Nina maswali kadhaa kuhusu mwenge

Nina maswali kadhaa kuhusu mwenge

Halafu mbona km kiongozi wa wakimbiza mwenge mara nyingi naonaga muislamu
 
Chukulia kuwa mwenge ni fursa tu ya watu kupiga pesa.

Wajinga ndiyo waliwao.
Katika hili bibie tuko pamoja. Jumamosi ijayo hebu fanya uje huku Lushoto tuje tupate kinywaji pamoja. Yaani umenifurahisha sana. Gharama zote juu yangu.

Kiukweli mbio za mwenge kwa sasa zimegeuka kuwa kichaka cha watu wachache kuchezea hela za walipa kodi. Maana hazina faida/tija yoyote ile.
 
Hua nashangaa Sana serikali inavyo teketeza mabilioni ya fedha kuzungusha ule moto,

na wakati huo bado zahanati na wataalamu wa afya hawatoshelezi mahitaji, bado maji ni tatizo lisilo na ufumbuzi, umeme pia bado hautoshi, shule na vifaa vya kufundishia ni mgogoro usio na mwisho na mengine mengi ambayo hiyo fedha wanayo iharibu kwenye kuzungusha moto ingetosha kufanya, alafu fedha zenyewe bado wanakopa Kila mwaka na kuja kuziharibu,

Kwa nini ule moto usiwekwe makumbusho tuu atakae kuuona aufate makusho akautazame, mbona uingereza walio itawala hii nchi Wana mwenge lakini hawa potezi fedha na muda kwa kuukimbiza 🤔🤔 serikali iache kuchezea pesa na wakati zina mahitaji mengi Sana ya msingi
Umenena vema mkuu
 
Kinachotakiwa, kama unatumika Kiserikali usitumike au kutumia bajaeti za kiserikali, kama unatumika kichama, watabaki wajinga ndiyo waliwao.
 
1. Faida: Kukagua miradi mbalimbali iliyojengwa kwa fedha za umma na ile iliyotokana na michango ya Wananchi. Lengo kuwakumbusha watendaji kutolala kwani Mwenge utawaunguza. Pesa zinazohudumia Mwenge wa Uhuru zinatokana na michango ya hiari kutoka kwa Watanzania Wazalendo. Serikali inatoa bajeti ndogo sana ya Mwenge.

2. Baada ya kuzimwa, Mwenge wa Uhuru unahifadhiwa kwenye Makumbusho ya Taifa.

3. Ni jukumu la Rais wa JMT kumchagua Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru akishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) ambao nao huchagua Wakimbiza Mwenge wa Uhuru wengine kufanya wawe Sita Kitaifa.

4. Literary, hauzimwi, lakini linapokuja suala la kuongeza mafuta na kuufanyia services ndogo ndogo, unazimwa ila kwenye sehemu maalum.

5. Kufa ni kwa binadamu yeyote, anayekimbiza na hata ambaye hajawahi kuuona licha ya kuukimbiza wanakufa. Wapo ambao waliwahi kufa, lakini wapo wengine wapo hai hadi Sasa. Mfano, Kamanda Jordan Rugimbana na Mzee Sukwa Said Sukwa kutaja wachache.

6. Wanaouzunguka mara nyingi ni askari (FFU), Skauti au Vijana Shupavu kutoka UVCCM, ila LAZIMA wawe wameandaliwa kwa kazi hiyo. Lengo ni kuukinga na upepo usizimike.

7.Kila mwaka unatengenezwa mpya kwa ajili kuukimbiza kwa mwaka husika. Mwl. Nyerere alikuwa na vifimbo zaidi ya mia, lakini watu waliamini ni kamoja tu! Ahahahahaha!!!

8. Ulianza rasmi mwaka 1961 pale Ndugu Nyirenda alipouweka juu ya Mlima Kilimanjaro. Asili yake ni kutokana kauli ya hekima kutoka kwa Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliposema, " Sasa tunakwenda kuwasha Mwenge Ili umurike ndani na nje ya mipaka yetu.....!" Hakuna Imani za kishirikina wala nini ingawa huwezi kuzuia waja kunena!

Naamini kwa majibu yangu hayo umepata uelewa kidogo kuhusu Mwenge wa Uhuru. Karibu kwa maswali mengine!
Mkuu Hongera kwa kuwa mtu wa kwanza kujibu maswali yangu tena kwa ufasaha
 
muislam siyo Uislam. Kuna Waislam jina wengi sana tu.
Sawa nakubaliana na Hilo lakini ndio swali langu mbona Mara nyingi mwenge unakimbizwa na wenye majina ya kiislamu. Fuatilia viongozi wa wakimbiza mwenge kwa miaka kumi nyuma sidhani kama utakuta wenye majina ya kikristo zaidi ya wawili
 
Najibu swali la 4.
Siyo kweli kwamba mwenge hauzimwi.
Mwenge hauwezi kumaliza masaa 7 bila kuzimwa na kusafishwa alaf unawashwa tena ila kazi hiyo haifanywi hadharan unaingizwa kwenye chumba kilichoandaliwa kwa kazi hiyo.
Ukienda kwenye mkesha wa mwenge usiku utaona kila baada ya masaa mawili unabebwa na kuondolewa alaf baada ya muda mfupi unarudishwa hadharani.

Hata kwenye kuzindua miradi tu wakiona utambi umeamza kukauka unaweza kuzimika kinatafutwa chumba chap unapelekwa kusafishwa

Ni lazima usafishwe na kuwekewa mafuta na kubadilishiwa utambi mara kwa mara
 
Najibu swali la 4.
Siyo kweli kwamba mwenge hauzimwi.
Mwenge hauwezi kumaliza masaa 7 bila kuzimwa na kusafishwa alaf unawashwa tena ila kazi hiyo haifanywi hadharan unaingizwa kwenye chumba kilichoandaliwa kwa kazi hiyo.
Ukienda kwenye mkesha wa mwenge usiku utaona kila baada ya masaa mawili unabebwa na kuondolewa alaf baada ya muda mfupi unarudishwa hadharani.

Hata kwenye kuzindua miradi tu wakiona utambi umeamza kukauka unaweza kuzimika kinatafutwa chumba chap unapelekwa kusafishwa

Ni lazima usafishwe na kuwekewa mafuta na kubadilishiwa utambi mara kwa mara
Ni nafuta gani wanatumia
 
1. Faida: Kukagua miradi mbalimbali iliyojengwa kwa fedha za umma na ile iliyotokana na michango ya Wananchi. Lengo kuwakumbusha watendaji kutolala kwani Mwenge utawaunguza. Pesa zinazohudumia Mwenge wa Uhuru zinatokana na michango ya hiari kutoka kwa Watanzania Wazalendo. Serikali inatoa bajeti ndogo sana ya Mwenge.

2. Baada ya kuzimwa, Mwenge wa Uhuru unahifadhiwa kwenye Makumbusho ya Taifa.

3. Ni jukumu la Rais wa JMT kumchagua Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru akishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) ambao nao huchagua Wakimbiza Mwenge wa Uhuru wengine kufanya wawe Sita Kitaifa.

4. Literary, hauzimwi, lakini linapokuja suala la kuongeza mafuta na kuufanyia services ndogo ndogo, unazimwa ila kwenye sehemu maalum.

5. Kufa ni kwa binadamu yeyote, anayekimbiza na hata ambaye hajawahi kuuona licha ya kuukimbiza wanakufa. Wapo ambao waliwahi kufa, lakini wapo wengine wapo hai hadi Sasa. Mfano, Kamanda Jordan Rugimbana na Mzee Sukwa Said Sukwa kutaja wachache.

6. Wanaouzunguka mara nyingi ni askari (FFU), Skauti au Vijana Shupavu kutoka UVCCM, ila LAZIMA wawe wameandaliwa kwa kazi hiyo. Lengo ni kuukinga na upepo usizimike.

7.Kila mwaka unatengenezwa mpya kwa ajili kuukimbiza kwa mwaka husika. Mwl. Nyerere alikuwa na vifimbo zaidi ya mia, lakini watu waliamini ni kamoja tu! Ahahahahaha!!!

8. Ulianza rasmi mwaka 1961 pale Ndugu Nyirenda alipouweka juu ya Mlima Kilimanjaro. Asili yake ni kutokana kauli ya hekima kutoka kwa Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliposema, " Sasa tunakwenda kuwasha Mwenge Ili umurike ndani na nje ya mipaka yetu.....!" Hakuna Imani za kishirikina wala nini ingawa huwezi kuzuia waja kunena!

Naamini kwa majibu yangu hayo umepata uelewa kidogo kuhusu Mwenge wa Uhuru. Karibu kwa maswali mengine!
Vipi haijawahi kutokea ukazimika na upepo,kuna gari landcruiser pickup niliiona ina kile kimbao cha kuwekea mwenge na ina bango la mwenge,je mwenge unapopakizwa kwenye ile gari na kwenyewe huwa wanaukinga vipi usizimike maana gari ikiwa inasonga lazima ikate upepo
 
Uchawi wa kuzindika nchi ulianza mapangoni bagamoyo baada ya wazee kumuomba shetani awasaidie kuwafukuza wakoloni.
Shetani akawaambia wakoloni wataondoka lakini mtakuwa masikini.,wazee wakaona sawa bora wananchi wawe masikini lakini wakoloni waondoke.
Wakapewa mwenge baada ya kukubali masharti ili kuwapumbaza watu
 
Back
Top Bottom