Nimeamini masharti ya marehemu wakiyasema kabla ya kukata roho

Nimeamini masharti ya marehemu wakiyasema kabla ya kukata roho

Hiyo ya 'sitaki fulani afike siku nikifa' nimeshuhudia matukio mawili maeneo tofauti.

La kwanza ilikuwa mke alikula njama kumwua mumewe kwa sumu. Alihangaika kwa matibabu ilishindikana. Kabla hajafa akasema mkewe asisogee msibani. Kwa jeuri ya pesa alikodi polisi wakamsindikiza kijijini kumzika mumewe wakati muda wote wa kuumwa hakujali. Aliposogelea jeneza aiangalie maiti, marehemu alifungua macho live.

La pili ni ndugu waligombana. Mmoja akasema hata nife mdogo wangu asisogee kunizika.Siku ilipofika dogo akajitosa kwenda msibani. Kiangazi mvua ilinyesha na ilipiga radi ya kutisha. Bahati nzuri haikuleta madhara. Dogo akaondolewa eneo la tukio na mvua ikaisha jua likawaka.
Huyo marehemu ni mpumbavu? Sasa kuna faida gani? Umekataa asije kukuzika lakini mali zako anatumbua na hawara yake? Halafu unakimbilia kufumbua macho ndani ya jeneza, hivi ana akili kweli huyo mume? Na ndiyo maana akapewa sumu. Alitakiwa na yeye kulipa kisasi kabisa, sio kujifumbulisha fumbulisha macho, shame on him!
 
My God, yaai anajivua gamba? Ulikuwa utajiri wa giza huo.
Hapana Ni UGONJWA ambao alitendwa na mhindi mmoja ambae alikuwa mmewake aliilazimisha waondoke kwenda India kuishi mamkubwa akakataa ndo akampa Hilo janga la ngozi kubanduka
 
Magufuli alikuwa ni takataka na taahira na ndio maana hata COVID ilipita naye. Hakuwa na akili halafu alikuwa katili
Yes, kiongozi bora ni lazima uwe katili. Ukiwa katili tu, yaani hata usipokuwa na akili, ukawa taahira au ukawa taka taka, yaani unabaki kuwa mwamba tu. Magufuli ni mwamba na ni machine, vyeti fake, watumbuliwa, wapigaji lazima haja kubwa zigonge chupi, jamaa hacheki na kima.
 
Huyo marehemu ni mpumbavu? Sasa kuna faida gani? Umekataa asije kukuzika lakini mali zako anatumbua na hawara yake? Halafu unakimbilia kufumbua macho ndani ya jeneza, hivi ana akili kweli huyo mume? Na ndiyo maana akapewa sumu. Alitakiwa na yeye kulipa kisasi kabisa, sio kujifumbulisha fumbulisha macho, shame on him!

Sasa akili azipate wapi na amekufa..!![emoji2377]
 
Yes, kiongozi bora ni lazima uwe katili. Ukiwa katili tu, yaani hata usipokuwa na akili, ukawa taahira au ukawa taka taka, yaani unabaki kuwa mwamba tu. Magufuli ni mwamba na ni machine, vyeti fake, watumbuliwa, wapigaji lazima haja kubwa zigonge chupi, jamaa hacheki na kima.
Vyeti feki wengi wapo kazini wanadunda, hata ndugu zangu na marafiki zangu wapo wengi jeshini kwa vyeti feki wanadunda.

Kibwengo Magu alikuwa mwamba wa kuinea vidagaa huko, walimu wa UPE
 
Hapana Ni UGONJWA ambao alitendwa na mhindi mmoja ambae alikuwa mmewake aliilazimisha waondoke kwenda India kuishi mamkubwa akakataa ndo akampa Hilo janga la ngozi kubanduka
Na ndio maana nakuambia, sio ugonjwa wa kawaida hata kidogo! Alirogwa, pia naye alikuwa mshirikina. Haiwezekani mali zianze kuwasumbua watumiaji. Huyo ndugu yenu alijua kila kitu kuhusu ugonjwa na mali zake, aliwaficha.
 
Mshana uko wapi???.........naomba utupie neno hapa.............maana mie kuna mtu alishaniambia nisisogelee kaburi (maziko) yake, alimaanisha japo kwa sasa naona kama amejivua gamba kimya kimya.....
 
Ndugu popote pale ulipo pokea Saluti yangu ya Kipekee kabisa Kwako kwa Elimu hii nzuri na Kubwa ambayo nakuhakikishia nimeipokea vyema na naamini Watu wengi pia wamefaidika nayo.

Ubarikiwe mno na Asante sana sasa Marehemu wetu Wabishi na wenye Masharti ya Kukomoana watatukoma kwani tumeshapata sasa Dawa yao ya Kuwatuliza Udongoni bila Kututesa na Kutusumbua pia.
Hata mkalete udongo ndoo nzima nilisema nikifa nizikwe hapa hapa shambani.

Najua mtatamani kuuza hapa maana nimeshapaendeleza. Jaribuni na huo udongo wenu gari litaanguka tu.

Natamani Mshana Jr usikose uhakikishe padre yupo pia. Mmh tena sitaki niwekwe kwenye friji.

Niko serious namba zenu nitampa lulu.
 
Akikataa kuzikwa eneo A, akang'ang'ania kuzikwa eneo B. Na ninyi ndugu kwa sababu za msingi sana mkaona azikwe eneo A msipate shida sana. Kukwepa hayo mabalaa tumeni ndugu mmoja wa Kiume eneo B akachukue udongo kidogo katika kisado aulete eneo A.

Mkichimba kaburi miminieni udongo mloleta kutoka eneo B, bakisheni kidogo. Jeneza likishawekwa chini kaburini ule muda wa kuweka udongo malizieni na ule mlobakisha.

Muhimu kukumbuka udongo ulioletwa ufike siku moja au zaidi kabla ya maiti kutolewa mortuary. Kwenyw udongo ule kuwe na mawe madogo madogo kadhaa. Chukueni jiwe moja miliweke kwenye gari itakayosafirisha maiti kutoka mortuary mpaka makaburini.

Baada ya shughuli yote kukamilika. Gari lililombeba marehemu lisiende nyumbani kabla halijaoshwa. Lioshwe na mtu/watu baki (wasio ndugu) prefferably kwenye Car Wash za mitaa jirani au mtoni. Yule ndugu aliefuata udongo eneo B asiende kwake moja kwa moja baada ya msiba, wengi hupitia Bar kuzuga zuga walau three hours hivi, ikiwezekana kulipia lodge akaoge huko kwanza itapendeza.
Ufafanuzi mzuri, umeweka details nyingi ndogo ndogo kiasi kinachofanya niamini kuwa unayosema hujayabuni tu(sina maana ni ya kweli au si kweli)

Tatizo ambalo mimi linaniwia vigumu kuamini aina hizi za story, ni kwamba zina base kwenye correlation yaani Tukio B linatokea baada ya tukio A bila tukio A kuwa sababu ya tukio B

Na sio causation, yaani pale tukio B linapotokea baada ya kusababishwa na tukio A

Kwanini naamini haya matukio ni correlation?
Let say kuna case 1000 kila mwezi ambapo marehemu kwa sababu anazozijua yeye anatoa masharti fulani ambayo yanapaswa kutekelezwa baada ya kifo chake

Then case 50 tu kati ya hizo, ndio zikaonyesha hayo madhara ya kutotimiza hayo masharti

Je cases 950 kwanini hazionyesha madhara?

Pia kwenye maelezo yako... Umefafanua kiasi gani tunaweza epuka hayo madhara

Swali langu ni "how" hii njia inafanya kazi?
Mfano Daktari akinambia ninywe hizi dawa kutwa mara tatu, kuna reason za "how" hii dawa inafanya kazi na kwanini napaswa kunywa kutwa mara tatu

Sio kwa ubaya, unaweza nipa maarifa kidogo on behalf ya kina "Tomaso" wenzangu kivipi hii njia inafanya kazi?

Kivipi jiwe dogo juu ya jeneza linaweza kuzuia kauli ya marehemu isifanye kazi

Na hii kauli ya marehemu ni nini haswa?... Masharti ya mwisho ya marehemu au "natural force" nyingine tusiyo ifahamu
Na kivipi inafanya kazi?... Ina base kwenye inverse square law pia (like 1/d^2)
 
Asikudanganye Mtu popote pale ulipo kuwa kauli za Watu waliokufa namaanisha Marehemu wakizisema huwa hazitimii. Ni kwamba huwa hawatanii kabisa na wayasemayo hutokea na hutimia.

Mwaka jana nilihudhuria Msiba Mmoja ambapo kumbe Marehemu wakati anakata Roho alisema akifa azikwe Dar es Salaam na Ndugu wakampuuza wakamsafirisha wanafika tu Segera wakapata Ajali na wale wale waliolazimisha asafirishwe Wakafa na Msafara ukageuka na kuja Kuzikwa Dar kama ambavyo Marehemu aliagiza.

Mwaka huu Mwezi February kuna Marehemu alisema akifa tu asizikwe Dar es Salaam na akazikwe Kijiini Kwao na Ndugu walipolazimisha Kumzikia Dar es Salaam kwa Kigezo cha Kuokoa Gharama Jeneza lake liligoma Kubebeka ila baada ya muda tu Ndugu walipokubaliana asafirishwe kama alivyoagiza Jeneza lilikuwa jepesi mno Kubebeka na akasafirishwa Kijiini Kwake kwa Maziko.

Leo hii kwa wale Wakazi wa Chang'ombe Temeke nadhani Ajali mbaya iliyotokea Mataa na kusababisha Vifo na Majeruhi mmeisikia.

Ni kwamba Marehemu ambaye ndiyo alikuwa anasafirishwa kwenda Kuzikwa kabla ya kufa kwa Hasira alisema kuna Watu Wawili katika Familia yake akifa hataki waende Kumzika kwani wakati anaumwa na Kalazwa Hospitali walishindwa kwenda Kumuona huku uwezo huo wakiwa nao isipokuwa Dharau na Kupuuza kuliwatawala.

Na katika Ajali hi ya leo ambayo ilikuwa na Msafara wa Gari kadhaa Gari ambayo imegongwa na Kuharibika vibaya ni ya Watu wale wale Walengwa Wawili ambapo wote Wamefariki huku Mmoja Viganja vyake vikikatika.

Hivyo basi baada ya Msiba huu kutokea Msafara wa kumsafirisha Marehemu umeendelea na wale Watu aliowakataa wasimzike nao Wamefariki hivyo Maiti zao zipo Mochwari kwa sasa ukisubiri Msafara ulio Safarini ukirejea ndiyo waanze Kuhangaika nao na Wawazike.

Hata hivyo kuna Mbinu moja nilipewa na Wabobezi wa Kusafirisha Maiti / Marehemu wenye Masharti magumu hasa ya Kusafirishwa kuwa mkianza tu Safari tafuta Jiwe Kubwa / Jiwe Dogo liweke juu ya Jeneza na Marehemu / Mwili hautowasumbueni hadi mnafika. Bado sijaiamini ila kama hapa JamiiForums kuna wenye kuijua zaidi watufafanulie tafadhali.

Jamani tujitahidi mno na sana Kuziheshimu Kauli za mwisho mwisho za Marehemu kwani nimeamini kuwa kwa 85% huwa zinatimia japo kwa 15% zinaweza zisitimie vile vile kama ilivyo kwa Chanjo ya UVIKO-19 ambapo kwa 15% inaweza isikusaidie na ikakuathiri ila kwa 85% huwa inasaidia Kukukinga.
Unapiga ramli?
 
Asikudanganye Mtu popote pale ulipo kuwa kauli za Watu waliokufa namaanisha Marehemu wakizisema huwa hazitimii. Ni kwamba huwa hawatanii kabisa na wayasemayo hutokea na hutimia.

Mwaka jana nilihudhuria Msiba Mmoja ambapo kumbe Marehemu wakati anakata Roho alisema akifa azikwe Dar es Salaam na Ndugu wakampuuza wakamsafirisha wanafika tu Segera wakapata Ajali na wale wale waliolazimisha asafirishwe Wakafa na Msafara ukageuka na kuja Kuzikwa Dar kama ambavyo Marehemu aliagiza.

Mwaka huu Mwezi February kuna Marehemu alisema akifa tu asizikwe Dar es Salaam na akazikwe Kijiini Kwao na Ndugu walipolazimisha Kumzikia Dar es Salaam kwa Kigezo cha Kuokoa Gharama Jeneza lake liligoma Kubebeka ila baada ya muda tu Ndugu walipokubaliana asafirishwe kama alivyoagiza Jeneza lilikuwa jepesi mno Kubebeka na akasafirishwa Kijiini Kwake kwa Maziko.

Leo hii kwa wale Wakazi wa Chang'ombe Temeke nadhani Ajali mbaya iliyotokea Mataa na kusababisha Vifo na Majeruhi mmeisikia.

Ni kwamba Marehemu ambaye ndiyo alikuwa anasafirishwa kwenda Kuzikwa kabla ya kufa kwa Hasira alisema kuna Watu Wawili katika Familia yake akifa hataki waende Kumzika kwani wakati anaumwa na Kalazwa Hospitali walishindwa kwenda Kumuona huku uwezo huo wakiwa nao isipokuwa Dharau na Kupuuza kuliwatawala.

Na katika Ajali hi ya leo ambayo ilikuwa na Msafara wa Gari kadhaa Gari ambayo imegongwa na Kuharibika vibaya ni ya Watu wale wale Walengwa Wawili ambapo wote Wamefariki huku Mmoja Viganja vyake vikikatika.

Hivyo basi baada ya Msiba huu kutokea Msafara wa kumsafirisha Marehemu umeendelea na wale Watu aliowakataa wasimzike nao Wamefariki hivyo Maiti zao zipo Mochwari kwa sasa ukisubiri Msafara ulio Safarini ukirejea ndiyo waanze Kuhangaika nao na Wawazike.

Hata hivyo kuna Mbinu moja nilipewa na Wabobezi wa Kusafirisha Maiti / Marehemu wenye Masharti magumu hasa ya Kusafirishwa kuwa mkianza tu Safari tafuta Jiwe Kubwa / Jiwe Dogo liweke juu ya Jeneza na Marehemu / Mwili hautowasumbueni hadi mnafika. Bado sijaiamini ila kama hapa JamiiForums kuna wenye kuijua zaidi watufafanulie tafadhali.

Jamani tujitahidi mno na sana Kuziheshimu Kauli za mwisho mwisho za Marehemu kwani nimeamini kuwa kwa 85% huwa zinatimia japo kwa 15% zinaweza zisitimie vile vile kama ilivyo kwa Chanjo ya UVIKO-19 ambapo kwa 15% inaweza isikusaidie na ikakuathiri ila kwa 85% huwa inasaidia Kukukinga.
kwa chanjo hapana
 
Back
Top Bottom