Nimeyakanyaga kwa mtoto wa kishua, napasuka kibunda kujifanya ninazo

Nimeyakanyaga kwa mtoto wa kishua, napasuka kibunda kujifanya ninazo

Nipo Mbeya kikazi hapa naishi karibu na mbuga ya mabinti wa vyuo takribani vitano huku maeneo ya forest.

Ukitaka mwendo tia gia havijileti, kidume nimejikoki kwa pisi kali ya chuo lakini mziki naopitia siyo poa.

Nilitaka nipige na kusepa lakini wahenga walisema ukionja asali huwezi kutosheka kwa kuchovya mara moja, binti kaninogea acheni tu, ni first year wale wa mwaka wa kwanza kutoka form 6.

huyu binti ni siku ya 10 hii nimegharamika takribani laki 2 kumpeleka hotelini na kuna siku 1 alikuja na mabesti zake watatu.

Uzuri tu ni kwamba kifedha naona yupo vizuri na hana mkopo anatumiwa pesa na mzee wake, sijawahi kumnunulia bando Wala kumpa hela ya usafiri wala nywele

nagharamika hotelini tu, hanywi pombe na kula yake ni ya kistaarabu sio ya kufakamia, hata ulaji wake tu unaonekana haya mambo ya hotel kwake kawaida

Penzi na enjoy lakini chamoto nakiona, hizi gharama kwangu zinanipiga ngumi ndoike maana hazikwepeki
Mkuu unatuzalilisha, ani kutumia laki mbili tu kwa siku 10 ndo unakuja hapa kulia lia kuwa umegharamika sana [emoji16][emoji16][emoji16]
 
Sasa mkuu mbona huku jiamini? Wewe umempa offer mwanamke mmoja yeye kaja na wenzake we wenzake ungeachana nao tu we ungelipa bill ya watu wawili
😂😂😂 Daah kiukweli ujasiri huo sikuwa nao boss, na sidhani Kama naweza kuwa nao kirahisi. Ila niliamua kumpiga chini mazima coz ndo ilikuwa hatua za mwanzomwanzo.
 
Back
Top Bottom