Nimempiga mke wangu milioni 2 kizembe sana

Nimempiga mke wangu milioni 2 kizembe sana

Dah, very disappointing sana. Mwanaume anaiba Hela ndani ya familia halafu anajiona mjanja kwa ku-justify na other issues, ni changamoto sana. Hana tofauti na mwanaume aliyenunuliwa kiwanja na mchepuko wa mkewe alafu anafurahia utadhani jambo jema sana.
Sasa huyu anaeiba hela ndani ya familia na anayeficha hela ndani ya familia yupi bora
 
Kwa ufupi sana.
Kuna wakati wife alipata changamoto ya kiafya. Matibabu yalikuwa gharama kidogo kutokana na safari za hapa na pale. Kuna wakati akiba ikakata ikabidi nijikopeshe kupitia vyanzo vingine.

Siku moja nikachukua kadi na kuchungulia akaunti yake nikakuta ina milioni saba imetulia. Ikaniuma sana. Baada ya miezi mitatu nikachngulia tena nikakuta ile fedha bado imetulia.

Juzi kati tukapata shamba kwa milioni tatu. Nikampa idea ila nikampanga shamba linauzwa milioni 5. Akaikubali akanipa milioni 2 nimalize kazi.

Nikamaliza biashara na mkataba ukasoma 5m mwenye shamba akachukua 3m. Nikapiga 2m bila kelele.

My Take
Wake zetu mnaficha hela ili iweje? Kuweni mstari wa mbele kushughulika na changamoto za kifamilia
Safia sana
 
😊

Wakati mwingine usizipatie nafasi gharama za matibabu zikuumize zaidi. Chukua hatua, check in here,

Mkuu bima kwa familia ipo. Nakukumbusha tu kwamba bima hawakulipii nauli ya bombadia, hawakuwekei mafuta, hawakulipii lodge,
 
Hamna siku ntakuja kutamani pesa ya mke wangu, mimi ni mwanaume sitakuja kutumia utapeli na wizi kuumiza mke wangu eti nionekane mimi nina akili, maisha ya wizi wizi na kutoaminiana siapendi bora nikae kama nilivo kuliko kuiba kwa ujanjajanja......."good relation in marriage is every thing en is beyond money"
Idiot
 
Imekukuta kama mimi, mimi namba ya siri ya mke wangu ya benki na SIM card zak zote nazijua vizuri tu, yeye hajui yangu ya benki ila za SIM zote anazo na wakati fulani huwa namtuma kutoa hela au kulipia vitu nikiwa busy.

Kuna siku sijui roho gani ilinituma kufungua app yake ya SIMBANKING nikaangalia salio nikakuta 8.4M (jamani hawa wenzetu wanatunza hela), nilishangaa sana kwasababu ni mtu wa kupenda kuomba hela kwa 70% ya matumizi yake na kiukweli hata mimi roho iliniuma bwana, ila niliamua kutulia kwakua sikuwa na namna ya kukisanua.

Baada ya miezi kadhaa kuna ugomvi ulitokea( wa kawaida tu) akawa anaomba msamaha ila nikawa navunga kama nimekasirika sana kumbe moyoni silichukulii hata kama ni kosa kubwa, hapo sasa likaja wazo la kumtoa hela kutokana na majuto yake, ghalfa tu nikamwambia nisaidie 1.5M kama unazo nimekwama sana.

Bila kuuliza ni za nini, aliuza tu atume kwenye namba gani na akatuma na wala hajawahi kuziomba.

Sema hanipi hela ila vitu vya ndani na mavyombo kila siku yanaongezeka, kwakweli simlaumu sana.
 
Hamna siku ntakuja kutamani pesa ya mke wangu, mimi ni mwanaume sitakuja kutumia utapeli na wizi kuumiza mke wangu eti nionekane mimi nina akili, maisha ya wizi wizi na kutoaminiana siapendi bora nikae kama nilivo kuliko kuiba kwa ujanjajanja......."good relation in marriage is every thing en is beyond money"
Watu wa Jf bwana[emoji23]
 
Ila binafsi utegemezi pesa ya mtu sijui naonaje tena mwanamke
Naona kuliko nimwombe pesa mwanamke kama shida kweli imenibana ni bora nimwombe mzazi wangu anisaidie
 
Kwa ufupi sana.
Kuna wakati wife alipata changamoto ya kiafya. Matibabu yalikuwa gharama kidogo kutokana na safari za hapa na pale. Kuna wakati akiba ikakata ikabidi nijikopeshe kupitia vyanzo vingine.

Siku moja nikachukua kadi na kuchungulia akaunti yake nikakuta ina milioni saba imetulia. Ikaniuma sana. Baada ya miezi mitatu nikachngulia tena nikakuta ile fedha bado imetulia.

Juzi kati tukapata shamba kwa milioni tatu. Nikampa idea ila nikampanga shamba linauzwa milioni 5. Akaikubali akanipa milioni 2 nimalize kazi.

Nikamaliza biashara na mkataba ukasoma 5m mwenye shamba akachukua 3m. Nikapiga 2m bila kelele.

My Take
Wake zetu mnaficha hela ili iweje? Kuweni mstari wa mbele kushughulika na changamoto za kifamilia

Huyo
Utakuja kuumwa atakuomba hela
Ya matumiz achana nae mm binafsi sitaweza kuoa mwanamke mbinafsi
 
Ni ujinga serious,, kuna shetani mmoja na yeye tuligombana kisa kaki tu...nimetumia pesa nyingi sana kwake siku ana elf tano niliichukua nikamwambia nampa ila nikawa akinikumbusha namwambia nitampa at the same time narudi na kitu as gift yake tu cha zaidi ya hio hela .. vocha yake ni mm naweka bado anathubutu nipa kauli za ajabu kisa elf tano niliitupilia mbali

Aisee huyu utaumwa then atakuomba hela ya matumizi
 
Kwa ufupi sana.
Kuna wakati wife alipata changamoto ya kiafya. Matibabu yalikuwa gharama kidogo kutokana na safari za hapa na pale. Kuna wakati akiba ikakata ikabidi nijikopeshe kupitia vyanzo vingine.

Siku moja nikachukua kadi na kuchungulia akaunti yake nikakuta ina milioni saba imetulia. Ikaniuma sana. Baada ya miezi mitatu nikachngulia tena nikakuta ile fedha bado imetulia.

Juzi kati tukapata shamba kwa milioni tatu. Nikampa idea ila nikampanga shamba linauzwa milioni 5. Akaikubali akanipa milioni 2 nimalize kazi.

Nikamaliza biashara na mkataba ukasoma 5m mwenye shamba akachukua 3m. Nikapiga 2m bila kelele.

My Take
Wake zetu mnaficha hela ili iweje? Kuweni mstari wa mbele kushughulika na changamoto za kifamilia
Nakushauri ufanye uwezalo urejeshe hiyo hela hata kwa kusema umepiga deal fulani umepata hela akaweke ktk akaunti.

Kosa baya sana umefanya kujiibia mwenyewe
 
Binafsi Huwa ninafanyaga baadhi ya arguments na Mzee wangu, ambaye namshukuru Mungu kwa kumweka hai mpaka sasa. Huwa ananiambiaga kama kijana wake, mwanaume ni lazima uwe na high bar kwenye maswala ya kimaadili na hekima kama baba, mwanaume ni lazima awe na busara kwelikweli na uongozi usio na hitilafu na mwenye uwezo wa kufanya maamuzi yenye mantiki pasipo mabavu maana yeye ndo symbol ya familia nzima, Ili pale familia inapopata changamoto nzito na ngumu aweze kuwa kimbilio na source of wisdom, solution, and stability. Mwanaume akishakosa moral authority kwa kujihusisha na mambo ya hovyo atatengeneza instability ndani ya familia kupitia chaos either baina yake na mke wake au watoto, atadharaulika kutokana na uovyo wake na hakuna atayemsikiliza Wala kumheshimu Ikiwemo mbwa wake mwenyewe. Mwanaume akiwa mdokozi na mwenye makandokando ya kijinga Hana tofauti na kibaka wa mtaani. Baba ni lazima achape kazi kwelikweli Ili amtunze mke wake, wazazi wake,jamii inayomzunguka na watoto wake kwa juhudi na maarifa.

Daaah hujaelewa uzi wa jamaa
 
Back
Top Bottom