Nimempiga mke wangu milioni 2 kizembe sana

Nimempiga mke wangu milioni 2 kizembe sana

Kwa ufupi sana.
Kuna wakati wife alipata changamoto ya kiafya. Matibabu yalikuwa gharama kidogo kutokana na safari za hapa na pale. Kuna wakati akiba ikakata ikabidi nijikopeshe kupitia vyanzo vingine.

Siku moja nikachukua kadi na kuchungulia akaunti yake nikakuta ina milioni saba imetulia. Ikaniuma sana. Baada ya miezi mitatu nikachngulia tena nikakuta ile fedha bado imetulia.

Juzi kati tukapata shamba kwa milioni tatu. Nikampa idea ila nikampanga shamba linauzwa milioni 5. Akaikubali akanipa milioni 2 nimalize kazi.

Nikamaliza biashara na mkataba ukasoma 5m mwenye shamba akachukua 3m. Nikapiga 2m bila kelele.

My Take
Wake zetu mnaficha hela ili iweje? Kuweni mstari wa mbele kushughulika na changamoto za kifamilia
Kijana una muibia vipi mtu ambaye unamlisha, unamvisha, una muhudumia, unamsimamia na yasiyo kuwa hayo ? Au mkeo ndiyo muendesha nyumba ?
 
Imekukuta kama mimi, mimi namba ya siri ya mke wangu ya benki na SIM card zak zote nazijua vizuri tu, yeye hajui yangu ya benki ila za SIM zote anazo na wakati fulani huwa namtuma kutoa hela au kulipia vitu nikiwa busy.

Kuna siku sijui roho gani ilinituma kufungua app yake ya SIMBANKING nikaangalia salio nikakuta 8.4M (jamani hawa wenzetu wanatunza hela), nilishangaa sana kwasababu ni mtu wa kupenda kuomba hela kwa 70% ya matumizi yake na kiukweli hata mimi roho iliniuma bwana, ila niliamua kutulia kwakua sikuwa na namna ya kukisanua.

Baada ya miezi kadhaa kuna ugomvi ulitokea( wa kawaida tu) akawa anaomba msamaha ila nikawa navunga kama nimekasirika sana kumbe moyoni silichukulii hata kama ni kosa kubwa, hapo sasa likaja wazo la kumtoa hela kutokana na majuto yake, ghalfa tu nikamwambia nisaidie 1.5M kama unazo nimekwama sana.

Bila kuuliza ni za nini, aliuza tu atume kwenye namba gani na akatuma na wala hajawahi kuziomba.

Sema hanipi hela ila vitu vya ndani na mavyombo kila siku yanaongezeka, kwakweli simlaumu sana.
Yani haya maishaa ya wanaume tuna changamoto sana ila inabdi tuwaelewa tu wanawake...!! Kama akiwa na hela ukikwama anakusaidia bhasi huyo ni mkeee pia hata ukimdanganya akukopee lakini Hajawahii kuidai hiyo helaa bhasi Muoeee...!!
 
Ila binafsi utegemezi pesa ya mtu sijui naonaje tena mwanamke
Naona kuliko nimwombe pesa mwanamke kama shida kweli imenibana ni bora nimwombe mzazi wangu anisaidie
Bhasi hujapata mwanamke sahihi badooo...!!
 
Hamna siku ntakuja kutamani pesa ya mke wangu, mimi ni mwanaume sitakuja kutumia utapeli na wizi kuumiza mke wangu eti nionekane mimi nina akili, maisha ya wizi wizi na kutoaminiana siapendi bora nikae kama nilivo kuliko kuiba kwa ujanjajanja......."good relation in marriage is every thing en is beyond money"
Ngoja uje uletewe taarifa mkeo kajenga nyumba kisiri utuletee mrejesho.
Wanawake ni wasiri sana na wanapotoshana sana wakikutana tegemea chochote kutoka kwao.
Hawana siri lakini hawana uwezo wa kuficha siri pia
 
Kwa ufupi sana.
Kuna wakati wife alipata changamoto ya kiafya. Matibabu yalikuwa gharama kidogo kutokana na safari za hapa na pale. Kuna wakati akiba ikakata ikabidi nijikopeshe kupitia vyanzo vingine.

Siku moja nikachukua kadi na kuchungulia akaunti yake nikakuta ina milioni saba imetulia. Ikaniuma sana. Baada ya miezi mitatu nikachngulia tena nikakuta ile fedha bado imetulia.

Juzi kati tukapata shamba kwa milioni tatu. Nikampa idea ila nikampanga shamba linauzwa milioni 5. Akaikubali akanipa milioni 2 nimalize kazi.

Nikamaliza biashara na mkataba ukasoma 5m mwenye shamba akachukua 3m. Nikapiga 2m bila kelele.

My Take
Wake zetu mnaficha hela ili iweje? Kuweni mstari wa mbele kushughulika na changamoto za kifamilia
Mbona ulivyompa hio idea alitoa hela? Au ukimuuliza huwa anasema hana hela? Kukubali kutoa hela yake kununua shamba ameonesha Hana issue.
 
Yani haya maishaa ya wanaume tuna changamoto sana ila inabdi tuwaelewa tu wanawake...!! Kama akiwa na hela ukikwama anakusaidia bhasi huyo ni mkeee pia hata ukimdanganya akukopee lakini Hajawahii kuidai hiyo helaa bhasi Muoeee...!!
Na pale niliamua nimuombe ili kumpima tu imani baada ya kugundua anapesa nyingi, ingetokea akaninyima ningesononeka sana kujua hanijali.
 
Yaani tatizo Ni kubwa,,kuishi na mwizi ndani Ni Bora kuficha tu hiyo laki mwizi ajue Kuna sabini tu.
Shenzee kabisa Joannah Ahahahahahahaaaa..!! Kwani huwa mnaogopa kuibiwa? Wala si kuibiwa, nyie hata LUKU ikiisha na upo nyumbani, kutoa hela yako kununu LUKU ni shida. Utampigia simu mtu yupo safarini hukoo anunue LUKU
 
Shenzee kabisa Joannah Ahahahahahahaaaa..!! Kwani huwa mnaogopa kuibiwa? Wala si kuibiwa, nyie hata LUKU ikiisha na upo nyumbani, kutoa hela yako kununu LUKU ni shida. Utampigia simu mtu yupo safarini hukoo anunue LUKU
Mwanamke anaweza kukuomba umnunulie vocha na kwenye simu yake ana salio la tigopesa au mpesa..
 
Nyakati na zama zimebadilika....hatuwezi kuishi kwenye zama hizi tukiwa na fikra na mawazo ya zama za mawe.....

Zama hizi jukumu la utafutaji lipo kwa wote na sio mwanaume peke yake hivyo basi kama kila mmoja anaingiza kipato hivyo anawajibika kwenye Ujenzi wa familia kwa Hali na Mali...kama mwanamke anaingiza kipato basi anawajibika kumsaidia mumewe baadhi ya majukumu hii inaleta mshikamano na kuongeza upendo ndani ya familia........

Zamani mwanamke alikuwa hana kipato hivyo jukumu la kuhudumia familia linabakia kuwa la mwanaume lakini sio kwa zama hizi ambapo jamii inatoa fursa sawa kwa jinsia zote mbili.......

Ukiona mkeo anajiweka kando kwenye mambo yanayojumuisha muskatabali mzima wa familia yenu basi ujue huyo mkeo mpo naye kimwili tu na sio kiroho na kiupendo.......

Mwanamke akiwa kama mwenza wa familia sio mpaka umuambie namna ya kiwajibika kwani anaona na anakujua mumewe hivyo sehemu unayokwama anaweza kutatua bila hata ya kumuuliza....ubinafsi ni dalili ya anguko la ndoa....... kwenye ndoa wote mnatakiwa muwe na dira na lengo moja.........

Kuishi na mwenza mbinafsi ni hatari sana

NB;
Wanaume tunapaswa tuweke mbele uwazi ili kuwa mfano kwa Wenzetu........
 
Nyakati na zama zimebadilika....hatuwezi kuishi kwenye zama hizi tukiwa na fikra na mawazo ya zama za mawe.....

Zama hizi jukumu la utafutaji lipo kwa wote na sio mwanaume peke yake hivyo basi kama kila mmoja anaingiza kipato hivyo anawajibika kwenye Ujenzi wa familia kwa Hali na Mali...kama mwanamke anaingiza kipato basi anawajibika kumsaidia mumewe baadhi ya majukumu hii inaleta mshikamano na kuongeza upendo ndani ya familia........

Zamani mwanamke alikuwa hana kipato hivyo jukumu la kuhudumia familia linabakia kuwa la mwanaume lakini sio kwa zama hizi ambapo jamii inatoa fursa sawa kwa jinsia zote mbili.......

Ukiona mkeo anajiweka kando kwenye mambo yanayojumuisha muskatabali mzima wa familia yenu basi ujue huyo mkeo mpo naye kimwili tu na sio kiroho na kiupendo.......

Mwanamke akiwa kama mwenza wa familia sio mpaka umuambie namna ya kiwajibika kwani anaona na anakujua mumewe hivyo sehemu unayokwama anaweza kutatua bila hata ya kumuuliza....ubinafsi ni dalili ya anguko la ndoa....... kwenye ndoa wote mnatakiwa muwe na dira na lengo moja.........

Kuishi na mwenza mbinafsi ni hatari sana

NB;
Wanaume tunapaswa tuweke mbele uwazi ili kuwa mfano kwa Wenzetu........
shida wanaume hatuwi wawazii mkuu mtu unajua kabisa hela ushatumia kwenye mambo ya kifamiliaa sijui kulipa kodi mara adaa lakini unashindwa kummwambia mwenzio nimekwamaa... mwanamke nae akikuomba hela unaona bora ukope umridhishe yeye kuliko kusema ukweli hela hunaa
 
Mimi ninachojua mama lazima uwe na bajeti siku vimebuma kabisa kabisa nitatoa kama hapo kaumwa umemtumia 2 m it's okay si ilikuwepo? Otherwise front seat tunaominya Hela mpambane Tu msitupigie mahesabu.
 
nitarejesha vipi hela ambayo imetumika kwenye matumizi halali ya familia
Suala siyo kurejesha suala ni kumuibia unae mlisha, ndiyo maana nimekuuliza au mkeo ndiyo muendesha nyumba. Kama msimamizi ni yeye hapo sawa, lakini kama msimamizi ni wewe hapo umejipiga mwenyewe na hujampiga mkeo.
 
Hamna siku ntakuja kutamani pesa ya mke wangu, mimi ni mwanaume sitakuja kutumia utapeli na wizi kuumiza mke wangu eti nionekane mimi nina akili, maisha ya wizi wizi na kutoaminiana siapendi bora nikae kama nilivo kuliko kuiba kwa ujanjajanja......."good relation in marriage is every thing en is beyond money"
Maisha hayakuchapa ipasavyo. Siku yakikuchapa ipasavyo lazima utajiuliza maswali kwanini mali za mkeo si sehemu ya mali za familia, na utastaajabu sana jinsi mfumo haupo fair.

Unamuuguza, unakopa hadi unaweka bond nyumba lkn yeye kakalia 5M hata hakwambiii! Imagine this situation! Mnaosema hamuwezi tamani vipato vyao, hilo ni kweli kama tu una kipato kikubwa sana na maisha yapo smooth. Kwa mazingira hayo huwezi fikiria hata kidogo alichonacho mkeo. But when things goes the other way around lazima utarudi kwenye akiba za mkeo...
 
Kwanini uchukue 5k ya mwana mke na hutaki kuirudisha, ntampa je zawadi wakati bado anakudai pesa yake 5k,....Wanaumme jifuzeni jinsi ya kuishi na wanawake ni kama watoto katika masuala ya pesa na hisia emotions, kwanini umuahidi kumlejeshea pesa yake af unabadilisha gia angani.
Acha mawazo ya kizamani. Zama hizi zimebadilika, mambo ni 50 kwa 50. Wanawake ni wabunge, ni majenerali ni ma rais. Mwanamke si yule kiumbe dhaifu uliyemfahamu hapo zamani. Hizi si zama za mwanamke anakaa nyumbani kulea watoto na kuangalia nyumba halafu mwanaume anaenda kutafuta kwa ajili yake na familia. Hizi ni zama ambazo asubuhi mke na mume mnatoka mnamwacha dada wa kazi na watoto mnaenda kazini! Hivyo, kama wote mnatafuta, basi jua wote mnawajibika. Nyakati zimebadilika, Usikariri

Kwa kuongezea, mwanamke anayekupenda na mwenye nia ya kujenga familia nawewe mpaka kufa, lazima atashiriki kikamilifu katika kujenga uchumi wa familia.
 
shida wanaume hatuwi wawazii mkuu mtu unajua kabisa hela ushatumia kwenye mambo ya kifamiliaa sijui kulipa kodi mara adaa lakini unashindwa kummwambia mwenzio nimekwamaa... mwanamke nae akikuomba hela unaona bora ukope umridhishe yeye kuliko kusema ukweli hela hunaa
Mwanamke anayekupenda na mwenye nia ya dhati ya kuijenga taasisi ya familia na wewe hamuwezi kufikia huko kwani hilo jambo linajadiliwa kwa upana na kufikiwa muafaka mapema kabisa....na kila linaloendelea litakuwa kwenye mpango kazi mliojiwekea.......nasisitiza tena uwazi ni jambo la msingi sana kwenye ndoa.......huwezi kumhukumu mkeo kwa jambo ambalo hata wewe hulifanyi......wakati mwingine ubinafsi sisi ndio tuwafundisha wanawake kwa matendo yetu..... wakati mwingine anachohitaji mwanamke ni kuhakikishiwa tu uhakika wa kujenga familia na wewe kupitia matendo yako.........Imani hiyo inapotea na kuisha kutokana na mtiririko wa matukio yaliyokithiri ya uzinzi na uasherati.....hali hiyo inamfanya mwanamke ajiondoe kwako taratibu kimipango na kujijengea yeye mwenyewe kwa manufaa ya watoto wake.........anaweza kujituma kujijenga na wewe alafu wakaja watoto saba wa nje nao wakidai mgao......
 
Binafsi Huwa ninafanyaga baadhi ya arguments na Mzee wangu, ambaye namshukuru Mungu kwa kumweka hai mpaka sasa. Huwa ananiambiaga kama kijana wake, mwanaume ni lazima uwe na high bar kwenye maswala ya kimaadili na hekima kama baba, mwanaume ni lazima awe na busara kwelikweli na uongozi usio na hitilafu na mwenye uwezo wa kufanya maamuzi yenye mantiki pasipo mabavu maana yeye ndo symbol ya familia nzima, Ili pale familia inapopata changamoto nzito na ngumu aweze kuwa kimbilio na source of wisdom, solution, and stability. Mwanaume akishakosa moral authority kwa kujihusisha na mambo ya hovyo atatengeneza instability ndani ya familia kupitia chaos either baina yake na mke wake au watoto, atadharaulika kutokana na uovyo wake na hakuna atayemsikiliza Wala kumheshimu Ikiwemo mbwa wake mwenyewe. Mwanaume akiwa mdokozi na mwenye makandokando ya kijinga Hana tofauti na kibaka wa mtaani. Baba ni lazima achape kazi kwelikweli Ili amtunze mke wake, wazazi wake,jamii inayomzunguka na watoto wake kwa juhudi na maarifa.
Mi nashangaa watu wanaongea habari za moral authority lkn wengi wao wana michepuko au wamewahi kuwa na michepuko. Hivi mnajua huo nao ni wizi? Ni sawa na umeiba penzi la mkeo na kupeleka kwengineko. Hivyo, mnavozungumza hapa muhakikishe mpo clean dhidi ya makandokando.

NB. Sitetei wizi. Jamaa aliatakiwa amchane mke wake kuwa kwanini anaficha pesa yeye anahangaika kukopa huku na kule kwa ajili ya ugonjwa wake mwenyewe. (Binafsi mimi mke wangu, hana hata chembe ya ubinafsi kwenye maswala ya pesa)
 
Mke nadhani ndiye msaidizi namba moja wa mume wake,suala la eti una mke,umezidiwa majukumu,unamuomba msaada anakukatalia,kisa pesa ni ya kwake,huyo ni wanini sasa ndani kwangu?

Yaani niende nikadharaulike huko mtaani,nayeye anao uwezo wa kunisaidia halafu anakataa,hapana kwakweli,tena hawa wanawake ambao wakimpenda bodaboda au dereva bajaji,safari ya buku 8,dereva anapewa elfu 20?Hapana kwakweli,ndiyomaana hata wadada ambao ni waajiriwa,mi huwa naona wanaowashobokea kuwaoa,eti wanaweza kusaidiana kwenye majukumu,huwa nawashangaa,ni bora uoe mama wa nyumbani tu,alee watoto ipasavyo,na ujue mimi ndiyo kila kitu.
Fact
 
Nyakati na zama zimebadilika....hatuwezi kuishi kwenye zama hizi tukiwa na fikra na mawazo ya zama za mawe.....

Zama hizi jukumu la utafutaji lipo kwa wote na sio mwanaume peke yake hivyo basi kama kila mmoja anaingiza kipato hivyo anawajibika kwenye Ujenzi wa familia kwa Hali na Mali...kama mwanamke anaingiza kipato basi anawajibika kumsaidia mumewe baadhi ya majukumu hii inaleta mshikamano na kuongeza upendo ndani ya familia........

Zamani mwanamke alikuwa hana kipato hivyo jukumu la kuhudumia familia linabakia kuwa la mwanaume lakini sio kwa zama hizi ambapo jamii inatoa fursa sawa kwa jinsia zote mbili.......

Ukiona mkeo anajiweka kando kwenye mambo yanayojumuisha muskatabali mzima wa familia yenu basi ujue huyo mkeo mpo naye kimwili tu na sio kiroho na kiupendo.......

Mwanamke akiwa kama mwenza wa familia sio mpaka umuambie namna ya kiwajibika kwani anaona na anakujua mumewe hivyo sehemu unayokwama anaweza kutatua bila hata ya kumuuliza....ubinafsi ni dalili ya anguko la ndoa....... kwenye ndoa wote mnatakiwa muwe na dira na lengo moja.........

Kuishi na mwenza mbinafsi ni hatari sana

NB;
Wanaume tunapaswa tuweke mbele uwazi ili kuwa mfano kwa Wenzetu........
Kama mwanamke unafanya kazi halafu hela zako hazichangii kwenye ustawi wa familia yako ni bora ukae nyumbani tu. Wengine tuko proud kabisa kuchangia maendeleo ya familia. Kila siku unaenda kazini kufanya nini sasa. Wanawake tuache ubinafsi . Mtu unashindwa kununua hata umeme au kulipia maji. Sisi tumezaliwa kijijini huko lakini baba na mama walishirikiana kutulea sisi mpaka tukasoma vizuri. Ingekuwa baba anabeba majukumu yote sijui kama tungefika hapa tulipo. Na waliisha pamoja mpaka kifo kikawatenganisha. Dada zangu wote pia nimeona walivyo bega kwa bega na waume zao na unaweza kuona jinsi maisha yao yalivyo mazuri.
 
Back
Top Bottom