Nimempiga mke wangu milioni 2 kizembe sana

Nimempiga mke wangu milioni 2 kizembe sana

Imekukuta kama mimi, mimi namba ya siri ya mke wangu ya benki na SIM card zak zote nazijua vizuri tu, yeye hajui yangu ya benki ila za SIM zote anazo na wakati fulani huwa namtuma kutoa hela au kulipia vitu nikiwa busy.

Kuna siku sijui roho gani ilinituma kufungua app yake ya SIMBANKING nikaangalia salio nikakuta 8.4M (jamani hawa wenzetu wanatunza hela), nilishangaa sana kwasababu ni mtu wa kupenda kuomba hela kwa 70% ya matumizi yake na kiukweli hata mimi roho iliniuma bwana, ila niliamua kutulia kwakua sikuwa na namna ya kukisanua.

Baada ya miezi kadhaa kuna ugomvi ulitokea( wa kawaida tu) akawa anaomba msamaha ila nikawa navunga kama nimekasirika sana kumbe moyoni silichukulii hata kama ni kosa kubwa, hapo sasa likaja wazo la kumtoa hela kutokana na majuto yake, ghalfa tu nikamwambia nisaidie 1.5M kama unazo nimekwama sana.

Bila kuuliza ni za nini, aliuza tu atume kwenye namba gani na akatuma na wala hajawahi kuziomba.

Sema hanipi hela ila vitu vya ndani na mavyombo kila siku yanaongezeka, kwakweli simlaumu sana.
Kama ananunua vitu vya ndani, kukitokea dharura anasaidia kubeba pale ulipokwama, na ukikwama sana ukimuomba anakupa. Basi huyo hupaswi kumuuliza hata kama ana 80M kwenye account. Huyo ni mwenzako, tatizo lipo kwako huwa humshirikishi mkeo kwenye mipango ya maendeleo ya familia. Kwa maana nyingine ni matokeo ya baba kuwa mbinafsi
 
Mbona ulivyompa hio idea alitoa hela? Au ukimuuliza huwa anasema hana hela? Kukubali kutoa hela yake kununua shamba ameonesha Hana issue.
Afadhali wewe umekuja na hoja madhubuti. Tatizo limeanza pale ambapo mke anaumwa, mume anahangaika, pesa imeisha, anakopa huku na kule kwa ajili ya kumsaidia mke. Lkn mke kakalia hela kwenye akaunti!!! Hiyo ndio inastaajabisha...
 
Kwa ufupi sana.

Kuna wakati wife alipata changamoto ya kiafya. Matibabu yalikuwa gharama kidogo kutokana na safari za hapa na pale. Kuna wakati akiba ikakata ikabidi nijikopeshe kupitia vyanzo vingine.

Siku moja nikachukua kadi na kuchungulia akaunti yake nikakuta ina milioni saba imetulia. Ikaniuma sana. Baada ya miezi mitatu nikachngulia tena nikakuta ile fedha bado imetulia.

Juzi kati tukapata shamba kwa milioni tatu. Nikampa idea ila nikampanga shamba linauzwa milioni 5. Akaikubali akanipa milioni 2 nimalize kazi.

Nikamaliza biashara na mkataba ukasoma 5m mwenye shamba akachukua 3m. Nikapiga 2m bila kelele.

My Take
Wake zetu mnaficha hela ili iweje? Kuweni mstari wa mbele kushughulika na changamoto za kifamilia
Kama mke wako ni "Kigwasa" umefanya jambo zuri sana. Ila kwa wale tuliobahatika ambaye unaweza muomba hata 1M ukikwama akakugea sioni sababu ya kumchapa.
 
Nyakati na zama zimebadilika....hatuwezi kuishi kwenye zama hizi tukiwa na fikra na mawazo ya zama za mawe.....

Zama hizi jukumu la utafutaji lipo kwa wote na sio mwanaume peke yake hivyo basi kama kila mmoja anaingiza kipato hivyo anawajibika kwenye Ujenzi wa familia kwa Hali na Mali...kama mwanamke anaingiza kipato basi anawajibika kumsaidia mumewe baadhi ya majukumu hii inaleta mshikamano na kuongeza upendo ndani ya familia........

Zamani mwanamke alikuwa hana kipato hivyo jukumu la kuhudumia familia linabakia kuwa la mwanaume lakini sio kwa zama hizi ambapo jamii inatoa fursa sawa kwa jinsia zote mbili.......

Ukiona mkeo anajiweka kando kwenye mambo yanayojumuisha muskatabali mzima wa familia yenu basi ujue huyo mkeo mpo naye kimwili tu na sio kiroho na kiupendo.......

Mwanamke akiwa kama mwenza wa familia sio mpaka umuambie namna ya kiwajibika kwani anaona na anakujua mumewe hivyo sehemu unayokwama anaweza kutatua bila hata ya kumuuliza....ubinafsi ni dalili ya anguko la ndoa....... kwenye ndoa wote mnatakiwa muwe na dira na lengo moja.........

Kuishi na mwenza mbinafsi ni hatari sana

NB;
Wanaume tunapaswa tuweke mbele uwazi ili kuwa mfano kwa Wenzetu........
Umenena vyema sana. This is a matured mind. Umeweza linganisha vizuri sana mabadiliko ya nyakati. Watu wengi wanaleta mifano ya Saudi arabia ambako mwanamke hata kuendesha gari haruhusiwi. Huku kwetu mazingira hayo haya apply, jamii imetoa fursa sawa na zaidi sana mwanamke amepewa fursa zaidi hadi za upendeleo. Katika mazingira haya mke na mume wanapaswa kuwajibika kikamilifu kwa hali na mali zao ndani ya familia bila kuhitaji kukumbushwa.
 
Mwanamke anayekupenda na mwenye nia ya dhati ya kuijenga taasisi ya familia na wewe hamuwezi kufikia huko kwani hilo jambo linajadiliwa kwa upana na kufikiwa muafaka mapema kabisa....na kila linaloendelea litakuwa kwenye mpango kazi mliojiwekea.......nasisitiza tena uwazi ni jambo la msingi sana kwenye ndoa.......huwezi kumhukumu mkeo kwa jambo ambalo hata wewe hulifanyi......wakati mwingine ubinafsi sisi ndio tuwafundisha wanawake kwa matendo yetu..... wakati mwingine anachohitaji mwanamke ni kuhakikishiwa tu uhakika wa kujenga familia na wewe kupitia matendo yako.........Imani hiyo inapotea na kuisha kutokana na mtiririko wa matukio yaliyokithiri ya uzinzi na uasherati.....hali hiyo inamfanya mwanamke ajiondoe kwako taratibu kimipango na kujijengea yeye mwenyewe kwa manufaa ya watoto wake.........anaweza kujituma kujijenga na wewe alafu wakaja watoto saba wa nje nao wakidai mgao......
Fact, ukweli na uwazi ndio wake zetu wanataka. Kama wewe mwenyewe unaficha ulichonacho, usitarajie mkeo awe muwazi kwako hata siku moja. Mimi binafsi huenda mke wangu ni muwazi kwangu kwasababu kila jambo tunalipanga pamoja na tunaenda pamoja katika kulitekeleza. Kila mali tunayonunua tunaandika majina yetu sote, zipo zingine namwandika yeye peke yake kwa ajili ya kumpa moyo kutokana na kujitoa kwake ndani ya familia. Mwanaume kuwa mkweli na muwazi ni nguzo muhimu katika kujenga familia ya mwili mmoja
 
Kama mwanamke unafanya kazi halafu hela zako hazichangii kwenye ustawi wa familia yako ni bora ukae nyumbani tu. Wengine tuko proud kabisa kuchangia maendeleo ya familia. Kila siku unaenda kazini kufanya nini sasa. Wanawake tuache ubinafsi . Mtu unashindwa kununua hata umeme au kulipia maji. Sisi tumezaliwa kijijini huko lakini baba na mama walishirikiana kutulea sisi mpaka tukasoma vizuri. Ingekuwa baba anabeba majukumu yote sijui kama tungefika hapa tulipo. Na waliisha pamoja mpaka kifo kikawatenganisha. Dada zangu wote pia nimeona walivyo bega kwa bega na waume zao na unaweza kuona jinsi maisha yao yalivyo mazuri.
Fact, umeeleza vyema sana. Mi naona familia ambazo mume na mke hawashirikiani na wanafichanafichana, chanzo chake kitakuwa ni familia walizolelewa zilikuwa na ubinafsi uliopindukia mipaka.
 
Mwanamke anayekupenda na mwenye nia ya dhati ya kuijenga taasisi ya familia na wewe hamuwezi kufikia huko kwani hilo jambo linajadiliwa kwa upana na kufikiwa muafaka mapema kabisa....na kila linaloendelea litakuwa kwenye mpango kazi mliojiwekea.......nasisitiza tena uwazi ni jambo la msingi sana kwenye ndoa.......huwezi kumhukumu mkeo kwa jambo ambalo hata wewe hulifanyi......wakati mwingine ubinafsi sisi ndio tuwafundisha wanawake kwa matendo yetu..... wakati mwingine anachohitaji mwanamke ni kuhakikishiwa tu uhakika wa kujenga familia na wewe kupitia matendo yako.........Imani hiyo inapotea na kuisha kutokana na mtiririko wa matukio yaliyokithiri ya uzinzi na uasherati.....hali hiyo inamfanya mwanamke ajiondoe kwako taratibu kimipango na kujijengea yeye mwenyewe kwa manufaa ya watoto wake.........anaweza kujituma kujijenga na wewe alafu wakaja watoto saba wa nje nao wakidai mgao......
Exactly- The back stops with him.
 
Kwa ufupi sana.

Kuna wakati wife alipata changamoto ya kiafya. Matibabu yalikuwa gharama kidogo kutokana na safari za hapa na pale. Kuna wakati akiba ikakata ikabidi nijikopeshe kupitia vyanzo vingine.

Siku moja nikachukua kadi na kuchungulia akaunti yake nikakuta ina milioni saba imetulia. Ikaniuma sana. Baada ya miezi mitatu nikachngulia tena nikakuta ile fedha bado imetulia.

Juzi kati tukapata shamba kwa milioni tatu. Nikampa idea ila nikampanga shamba linauzwa milioni 5. Akaikubali akanipa milioni 2 nimalize kazi.

Nikamaliza biashara na mkataba ukasoma 5m mwenye shamba akachukua 3m. Nikapiga 2m bila kelele.

My Take
Wake zetu mnaficha hela ili iweje? Kuweni mstari wa mbele kushughulika na changamoto za kifamilia
Nawe ukamuibia mkeo 2m!
 
Dah, very disappointing sana. Mwanaume anaiba Hela ndani ya familia halafu anajiona mjanja kwa ku-justify na other issues, ni changamoto sana. Hana tofauti na mwanaume aliyenunuliwa kiwanja na mchepuko wa mkewe alafu anafurahia utadhani jambo jema sana.
Hahahahah mke ambaye anaficha hela yake na kujidai mchungu sana hio ndio dawa yake. Kuna mwanamke unaweza kuwa on your dead end na hela anayo unajua kabisa ila hakupi huyo ni kumchapa tu.

Ila kama mke ni generous sio mchoyo ukihitaji support yake huyo kumuibia ni dhambi hata Mungu hafurahii. Kuna midemu mibinafsi bana we ila kwenye kula hela zako yuko mstari wa mbele kama tai.
 
Kwani ela za mwanaume za kumtibia anajua mwanaume amezitolea wap? Kazi ya pesa ni matumizi wala sio swala la kujua ni ya nani au imetokea wap?

Kwamba unataka kutetea alito-mbwa nje ndo akapewa hiyo m7? Kama ni hivyo huyo ni mke au malaya

Sent using Jamii Forums mobile app
Utetezi wa kijinga kabisa, kuna mwana namjua ana mke na watoto mkoa. Ila yuko bongo anagonga jimama flani ndio linamuweka mjini kistaa kabisa hizi 2-3M hazimpi shida kabisa.

Sio kwamba ni Marioo, jamaa ni lecturer chuo flani ila kama mnavyojua mshahara wa Lecturer hauwezi endesha maisha ya dar na mke mkoani.

Mke mkoa amenunuliwa Raum, jamaa ana premio mayai ila hela nyingi inatoka kwa jimama. Linalipa na kodi maeneo flani katikati ya mji kabisa limemuwekea na Harrier tako la nyani uwani.

Sasa kwa scenario hii utasema justification ya kuwa eti hujui hela ya mke imetoka wapi ina maana hela ya mwanaume kama huyu nae mke asiitumie sababu hajui imetokea wapi?
 
Kuna uzi humi ulishapita na kusema usimuonee huruma mwanamke never ever wanawake wengi ni wana roho ya kichawi na uselfish ni wachache sana ambao wako na roho ya utoaji panapo hitajika utoaji kwa mwanaume wake.
Wewe ni mimi haswaaaa siwezi kuwa na kopeshwa na mke wangu ina kua haina maana ya mke na mume sasa
 
Kama mwanamke unafanya kazi halafu hela zako hazichangii kwenye ustawi wa familia yako ni bora ukae nyumbani tu. Wengine tuko proud kabisa kuchangia maendeleo ya familia. Kila siku unaenda kazini kufanya nini sasa. Wanawake tuache ubinafsi . Mtu unashindwa kununua hata umeme au kulipia maji. Sisi tumezaliwa kijijini huko lakini baba na mama walishirikiana kutulea sisi mpaka tukasoma vizuri. Ingekuwa baba anabeba majukumu yote sijui kama tungefika hapa tulipo. Na waliisha pamoja mpaka kifo kikawatenganisha. Dada zangu wote pia nimeona walivyo bega kwa bega na waume zao na unaweza kuona jinsi maisha yao yalivyo mazuri.
UPENDO ndio nguzo muhimu katika ndoa.... upendo unajumuisha mambo ya msingi na ya kujenga taasisi ya ndoa....... Upendo unaokuza na kujenga ndoa unajumuisha juhudi za pande zote mbili na kila mmoja akijitoa kwa ajili ya huo Muunganiko.......

Unapotoweka upendo ndio huzaliwa ubinafsi......kwa kuwa upendo unajumuisha huruma, kujali, kuthamiana na kuthaminiana.........ubinafsi unazaa utengano wa nafsi na mwili na matokeo huzaa chuki..........
 
Back
Top Bottom