Nimemtimua Nabii aliyekuja kumtembelea Mke wangu

Duh wewe ndio mmojawao mnaojifedhehesha kwa Hawa msnsbii wa UONGO yaani uiache nyumba mkeo na wezi, wakimbadili? huyo mwamposa mpaka leo hajaoa
TAFADHALI FUKUZA WOTE NDIO UANAUME na mke skiendelea FUKUZA, hawana faida yoyote na hawajui lolote
Mwamposa hajaoa!! Yakweli haya kiongozi wangu?
 
mkuu si ungeacha tu wafanye wanacho fanya kwani wangekaa muda gani.by the way hongera kwa kujipatia tiket ya VIP kuelekea kuzimu...
 
Neno tunalisoma na kulielewa.
Nakushauri rudia kusoma kwa kuwa imeandikwa kuwa siku za mwisho "nitamimina roho juu ya wote wenye mwili, wana wenu watatabiri, ....wazee wataota ndoto, vijana wataona maono (Yoel 2:28-29)" (Soma pia Warumi na Isaya).

Katika Agano Jipya Yesu anawaambia wanafunzi wake wakiaamini na kuwa na imani watafanya makubwa kuliko yeye...

Yesu alikuwa nabii...na yeye alikuwa na karama na vipawa kibao...hivyo ametupa uwezo wa kufanyika wana wake (Yohana 1:12) wenye kujawa na Roho wake (Matendo 1:8) ambaye anatupa nguvu na uwezo wa kufanya makubwa yanayozidi akili na ufahamu wa kibinadamu.

Tuishike kweli ya neno la Mungu (Yohana 17:17; Yohana 14:6), na sio kuishika dini na taratibu zake, hizi taratibu ni maagizo ya watu. Hivyo, karama za kinabii na utume zipo na hazitaondoka kwao wamchao Mungu hadi mlango wa neema utakapofungwa, ambao ndio ule mwisho.

Mitume na Manabii makajanja wapo wengi tu, na tuwe makini. ILA ukweli ni huu watumishi wa Mungu wapo wengi sana na wanasema yatakayo kwa Mungu.
 
Nimekupenda bure mkuu uliposema hukubaliani na manabii wa mafuta na wale ambao ili uwaone unatoa Pesa hao hata mimi nawakataa kwa jina la Yesu Kristo aliyehai
 
Kwakweli mimi nabii atakayekuja na vimafuta na vimaji namchana live mlangoni wewe ni Mchawi utoke
 
Kuna nabii alimwambia mke Wangu aachane na jina nililompa mwanangu wa kiume akampa jina analotaka yeye ajabu mke Wangu akakabali akawa anamuta wakati mimi sipo bad enough akadiriki hata kumuandika clinic kwa jina hilo aisee nilipolifuma maana alikuwa ameficha kadi huo mziki wake usipime nikamuambia huyo mtoto utakuwa umezaa na huyo nabii ikabidi aombe radhi
 
Kama umewaambia waje kwa ishu nyingine na umekataa wasiombe basi ngoja waje kwa ishu ya kumla mkeo!
 
Kwenye suala la hekima nakubaliana na wewe mkuu maana mimi tulipishana na wife baada ya kugundua namcheat alichofanya akachukua picha yetu ya harusi akaipeleka kwa nabii akamwambia niangalizie kama ndoa yangu iko salama ajabu nabii akamwambia mumeo anakucheat anatembea na binti wa kiislamu na kamwendea kwa waganga ili amkamate kisawasawa sasa hapo nabii alitumia hekima gani sikumuelewa
 

Vita na manabii kuhusiana na wake zetu ni muhimu viwe endelevu
 
πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½
Naisubiria hii siku nami nitekeleze zoezi hili
Kufukuza hawa wadanganyifu pindi wakifika nyumbani kwetu
Huwa natamani niwafuate huko kwenye mahekalu yao lakini naogopa nitakuwa nimevamia eneo la wenyewe.... Ila siku wakijisahau wafike kwetu watasimulia na ushuhuda watatoa

Ulifanya vyema hawa manabii sijui mitume ni waongo wasumbufu matapeli waharibifu wa familia za watu
 
Wakuuu kuabudu sio uchawi tufikie wanaume tukue kiakili huyo hakulogi anamuabudu Mungu ww kama unaona huendi na falisafa hizo ondoka lakini usimfukuze nikukosa hekima
 
Wachache sana watakao kuelewa..

#MaendeleoHayanaChama
Wanawake ni viumbe wa ajabu sana.
Huwa wanadharau wanako heshimiwa na kuheshimu wanako dharauliwa.

Ukimuheshimu mwanaume naye atakuheshimu, lakini ukimuheshimu mwanamke yeye anatafsiri kama udhaifu.
 
Safi,siku nyingine wakija usiwafukuze weka bakuli la sadaka harafu watoe sadaka kwanza kabla ya maombi kisha kusanya fedha weka mfukoni agana nao kibingwa hawatakaa waje tena!!
 
Alafu anaishia kuwa omba omba Hawa jamaa huwa wanawapa nn waumini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…