Nimemgombeza askari wa usalama barabarani, wenzake wameniomba msamaha

Nimemgombeza askari wa usalama barabarani, wenzake wameniomba msamaha

Angekuwepo Magufuli lupango ilikuwa halali yako kwa kumugombeza askari kwa kuchukua hela ya kiwi.
 
Mkuu hiyo hela ni ya kubrush viatu! Ukisikia mishahara yao utaona huruma.
 
Ni kituo cha mabasi cha mawasiliano. Wako maaskari wengi lango wa kuingilia, kila gari linaloingia linasimamishwa na kuchukua hela kwa konda. Bahati nzuri nikashuhudia askari wa kike akipokea hela, nikamfuata na kumweleza nichokiona, akanijibu vibaya.

Nikatishia kuchukulia hatua zaidi lakini wenzake wa kiume wakaniomba msamaha. Hili jeshi limeoza kabisa.
Ungempiga picha akichukua rushwa
 
Mkuu ungemuacha tu, hao ni dagaa tu a mbao wanachukua 2000 na wengine 5000 ambazo haziwewi kiathiri sana.

Wanaotuumiza ni ma papa ambao wametajwa kwenye ripoti ya CAG kama vile upotevu wa trillioni moja ya tanrod, matumizi makubwa ya mama kwenda dubai na kulipa mabilioni ya pesa huku watz tunataabika na miundombinu mibovu nchi nzima.
Nchi imejaa majangili tupu
 
Ni kituo cha mabasi cha mawasiliano. Wako maaskari wengi lango wa kuingilia, kila gari linaloingia linasimamishwa na kuchukua hela kwa konda. Bahati nzuri nikashuhudia askari wa kike akipokea hela, nikamfuata na kumweleza nichokiona, akanijibu vibaya.

Nikatishia kuchukulia hatua zaidi lakini wenzake wa kiume wakaniomba msamaha. Hili jeshi limeoza kabisa.
Shukuru sana mkuu 'Gulwa', bahati yako nzuri hukuumizwa kwenye mkasa huo.

Nchi inaoza tukiiangalia kwa macho yetu sisi wenyewe!
 
Kuna siku nilikwenda kwenye ATM ya CRDB kutoa pesa nadhani ilikuwa siku ya Jumamosi, nilitoa pesa kwenye ATM mara 3, huo muda nilikuwa peke yangu kwenye kutoa pesa kwenye mashine ya ATM.

Sasa wakati nataka kutoka, ndani ya zilipo Mashine za ATM pembeni pana kijumba wnakaa Askari Polisi, walikuwa 2 wa kike na wa kiume.

Yule askari wa kiume ambaye alikuwa na silaha akaniita akaniomba pesa kwa ajili ya kupata chochote mchana, basi nikatoa 5,000 nikampatia akashukuru nikaondoka zangu.

Askari Polisi hawa wa kawaida na trafiki nawachukia sona, wakiniomba pesa ama lifti uwa siwapi.

Kabla ya hiyo siku nilishafikiriaga nikaweka mtazamo wangu kama ikitokes natoa pesa kwenye ATM alafu askari aliyepo akaniomba pesa sitoweza kukataa sababu ya kiusalama uwezi fahamu hiyo siku yuko katika hali gani, mtu anayo salaha anaweza akakufanya chochote.
 
Kwa asubuhi hii hiyo inaitwa ya chai, baadae mchana watatafuta ya lunch, na jioni watatafuta ya chakula cha usiku.

Mishahara yao wanajengea tu mijumba.
Mh mijumba wakati kuna jamaa ni jirani yangu kabla sijanunua kiwanja yeye alishajenga ila mpka leo nimehamia kitambo kidogo yeye kaweka wavu madirishani nikikaa nae anajisifu ana ng'ombe wengi kanda ya ziwa ila haishi kuniomba hela muda mwingine mkewe anamuomba wife hadi mafuta ya kula. Hela za rushwa zinalaana na mwamba yupo mataa ya veta pale anawapuna boda hela zao kama zote. Ila hana cha maana anachofanya zaidi ya kunywa pombe.
 
Bora wao wanaomba wanapewa kuliko wale wanaopiga mabilioni chini ya serikali ya samia. Huyo askari umemuonea tu.
Lah, inabidi kukubaliana nawe katika hili.

Kwa kweli ni bora kabisa kwa hao wanaoomba, kwa sababu unayo hiari ya kukataa, hata kama utanyimwa haki yako kwa kutotaka kushiriki kwenye hujuma hiyo.
Hawa walioko huko serikalini, hata hawatupi nafasi ya kuwakatalia wasizoe mali zetu!
 
acha tuwape we inakuuma nini, bora kutoa elf 2 kuliko fine ya elf 60, hamna daladala lililokamilika 100%, hiyo haiitwi rushwa hiyo mlishaambiwa ni yakubrashia viatu, huwezi kumpeleka popote boya wewe, hiyo chain ya mgao ni mkubwa kuliko kichwa chako kibovu
Sasa 2k kwa mwezi mzima si 60k na bado maisha yanakua hatarini kwa kuwa na gari mbovu barabarani. Inaeleweka rushwa sio leo wala kesho itaisha ila kuikemea ni jukumu letu.
 
Acheni kuyafanya maisha kuwa magumu kiasi hicho, sijaona haja ya wewe kubishana na huyo askari
Wewe na hao waliofurahia haya maneno yako ni polisi hao hao wabovu. Baada ya hapa mtakuwa mnaingia hata kwenye majumba ya watu na kuwapora mali zao, na bado utaona hakuna sababu ya kulalamikiwa majambazi nyie.
 
Mimi nimewagombeza Dstv na nimewaambia warudishe hela yangu niliyolipa.

Hovyo kabisa wanapandisha vifurushi na bei zao kandamizi sana wanyonyaji hawa
 
Ndio urefu wa kamba yake huo.
Si unasukia wengine wanajitwalia na T huko
 
Ni kituo cha mabasi cha mawasiliano. Wako maaskari wengi lango wa kuingilia, kila gari linaloingia linasimamishwa na kuchukua hela kwa konda. Bahati nzuri nikashuhudia askari wa kike akipokea hela, nikamfuata na kumweleza nichokiona, akanijibu vibaya.

Nikatishia kuchukulia hatua zaidi lakini wenzake wa kiume wakaniomba msamaha. Hili jeshi limeoza kabisa.
Vijana mna masifa kweli kweli mkipata vi cheo kidogo tu basi ,sasa ulimgombeza Askari alikuomba wewe hiyo rushwa?
 
Kama ni Kwa asubuhi hilo limezoeleka ukishatoa hiyo husumbuliwi Tena labda ufanye makosa ya mengine Kila daradara ndivo ilivyo
Na huo ni mradi wa watu,wenyewe wapo wametulia tuli
Hao askari barabarani wanatumwa tu

Ova
 
Back
Top Bottom