Nimezidiwa na maisha, niokoeni Watanzania wenzangu

Nimezidiwa na maisha, niokoeni Watanzania wenzangu

Endelea sasa hapo "The rest is history" ili tujue kama ni maisha ya kweli au wewe ni motivisheni spika tu.
Katika umri sawa nyakati tofauti
Mji ulele
Ni kiwa ndo nimemaliza chuo(nakuacha madeni kila kona)

Nikiwa namalizia research nilifikiria vitu vingi vya kufanya kujinasua nkaona mambo na kazi nyingi zilitakiwa niwe na mtaji au konection wakati sikua na chochote (ata ela ya kubind niliunga vibaya mno, achana na nauli, ilikua kazi sana.) Wala sikua na yoyote.

Basi siku ya 3 baada yakupumzika hom kwa Bro Mushono, nikaingia mjin nilikua na visimu vidogo viwili nikaulizia maduka ya wamachinga apo mmjin nkaeka bondi simu yangu moja nkachukua betri za elfu mbili mbili 4,

Nkaenda ofisi ya Airtel nkaomba kua msajili nkapewa code na line za kuanzia nkaingia mitaani
.siku ya 3 nkawa nishaikomboa simu yangu na nina mtaji wa betri 10

The rest is history.
 
Kama ni sound ni utapeli na hausaidii watu.
Kumotivate mtu na kumpa way foward for free ni jambo kubwa iwe realy au sound....!

Mzee kama haujapitia izi Mbanga za Mwanaukome uwezi elawa,
kama umekuta mitaro ipo ogelea tu na mshukuru Mungu,

wengine tunapitia moto mkali kubreak poverty cycle
 
Mkuu jiajiri kama dalali tu wa mitandaoni.

mimi ndio kazi inanifanya niishi. Ajira kama huna mtu wa kukushika.mkono ni changamoto, labda ukafanye kazi za ulinzi.

mfano kuna jamaa humu jf alikuwa anauza projector kwa 150,000

ikakaa miezi miwili.bila mteja,, akashusha.mpaka elfu 50, ehee nikaona dili.

nikampigia.simu tukaelewana, nitafute mteja bei ninayojua, 50 yake siigusi. Akakubali

Projector baada ya siku 3 nikapata mteja kwa 130,000!

nikaiuza, jamaa akawa.mwaminifu akanitumia elfu 80,000 akabaki na 50,000 yake
Thank you very much huu ndio u smart sio unapiga kelele mtandaoni hapa shababu wa miaka 25 ingia msituni kata kuni utapata pesa .
 
Habari, nina diploma ya ugavi na udhoefu wa mikopo, individual and groups (microfinance) nahitaji kazi yoyote kwa sasa,nikipata usimamizi na utendaji kwenye biashara yako nitakuingizia faida sana, nina management skills kubwa sana
0712605935
Nipo DSM
26yrs
 
Acha kuni please sio poa.
Nitakutafuta soon kwa sasa nimetingwa na Kazi na nilipo siwezi kukupigia maana namba yako haiko WhatsApp na nilipo gharama za kupiga simu TZ ni noma; cha msingi anza kutafuta Nauli. Ya kukufikisha japo Dar au usubiri nije Arusha.
Nashukuru sana mkuu. Ila hiyo namba ipo WhatsApp
 
Bwana bwana na Mimi leo nitoe yangu kidogo;
Ilikuwa mwaka 2019 nimemaliza chuo kikuu nje ya nchi nikatinga Tanzania. Nilikuwa na kimtaji kiasi kwa hiyo wakati nasaka ajira nilikuwa napiga biashara biashara bila uzoefu wowote, mara papu mtaji ukaisha baada ya kama mwaka hivi na ajira hakuna hata matumaini japo nilipiga Hadi level ya masters degree.
Sasa bwana nikawa nimeamua tu kuoa maana umri nao ulikuwa unaota mabawa. Wakati naona kuna rafiki yangu niliyesoma naye kutoka Ireland akawa amenitumia kama 2M hivi lakini kama unavyojua maswala ya kwenda ukweni, kununua hiki na kile n.k hii pesa nayo ilifika wakati ikaisha japo nilijaribu kununua mpunga wa 1M na bahati mbaya hata haukupanda bei hata buku.

Kizungumkuti kikaja wakati wife ana ujauzito kama miezi 7 kwenda 8, ndani nina 100K tu bado kodi, msosi, na mazagazaga mengine. Basi bwana nikaona hapa njia ni moja tu.
Asubuhi moja nikachukua 50K wife nikampatia 50K nikamuaga nikamwambia kuna mchongo nimepata sehemu naenda. Nikapanda lori kigumukigumu toka Dar hadi Mwanza kisha nikaingia Sirari. Kwanini Sirari? Niliona mchongo niliokuwa nao kichwani kama nikifanyia Dar au Mwanza itakuwa issue sana kwani mara kibao nilikuwa nakutana na washikaji nilipiga nao shule na chuo hapa Tz kabla sijapata mchongo wa scholarship.
Haya sasa nimeingia Sirari kule naamini kabisa kukutana na mtu anayenijua ukizingatia mkoa naotokea ni nadra sana. Nimefika kule nikiwa na 10K, namshukuru dereva wa Lori niliongea naye kiutu-uzima akanifikisha Mwanza tokea Dar kwa 30K.
Kufika Sirari nikalala guest ya 4K nikala 1K nikawa na balance ya 5K, hapo nimeshamwomba dogo langu ambaye yuko chuo walau kiasi kidogo lakini naye anazingua sana japo nilimsupport sana wakati nipo Europe.
Imefika asubuhi kazi yenyewe nilikuwa nawaza “KUSUKUMA TOROLI” dadeq. Bahati nzuri mimi huwa nina bahati ya kuwahi kuaminiwa na watu kwa hiyo kuna jamaa niliongea naye vema akakubali nikae kwake kwa siku kadhaa wakati najipanga. Mungu ambariki sana. Bwana bwana baada kama ya siku tatu huyu jamaa akanikopesha pesa nikanunua toroli nikaingia barabarani. A masters degree holder from a well recognized and highly respected university in the United Kingdom. Unaweza dhania ni hadithi lakini trust me nilifikia hatua hii.

Sasa kizungumkuti kikawa ni kupata wateja, kila mtu akiwa na mzigo anawaita wengine ambao tumepack matoroli pamoja, pengine nadhani kwa kuniangalia walijua vema ningeweza kuwa charge zaidi hivyo waliangalia wale wenye hali ya chini sana kimwonekano. Kazi ikawa ngumu sana. Wife 50K imeisha, bado mwezi mmoja ajifungue, huku hata nauli ya kurudi Dar sina.

Kama baada ya siku mbili hivi nikawa napiga stori na jamaa hivi naye Mungu ambariki. Nikamshirikisha wakati nilionao. Jamaa bwana akanipa wazo na akaniunganisha na mtu mwingine. Wazo lenyewe sasa, kwa kuwa nina passport ni rahisi kuingia Kenya kutokea Sirari. Kule inabidi nifuate MIRAA au mchicha kama hii kitu wanavoiita. Haki ya Mungu kwa wakati ule niliona kama NEEMA ya Mungu. Kesho yake nikajiandaa mapema mapema jamaa akanipatia cash ya Kenya safari ikaanza bwana. Mimi ilikuwa kwamba nahakikisha mzigo unafika Sirari. Mimi nikamuuga jamaa yangu aliyenipokea japo sikumwambia kama nafuata miraa Kenya badala yake nilimwambia naenda kupakia mzigo kwenye gari kule na kushusha tena Sirari kwa hiyo nitapata pesa.

Aliyesema Mungu si Athumani alikuwa sahihi bwana. Mzigo nikafikisha na nikapata kama 200K hivi. Mara 2nd round mara 3rd. Nikawa na kama 500K ikabidi nitume 400K kwa ajili ya maandalizi yote ya kujifungua wife ikiwa ni pamoja na kumsafirisha bimkubwa kutoka bush ili aende kusaidia kwani ndo ilikuwa uzao wa kwanza.
Mungu anisamehe hii kazi nilipiga karibu mwezi mzima na nusu nikapata pesa nzuri na kuja Dar kwa ajili ya kuwa na wife wakati anajifungua. Kweli nimefika ndani ya week akajifungua na ndani ya week hiyo hiyo nikapata mchongo halali na hadi sasa nimeajiriwa na maisha yanaenda poa sana.

HUU NI USHUHUDA TU SIYO USHAURI.

Aquila non capit muscas!
Mkuu ichi ulichokiandika ndo nakipitia sasa, ni bachelor digrii holder,sina kazi,sina mtaji,sina mchongo mbaya zaidi wife ana ujauzito wa miezi 8. Hivi hapa natafuta ela kdg kuna mji nataka nizamie, hapa hapa Tz nikatafute hela (Siwez fanya shughuli zangu za level ya chini nikiwa huu mkoa niliopo sababu zinaendana na izo ulizozitoa ww kipindi icho). Eeh Mungu saidia mja wako[emoji120]
 
Mkuu ichi ulichokiandika ndo nakipitia sasa, ni bachelor digrii holder,sina kazi,sina mtaji,sina mchongo mbaya zaidi wife ana ujauzito wa miezi 8. Hivi hapa natafuta ela kdg kuna mji nataka nizamie, hapa hapa Tz nikatafute hela (Siwez fanya shughuli zangu za level ya chini nikiwa huu mkoa niliopo sababu zinaendana na izo ulizozitoa ww kipindi icho). Eeh Mungu saidia mja wako[emoji120]

Ni PM Mkuu kama hutojali.
 
  • Thanks
Reactions: hnp
Habari, nina diploma ya ugavi na udhoefu wa mikopo, individual and groups (microfinance) nahitaji kazi yoyote kwa sasa,nikipata usimamizi na utendaji kwenye biashara yako nitakuingizia faida sana, nina management skills kubwa sana
0712605935
Nipo DSM
26yrs
Tatizo kubwa wa wabongo ni kukosa uaminifu, tamaa ya mfanikio ya haraka na kuwa na tamaa.
 
kama huchagui kazi...ebu njoo kwenye kampuni yetu ya gardaworld....hii ni kampuni ya ulinzi njoo ujishikize hapa kwa mwezi wanakulipa 250k na kuendelea...

unatakiwa uwe mrefu...nadhani ni kuanzia ft 5.64
tumia cheti chako cha kidato cha nne tu...!
uwe na cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha nida...na wadhamini wawili ambao watakuwa teyari kuja kukudhamini phisicaly...

nakutakia heri na mafanikio rafiki yangu
 
Kumotivate mtu na kumpa way foward for free ni jambo kubwa iwe realy au sound....!

Mzee kama haujapitia izi Mbanga za Mwanaukome uwezi elawa,
kama umekuta mitaro ipo ogelea tu na mshukuru Mungu,

wengine tunapitia moto mkali kubreak poverty cycle
kweli kabisa mkuu....kuna wengine tumerithi majina tu...tupo tunahangaika kuzitafuta kesho za wazazi wetu...sasa wenzetu wengine kesho yao ilishatengenezwa na wazazi wao...haya maisha hayana usawa kabisa ndugu yangu
 
  • Thanks
Reactions: Oxx
kweli kabisa mkuu....kuna wengine tumerithi majina tu...tupo tunahangaika kuzitafuta kesho za wazazi wetu...sasa wenzetu wengine kesho yao ilishatengenezwa na wazazi wao...haya maisha hayana usawa kabisa ndugu yangu
Ndo maisha mkuu, tena ukute bahati mbaya unakabiziwa mjukumu na huna pakushika....! Unajikusanya upate mtaji, ukigeuka kuna watu wanamahitaji...

Tupambane na tusikate tamaa, naamini tukijishughulisha bila kujali Mungu analeta mkuu, tutapitia changamoto nyingi ila tutafika tu iwe jua iwe mvua....!
 
kama huchagui kazi...ebu njoo kwenye kampuni yetu ya gardaworld....hii ni kampuni ya ulinzi njoo ujishikize hapa kwa mwezi wanakulipa 250k na kuendelea...

unatakiwa uwe mrefu...nadhani ni kuanzia ft 5.64
tumia cheti chako cha kidato cha nne tu...!
uwe na cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha nida...na wadhamini wawili ambao watakuwa teyari kuja kukudhamini phisicaly...

nakutakia heri na mafanikio rafiki yangu
Shukrani sana mkuu, nimekuja PM
 
Shukrani sana mkuu, nimekuja PM
kama unavyo vigezo nilivyokutajia kwa dar es salaam ofisi zipo mikocheni ile njia inayoelekea kawe......ukiwa unatokea kinondoni, kupita makao makuu ya zantel....kuna kituo kinaitwa kwamwinyi....ukifika hqpo ukimuuliza mtu yeyote atakuelekeza ofisi za garda zilipo...ukifanikiwa njoo utoe mrejesho...kitakacho kubeba hapo ni vigezo tu hakuna rushwa wala hongo ya aina yoyote

Arusha​

Plot Number 11 Simeon Road Kijenge Area
GW - Arusha Branch
Arusha
Tanzania
+255 754 250 600
 
Habari, nina diploma ya ugavi na udhoefu wa mikopo, individual and groups (microfinance) nahitaji kazi yoyote kwa sasa,nikipata usimamizi na utendaji kwenye biashara yako nitakuingizia faida sana, nina management skills kubwa sana
0712605935
Nipo DSM
26yrs
kama huchagui kazi...ebu njoo kwenye kampuni yetu ya gardaworld....hii ni kampuni ya ulinzi njoo ujishikize hapa kwa mwezi wanakulipa 250k na kuendelea...

unatakiwa uwe mrefu...nadhani ni kuanzia ft 5.64
tumia cheti chako cha kidato cha nne tu...!
uwe na cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha nida...na wadhamini wawili ambao watakuwa teyari kuja kukudhamini phisicaly...

kama unavyo vigezo nilivyokutajia kwa dar es salaam ofisi zipo mikocheni ile njia inayoelekea kawe......ukiwa unatokea kinondoni, kupita makao makuu ya zantel....kuna kituo kinaitwa kwamwinyi....ukifika hqpo ukimuuliza mtu yeyote atakuelekeza ofisi za garda zilipo...ukifanikiwa njoo utoe mrejesho...kitakacho kubeba hapo ni vigezo tu hakuna rushwa wala hongo ya aina yoyote
nakutakia heri na mafanikio rafiki yangu
 
kama unavyo vigezo nilivyokutajia kwa dar es salaam ofisi zipo mikocheni ile njia inayoelekea kawe......ukiwa unatokea kinondoni, kupita makao makuu ya zantel....kuna kituo kinaitwa kwamwinyi....ukifika hqpo ukimuuliza mtu yeyote atakuelekeza ofisi za garda zilipo...ukifanikiwa njoo utoe mrejesho...kitakacho kubeba hapo ni vigezo tu hakuna rushwa wala hongo ya aina yoyote

Arusha​

Plot Number 11 Simeon Road Kijenge Area
GW - Arusha Branch
Arusha
Tanzania
+255 754 250 600
Shukrani sana mkuu, Mungu akubariki
 
Back
Top Bottom