Nimetembea mikoa mingi Tanzania nimegundua kuwa Dodoma kuna nyoka wengi hatari kuliko mikoa yote Tanzania

Nimetembea mikoa mingi Tanzania nimegundua kuwa Dodoma kuna nyoka wengi hatari kuliko mikoa yote Tanzania

Habari za mida hii ndugu wananchi, kifupi mimi siyo mtaalamu wa wanyama ila ni mpenzi na mfuatiliaji wa masuala ya wanyama na makala zao kupitia TV na mitandao.

Nimetembea mikoa karibu yote Tanzania ila nimegundua kuwa dodoma ndo mkoa wenye NYOKA wengi hatari kuliko mikoa yote Tanzania. Pia nimekutana na watu wengine ambao pia wanadai dodoma hakufai, kisa wingi wa NYOKA.

Hii ni orodha ya nyoka ''HATARI" niliowaona kwa macho yangu katika ardhi ya Dodoma.

Koboko (black mamba)
Swila wa msituni (forest cobra)
Nyoka kijiti (twig snake)
Boomslang
Kifutu (puff adder)
Kifutu magamba (saw scalled viper)
Swila mweusi (spitting cobra)

THIBITISHENI AU BATILISHENI HILI KUHUSU DODOMA.
Umefika Morogoro?
 
Niliwahi kuumwa na joka kubwa saizi ya mkono wangu Wilayani Rombo kijiji cha Kirokomu mashambani, kama unakaribia Kiraeni, bahati nzuri lilinigonga kwenye kiatu. Nilikua huko masomoni form one.mkuu shule gan hiyo sio kili boys kweli hii mtoni kule nyuma ya shule ya msingi mto kuruuru
 
Niliwahi kuumwa na joka kubwa saizi ya mkono wangu Wilayani Rombo kijiji cha Kirokomu mashambani, kama unakaribia Kiraeni, bahati nzuri lilinigonga kwenye kiatu. Nilikua huko masomoni form one.
Pole na bahati yako ila huwezi weka kilimanjaro kwenye list ya mikoa yenye nyoka wakali.....Tabora, Kigoma, Shinyanga, Nachingwea huko, Dodoma, Singida, Morogoro na Tanga na list goes on lakini Tabora na Kigoma ndiyo baba zao.
 
Alichokisema mtoa mada hajakosea dodoma wapo nyoka wenye sumu kali na wakubwa nyoka ana rangi rangi kila mahali......

Tabora kuna nge, kenge, mamba, bila kusahau nyoka wakali kabisa, kwenye vichuguu, mibuyu, mashamba ya bangi koboko wanapenda sana kula bangi.....

Kanda ya kati yote kuna nyoka nenda singida apo Itigi mapori uone balaa la koboko.
 
Pole na bahati yako ila huwezi weka kilimanjaro kwenye list ya mikoa yenye nyoka wakali.....Tabora, Kigoma, Shinyanga, Nachingwea huko, Dodoma, Singida, Morogoro na Tanga na list goes on lakini Tabora na Kigoma ndiyo baba zao.
Nakubaliana na wewe 100%
 
Habari za mida hii ndugu wananchi, kifupi mimi siyo mtaalamu wa wanyama ila ni mpenzi na mfuatiliaji wa masuala ya wanyama na makala zao kupitia TV na mitandao.

Nimetembea mikoa karibu yote Tanzania ila nimegundua kuwa dodoma ndo mkoa wenye NYOKA wengi hatari kuliko mikoa yote Tanzania. Pia nimekutana na watu wengine ambao pia wanadai dodoma hakufai, kisa wingi wa NYOKA.

Hii ni orodha ya nyoka ''HATARI" niliowaona kwa macho yangu katika ardhi ya Dodoma.

Koboko (black mamba)
Swila wa msituni (forest cobra)
Nyoka kijiti (twig snake)
Boomslang
Kifutu (puff adder)
Kifutu magamba (saw scalled viper)
Swila mweusi (spitting cobra)

THIBITISHENI AU BATILISHENI HILI KUHUSU DODOMA.
Bado haujafika Tabora
 
Ndiyo mkuu wapo

Siha kuna sehemu ukitoka Ngarenairobi, ukifika Roseline. Kuna camp inaitwa Endarakwai.

Hapo kuna nyoka kibao. Ila si wengi sana. Kuna mpaka chatu. Ila si wale nyoka hatari.
Majina ya maeneo siyajui sana tulifata karoti kule, katika kutembea tembea kidogo kwenye majani marefu nlikanyaga nyoka mkubwa aiseee nlitoka nduki nimefika sehemu plain miguu inatetemeka siamini kama nipo salama
 
Back
Top Bottom