Nimefuta Biblia kwenye simu yangu

Nimefuta Biblia kwenye simu yangu

Mambo yote chombo kipigwe dhoruba ndipo Dua na Sala husomwa kwa sauti.
 
Kwani unafikiri majina yanakuwa ya nini sasa?

Dah, usiku mwema aisee!
Kwamba Roman Empire ndio kale ka Vatican ndani ya Italia? Hivi unaijua Roman Empire wewe?
Kalale tu sasa. Naona hizi pumba sasa. Yaani daah!
Hatujadili Roman empire bible imeandikwa na nan?
Acha ku-diverge mada.
 
Scars kwa uelewa wako Mungu maanake nini?
as my personal opinion Mungu ni dhana ya kizamani sana ya kujaribu kuelezea ulimwengu na kutatua maswali mgumu dhana hiyo iliyopewa sifa kubwa za kurahisisha mambo kama muweza wa yote, kua anauwezo wa kufanya vitu ambavyo huvielewi
 
View attachment 2099557
Sasa nimeamini kuwa dini ni kwaajili ya maskini na waoga tu.

Mpaka leo hakuna mwanadamu au kitu chochote ikiwemo Mungu alitethibitisha kuwa Mungu yupo.

Kila mtu atakuthibitishia kwa maandiko ambayo yameandikwa kwa mkono wa mtu.

Ukiondoa maandiko hakuna mtu wa dini kukuthibitishia uwepo halisi wa Mungu.

Waislamu kwa kitabu chao watakuthibutishia uwepo wake, Wahindu, Wabudha, Waktisto n.k watakuthibutishia uwepo wa Mungu kwa maandiko na hadithi tu ila hawataweza kukuthibitishia kwa njia nyingine ya reality.

Kwa taabu wanazopata watu duniani ni kama nature ndio inatawala.

Haiwezekani Mungu ambaye wanasema aliupenda ulimwengu aruhusu vita, ubakaji, kuchinjana, kudhulumiana, ufukara, njaa n.k huku hivyo vitu ni vidogo kwake angevikomesha ndani ya sekunde.

Je, Mungu kazidiwa utu na upendo na mwanadamu?

Hii amani na hali ya maendeleo tunayoiona ni fikra na utu wa binadamu kwa ulimwengu.

Binadamu anaunda mabaraza ya kitaifa kupambana na majanga mbalimbali, pasipo na haya mabaraza Dunia isingekalika kabisa kwa idadi hii ya watu ilivyo kwa sasa.

Illusion ndizo zinatawala watu ndio maana kila dini na dhehebu wanajiona kuwa wako sahihi na wana ushahidi kuwa dhehebu lao ndilo sahihi mbele za Mungu na wao tu ndio wataingia mbinguni au peponi.
View attachment 2099556
Ee Bwana mtokee huyu mtu hata kwa nusu sekunde inatosha ili athibitishe unaishi!
 
Tunachohitaji is the cause of every cause.
Mungu ametuumba kama ni hivyo yeye ameumbwa na nani?
Na kama hajaumbwa kwa nini sisi iwe lazima tumeumbwa!?
Kwani kuna mtu kasema Mungu kaumbwa? Maana huyo alitesema hivyo atakuwa na jibu la nani aliyemuumba huyo mungu.
 
Ukitaka kuthibitishiwa uwepo wa Mungu kwakutumia vitabu vya dini utakua hutumii maarifa uliyopewa na Mungu sawasawa.Kwasababu dini zilikuja badae kumuelezea.Unatakiwa ujithibitishie mwenyewe uwepo wa Mungu kwakujiuliza mwenyewe.Maana sidhani kama uwepo wa Mungu ni hadi uambiwe na watu wengine.Binadamu wenzetu walioendelea walishaacha kujiuliza hilo swali zamani sana wakaamua kutumia maarifa waliyopewa kurahisisha maisha.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
as my personal opinion Mungu ni dhana ya kizamani sana ya kujaribu kuelezea ulimwengu na kutatua maswali mgumu dhana hiyo iliyopewa sifa kubwa za kurahisisha mambo kama muweza wa yote, kua anauwezo wa kufanya vitu ambavyo huvielewi
Miungu yote iliyopo inaangukia kwenye maana hiyo ya Mungu uliyoeleza? Maana miungu mingi ya kila aina.
 
Miungu yote iliyopo inaangukia kwenye maana hiyo ya Mungu uliyoeleza? Maana miungu mingi ya kila aina.
Kwanza nimejibu kulingana na aliyeuliza, sijafunganishwa kwamba niwe specific kwa mungu aina gani

Na vile vile nimesema ni maoni binafsi
 
Ukitaka kuthibitishiwa uwepo wa Mungu kwakutumia vitabu vya dini utakua hutumii maarifa uliyopewa na Mungu sawasawa.Kwasababu dini zilikuja badae kumuelezea.Unatakiwa ujithibitishie mwenyewe uwepo wa Mungu kwakujiuliza mwenyewe.Maana sidhani kama uwepo wa Mungu ni hadi uambiwe na watu wengine.Binadamu wenzetu walioendelea walishaacha kujiuliza hilo swali zamani sana wakaamua kutumia maarifa waliyopewa kurahisisha maisha.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Kama ukitaka kuwa daktari lazima uende kusoma ili upate huo ujuzi huwezi kukaa tu ukatafakari mwenyewe na ukapata ujuzi wa kuwa daktari, sasa najiuliza kila mtu akikaa na kutafakari kivyake kuhusu mungu si kila mtu atakuja na maelezo tofauti na mwenzake kuhusu huyo Mungu? Maana hatufanani mawazo.
 
Kwanza nimejibu kulingana na aliyeuliza, sijafunganishwa kwamba niwe specific kwa mungu aina gani

Na vile vile nimesema ni maoni binafsi
Sijasema uwe specific kwa aina yeyote ya mungu, jamaa kauliza maana ya hili neno Mungu na wewe ukaeleza kwa unavyoelewa na ndio mimi nikauliza kuwa miungu yote inaangukia kwenye hiyo maana uliyoeleza au ni baadhi tu?
 
Sijasema uwe specific kwa aina yeyote ya mungu, jamaa kauliza maana ya hili neno Mungu na wewe ukaeleza kwa unavyoelewa na ndio mimi nikauliza kuwa miungu yote inaangukia kwenye hiyo maana uliyoeleza au ni baadhi tu?
miungu yote ipi na ipi?

kuna miungu ipo na haijihuishi na dhana ya uumbaji

Mi nimejibu kwa muktadha wa abrahmic religions ambayo 99.09% waumini wake wapo humu
 
Hilo swali nitalijibu kwa swali.
Huyo Mungu aliumbwa na nani?
Au wazo la kujiumba alipewa na nani?
Siyo kila swali linajibiwa kwa swali mpaka likidhi vigezo. Ndiyo maana umekosea kwenye kujibu.

Ili uone kwamba jibu lako kwa mtindo wa swali ni uongo,naomba unipe sababu za Muumba yaani Mola awe ameumbwa ? Kinyume chake humjui unaye mjadili, na huu ujinga nauona sana humu jf.
 
miungu yote ipi na ipi?

kuna miungu ipo na haijihuishi na dhana ya uumbaji

Mi nimejibu kwa muktadha wa abrahmic religions ambayo 99.09% waumini wake wapo humu
Hapo sasa ndio umeweka sawa kwamba ulikuwa unazungumzia Abrahmic religions.
 
Siyo kila swali linajibiwa kwa swali mpaka likidhi vigezo. Ndiyo maana umekosea kwenye kujibu.

Ili uone kwamba jibu lako kwa mtindo wa swali ni uongo,naomba unipe sababu za Muumba yaani Mola awe ameumbwa ? Kinyume chake humjui unaye mjadili, na huu ujinga nauona sana humu jf.
Sababu zilizokufanya utafute vyanzo vya vitu vingine mpaka ukafikia jibu la mungu, ndio sababu hizo zinazo kulazimu utafute kujua nini chanzo cha mungu

Kama uliweza kufikiria mungu hana chanzo manake uligundua chanzo di muhimu ili kilichopo kiwepo, kwa maana hiyo wewe ndio unapaswa kua mtu wa kwanza kabisa kumkubalia mtu anayesema kitu fulani kipo na hakina chanzo
 
Sababu zilizokufanya utafute vyanzo vya vitu vingine mpaka ukafikia jibu la mungu, ndio sababu hizo zinazo kulazimu utafute kujua nini chanzo cha mungu
Huu utoto mwingine ambao umeonyesha wazi ya kuwa umeshindwa kutofautisha kati ya matawi na msingi. Hapa naongelea msingi, sasa usilinganishe na tawi.
 
Sababu zilizokufanya utafute vyanzo vya vitu vingine mpaka ukafikia jibu la mungu, ndio sababu hizo zinazo kulazimu utafute kujua nini chanzo cha mungu
Naomba unitajie hizo sababu.
 
Kama uliweza kufikiria mungu hana chanzo manake uligundua chanzo di muhimu ili kilichopo kiwepo, kwa maana hiyo wewe ndio unapaswa kua mtu wa kwanza kabisa kumkubalia mtu anayesema kitu fulani kipo na hakina chanzo
Hakuna sehemu niliyofikiria bali nina uhakika,kijana inakuwaje unajenga hoja kwa dhana ?

Sharti la kwanza ni elimu na maarifa,huwezi kujisemea tu huku huna maarifa ya jambi husika, huu ni uhayawani.

Swali langu liko pale pale, nipeni sababu zinazo wafanya muhoji ya kuwa Mola ameumbwa na nani ?
 
Huu utoto mwingine ambao umeonyesha wazi ya kuwa umeshindwa kutofautisha kati ya matawi na msingi. Hapa naongelea msingi, sasa usilinganishe na tawi.
Unajuaje kwamba unachokiita wewe kua ni msingi, sio msingi potofu?
 
Back
Top Bottom