Makabila ya kanda ya ziwa yana majina ya watu wanaovuruga uchumba wa mtu, wanaitwa 'bhasobhezi', hiyo ni title kabisa yaani.
Kwa hoja yako hiyo embu ichimbe kiundani zaidi ili uelewe mantiki ya wewe kupewa taarifa hiyo katika kipindi hiki ni nini hasa?
Je mtu asiyekufahamu wewe, anaweza kukupenda zaidi kukuhabarisha habari za faida?
Rudi kwenye nafsi yako, hivi kweli wewe ni msafi wa mfano kuweza kumnyooshea mwenzako kidole kwa haki juu ya mambo anayofanya ambayo hujawahi kuyafanya?
Rudi kwenye jamii, hivi tamaduni za kuoa mabinti mabikra bado zipogo, wangapi wanyooshe mikono juu kutudhihirishia kuwa wao walioa vigori na bikra zao og sealed, na siyo zile bikra feki?
Kijana, angalia mizani ya upendo wenu na huyo mwenzako upoje?
Huyo msichana mchumba wako yupo kwenye vita ngumu sana na wabaya wake pamoja na mahawara zake ili asiweze kufanikiiaha ndoto zake za kuolewa.
Badala yake anatakiwa abaki nao hao warusha picha wakimtumia kama mtumwa wao wa kingono bila ya uelekeo, embu okoa jahazi kiume.
Kihunzi cha kwanza cha asessment muhimu katika maisha ya ndoa umekiruka kirahisi tena kwa kurahisishiwa na vishoka, sasa umebakiza vichache virahisi ambavyo utakuja kuvimalizia mkianza kuishi pamoja na utamuwini vizuri sana huyo mwanamke utapoishi naye.
Huwa ni mtihani mkubwa sana kudhani umeoa mwanamke 'wautulie' kumbe ni kipanga kisichokosa mawindo!
Umeshamwelewa baadhi ya background ya tabia zake ni rahisi sasa kuweza kuishi naye kama ni kweli aliyopigwa nayo picha aliyafanya sijui mwaka gani, atajirekebisha na kuachana nayo, maana mambo haya ni hulka ya vijana wote wa rika lenu.
Na mkiona mmefanikiwa na kuanza kuishi pamoja na kwa malengo, tabia hizo hujivua zenyewe mwilini mwa mtu kama vile Ccm ya Kikwete na Mukama ilivyojivua gamba 2011😁😁😜.
Itapendeza ukimuoa na kuzipangua figisu na fitina zote anazopigwa nazo mwenzako.
Maana saazingine yawezekana naye huko kashatumiwa kashifa zako ili kuwavuruga ili lengo lenu lisiwezekane kama nilvyokwisha sema.