Nimeamini masharti ya marehemu wakiyasema kabla ya kukata roho

Nimeamini masharti ya marehemu wakiyasema kabla ya kukata roho

Mnapotoa haya masharti uchwara muwe mnahakikisha mmeacha pesa pia, sio usafirishwe tu kwa kuchangisha wengine.
Nawaambia kila siku hivyo hivyo!
Unakuta mtu yuko huko Belgium anaponda raha uhai wake wote hana akiba hana pensheni. Akifa anaacha wosia ooh nikifa nirudisheni nyumbani tena kijijini WTF!Umeacha bei gani ?0

Gharama kusafirisha maiti mpk Dar tu 25 000+$, Bado hamjampeleka kijijini na gharama zingine. Anawaachia mzigo wanae km anao na marafiki michango inaanza mpk inabidi pombe ziuzwe hela ipatikane,watoto mpaka wanakopa benki.

Marehemu ye kalala tu na wosia wake.

Hata mchango hatoi
 
Kuna kisa kilitokea katika msiba wa mfanyakazi mwenzetu Tabora. Maeneo ya mirambo barracks kulikua na mochwari, tulipeleka nguo za marehemu kutoka kwake kwa ajili ya kumsitiri ili asafirishwe kwenda kuzikwa kwao kijijini, tulienda na timu ya staff hakuwepo ndugu yoyote

Tukaingiza jeneza ndani ya chumba cha mochwari, sasa ikafika wakati wa kumvalisha nguo marehemu, yule jamaa wa mochwari akaita staff wawili wanawake waingie na nguo kusaidiana kumvalisha marehemu, sisi tulibaki nje basi baada ya muda wale wenzetu wawili waliambiwa watoke nje sababu marehemu alikataa kuvaa nguo ikabidi sisi tuliokua nje kuingia na kusaidia kumvalisha marehemu na kumuandaa, yule jamaa wa mochwari akatuambia kuwa marehemu aligoma kabisa kuvaa walipoingia wale wadada.

Tulipoingia sisi tukamvalisha na akaandaliwa fasta ila tulikumbuka kuwa kati ya wale wafanyakazi wenzetu kuna mmoja alikuwa haelewani kabisa na marehemu ila ilibidi aingie sababu alikuwa ni kiongozi wetu.

Wakati tupo ndani tulikuwa tuna mdadisi mambo mengi yule jamaa anayefanya kazi mochwari akatuambia maiti zinakuaga na vituko vingi sana na pia kuna watu wanawapokea kama maiti mochwari na wanakuwa hawajafa ila jamaa alisema huwa anawamalizia au anawaacha wafe kiukweli kuepuka taharuki.

Alitupa stori ya bibi mmoja wa miaka zaidi ya themanini ambaye aliletwa mochwari kuhifadhiwa ila hakupoa na kuwa wabaridi na alikuwa akipumua kwa mbali na kila ndugu wakija kuchukua mwili kwa ajili ya kwenda kuzikwa ilibidi wawaambie ndugu wasubiri hadi waliposhirikisha wazee wa Mila ikagundulika kuwa kuna kipenzi cha huyo bibi alihitajika kumvalisha na kumsafisha bibi yake ndio mambo yawe sawa.
 
Niliwahi ona pia miaka hiyo kuna mzee kabla ya kufariki alitoa maagizo akifa azikwe pale pale nyuma ya nyumba yake.
Sasa alipofariki ndugu wakakubaliana wakazike kwenye makaburi ya kijiji badala ya pale nyumbani kwake,,,aisee walizika fresh tu ila usiku ulipoingia hakuna aliyelala siafu walitanda nyumba nzima haieleweki walikotoka wanang'ata watu si wafiwa si ndugu yaani wote waliopo ndani ya nyumba yake, Ikabidi watu wakimbie wakalala nje.

Asubuhi taarifa zikaja watu wanaopita kule makaburini hasa wanakijiji wakadai wanamuona marehemu kakaa juu ya kaburi, baadhi ya ndugu wakaona waende kujionea kweli wakaenda ajabu wakawa hawamuoni ila mtoto mdogo umri wa miaka kama 8/9 hizi ambaye waliongozana nae ndio akawa anamuona.

Siku hiyo hiyo wanaukoo wakakaa kikao watafanyaje na tayari marehemu alishazikwa sehemu tofauti na aliyoagiza na kufukua hawawezi, mwisho wakakubaliana kutafuta wazee wa mila wa pale kijijini wakaenda kufanya yao kaburini kwa marehemu yaani kama kumtuliza hivi ndio vituko kuishaa.
 
Tusidanganyane hapa. Hizi ni hadithi za Abunuasi tu. Eti jeneza linagoma kubebeka??

Acheni hekaya zenu za vijiweni na imani potofu zilizojaa udanganyifu. Hizi porojo hazina ukweli wowote. Mtu akifa, amekufa. Hana uwezo wa kufanya chochote kwa walio hai.
 
Back
Top Bottom