Nimekuwa na mahusiano na mume wa mtu kwa miaka 3 nahitaji kuachana naye, nimuachaje bila yeye kuweka kinyongo

Nimekuwa na mahusiano na mume wa mtu kwa miaka 3 nahitaji kuachana naye, nimuachaje bila yeye kuweka kinyongo

Wanawake hivi kwenye maisha huwa mnataka vitu gani hasa???
Mimi ninayemuona mpumbavu ni huyo mzee, huwezi kufanya heavy investment namna hiyo kwa mchepuko, bora hata angekuwa amezaa naye hapo Sawa mtoto wake angenufaika in future. Na unaweza kukuta mkewe wa ndoa hajampa zawadi ya nyumba na Gari kwa Jina lake.. Sasa subiri huyo mchepuko aolewe unaweza kusikia mzee kapata stroke au mzee kaua akaishia jela au mzee kauwawa na huyo Kijana wa mpya wa mchepuko.
 
Baada ya kujengewa nyumba,kununuliwa gari na kutafutiwa kazi.Sasa una kila kitu saivi ndo unaona anakubana.

Dada kama unataka kutoka clean kwenye hayo mahusiano

Atleast usinyongwe na ubaki na uwahi wako

Mambo mawili hayakwepeki
1.kurudisha nyumba ya watu
2.kurudisha gari ya watu

Sasa swali langu ni upo tyr kuachiwa nini na nini alichokupa ili uwe huru na maisha yako.Ukiweza kujibu hilo then nitajua nianzie wapi kukushauri

Otherwise wewe ni limbukeni mwingine uliyeinuliwa kimaisha na kuanza kuona aliyekuinua ni mjinga na hilo litaku cost sababu mtu unaye deal nae kwa jinsi navyomuona ni wale type za kupenda sana na hao ndo kutoa roho ya mtu ni sekunde tu

Be careful mbwa wewe
 
This is amaizing hela tamu, unaitwa mama mwenye mjengo, gari na kazi...ila sasa vyote hivyo vimewekwa na kiegemeo cha mtu, akitoa mguu unaogopa kuanguka.

Fanya yafuatayo:

1. Wekeza hela kuanzia sasa hadi miez 6 ikibid kopa hapo kazini ziwe nyingi zaidi.

2. Uza hiyo gari ikiisha hiyo miezi 6

3. Kwa vile nyumba yako ina hati na jina lako uza kimia kimia

4. Uza viwanja kimia kimia.


Ule mwezi wa mwisho uza vitu vyako vya ndani vyoote.

Hakikisha unabadili kila kitu kuwa hela, na hizo hela weka account, usiweke account moja anaweza kufanyia ujinga, ikibidi kama una ndugu yako ana account hatumii muazime utunzie hela.


Kisha ukiona kila kitu kiko kwenye mahala pake yani huna kitu cha kukushikilia amka safarini nenda tafuta Mkoa kaa utulie udifanye chochote, zima simu badili laini chonga mpya.

Atapata hasira ndani ya mwezi mmoja wa pili zilisha isha anarudi kutulizana kwa mkewe, na litakuwa libido linatia mkewe hadi mkewe atakuwa ananjiuliza kulikon natiwa hivi siku hizi.

Ukikosa mkoa njoo nikuelekeze nilipo ukae wakat unajiandaa upepo upite utumie hizo hela ulizokusanya kufanyia baishara zako na kuishi maisha ya uhuru.

Nipe like basiiiiii[emoji3]
Akiamua kumloga jee?
 
nenda kamshitaki kwa mke wake na umwambie yote haya. ukimaliza hapo mwombe msamaha mwanamke mwenzio, na ukatubu kwa Mungu ili uanze maisha mapya. hayo aliyokutendea ni makaratasi tu, ni upepo tu, na umekufanya ukatengana na Mungu wako, hapo ulipo unaelekea jehanamu ya moto wa milele. furahia mali zinazotoka kwa Mungu sio hizo zinatoka kwa shetani. our God is a lifter of men, he can lift you hata zaidi ya huyo mume wa mtu.

nakuhakikishia kama ameshakugharimiia sana, hauwezi kumwacha kirahisi. dawa yake ni na wewe kuingia kwenye moto/mdomo wa simba, tafuta hata mtu fulani tu akamtonye mkewe kwamba mume wako anakufuatilia, akija kwako mwambie ni kweli ananifuatafuata, waachie msala huo uone kama hamtaachana. dawa ya moto ni moto.
Kwa ninavyojua mkewe atataka arudishe vitu vyote hasa nyumba na gari.
 
Habari wanajamii forum, ni matumaini yangu kuwa mko salama. Ama la, basi Mungu awafanyie wepesi.

Ndugu zangu nahitaji msaada wa mawazo yenu sana. Ninapitia sijui niseme ni wakati mgumu au ni ujinga wa kujitakia. Niko kwenye mahusiano na mume wa mtu sasa yapata miaka mitatu. Imefikia hatua nimechoka na nahitaji kujing’atua ila nakosa njia nzuri ya kuachana nae. Am not even proud with what i did so if you judge me i’ll understand.

Huyu mtu tangu nafahamiana nae ameyabadilisha sana maisha yangu maana ana mchango mkubwa sana. Alinisaidia kupata kazi nzuri na kuachana na kakazi kangu nilikokuwa nafanya, alinihamisha na kunipangishia sehemu nzuri zaidi. Baadae alininunulia gari nami nikawa natembea nimekaa, pia amenijengea nyumba iliyo kwa jina langu ila kwakuwa ipo nje ya mji nimeipangisha nakula kodi ila bado analipia kodi hapa ninapoishi.

Mahusiano yalipoanza sikufikiria hata yangechukua miezi 6, ila sasa ni miaka mitatu+. Ni mwanaume anayejali sana ila ana wivu balaa. Ni mara kadhaa amekuwa akinitishia kuwa akigundua ninamsaliti atanikata shingo. Sasa huwa najiuliza huyu ni mume wa mtu, anatarajia kweli niwe na yeye tu ili iweje?

Sasa nimechoka jamani, natamani niwe na mpenzi wangu na sio mume wa mtu. Kuna huyu kijana nimeanza nae mahusiano sasa ni miezi 5, kusema kweli nampenda na ninaona kabisa nae ananipenda. Haya ndio aina ya mahusiano niyatakayo. Nimekuwa nikitafuta visingizio kuwa asije kwangu maana sio maadili ila ukweli ni kuwa naogopa mlipa kodi akijua atanitoa roho.

Huyu mume wa mtu nishamtafutia visingizio ili tuachane ila inashindikana. Natamani yeye ndio aanze ili asije kuwa na kinyongo. Ila kuna wakati najipa moyo kuwa nimwambie tu tuachane lakini nikikumbuka aliwahi kunikunja nusura anipige alipokuta msg asizozielewa kwenye simu nahisi kutetemeka. Aliwahi kunionyesha silaha anayomiliki, nilipomuuliza ni ya nini akasema hata mimi nikimletea ujinga ananifyatua. Japo ulikuwa utani ila niliogopa kusema kweli.

Balaa zaidi recently ameanza kung’ang’ania nimzalie. Nimekuwa nikijifanya mimba hazishiki ila kusema kweli natumia dawa zisishike maana siko tayari kuzaa nae. Kwanza nahisi kama suffocation maana ananibana sana. Kwangu anakuja tu muda wowote akijisikia, na ole wangu asinikute nyumbani ni tatizo kubwa. Kila ninachofanya anahitaji apate taarifa kwanza, yaani kama mkewe vile jamani.

Nimejaribu kuelezea haya ili angalau muelewe ni kwanini nahitaji msaada wa mawazo yenu ili nijikwamue kwenye hili shimo nililojichimbia. Nipeni ushauri naachanaje na huyu mwanaume bila kuleta madhara kwangu.
Chagua moja kati ya haya:
1) Mwambie umepima ukakutwa +ve, hapo nae atataka akapime na akikutwa - ve anakuacha kiroho safi.
2) Mlengeshe kwa shosti yako ambae unaona anam feel.
Hata mdogo wako wee mwachie tuu aruke nae maana tayari ni mbwai acha iwe mbwai.. Ili upate sababu ya kuachana nae
3) Rudisha nyumba, gari, fenitures, hama unapoishi, acha hiyo kazi aliyokutafutia na uvunje mahusiano
Na ukaanze maisha mapya (uhamie) kwa huyo mumeo mtarajiwa.
4) mweleze kuwa unahitaji kuolewa ila atabakia kuwa mchepuko wa kudumu
 
Pole sana binti kutoka kwenye mahusiano ya hivyo ni ngumu,maana hakuna mjinga atayewekeza vitu vyote hivyo alafu akubali kukuacha,yaani wewe kwake ni mchepuko wa kudumu,
Labda kwakujaribu ni kuamua kumrudishia kila kilicho chake,na mbaya zaidi huwezi kukubali kurudisha mali zake urudi zero

N.B wadada mwisho wa kudanga ni 27 years udangaji wenyewe ni udange kwa akili yaani unapata hela huko unaweka assets zako kimtindo wako lakini kama mwanaume anakujengea,anakununulia gari na vitu vingine usidhani ni rahisi kukuacha salama we sio binti yake et anakujengea afu badae ukaolewe na mwanaume mwingine
Danga ukijua badae nawe unataka kuwa na familia yako,sasa hapo ni akili kumkichwa
 
Kama unaweza tafuta no ya uyo mke wake alafu umtumie pics zenu( wewe pamoja na mmewe) kwa kutumia new no afu usikilizie [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Mmh huu ushaur hapana
 
Kwa ninavyojua mkewe atataka arudishe vitu vyote hasa nyumba na gari.
ndio unatakiwa urudishe viende kwa mwenye navyo, hapo wewe ni mwizi kama wezi wengine tu, na ni mwizi anayejua anachokifanya, na Mungu anakuona. kifupi ni kwamba ukifa leo hii moja kwa moja jehanum na hizo mali utaziacha. tafuta kutengeneza maisha ya baadaye haya mengine ya hapa ni ya kupita, shetani amekuwekea hook/ndoana ya wizi wa ndoa na mali za watu ili atakapokuvua hata usitarajie, mkaungane naye motoni. upo kwenye wimbi la hatari ya milele, stuka na gauka ghafla kabla wakati wako haujaisha hapa duniani.
 
Mimi pia na mke mdogo( enzi alikuwa mchepuko akisoma chuo nikampangia na kumpa gari na biashara alipomaliza chuo nikamjengea then et anataka aniache nilimfata mamake nikamwambia nitawaua ukoo mzima)
Wakat natoa hela mtoto anasoma na kuishi vzr dar why hawakumzuia sahiz ndo wanawaza aolewe? Never
Ilibid waongee nae vzr akakubali nikamuoa mke wa pili ndo kesi ikaisha


Mmnh hapo umelazimisha kupendwa!
 
Kwa nini usiolewe mke wa pili? Hivi unaujua uchungu wa kumchuna vyote hivyo halafu umuache? Hivi hujawahi kusikia matukio ya watu kuuana kwa sababu ya wivu wa kimapenzi? Fikiria kabla ya kutenda. Huo ndio ushauri wangu.


Hata kama hampendi? Je dini yake inaruhusu?

N.k.

Halafu mke original atakubaliana na uke wenza?

Akiamua kuondoka zake ?!
 
Habari wanajamii forum, ni matumaini yangu kuwa mko salama. Ama la, basi Mungu awafanyie wepesi.

Ndugu zangu nahitaji msaada wa mawazo yenu sana. Ninapitia sijui niseme ni wakati mgumu au ni ujinga wa kujitakia. Niko kwenye mahusiano na mume wa mtu sasa yapata miaka mitatu. Imefikia hatua nimechoka na nahitaji kujing’atua ila nakosa njia nzuri ya kuachana nae. Am not even proud with what i did so if you judge me i’ll understand.

Huyu mtu tangu nafahamiana nae ameyabadilisha sana maisha yangu maana ana mchango mkubwa sana. Alinisaidia kupata kazi nzuri na kuachana na kakazi kangu nilikokuwa nafanya, alinihamisha na kunipangishia sehemu nzuri zaidi. Baadae alininunulia gari nami nikawa natembea nimekaa, pia amenijengea nyumba iliyo kwa jina langu ila kwakuwa ipo nje ya mji nimeipangisha nakula kodi ila bado analipia kodi hapa ninapoishi.

Mahusiano yalipoanza sikufikiria hata yangechukua miezi 6, ila sasa ni miaka mitatu+. Ni mwanaume anayejali sana ila ana wivu balaa. Ni mara kadhaa amekuwa akinitishia kuwa akigundua ninamsaliti atanikata shingo. Sasa huwa najiuliza huyu ni mume wa mtu, anatarajia kweli niwe na yeye tu ili iweje?

Sasa nimechoka jamani, natamani niwe na mpenzi wangu na sio mume wa mtu. Kuna huyu kijana nimeanza nae mahusiano sasa ni miezi 5, kusema kweli nampenda na ninaona kabisa nae ananipenda. Haya ndio aina ya mahusiano niyatakayo. Nimekuwa nikitafuta visingizio kuwa asije kwangu maana sio maadili ila ukweli ni kuwa naogopa mlipa kodi akijua atanitoa roho.

Huyu mume wa mtu nishamtafutia visingizio ili tuachane ila inashindikana. Natamani yeye ndio aanze ili asije kuwa na kinyongo. Ila kuna wakati najipa moyo kuwa nimwambie tu tuachane lakini nikikumbuka aliwahi kunikunja nusura anipige alipokuta msg asizozielewa kwenye simu nahisi kutetemeka. Aliwahi kunionyesha silaha anayomiliki, nilipomuuliza ni ya nini akasema hata mimi nikimletea ujinga ananifyatua. Japo ulikuwa utani ila niliogopa kusema kweli.

Balaa zaidi recently ameanza kung’ang’ania nimzalie. Nimekuwa nikijifanya mimba hazishiki ila kusema kweli natumia dawa zisishike maana siko tayari kuzaa nae. Kwanza nahisi kama suffocation maana ananibana sana. Kwangu anakuja tu muda wowote akijisikia, na ole wangu asinikute nyumbani ni tatizo kubwa. Kila ninachofanya anahitaji apate taarifa kwanza, yaani kama mkewe vile jamani.

Nimejaribu kuelezea haya ili angalau muelewe ni kwanini nahitaji msaada wa mawazo yenu ili nijikwamue kwenye hili shimo nililojichimbia. Nipeni ushauri naachanaje na huyu mwanaume bila kuleta madhara kwangu.
Ushauri wangu kama kakufanyia yote hayo na ukaridhika mzalie mtoto/watoto najua unataka uwe na mwenza wako akuoe lakini unaweza ukamuacha na ukajikuta unaangukia Kwa Jamaa akakumega na asikuoe na hapo wanaokutaka wote wanaona Kwa vile unagari na maisha Fulani mazuri, nakushauri endelea nae mpe moyo wako wote kama ni kwenda kwenu akajitambulishe mwambie
 
Huyo ni mumeo,Huko unakotaka kwenda kunaonesha una wenge.Au unafikiri MUME maana yake ni nini?Hivi nyie wanawake mnatuonaje wanaume.KAZI,KODI,NYUMBA,GARI,PENZI na bado unawashwa.Naweka BET huyo Jamaa ukiachana naye unaweza ukadanda maisha yako yote.MARK this POST


Sasa kama moyoni hampendi na wala hisia naye hana afanyeje ?

Iwapo akiwa naye raha ya nafsi haipati afanyeje?
 
Ushauri wangu kama kakufanyia yote hayo na ukaridhika mzalie mtoto/watoto najua unataka uwe na mwenza wako akuoe lakini unaweza ukamuacha na ukajikuta unaangukia Kwa Jamaa akakumega na asikuoe na hapo wanaokutaka wote wanaona Kwa vile unagari na maisha Fulani mazuri, nakushauri endelea nae mpe moyo wako wote kama ni kwenda kwenu akajitambulishe mwambie

Kwetu tayari wanamfahamu ila hawajui kama ni mume wa mtu.
 
Ushauri wangu kama kakufanyia yote hayo na ukaridhika mzalie mtoto/watoto najua unataka uwe na mwenza wako akuoe lakini unaweza ukamuacha na ukajikuta unaangukia Kwa Jamaa akakumega na asikuoe na hapo wanaokutaka wote wanaona Kwa vile unagari na maisha Fulani mazuri, nakushauri endelea nae mpe moyo wako wote kama ni kwenda kwenu akajitambulishe mwambie


Awe single mother?

Aweke doa kwenye ndoa ya huyo jamaa ?
 
Awe single mother?

Aweke doa kwenye ndoa ya huyo jamaa ?
Kwani wakati anakula malinzake hakumjua kuwa ni mume wa mtu? Mwanaume awekeze Kwa mwanamke hafu baada ya kuwezeshwa ajifanye hamtaki kama ni mm sikuachi salama ni zarau sana Bora ungenikataa mapema kabisa au ungempa Condition Ili na mm asijitoe sana kumsaidia
 
Siku zote Kaa ukijua Kila jambo unalofanya ni mbegu. Liwe zuri au baya. Haya uliyoyafanya ni makosa na tayari umeshajua. Ni heri ukafanya jambo sahihi la kutoka kuliko kuendelea kuharibu ndoa ya mwenzako.

Mbegu nzuri huzaa sana. Tendo zuri Lina matunda na baya Lina matunda vile vile. Machozi anayolia mwanamke kama wewe sio mazuri yasije yakaja kukugharimisha.

Acha vyote Anza upya hutakufa. Vyote hivi ni ubatili. Ni heri chako Cha amani kuliko Cha wizi, dhulma(umemdhulumu mwenzio upendo wa mume wake)..and you knew it...the greens zikakuvuta. Just leave him Anza upya.
Usiendelee kuharibu..tengeneza maisha yako mapya.
 
Back
Top Bottom