Nimeanza safari ya ufugaji Sungura mwaka jana (2024) mwezi wa kumi, namshukuru Mungu, nimeanza kuona maendeleo taratibu, hatua kwa hatua

Nimeanza safari ya ufugaji Sungura mwaka jana (2024) mwezi wa kumi, namshukuru Mungu, nimeanza kuona maendeleo taratibu, hatua kwa hatua

Calonga

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2010
Posts
246
Reaction score
537
Baada ya kukaa muda mrefu bila kujihusisha na ufugaji wa aina yoyote, kuacha mbwa mmoja ambae namfuga kwaajili ya ulinzi, mwaka jana, 2024 mwezi wa kumi mwanzoni, niliamua kuanza ufugaji wa Sungura kwaajili kupata mboga kwa matumizi ya nyumbani na pale patakapokuwa na Sungura wa ziada, basi nitawauza niingize kipato kwaajili ya kuendeleza zaidi ufugaji huo.

Katika thread hii ntajitahidi kutoa taarifa kwa kadri ya uwezi wangu, kadri mradi huo utakavyokua ukiendelea, ninakaribisha maoni, ushauri, na maswali. Namuomba Mwenyezi Mungu aniongoze katika hili jambo.🙏🏿

baada ya kufanya utafiti kidogo, kukusanya taarifa na kuandaa fungu la pesa kwaajili ya mradi huo, niliamua kuanza ujenzi wa kibanda cha kufugia chenye vyumba viwili. Niliamua kujenga banda kwa kutumia vifaa vya chuma, na nyavu za chuma. (nita weka picha baadae kidogo)

Nilitafuta fundi, akafanya kazi hiyo vizuri sana, namshukuru Mungu, banda likaisha salama kabisa. Baada ya kujenga banda, nikatengeneza viboksi vya kuzalia (nesting boxes) viwili, kwaajili ya kila chumba (cages) hapo banda likawa limekamilika. Kazi yote ya kujenga banda pamoja na kutengeneza nesting boxes ilichukua wiki moja. Baada ya hapo, nikapumzika kwanza.

Itaendelea.....

Updates zote ziko kwenye posts zilizofwata huko mbele kwenye huu uzi
 
FB_IMG_1736279750753.jpg
FB_IMG_1736279746535.jpg
FB_IMG_1736279742127.jpg
 
We kijana nyama ya sungura ya kuku ikasome, sungura ni mtamu kishenzi.
Mkuu sio kweli labda upenzi/ushabiki tu ya kuku ni tamu sana. tumewawinda sana machungani na kula sana nyama zao mwaka 2006 nikafuga kienyeji wakatoroka wote walikuwa 4. mmoja akawa anarudi yaani anapotea kama siku3 au wiki halafu usiku anarudi .

Sasa hivi sili sio kwamba wamenishinda yaani kuamua tu na kutokuvutiwa nayo tena
 
Sungura wamegoma kupigwa picha.?
KAZI ni kipimo cha UTU
 
Tupe muendelezo mkuu mimi nilianza mwaka juzi mwishoni pamoja na kuku ila niliamua kuachana na sungura na kufocus na kuku pekee
Poa mkuu, naongeza updates taratibu kutokana na wingi wa majukumu. ila tutafika tu.👍🏿
 
Mods, naomba msaada nime update hii thread lakini naona bado iko vile vile, nifanyeje?
 
Baada ya kukaa muda mrefu bila kujihusisha na ufugaji wa aina yoyote, kuacha mmbwa mmoja ambae namfuga kwaajili ya ulinzi, mwaka jana, 2024 mwezi wa kumi mwanzoni, niliamua kuanza ufugaji wa Sungura kwaajili kupata mboga kwa matumizi ya nyumbani na pale patakapokuwa na Sungura wa ziada, basi nitawauza niingize kipato kwaajili ya kuendeleza zaidi ufugaji huo.

Katika thread hii ntajitahidi kutoa taarifa kwa kadri ya uwezi wangu, kadri mradi huo utakavyokua ukiendelea, ninakaribisha maoni, ushauri, na maswali. Namuomba Mwenyezi Mungu aniongoze katika hili jambo.🙏🏿

baada ya kufanya utafiti kidogo, kukusanya taarifa na kuandaa fungu la pesa kwaajili ya mradi huo, niliamua kuanza ujenzi wa kibanda cha kufugia chenye vyumba viwili. Niliamua kujenga banda kwa kutumia vifaa vya chuma, na nyavu za chuma. (nita weka picha baadae kidogo)

Nilitafuta fundi, akafanya kazi hiyo vizuri sana, namshukuru Mungu, banda likaisha salama kabisa. Baada ya kujenga banda, nikatengeneza viboksi vya kuzalia (nesting boxes) viwili, kwaajili ya kila chumba (cages) hapo banda likawa limekamilika. Kazi yote ya kujenga banda pamoja na kutengeneza nesting boxes ilichukua wiki moja. Baada ya hapo, nikapumzika kwanza.

Itaendelea.....
Baada ya kumaliza kujenga banda nikaanza kutafuta mbegu. Kwasababu ya ufinyu wa bajeti, nikaamua kuanza na sungura wachache. Nilianza na New zealand white wawili, mmoja dume.na mmoja jike, pamoja na flemish jike mmoja.

Chakula wanachokula mpaka sasa ni majani, matembele, mchunga, kabech na karoti. Pia mara moja moja nawapa na rabbit pellets ambazo zinauzwa kwenye maduka ya vyakula vya mifugo. Mwanzo nilimuweka dume wa newzealand white pamoja na jike wa newzealand white ili wapandane. Nikawaacha wakae pamoja kwa wiki mbili, baada ya hapo nilamtoa yule dume, na kumuamishia kwa jike la flemish, na huko akakaa kwa wiki mbili. Hapo nikashinda kumhamisha kwasababu banda lenyewe lina cages mbili tu. Nikagundua nimechemka 😀 nikaona inabidi niwe na vyumba zaidi ya viwili.

Nikamwita fundi, tuka design jinsi ya kugawa lile banda ili tupate vyumba zaidi. Tukafanikiwa tukapata vyumba (cages) vinne. Hapo sasa nikaweza kumhamisha dume na kumweka kwenye chumba cha peke yake.

Baada ya mwezi mmoja na siku kama nne hivi tokea lile jike la new zealand white amalize dozi yake ya kupandwa, akazaa vitoto vitano, vizuri vyenye afya. Mpaka sasa vimeanza kuacha kunyonya na kuanza kula vyakula vya sungura wakubwa. Sasa kimeo kikawa kwa huyu jike aina ya flemish.


Itaendelea....
 
Back
Top Bottom