Nimegundua ni hatari kuhifadhi pesa benki ukiwa unafanya biashara Tanzania

Nimegundua ni hatari kuhifadhi pesa benki ukiwa unafanya biashara Tanzania

As long as unafanya biashara pasipo kona kona sasa wasiwasi wa nini...Kwa kati ya hao umesikia Bakhresa,Mo Dewji, au hata wamiliki wa biashara za mashule na hotels wanalalamika kuzuiliwa pesa zao bank..Hao wanaolalamika ni wapumbavu kwenye industry business na ni watakatishaji wa pesa haramu, Hakika huwezi kuwa Mfanyabiashara mzuri katika nchi yako na mlipaji wa kodi kwa wakati halafu ukasumbuliwa na mambo kama hayo, Mara nyingi huwa serikali yako itakulinda kwa hali yeyote ile kwani tayari umeshakua ni faida kwao...Achana na wapumbavu wachache wasikufanye ukapoteza ufikiri wako kwa upuuzi wao..
Sina ushahidi wa hili lakini nadhani lina ukweli asilimia 99. Kama mambo yako yako straight hata kama hao jamaa wanataka kukuonea watakosa pa kuanzia. Mtu hata akikutafuta kisa huwa anaangalia penye weakness ndipo anapokuzolea. So am sure hao jamaa kuna jinsi mapato yao hawaeleweki kabisa. Ila huwa hakuna mkosaji anayekubali kosa😀😀
 
Huu uhuni unapaswa kukemewa vikali mno, kinachosikitisha wanafunga Hadi account zisizohusika na biashara husika.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huu ndio ulikuwa wakati wa kupaza sauti kwa umoja wetu. Tatizo tuaangalia vitu kichama sana. Tazama Diamond wengine walivyotekwa na Makonda yeye akaimba kukaa kimya. Leo yamemfika
Kufunga account ni upuuzi
 
Nunua assets kama ardhi n.k au nenda kahifadhi uswisi kama wanasiasa wanavyofanya.
Hizo ardhi zenyewe hukawii kuambiwa ni hifadhi ya barabara au kumepita bomba la kinyesi hivyo ni mali ya serikali.

Huko Uswiss rate ya kumaintain account ukute ndio akiba yako yote ya maisha.

Kwa kifupi ni kumuomba Mungu yasikukute tu maana nchi hii kila mtu analia kivyake. Maskini analia kwa ugumu wa maisha na tajiri analia kwa kutaka kufilisiwa na serikali.

Nahisi kipaumbele cha serikali hii japo hawajakiweka wazi ni kuwa kila mwananchi awe fukara. Utajiri uwe wa wachache tu waliojichagua.
 
Wafanyabiashara wengi, wakubwa, wa kati kwa wadogo huu mwisho wa mwaka wamekutwa na dhahama la kusikitisha na kuhuzunisha, wamefungiwa account binafsi za benki na zile za biashara na mamlaka moja yenye nguvu.

Kwenye mazingira kama haya ambapo unaporwa hela zako zote, kuna haja gani ya kuweka pesa benki?

Waswahili wanasema tunajifunza kutokana na makosa. Makosa ya walioporwa pesa zao zilizopo benki tanatufundisha nini?

Weka pesa bank, at your own risk
Ahsante kuanzia sasa naweka fedha zangu zote kwenye kibubu.

Hao TRA wakachukue fedha za Baba zao waliowaajiri.
 
Hapo dawa ni kuwa na akaunti nyingine ambayo haijulikani kwenye biashara zako na wala haina jina lako
 
Wafanyabiashara wengi, wakubwa, wa kati kwa wadogo huu mwisho wa mwaka wamekutwa na dhahama la kusikitisha na kuhuzunisha, wamefungiwa account binafsi za benki na zile za biashara na mamlaka moja yenye nguvu.

Kwenye mazingira kama haya ambapo unaporwa hela zako zote, kuna haja gani ya kuweka pesa benki?

Waswahili wanasema tunajifunza kutokana na makosa. Makosa ya walioporwa pesa zao zilizopo benki tanatufundisha nini?

Weka pesa bank, at your own risk
Sio kwa wafanyabiashara tu, hata kwa wafanyakazi na waajiriwa, ukizinguana na mwajiri wako tu boss anakwenda ku bloki akaunti yako. Hatari!!!
 
Ni ujinga tu wa tz umewajaa kuanzia wa ngazi ya chini Hadi ya juu.
Tax system ni mbovu na Ina mianya mingi,,Sheria nyingi ni mbovu,,watu wanatamaa na uchu tu wa kupora Mali za watu.
Kama una pesa mingi fanya kama wafanyavyo wahindi na wachina nenda kawekeze nje ya nchi kule Kunako usalama.
Ndiyo maana nchi haiendelei. Mtu kuwekeza nje ya nchi na serikali wala haina habari na wewe ni hatari
 
As long as unafanya biashara pasipo kona kona sasa wasiwasi wa nini...Kwa kati ya hao umesikia Bakhresa,Mo Dewji, au hata wamiliki wa biashara za mashule na hotels wanalalamika kuzuiliwa pesa zao bank..Hao wanaolalamika ni wapumbavu kwenye industry business na ni watakatishaji wa pesa haramu, Hakika huwezi kuwa Mfanyabiashara mzuri katika nchi yako na mlipaji wa kodi kwa wakati halafu ukasumbuliwa na mambo kama hayo, Mara nyingi huwa serikali yako itakulinda kwa hali yeyote ile kwani tayari umeshakua ni faida kwao...Achana na wapumbavu wachache wasikufanye ukapoteza ufikiri wako kwa upuuzi wao..
Pointtless kabisa!
Kama kuna changamoto ya kodi, mteja aitwe ahojiwe, ikishindikana mahakama ya kodi ipo. Siyo mtu mmoja anaamua kublock account yako!
Sasa nimeelewa kwa nini waarabu hawapeleki pesa Bank
 
Ila tuongee ukweli, walichofanya kitaligharimu sana taifa, maana watu wataanza kuondoaha pesa zao bank kwa kasi, na wengine watazihamishia nje ya mchi pesa zao, tena baada ya kuzibadilisha kuwa dollar, madharavyake ni kama yafuatayo

1.) Benki nyingi kufa

2. Mzunguko wa pesa kupungua mtaani

3.) Pesa yetu kushuka thamani

4.) Ajira na uwekezaji kupungua

5.) Mdororo wa uchumi
 
Hela inatakiwa izungushwe sio ichimbiwe Uswiss
Rule number one katika uwekezaji, Never lose money, yaani hutakiwi kupoteza pesa. Ni Mara Mia uichimbie sehemu salama kuliko kuiacha, iliwe na binadamu
 
Back
Top Bottom