Nimemtimua Nabii aliyekuja kumtembelea Mke wangu

Nimemtimua Nabii aliyekuja kumtembelea Mke wangu

Duh wewe ndio mmojawao mnaojifedhehesha kwa Hawa msnsbii wa UONGO yaani uiache nyumba mkeo na wezi, wakimbadili? huyo mwamposa mpaka leo hajaoa
TAFADHALI FUKUZA WOTE NDIO UANAUME na mke skiendelea FUKUZA, hawana faida yoyote na hawajui lolote
Mwamposa hajaoa!! Yakweli haya kiongozi wangu?
 
mkuu si ungeacha tu wafanye wanacho fanya kwani wangekaa muda gani.by the way hongera kwa kujipatia tiket ya VIP kuelekea kuzimu...
 
Mamabii na mitume walishapita, wapakwa mafuta wa Mungu walishapita kwa sasa tunao wacha Mungu tu...nao wanatumia neno la manabii na mitume wa kitabu cha Bibilia takatatifu...!! Kila kitu kiko wazi ktk Biblia shida tuliyonayo 1.Hatusomi maandiko wala hatutaki kujifunza ma wala hatuna muda wa kutafakari neno la Mungu hata tukitoka church jpili kifuatacho ni element, club nk 2. Tumweka imani yetu kwa watu/mitume na mnabii badala ya Mungu/Kristo kwanza yaani tunaanza kuamini kwa mtu baade ndio kristo ndio maana kila nabii annakuja na cha kutokea mafuta, maji, sabuni chumvi nk..ila hivi vyote kwenye bibilia vipo. Hakuna ibada nzuri kama kuwajari wasio nacho tutoe sadaka kwa unyenyekevu kwwnye makanisa tujifunze neno la Mungu na kimtii Mungu...3. Siku hizi ibada zimekuwa za kudeal na wachawi, mafanikio,majumba , magari nk na hata kupangiana kiwango cha sadaka wenye 50000 wapite mbele, wenye elfu 30...yaani ni mwendo wa fedha tu...sasa inafika muda wenye pesa ndio kipaumbele cha kanisa...sasa inafika mahali wenzangu na.mie nao wanjimaliza, tutumie pesa kdg kuanzisha biashara badala ya kujimaliza ili ukifanikiwa uendelee kumtolea Mungu Malimbuko na fungu la 10. Shida tumeshikwa pabaya na mafanikio na miujiza.
Neno tunalisoma na kulielewa.
Nakushauri rudia kusoma kwa kuwa imeandikwa kuwa siku za mwisho "nitamimina roho juu ya wote wenye mwili, wana wenu watatabiri, ....wazee wataota ndoto, vijana wataona maono (Yoel 2:28-29)" (Soma pia Warumi na Isaya).

Katika Agano Jipya Yesu anawaambia wanafunzi wake wakiaamini na kuwa na imani watafanya makubwa kuliko yeye...

Yesu alikuwa nabii...na yeye alikuwa na karama na vipawa kibao...hivyo ametupa uwezo wa kufanyika wana wake (Yohana 1:12) wenye kujawa na Roho wake (Matendo 1:8) ambaye anatupa nguvu na uwezo wa kufanya makubwa yanayozidi akili na ufahamu wa kibinadamu.

Tuishike kweli ya neno la Mungu (Yohana 17:17; Yohana 14:6), na sio kuishika dini na taratibu zake, hizi taratibu ni maagizo ya watu. Hivyo, karama za kinabii na utume zipo na hazitaondoka kwao wamchao Mungu hadi mlango wa neema utakapofungwa, ambao ndio ule mwisho.

Mitume na Manabii makajanja wapo wengi tu, na tuwe makini. ILA ukweli ni huu watumishi wa Mungu wapo wengi sana na wanasema yatakayo kwa Mungu.
 
kuna siku utakamatika hapo, hata kunyanyua ulimi uongee hutaweza, hata kunyanyua mguu uende chooni hutaweza. utahitaji msaada wa wanadamu hautakuwepo, utahitaji msaada wa madoctor hautakuponya, utaanza mwenyewe kuhitaji watu waje hapohapo nyumbani waimbe mapambio na kukuombea kwa Mungu. nina ndugu yangu alikuwa kama wewe, alikuwa na pesa, mtu mkubwa serikalini huko, shetani alikuja kumletea ugonjwa, nilipomtembelea nilikuwa nakuta muda wote ameweka channel za mahubiri tu tena ya walokole, mtu wa kulala tu kitandani kila kitu hapohapo hata tv wamemsogezea karibu na kitanda, imefika mahali akawa anaamini labda uwepo wa channel ya kidini utatransfer uponyaji uje kwake. kiburi chooote kwisha.

hata wewe ni kwasababu u mzima, na unaamini huhitaji hayo mambo. nakuhakikishia kuna siku utaikumbuka hii thread na utakuja kuwashauri watu wengine wenye moyo kama wa kwako.

jambo lingine, kila mtu atauchukua msalaba wake mwenyewe, na atahojiwa mbele za Mungu kwa habari zake binafsi, mke hatachukua mzigo wa mume wala mume kuchukua mzigo wa mke wala wa watoto wake. hivyo acha kubana mke wako. kwanza inaonekana ulimkuta akiwa mwamini ukambadilisha ili afuate imani yako ya dini isiyo ya kuokoka. baada ya miaka 9 bado unamchagulia cha kuamini na namna ya kuamini. huo ni ukoloni, mwache asali anavyoamini, si ukute yeye akawa sahihi akaja kukusaidia, au akakuta imani tofauti huko akaja kukushauri kuwa usiende huko alikokuwa ameenda.

kitu pekee ambacho tunaweza kukubaliana mimi na wewe ni kuhusu manabii wa mafuta, hao hata mimi siwaamini hasa hao wanaobase zaidi kwenye mafuta na materials na miujiza kuliko Jina la Yesu, na haao ambao kuwaona lazima utoe pesa, hao hata mimi ndugu zangu nitawashauri tu wasiende ila sitakuwa dictator kwao kama ulivyo wewe. ni ukoloni huo kuwa dictator nyumbani unachagulia watu namna ya kumtafuta Mungu, pia ni ushamba huo. ila kuokoka kupo palepale unatakiwa kuokoka ndugu, la sivyo haupo salama.
Nimekupenda bure mkuu uliposema hukubaliani na manabii wa mafuta na wale ambao ili uwaone unatoa Pesa hao hata mimi nawakataa kwa jina la Yesu Kristo aliyehai
 
Kwakweli mimi nabii atakayekuja na vimafuta na vimaji namchana live mlangoni wewe ni Mchawi utoke
 
Lione jinga hili, watumishi wa Mungu wa kweli wana Hekima na kamwe hawaruhusu mzozo Kati ya Mume na mke.

Unajua Mungu baada ya kuumba ulimwengu na kila kitu, hakuumba huduma au mapambio, Ndoa ilitangulia, Hawa manabii wa uongo washenzy tu.

Kwanza hakuna manabii Sasa kwa mujibu wa Biblia, maana pazia la hekalu lilipasuka na kila mtu a naingia uweponi mwa Mungu bila uwakilishi.

Warumi 8.14 kwa kuwa wanaoongozwa na roho wa Mungu ndiyo wana wa Mungu, si wanaoongozwa na manabii, aisee wakija tena fukuzs na MJELEDI.
Kuna nabii alimwambia mke Wangu aachane na jina nililompa mwanangu wa kiume akampa jina analotaka yeye ajabu mke Wangu akakabali akawa anamuta wakati mimi sipo bad enough akadiriki hata kumuandika clinic kwa jina hilo aisee nilipolifuma maana alikuwa ameficha kadi huo mziki wake usipime nikamuambia huyo mtoto utakuwa umezaa na huyo nabii ikabidi aombe radhi
 
Kama umewaambia waje kwa ishu nyingine na umekataa wasiombe basi ngoja waje kwa ishu ya kumla mkeo!
 
Lione jinga hili, watumishi wa Mungu wa kweli wana Hekima na kamwe hawaruhusu mzozo Kati ya Mume na mke.

Unajua Mungu baada ya kuumba ulimwengu na kila kitu, hakuumba huduma au mapambio, Ndoa ilitangulia, Hawa manabii wa uongo washenzy tu.

Kwanza hakuna manabii Sasa kwa mujibu wa Biblia, maana pazia la hekalu lilipasuka na kila mtu a naingia uweponi mwa Mungu bila uwakilishi.

Warumi 8.14 kwa kuwa wanaoongozwa na roho wa Mungu ndiyo wana wa Mungu, si wanaoongozwa na manabii, aisee wakija tena fukuzs na MJELEDI.
Kwenye suala la hekima nakubaliana na wewe mkuu maana mimi tulipishana na wife baada ya kugundua namcheat alichofanya akachukua picha yetu ya harusi akaipeleka kwa nabii akamwambia niangalizie kama ndoa yangu iko salama ajabu nabii akamwambia mumeo anakucheat anatembea na binti wa kiislamu na kamwendea kwa waganga ili amkamate kisawasawa sasa hapo nabii alitumia hekima gani sikumuelewa
 
Kuna nabii alimwambia mke Wangu aachane na jina nililompa mwanangu wa kiume akampa jina analotaka yeye ajabu mke Wangu akakabali akawa anamuta wakati mimi sipo bad enough akadiriki hata kumuandika clinic kwa jina hilo aisee nilipolifuma maana alikuwa ameficha kadi huo mziki wake usipime nikamuambia huyo mtoto utakuwa umezaa na huyo nabii ikabidi aombe radhi

Vita na manabii kuhusiana na wake zetu ni muhimu viwe endelevu
 
Mughonile!

Nilimuoa Mke wangu miaka 9 iliyopita. Kwa sasa tunawatoto wawili.
Mke wangu alikuwa amebobea kwenye Makanisa haya ya upako.

Baada ya kukubaliana na vigezo vyangu, ambacho kimoja wapo nilimuarisha aachane na manabii wa upako, akakubali.
Ndipo nilipomuoa Kwa ndoa takatifu ya kikristo.

Ni miaka 9 sasa imepita, juzi Yule Nabii na waumini wengine walikuja kumtembelea Mke wangu. Tuliwapokea vizuri wakapiga Stori zao.

Tatizo wakataka waanze kuomba na kabla ya kuomba waimbe mapambio Yao. Kwa kweli niliwazuia, niliwaambia tuheshimiane. Kelele nyumbani kwangu ni mwiko na ndio maana ninaishi sehemu yenye makazi tulivu.

Tukazozana, nikawafukuza! Mke wangu ananiambia ninaroho ngumu,
Nikamjibu sio roho ngumu tuu Bali roho mbaya kabisa.

Nimewapiga marufuku kuja kwenye nyumba yangu kujifanya wanajifanya wanaombea ombea watu. Nani anashida na kuombewa hapa!

Nimewaambia wakija waje Kwa inshu nyingine.

Pumbavu!
👏🏽👏🏽👏🏽
Naisubiria hii siku nami nitekeleze zoezi hili
Kufukuza hawa wadanganyifu pindi wakifika nyumbani kwetu
Huwa natamani niwafuate huko kwenye mahekalu yao lakini naogopa nitakuwa nimevamia eneo la wenyewe.... Ila siku wakijisahau wafike kwetu watasimulia na ushuhuda watatoa

Ulifanya vyema hawa manabii sijui mitume ni waongo wasumbufu matapeli waharibifu wa familia za watu
 
Wakuuu kuabudu sio uchawi tufikie wanaume tukue kiakili huyo hakulogi anamuabudu Mungu ww kama unaona huendi na falisafa hizo ondoka lakini usimfukuze nikukosa hekima
 
Wachache sana watakao kuelewa..

#MaendeleoHayanaChama
Wanawake ni viumbe wa ajabu sana.
Huwa wanadharau wanako heshimiwa na kuheshimu wanako dharauliwa.

Ukimuheshimu mwanaume naye atakuheshimu, lakini ukimuheshimu mwanamke yeye anatafsiri kama udhaifu.
 
Safi,siku nyingine wakija usiwafukuze weka bakuli la sadaka harafu watoe sadaka kwanza kabla ya maombi kisha kusanya fedha weka mfukoni agana nao kibingwa hawatakaa waje tena!!
 
Na uki entertain unakuta mke anamwamini kiongozi wa dini hata akisema askupe unyumba mwaka mzima hakupi, anakuwa anamwendesha kama remote.
Kuna dada alikuwa na shida sana hana kazi hata mtoto kashindwa mpeleka shule, kapata kazi kibaha eti mchungaji anamwambia asiende akienda nani ataimba mapambio. Na yeye kidogo akubali kutokwenda
Alafu anaishia kuwa omba omba Hawa jamaa huwa wanawapa nn waumini
 
Back
Top Bottom