Nimegundua ndugu yangu wa damu ni mshirikina

Nimegundua ndugu yangu wa damu ni mshirikina

Kwani mama, bibi hawawezi kuwa wachawi kukuroga?
Ndio mwanzo wa kuvunjika kwa familia. Mzazi akulee ufike miaka 30 aje akuroge ufe kwanini hakukuua tangu ukiwa mdogo?
 
Natamani kumwambia aisee ila naogopaaa kuna mtu kaniambia mchawi hakubali hata siku moja kuitwa mchawi yan vita yake sio ndogo…sasa najiangalia na hali yangu sasa sielewi
Kama una watu wengine ambao utakuwa nao mchane mchana kweupe, na hawezi kukubali na anaweza kulia sana nakusikitika mno, utasikia nakuhangaikia hivi leo unaniambia hivi? Wewe mwite YESU tu hakuna linalomshinda
 
Yan kanitia nuksi sasa yeye hana maisha yoyote mimi ndio naisaidia familia nzima.. mpaka pesa ya kula mimi ndio nampa. Nimechoka kisa ni kirefu na kinasikitisha napitia magumu sana
Pole sana
 
Nunua panga jipya linoe mbele na nyuma,kula bangi msokoto mmoja Kisha mfate mwambie habari zako zote na ubaya wote unaonifanyia Nisha jua Sasa ama zangu ama zako
Rudi kunishukuru
 
Wewe dini gani? Maana dini yenu itaamua kati yenu, mfano ingekuwa miye ningefanya Alhbadir mchana kweupe. Kati yetu anayemtafuta mwenzio atangulie huko. Haya mambo ni siri ya mtu na nafsi yake huwezi jua mpk likupate ndiyo utajua km wa karibu yako ndiyo mmbaya.
 
Habari zenu.
Nina jambo ambalo linanitatiza jamani. Mimi ni mkazi wa dar na asili yangu ni mkoa fulani ukanda wa pwani. Nimetokea kwenye familia za kiswahili, baadhi wamenielewa familia za namna gani.
Naomba niende straight to the point…ni hivi nimegundua ndugu yangu wa damu ni mshirikina yan mchawi au mwanga. Mimi nilikuwa naandamwa na mitihani mingi ya kiswahili magonjwa ya ajabu, vifungo yan kila aina ya nuksi imeniandama. Sasa huyu ndugu yangu alikuwa mstari wa mbele kunipeleka kwa waganga kutafuta suluhu. Na huko tulikuwa tunaambia watu fulani wananifanyia hivi. Sasa kumbe huyu mtu na yeye ni mshirika mkuuu na ila alikuwa ananizunguka kwa hao waganga.
Kisa ni kirefu sana na kuhusu kujihakikishia hili jambo nimejihakikisha kabisa mpaka nimefika kuandika hapa., ila sasa baada ya kugundua nimepata uoga sana maana ni ndugu wa damu na tunaishi nyumba moja. Nahofia maisha yangu sina amani, na hapa nilipo nimepigwa kombora mwili wote unauma yan nimekuwa kama mzee hata kutembea kwa dakika 10 siwezi.
Naomba mnisaidie ushauri japo kwa ufupi.

Wale wa matusi na kejeli naomba mnihurumie mpite kimya kimya
Bwege wewe ulikuwa hujui kuwa hata wazazi wenu ni vigagula!
 
Back
Top Bottom