kwa 85% huwa inasaidia Kukukinga.
Hao marehemu walikuwa wachawi. Hamna jipya hapo. Aliyekufa kafa
 
Ninayoikumbuka kuna mzee alisema sitaki siku ya kunizika mfanye mbwembwe kama sherehe kutokana na uwezo wa kifedha wa ile familia. Alisema anataka azikwe simple sio mambo ya vyakula, pombe n.k.

Sasa alipifariki watoto ni kama walifanya sherehe.. kitaa watu walihamia pale ni kula na kunywa. Siku ya maziko vivyo hivyo wakazika fresh.

Baada ya siku moja wakaja polisi wana kibali kwamba mtu aliyezikwa sio huyo. Kaburi likafukuliwa kuangalia kweli marehem sio wa familia husika. Ikabid waende tena mortuary kuchukua maiti yao na kuja kuzika kimya kimya bila mbwembwe.
[emoji1787][emoji1787] aiseee
 
Juzi Kati nilienda kufuata maiti Mortuary sijui hili wala lile kumbe unaweza ambua makubwa.Kwanza nahisi kuumwa umwa hovyo since then.

Sitokuja kwenda kufuata maiti zisizonihusu maana hii kitu nimefanya mara 2 kwa watu 2 tofauti nisiowafahamu ila tuu ni vifo vya mtaani kujifanya jirani mwema.
Mkuu kwa hili nakuunga mkono asilimia [emoji817]
 
andaa mshumaa
andaa sindano
andaa kitambaa cheupe
andaa tunda unalolipeda sana kulila
andaa udi
andaa chumvi ya mawe

ukimaliza kuviandaa ni PM tumalize kazi.
Aloooo
 
Akikataa kuzikwa eneo A, akang'ang'ania kuzikwa eneo B. Na ninyi ndugu kwa sababu za msingi sana mkaona azikwe eneo A msipate shida sana. Kukwepa hayo mabalaa tumeni ndugu mmoja wa Kiume eneo B akachukue udongo kidogo katika kisado aulete eneo A.

Mkichimba kaburi miminieni udongo mloleta kutoka eneo B, bakisheni kidogo. Jeneza likishawekwa chini kaburini ule muda wa kuweka udongo malizieni na ule mlobakisha.

Muhimu kukumbuka udongo ulioletwa ufike siku moja au zaidi kabla ya maiti kutolewa mortuary. Kwenyw udongo ule kuwe na mawe madogo madogo kadhaa. Chukueni jiwe moja miliweke kwenye gari itakayosafirisha maiti kutoka mortuary mpaka makaburini.

Baada ya shughuli yote kukamilika. Gari lililombeba marehemu lisiende nyumbani kabla halijaoshwa. Lioshwe na mtu/watu baki (wasio ndugu) prefferably kwenye Car Wash za mitaa jirani au mtoni. Yule ndugu aliefuata udongo eneo B asiende kwake moja kwa moja baada ya msiba, wengi hupitia Bar kuzuga zuga walau three hours hivi, ikiwezekana kulipia lodge akaoge huko kwanza itapendeza.
Hii process mbona refu. Si bora mumpeleke marehemu alipotaka tu jamani. Kwa maana hatopata nafasi nyingine ya kuchagua tena maneno yake bora yaheshimiwe.
 
Akikataa kuzikwa eneo A, akang'ang'ania kuzikwa eneo B. Na ninyi ndugu kwa sababu za msingi sana mkaona azikwe eneo A msipate shida sana. Kukwepa hayo mabalaa tumeni ndugu mmoja wa Kiume eneo B akachukue udongo kidogo katika kisado aulete eneo A.

Mkichimba kaburi miminieni udongo mloleta kutoka eneo B, bakisheni kidogo. Jeneza likishawekwa chini kaburini ule muda wa kuweka udongo malizieni na ule mlobakisha.

Muhimu kukumbuka udongo ulioletwa ufike siku moja au zaidi kabla ya maiti kutolewa mortuary. Kwenyw udongo ule kuwe na mawe madogo madogo kadhaa. Chukueni jiwe moja miliweke kwenye gari itakayosafirisha maiti kutoka mortuary mpaka makaburini.

Baada ya shughuli yote kukamilika. Gari lililombeba marehemu lisiende nyumbani kabla halijaoshwa. Lioshwe na mtu/watu baki (wasio ndugu) prefferably kwenye Car Wash za mitaa jirani au mtoni. Yule ndugu aliefuata udongo eneo B asiende kwake moja kwa moja baada ya msiba, wengi hupitia Bar kuzuga zuga walau three hours hivi, ikiwezekana kulipia lodge akaoge huko kwanza itapendeza.
Hii yote shida ya nini hasa?
 
Cha Ajabu ishu kama hizi za Ajali za kusafirisha Maiti, lawama anapewa Dereva, kumbe chanzo cha Ajali ni Marehemu.

Kama ile iliotokea miezi mitatu Morogoro eneo la nane nane usiku wa saa mbili walikuwa wanasafirisha mwili kuelekea Mbeya, wakakutana na Lori uso kwa uso
 
Back
Top Bottom